Propaganda za uongo: Elimu bure, CHADEMA ikishinda

Zawadi Ngoda

JF-Expert Member
Aug 13, 2009
3,804
1,871
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.
 
Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.

wewe ni boya sana
Hivi unajua serikali yetu inawasaidia wafanyabiashara wakubwa kufanya TAX AVOIDANCE/EVASION??? tena katika mpaka wa Kilimanjaro na Kenya usiseme yaani ukiwa kada wa CCM biashara zako hulipi kodi.

Hivi unajua ni kiasi gani KAMPUNI iliyobinafsishiwa Uwanja wa ndege wa KIA inapora kila mwaka???
Hivi unajua katika kipindi cha mwaka 2009-2010 kampuni hii haionekani katika orodha ya waingiza mapato wa Tanzania wakati 2008-2009 iliingiza bilioni kadhaa???
 
Naona sasa kuna haja ya kuwachunguza baadhi ya watu,naona kuna wengine sio raia wa nchi hii kabisa,we mleta mada unatokea nchi gani?
 
Huhitaji kwenda shule kuelewa hiyo hoja ya elimu bure!! Elimu bure inawezekana, fanya homework yako vizuri tutakuelewa kama utatuletea facts siyo kuturudisha nyuma wakati tuko karne ya 21.
 
magawanyo wa rasilimali za nchi hii hutegemei pale zinapotoka, mapato ya Dar es salaam au kwenye migodi yanawafaidisha hata wamakonde wa Newala na wamakua wa Masasi. Sasa jiulize, mapato ya serikali yanakwenda wapi? si ndani ya mifuko ya mafisidi waliorundikana serikalini na kwenye chama cha Magamba?

Nyerere alisema inchi corrupt haikusanyi kodi, Tanzania ni nchi corrupt, kodi haikusanywi hata kile kidogo kinaishia kugharamia kuiba kura kwenye hata vichaguzi vidogo, sahau Kagoda, Meremeta, EPA n.k Nchi ina viongozi wa ajabu sana (CCM) wawekezaji wanapewa tax relief ya miaka mitano ikiiisha anauza anaingia mwingine naye anapewa miaka mitano mpaka miaka 50 mingine ya uhuru(itakuwa 100) kodi haikusanywi.

Madini hayatusaidii chochote,tumeshindwa hata kujifunza kwa wenzetu wa Botwsana, Zambia nk. hebu jiulize wewe Ngonda, TZ sasa inaweza jifananisha na Rwanda waliochinjana miaka 15 tu iliyopita? posho za vikao na nguo za bure za kijani zisikufanye upoteze utu wako.
 
Mimi nashangaa sana watu wanavyoona CDM jinsi ilivyokuwa waongo wakasahau ahadi za JK zilivyokuwa za uongo na zisizotekelezeka.

Mimi naamini kabisa kama JK amekasirika kupita kiasi ukimpa mikanda ya kipindi cha kampeni yake ni LAZIMA atacheka sana na hasira kwisha kabisa kwa jinsi atavyojishangaa ujasiri wa uongo kiasi kile aliukoupatai! Hata leo zikifanyika kampeni natumani hawezi kudanganya kama awamu iliyopita.
 
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.


Ha ha ha ha ha! Nimegundua Kuna Watu Kilimanjaro Inawawasha Kama Upupu!
 
Really? kwanini alienda vitani?

Topical mbona unanishangaza? How old are you? Hujui IDD AMIN alichofanya Kagera. Yaani wewe ningekutukana vibaya hujui ndugu zangu na babu zangu waliokufa huko Minziro walikuwa wangapi yaani wewe zuzu. Akili zako kama za JK ambaye haijui Dowans, Hajui kwa nini Tanzania ni Maskini. Na wewe upo upo.
 
AHADI ZA KIKWETE KWA WAPIGA KURA KATIKA KAMPENI ZA URAIS 2010.

