Propaganda za uongo: Elimu bure, CHADEMA ikishinda

Ulianza vizuri lakini umemaliza vibaya. Ninachowaomba mimi ni bajeti yenu kivuli inayoambatana na ukusanyaji kodi (kwa muona wa CHADEMA) na matumizi ikiwa ni pamoja na utoaji wa elimu bure.

Pengine niwe wazi hapa- Kuwa cha BURE KABISA HAKIPO, SWALI ni nani atalipa. Nilivyowaelewa katika kampeni yenu 2010 ni kuwa mtatumia fedha za kodi ya wananchi kutoa elimu bure. Ninachowaomba ni kuiona bajeti hiyo hapa JF ili nielewa kama inawezekana au ni Propaganda za uongo za kuingilia IKULU.
Bado unajaribu kutumia akili ya Upinzani kuuliza swali. Chadema hata wakikupa maelezo yao maadam wewe unapoingana na sera zao huwezi kuona inawezekana! lazima utaona mapungufu upande wa pili kwa sababu sera zako ni pinzani.
Kwa mfano Chadema wakisema, watapunguza mishahara ya wanasiasa haswa rais, Mawaziri, Wabunge, Kuondoa kabisa manunuzi ya mashangingi na posho za vikao vya bunge, kupunguza gharama za safari na misafara ya rais na mawazirii zisokuwa lazima na kadhalika..Je, utaweza kuelewa na kutoshelezwa?

Hivi vyote, bado hutaelewa kitu kwa sababu huelkewi ni kiasi gani kitakusanywa kutokana na hayo, halafu utaanzisha Ubishi ktk sera ambazo hukubaliani na baadhi ya maamuzi kutokana na mtazamo wako. Halafu, tuacha kuwa wana Chadema au CCM, binafsi naamini kabisa inawezekana kama tukianza na kurekebisha sehemu muhimu za ukusanyaji wa kodi. TRA ifanyiwe marekebisho makubwa sana ktk utendaji kazi wake, iwezeshwe kwa vifaa vya kimataifa. Kila mwananchi awe na TIN namba yake - iwe lazima na ndicho kitambulisho.. Kodi ikishushwa na kuwa asilimia 10 hadi 15. KIla mapato yalipiwe kodi ktk transaction zote zenye kurekodiwa..Nina hakika wananchi na wafanyabiashara wengi watalipa kodi halali kuliko sasa hivi wanapotozwa kodi kubwa sana hivyo hupitia mlango wa nyuma. Kwa kutoza asilimia 10 serikali itaweza kukusanya zaidi pato la taifa kuliko leo hii bila ongezeko la uzalishaji. Licha ya hivyo less than 3 millioni ya wananchi ndio wanalipa kodi hata ukichukua hesabu ya watu wote waliojiandikisha kupiga kura - Hii ni aibu kwa nchi!

Moja ya sababu kubwa za Udini nchini zimetokana na mfumo tenge wa ELIMU..Mtazungumza yoote mnayoweza kuyasema lakini kwa mfumo wa ELIMU uliopo leo hii nchini, Udini utazidi kupata nguvu kubwa sana na pengine hata itakuja tokea vita. Nawasoma watu wote wanavyoandika hapa JF wenye jazba na majigambo, wengine matusi mazito mazito kwa sababu hakuna tsababu ya ujenzi wa chuki baina ya Muislaam na Mkristu isipokuwa kupitia Elimu..

JK sio sababu ya Udini nchini, yeye anatumia Udini uliopo kwa manufaa yake. Kwa wananchi wasiokuwa na Udini, JK hawezi kuwachonganisha atachekesha.. Hivyo nitawakumbusha tena Udini nchini Tanzania unatokana na mfumo wa elimu duni uliopo unatuathiri sote wazawa Waislaam kwa wakristu wakati wageni wanachukua nafasi hizi kutawala uchumi wetu..
 
hayo mapato ya kilimanjaro ni makusanyo ya mafisadi ccm,mapato ya chadema ni mara tano ya hayo .
halafu piga hesabu ya wanafunzi wanaonyanyasika na elfu ishirini za kata uone kama serikali ikilipa itatumia sh ngapi?
kuhusu kilimanjaro kuwa na shule nyingi waulize ccm ndio waliioongoza nchi kwa kipindi hicho chote.

