Consigliere
Platinum Member
- Sep 9, 2010
- 12,689
- 26,568
Inasikitisha kuona hadi miaka hii kuna watanzania wapo poor sighted kiasi hiki.Mafioso wana kaulimbiu yao inasema usifanye jambo kwa kukurupuka wala kwa shinikizo maana hutafaulu kutokana na makosa mengi ya kiufundi
Katika hali ya kuchanganyikiwa baada ya kushindikana kuuharibu uchaguzi wa CDM, plan B ikawa ni kulitumia kundi lililoshindwa
Njaa haina baunsa.. Watu wakajaa kwenye mfumo, wakajazwa shekeli na ufadhili wa kuunda G55.. Hili likatikisa kidogo tu kabla ya kukataliwa na hadhira
Halikuwa na maandalizi
Halikuwa na mfumo
Halikuwa na ajenda
Halikuwa na utararibu
Halikuwa na maono
Na mbaya zaidi asilimia 99 ya wajumbe walikuwa wa asili moja
Likabaki kama kundi sogozi la umbea fitina na majungu.. Kwakuwa halikuwa na ajenda wala maandalizi.. Umbea ule na majungu yale yakawarudi na kuanza kushutumiana na kutoaminiana tena..
Kwasasa linapumulia mashine baada ya wengi kujitoa.. Ni kama limesambaratika
Baada ya kugundua hilo kosa kubwa la kiufundi ikaletwa sub project nyingine ya viongozi mbalimbali kujiondoa CDM
Hawa wameahidiwa mengi ikiwemo kupata platform ya kujiweka busy
Project CHAUMA ndio inafuata.. Hapa pamewekezwa pesa nyingi bila mikakati ya kueleweka .. Hapa ndio litakuwa jalala kuu la wale wote kutoka CDM walio na watakaokubali kuchuuzwa kwa bei ya mnada wakiwemo wale mabaki wa G55
Project CHAUMA itafeli pengine hata project G 55 kwakuwa ni wapigaji watakuwa wamekutana na masikini waliojaa majungu fitina na kijicho
Wawakilishi wa wafadhili wanajipigia hapo.. Wawakilishi wa maskini nao wanajipigia hapo hapo! Mwisho kitakachowafikia maskini ni mkia wa mbuzi.. Na vita ya anguko kuu itaanzia hapo🤣
View attachment 3338326
Vijana wengi wa Kihindi na baadhi wa Kiarabu walioishi nchini Tanzania, wazazi wao waliwapeleka kusoma na kutafuta huko Ulaya na Marekani, sasa hivi wanarudi Tanzania wakiwa na projects, ndiyo hawa wana viwanda na makampuni Makubwa, ndiyo hawa wanafadhili siasa za Tanzania.
Ndiyo wanaamua nani awe mbunge, sababu kwenu ninyi mbunge ni muwakil8shi lakini kwao mbunge ni project. Mbali ya kupitisha na kutetea wayatakayo kule bungeni, pia ndiyo huwatumia kusafirisha nyara za serikali kupitia diplomatic passports za wabunge hao.
Kinachoumiza ni kuona watanzania wenyewe wakiwa usingizini wakitumiwa kwa mambo yasiyo na tija si kwao tu bali hadi kwa vizazi vyao. Watanzania wamegoma kubadilika, wakati wazazi wa wenzao wal9zitumia fursa za humohumo kuwaandaa na kuwapeleka watoto wao nje, wakapata glibal connections na sasa wanarudi kuendeleza pale wazazi wao waliishia.
Watanzania wenyewe wamebaki kama Mahoka tu...mae