1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora
2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini
3. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga
4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga
4. Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma
5. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini
6. Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma
7. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera
8. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera
9. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini
10. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
11. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera
12. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera
13. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera
14. Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino- Mbeya
15. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera
16. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
17. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza
18. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza
19. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita
20. Kulinda muungano kwa nguvu zote-Pemba
21. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro
22. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini
23. Kujenga bandari Kasanga –Rukwa
24. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
25. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya
26. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga
27. Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa
28. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani –Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro
29. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini
30. Kuboresha barabara za Igunga -Tabora
31. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu
32. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini
33. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara
34. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma
35. Kulinda haki za walemavu- Makete
36. Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini
37. Kujenga barabara Musoma–Mto wa Mbu Arusha-Arusha
38. Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
39. Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma– Kaliua,Tabora
40. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini
41. Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa,mpaka Singida-Dodoma
42. Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
43. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha –Arusha mjini
44. Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, .
45. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido
46. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
47. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara
48. Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini
49. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa
50. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa
51. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa
52. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda
53. kutokomeza malaria 2015-Bunda,mkoa wa Mara
54. kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo ,Iringa
55. ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar
56. Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kabandamaiti mjini Zanzibar
57. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti
58. Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma
59. Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400-Mbambabay Ruvuma
60. kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga(MBICU) –Ruvuma
61. Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania –Ruvuma
62. Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
63. Mtwara kuwa mji wa Viwanda –Mtwara
64. Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha
65. Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa-Kibaha
66. Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha
 

Attachments

  • AHADI ZA KIKWETE KWA WAPIGA KURA KATIKA KAMPENI ZA URAIS 2010.docx
    19.8 KB · Views: 65
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.


Najiuliza kama hoja hii imejengewa kichwani kwa mtu au Kwenye nyonyo!!!! Tunasubiri Meli Mpya aliyoahidi KIkwete kuliplace Mv Bukoba iliyosababisha niwe Orphan.
 
Topical mbona unanishangaza? How old are you? Hujui IDD AMIN alichofanya Kagera. Yaani wewe ningekutukana vibaya hujui ndugu zangu na babu zangu waliokufa huko Minziro walikuwa wangapi yaani wewe zuzu. Akili zako kama za JK ambaye haijui Dowans, Hajui kwa nini Tanzania ni Maskini. Na wewe upo upo.
unaweza kukuta Topical ana masters nzuri tu ila anashinda manzese bakresa kwenye midahalo ya dini manake pale manzese niliwahi kusikia hii hoja ya nyerere aliivamia UGANDA kumwondoa muislam madarakani.Foleni ilisogoa nikashindwa kujua kwa nini shehe alikuwa ya hayo madai.
 
Topical mbona unanishangaza? How old are you? Hujui IDD AMIN alichofanya Kagera. Yaani wewe ningekutukana vibaya hujui ndugu zangu na babu zangu waliokufa huko Minziro walikuwa wangapi yaani wewe zuzu. Akili zako kama za JK ambaye haijui Dowans, Hajui kwa nini Tanzania ni Maskini. Na wewe upo upo.

Sijui bana si wewe una akili sana niambie mkuu wangu?

Eh kulitokea nini huko kagera? aise nijuze
 
unaweza kukuta Topical ana masters nzuri tu ila anashinda manzese bakresa kwenye midahalo ya dini manake pale manzese niliwahi kusikia hii hoja ya nyerere aliivamia UGANDA kumwondoa muislam madarakani.Foleni ilisogoa nikashindwa kujua kwa nini shehe alikuwa ya hayo madai.

Programmed mind
 
wewe ni boya sana
Hivi unajua serikali yetu inawasaidia wafanyabiashara wakubwa kufanya TAX AVOIDANCE/EVASION??? tena katika mpaka wa Kilimanjaro na Kenya usiseme yaani ukiwa kada wa CCM biashara zako hulipi kodi.

Hivi unajua ni kiasi gani KAMPUNI iliyobinafsishiwa Uwanja wa ndege wa KIA inapora kila mwaka???
Hivi unajua katika kipindi cha mwaka 2009-2010 kampuni hii haionekani katika orodha ya waingiza mapato wa Tanzania wakati 2008-2009 iliingiza bilioni kadhaa???

Maneno mengi yanini. Wewe toa makadirio yako ya kodi na unipigie hesabu ya matumizi katika sekta zote mkoani na utoe balance. Usikosoe tu jaribu kuja na majibu mliyonayo kwa data unazozielewa wewe.
 
Back
Top Bottom