kuhusu nyerere na uganda kila kitu kinajulikana alitumia rasilimali za nchi kumwokoa rafiki yake obote na hayo ndiyo chadema wanalalamikia sasa wewe na akili yako ndogo ukafikiri alishindwa kuongoza kwa sababu ya kulipia elimu bure\?sikulaumu kwani ndio vijana wa green guard na akili zenu za kuua watu.
hata hapa nafikiri unatafuta watu wa kuuwa ila nikupe pole wachangiaji wote hapa ni watoto wa mjini hamuwezi kuuuwa hata mmoja na mafunzo yenu ya singida misigiri.
 
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.

1. Tanzania haikutembelea magoti kwa vile ilitoa elimu na huduma za afya bure bali kwa vile iwekewa vikwazo na IMF nad Benki ya Dunia kwa vile Mwalimu Julius Nyerere alikataa kusaini baadhi ya masharti yao.
2. Chadema wanachosema ni kutumia bajeti ileile ya serikali isipokuwa kubadilisha vipaumbele. Mfano, serikali ya sasa imetoa kipaumbele ukubwa wa baraza la mawaziri, kutokusanya kodi ipasavyo, kufuja mali ya umma, posho na safari za nje, Chadema wanasema: watapunguza baraza la mawaziri, watakusanya kodi, hawatafuja mali ya umma, watapunguza posho na safari za nje. Kwa namna hii, inawezekana kabisa kutoa elimu bure na hata huduma za afya bure. Nilienda Algeria mwezi wa 12 mwaka jana - nao wanatoa elimu bure hadi chuo kikuu na kwa huduma za afya wanalipia asilimia 20 tu na utaratibu amabo wamejiwekea hata mtu maskini ana uhakika wa matibabu mazuri. Ongea na baadhi ya Watanzania wanaosoma au kufanya kazi huko watakwambia.
3. CCM ndiyo yenye propaganda za uwongo - kwanza Watanzania waliahidiwa maisha bora ifikapo 2010 lakini muda ulipofika wakabadirisha kauli. Nikuulize: je, ni Watanzania wangapi wana maisha bora leo hii kama ardhi yao inaendelea kuporwa kila siku?
4. Miezi kadhaa iliyopita kulikuwa na 'allegations' kuwa nchi imefiriska na viongozi wakuu wa serikali wakaja juu. Waziri wa Fedha alianza kutoa takwimu kuonesha jinsi tulivyo na fedha za ziada (surplus) lakini hadi leo siyo wastaafu wote wa Afrika Mashariki hawajalipwa mafao yao achilia mbali walimu, waathirika wa mabomu Mbagala na Gongo la Mboto etc. So, nani mwenye propaganda za uwongo hapa?
5. Leo hii pamoja na madini na kilimo Kwanza na kila kitu tulicho nacho, Tanzania inaongoza in sub-Saharan Afrika kupewa misaada. Kwa nini? Kwa kukupa mfano tu, Ujerumani inaisaidia Tanzania kuliko nchi nyingine yoyote duniani.
 
Bado unajaribu kutumia akili ya Upinzani kuuliza swali. Chadema hata wakikupa maelezo yao maadam wewe unapoingana na sera zao huwezi kuona inawezekana! lazima utaona mapungufu upande wa pili kwa sababu sera zako ni inzani.
Kwa mfano Chadema wakisema, watapunguza mishahara ya wanasiasa haswa Mawaziri, Wabunge, Kuondoa kabisa manunuzi ya mashangingi na posho za vikao vya bunge, kupunguza gharama za safari na misafara ya rais na mawazirii zisokuwa lazima na kadhalika..

Hivi vyote, bado hutaelewa kitu kwa sababu huelkewi ni kiasi gani kitakusanywa kutokana na hayo, halafu utaanzisha Ubishi kwa sera hukubaliani na baadhi ya maamuzi kutokana na sera zako. Halafu, acha kuwa mwana Chadema au CCM, binafsi naamini kabisa inawezekana kama tukianza na kurekebisha sehemu muhimu za ukusanyaji wa kodi. TRA ifanyiwe marekebisho makubwa sana ktk utendaji kazi wake, iwezeshwe kwa vifaa vya kimataifa. Kila mwananchi awe na TIN namba yake - iwe lazima na ndicho kitambulisho.. Kodi ikishushwa hadi asilimia 10 hadi 15. Nina hakika wanananchi na wafanyabiashara wengi watalipa kodi halali kuliko kupitia mlango wa nyuma. Kwa kutoza asilimia 10 serikali itaweza kukusanya zaidi pato la taifa kuliko leo hii bila ongezeko la uzalishaji.


Moja ya sababu kubwa za Udini nchini zimetokana na mfumo tenge wa ELIMU..Mtazungumza yoote mnayoweza kuyasema lakini kwa mfumo wa ELIMU uliopo leo hii nchini, Udini utazidi kupata nguvu kubwa sana na pengine hata itakuja tokea vita. Nawasoma watu wote wanavyoandika hapa JF wenye jazba na majigambo, wengine matusi mazito mazito kwa sababu hakuna tsababu ya ujenzi wa chuki baina ya Muislaam na Mkristu isipokuwa kupitia Elimu..

JK sio sababu ya Udini nchini, yeye anatumia Udini uliopo kwa manufaa yake. Kwa wananchi wasiokuwa na Udini, JK hawezi kuwachonganisha atachekesha.. Hivyo nitawakumbusha tena Udini nchini Tanzania unatokana na mfumo wa elimu duni uliopo unatuathiri sote wazawa Waislaam kwa wakristu wakati wageni wanachukua nafasi hizi kutawala uchumi wetu..


Salute Mkandara nilijua hapa lazima utaibuka .Umefunika vyema ila mleta mada ana chongo kwenye ubongo .Yeye shida yake ni Chadema tuuu hakuwa na nia ya kutaka kujua .Yeye kama Bakwata
 
Mtoa mada una agenda yako thats for sure,i will ignore your agenda tuendeleze mjadala sababu ni mzuri,kuna mtu hapo mwanzo ali comment kwamba mgawanyo wa rasilimali haufuati mahali zilipokusanywa.

Hilo ni jibu tosha kabisa kurudisha hoja yako nyumbani,lakini kama una nia ya dhati ya kuelewa,ama ya kujadili, basi ulete uwezo wa hizo shule kuchukua wanafunzi,na utupe wastani wa gharama kwa kila mwanafunzi halafu ukizidisha ndio utuambie kwamba ni kiasi gani kinahitajika na kiasi gani kinakusanywa.

Pili wanafunzi mkoa wowote ule hutoka sehemu nyingi Tanzania hapa, na kilimanjaro kuna idadi kubwa sana ya boarding schools,ambapo karibu watu wa kila mkoa utawakuta.

Tatu utambue kwamba hata tulivyokuwa tunasoma bure au kwa gharama nafuu, shule za binafsi zilikuwa zinatoza karo, I dont think hiyo policy itawazimisha private school wasomeshe bure, ila iawasaidia wasio na uwezo wapate elimu.

Nne,student faculty ration ya hizo shule ikoje?utakuta kuna shule wanamaliza wanafunzi 20,ziko 100,kwengine kuna wanafunzi 150 ziko 20..
kachimbue tene uje na information zaidi tujadili.

Tano, swali je unakubali kwamba ni muhimu kuwa na watu wengi wenye elimu kwa kadiri inavyowezekana? Na kama jibu ni ndio, altenative ya elimu ya gharama nafuu ni ipi? Tufanyeje ili watu wamudu gharama za kusoma hizi? Maana yake uchumi mgumu? Kuku na yai
 
Well you deceived and blind

Justice will overaul injustice

Wether you love isra HELL or what

Kama hawafanyi justice watapigwa vibaya sana na MUUMBA (and my trust to MUUMBA is beyong reasonable)

I am very sorry for you Topical, because now I come to believe that you are an islam activist against other religions, especially christianity! I'm telling you my dear citizen, Israel will never fail against islamic terrorist and Palestine! It has been written in the Holly Bible and we all see it in reality!

Forget about fighting for your fellow islam rights that will never come true in this world or in the Paradise!

Believe in Jesus you will be Free! Jesus bless you!
 
I am very sorry for you Topical, because now I come to believe that you are an islam activist against other religions, especially christianity! I'm telling you my dear citizen, Israel will never fail against islamic terrorist and Palestine! It has been written in the Holly Bible and we all see it in reality!

Forget about fighting for your fellow islam rights that will never come true in this world or in the Paradise!

Believe in Jesus you will be Free! Jesus bless you!

Thanks you, but you are mixing things

Mimi sina shida na christians wala israel as long as they do justice to others period!

As for accepting jesus, that is debatable..

Accepting as whom? (Messiah yes I do ) accept him as God (No I do not and I will not)
 
Elimu bure inawezeka kabsa,kama Rais Kagame ameweza kla raia kumpatia ng'ombe wa kufuga ss ilo ndo tushindwe?labda ufisad uchukue mkondo wake
 
Kumbe kuachwa na mke ndio kuna madhara namna hii?

Mkuu pole kwa analysis za kijinga na legelege, CCM ni chama chenye uwezo mkubwa wa kuwafanya baadhi ya watanzania kuwa wavivu kufikiri na kuwa wapumbavu....

Kwanini uwa hamtaki mtu kuzungumzia maisha mazuri ya mtanzania? Mtu akisema hivyo nyie mnakuja na analysis majitaka...Jaribu kutulia ufatilie pesa zinazochotwa toka serikali za mitaa mpaka serikali kuu ndio uje na uchambuzi wa kisomi..tunapoteza pesa nyingi mno na hata huyo raisi wenu aliwai kukiri hili more than a billions per month...ukichukua hizo pesa na zile wanazotuibia kwenye migodi tunaweza tukapunguza kwa kiasi kikubwa haya matatizo ya elimu mnyalukolo Ngoda...
 
Ukiona Topic/Thread haina mashiko ipotezee tu. Huyu hataki kukubali kuwa SERIKALI YETU INAFANYA UFUJAJI WA RESOURCES SAAANA TU.
mwaka jana MH.Waziri mkuu PINDA alisema hataki tena VX mpya na kuwa workshop na semina zipewe kibali maalum. kama Agizo hilo la Mh.Waziri mkuu lingetekelezwa serikali ya JK ingeweza kuokoa pesa nyingi tu.ambazo nahisi zingeongeza idadi ya MADAWATI na Mashimo ya Choo ktk shule zetu.

Huo ni mfano mdogo tu wa kudhibiti matumizi ya serikali.HAPO bado kukamata Wakwepa KODI,na kuongeza asilimia za Pato la MADINI.swala la Elimu bure ni swala dogo sana ktk Serikali iliyojipanga na yenye rasilimali Asilia nyingi kama Tanzania na hata Serikali ya CCM inaweza kulifanyia kazi endapo Maagizo ya viongozi yange heshimiwa na kutekelezwa.

Sometime namfagilia sana Waziri Mkuu Aliyejiuzulu Mh.Lowasa kwani yeye Akitoa Agizo LAZIMA litekelezwe na ndio maana wengi walifurahi Alipojiuzulu ili wafanye wanavyotaka Including na Makada wa CCM
 
Mimi nashangaa sana watu wanavyoona CDM jinsi ilivyokuwa waongo wakasahau ahadi za JK zilivyokuwa za uongo na zisizotekelezeka. Mimi naamini kabisa kama JK amekasirika kupita kiasi ukimpa mikanda ya kipindi cha kampeni yake ni LAZIMA atacheka sana na hasira kwisha kabisa kwa jinsi atavyojishangaa ujasiri wa uongo kiasi kile aliukoupatai! Hata leo zikifanyika kampeni natumani hawezi kudanganya kama awamu iliyopita.

Mkuu umeona eh? Ahadi zisizotekelezeka..... Dar es salaam kuna joto sana, ntawaletea mlima kilimanjaro to cool the atmosphere.
 
Rose Migiro alipoanza UN siku za kwanza ulimsumbua 'utanzania'. Alikatwa gharama zote za simu ya ofisi kwa mambo binafsi. Akichukua gari la ofisi na kupitia sokoni, hukatwa gharama za mafuta na overtime ya dereva. Alinyooka. Hiyo ni good governance. Elimu bure tz yawezekana. Lakini ni nani wa kubana mikanda?
 
i knew from the beginning that this topic is religiously motivated even though the perpetrator was trying to use schools in Kilimanjaro and Dar as contents.

nyambaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaf.

Unajau kuna watu wa ajabu sana, Wakati watu wanafanya HARAMBEE za kujenga sekondari za wazazi, wao busy wanachanga hela za Ngoma na Harusi unategemea nini?
 
Zawadi,
Unapouliza swali ni vizuri uwe na back up ya mfumo unaotawala mpango wa matumizi ya maendeleo nchini. Sasa unapotaka kuona Mkoa wa Kilimanjaro ukiweza kujitosheleza wakati maendeleo ya nchi bado yako centralized kupitia serikali kuu, unajaribu kujenga hoja gani haswa?. Ingekuwa vizuri sana kama ungeuliza swali bila kuwapangia Chadema watosheleze Elimu bure kutokana na kitu unachofikiria wewe. Usitake kulazimisha majibu unayoyategemea wewe..

Hili sii swali bali umejijengea majibu akilini mwako na kuona haiwezekani kwa sababu hujui mikakati ilitowekwa isipokuwa ile unayofikiria wewe...Kwa hiyo badilisha usemi wako, Uliza - Chadema waliahidi Elimu bure kwa wote wangeweza vipi kufanikisha azma hiyo?..Hata mimi ningependa sana kusikia Chadema walitarajia kufanya nini ili kuhakikisha Elimu bure inapatikana.

Halafu Nyerere hakushindwa kutokana na Elimu bure..Labda nikukumbushe tu kwamba Nyerere alitumia kiasi kidogo sana cha bajeti ya serikiali ktk ELIMU ukilinganisha na leo hii, isipokuwa kila fedha yake ilikuwa accounted for wakati leo hii bajeti ya Elimu inatumikia zaidi vikao, misafara na matumizi ya wizara pamoja na kulipa mishahara hewa zaidi kuliko ujenzi wa elimu yenyewe.

Ninafahamu wazi kuwa kodi inapelekwa makao makuu_ centralised. Hata hivyo ni mgawanyo huo wa kodi toka mikoa yote inayorudishwa tena mikoani.

Ninachokuomba hapa ni kutoa wastani wa matumizi ya mkoa mmoja ili tuwe karibu sana na uelewo wa hicho mnachokidai. Hata kama bajeti ya shule ya chakula hutolewa kwa shule nzima, lakini tunaweza jua kila mwanafunzi kwa siku amepangiwa sh ngapi.

Katika mazingira hayo ndio nakuomba uniambie katika bajeti mlioipanga (CHADEMA) ya mikoa yote, NI KIASI GANI MLIKIPA MKOA WA Kilimanjaro. Kama hujui ni kiasi gani mkoa wa kilimanjaro ingepata eti kwa kisingizio kuwa kodi iko centralised basi nitakuona hauko makini na hata CHADEMA HAMPO MAKINI. Maana hata leo nikamuuliza mkuu wa shule moja tu mkoani Kilimanjaro amepangiwa sh ngapi kwa mwaka wa fedha 2010/2011 atanieleza lakini nyie hamjui kitu.
 
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.


Unao ufahamu kuwa serikali yako haikusanyi kodi ipasavyo katika sekta zote,zile zinazolipa hasa hapa duniani ndio imeprove madudu kwa kuwanufaisha viongozi wachache na matajiri wa kigeni,matumizi ya hiyo kodi kidogo nayo wanagawana kwa namna ambayo si sahihi hasa kwa kutumia mikataba mibovu kana kwamba nchi yetu haina wanasheria?naomba ujitafakari kama na wewe ni mzima hapo juu na hili umeonyesha unakahoja kakinafiki tu husaidii lolote katika taifa hili tajiri kupita Libya.Nyerere alitaka tufaidi mali yetu wenyewe kumbe hakujua anakaa na manyang'au(alikataa kuchimbwa madini akijua anatayarisha wataalamu kwa ajili ya nchi yao,kumbe kuna majitu kupe yanamg'ong'a kisogo, viongozi wetu wa sasa wakati ule walikuwa vijana).
Jioni njema
 
Bado unajaribu kutumia akili ya Upinzani kuuliza swali. Chadema hata wakikupa maelezo yao maadam wewe unapoingana na sera zao huwezi kuona inawezekana! lazima utaona mapungufu upande wa pili kwa sababu sera zako ni pinzani.
Kwa mfano Chadema wakisema, watapunguza mishahara ya wanasiasa haswa rais, Mawaziri, Wabunge, Kuondoa kabisa manunuzi ya mashangingi na posho za vikao vya bunge, kupunguza gharama za safari na misafara ya rais na mawazirii zisokuwa lazima na kadhalika..Je, utaweza kuelewa na kutoshelezwa?

Hivi vyote, bado hutaelewa kitu kwa sababu huelkewi ni kiasi gani kitakusanywa kutokana na hayo, halafu utaanzisha Ubishi ktk sera ambazo hukubaliani na baadhi ya maamuzi kutokana na mtazamo wako. Halafu, tuacha kuwa wana Chadema au CCM, binafsi naamini kabisa inawezekana kama tukianza na kurekebisha sehemu muhimu za ukusanyaji wa kodi. TRA ifanyiwe marekebisho makubwa sana ktk utendaji kazi wake, iwezeshwe kwa vifaa vya kimataifa. Kila mwananchi awe na TIN namba yake - iwe lazima na ndicho kitambulisho.. Kodi ikishushwa na kuwa asilimia 10 hadi 15. KIla mapato yalipiwe kodi ktk transaction zote zenye kurekodiwa..Nina hakika wananchi na wafanyabiashara wengi watalipa kodi halali kuliko sasa hivi wanapotozwa kodi kubwa sana hivyo hupitia mlango wa nyuma. Kwa kutoza asilimia 10 serikali itaweza kukusanya zaidi pato la taifa kuliko leo hii bila ongezeko la uzalishaji. Licha ya hivyo less than 3 millioni ya wananchi ndio wanalipa kodi hata ukichukua hesabu ya watu wote waliojiandikisha kupiga kura - Hii ni aibu kwa nchi!

Moja ya sababu kubwa za Udini nchini zimetokana na mfumo tenge wa ELIMU..Mtazungumza yoote mnayoweza kuyasema lakini kwa mfumo wa ELIMU uliopo leo hii nchini, Udini utazidi kupata nguvu kubwa sana na pengine hata itakuja tokea vita. Nawasoma watu wote wanavyoandika hapa JF wenye jazba na majigambo, wengine matusi mazito mazito kwa sababu hakuna tsababu ya ujenzi wa chuki baina ya Muislaam na Mkristu isipokuwa kupitia Elimu..

JK sio sababu ya Udini nchini, yeye anatumia Udini uliopo kwa manufaa yake. Kwa wananchi wasiokuwa na Udini, JK hawezi kuwachonganisha atachekesha.. Hivyo nitawakumbusha tena Udini nchini Tanzania unatokana na mfumo wa elimu duni uliopo unatuathiri sote wazawa Waislaam kwa wakristu wakati wageni wanachukua nafasi hizi kutawala uchumi wetu..

Mkuu Mkandara, nna'admire' uwezo wako wa kujenga hoja zenye mantiki. Kuna haja ya kujua tofauti za Uislam na muislam, ukristo na mkristo, utanzania na mtanzania. Udhaifu wa JK wa kutawala hautokani na yeye kuwa muislam bali udhaifu wake. Nadhani km angeweza kufuata nusu ya misingi na mafundisho ya uislam, taifa hili lingepiga hatua. Nnaongozwa na mkurugenzi muislam nami ni mkristo, uongozi wake haujakwamisha imani km mkristo wala kukwamisha maendeleo yangu kazini, bali umeniendeleza. Nakubaliana nawe lazima km taifa, tuongelee tofauti hz zinazokuzwa za udini kwa mpango maalum
 
Back
Top Bottom