Tinsley
JF-Expert Member
- Nov 16, 2020
- 14,590
- 38,211
Awwh , watoto ni baraka
Awwh , watoto ni baraka
Nimefuatilia kwa muda kidogo mambo haya na harakati za binadamu kwa mambo ya anga kwa bahati mbaya hii bado sikuwahi kuliona! Asante ndugu yangu umenipa hamasa ya kufatilia kila engo.Huu mjadala upo ndugu haohao wanasayansi walishachuana sana tu,mkuu zipo signals zinarushwa zaidi ya hizo na ndio zikiangukia kwa viumbe wabaya itakuwa tabu lkn ndugu unafikiri tukae tu hivihivi tusitafute changamoto..??
Asili ya binadamu ni kutaka kujua na hichi kitu kipo ndani yetu huwezi mzuia binadamu kufanya uchunguzi.. ukitaka kumfanya binadamu afanye uchunguzi mwambie hicho chumba usiingie!!! Lazima atataka kujua Kuna nini..?
Hili swala linamatokeo mawili tunaweza kupata kitu kibaya au kizuri pia muhimu kukabiliana na yote mi sisapoti kukaa tu!.
Zaidi tunatafuta intelligent life namaanisha viumbe vyenye ufahamu Kama wetu au zaidi,so hata hapa duniani ipo mitambo maalum inayodaka signals kutoka nje miaka ya zamani kuna signal ilishapatikana wakaiita Wow signal ila haikuleta majibu ilitokea wapi na maana yake,waliporudisha mitambo ktk frequency ileile hakuna kilichotokea!.. ulimwengu bado ni kimya sana..
Mi naunga mkono tafiti kuliko kukaa tu.
Haha! Mkuu sisi hatuna hulka ya kutulia sio kwamba hatupendi amani tunapenda Sana na ndio maana hata hapa duniani tunamantain amani japo si sehemu zote ila kwa wingi ipo,amani inatengenezwa tu.Nimefuatilia kwa muda kidogo mambo haya na harakati za binadamu kwa mambo ya anga kwa bahati mbaya hii bado sikuwahi kuliona! Asante ndugu yangu umenipa hamasa ya kufatilia kila engo.
Ila nimefurahi kujua mwanadamu huwa ni mtu wa kutafuta changamoto hapendi kuwa na amani yaani, inastaajabisha kwa kweli!
AmeenNapenda sana watoto .
Eh Mungu naomba uwajalie wamama wote wanaotafuta watoto uwapatie zawadi hii .
Hapana,lakini kama mimi,mavazi.Huyo ni wewe..?
Okay hongera yako..
Time to have Kaya now,,,kaya...kayaaa!!!Humu jukwaani natumia jina la Kayaman, napenda na navuta sana bangi, ninatumia profile pic ya bob marley kutokana na wimbo wake wa Kaya huwa unanihamasisha sana kuvuta bangi, mwanzo nilitamani kutumia picha ya peter tosh kutokana na wimbo wa legalize it ila nikaona acha niende na bob!
So wazilima bado..?Me mkulima na zao lililonitoa ni Pilipili hoho , nilizoea pilipili hoho za rangi ya kijani wakati fulani nilienda kutembea Dodoma nikiwa na marafiki zangu, kulikua na supermarket ikabidi tuingie kuosha macho kidogo palikua pakubwa sana ! Na ndo mara ya kwanza kuona hoho za rangi ya njano na nyekundu zilikua packed !! Nikasema hizi lazima nizilime ile kuingia mtandaoni kupata ABC nikakutana na hiyo picha ,Na ndo imekua profile pic yangu hadi leo !
Mimi natumia picha ya Chifu Mbelwa wa Tanga alieingia mkataba na mwakilishi wa Ujerumani kumpa sehemu ya Tanganyika 1884Nimegundua kitu watu huwasilisha ujumbe kwa kupitia profile picture zao,na moja kwa moja aidha ujumbe husika mara nyingi huwa unamhusu mtu husika,
Kinaweza kuwa kitu unachokipenda au ambacho kinahusu maisha yako ktk namna fulani, karibuni hapa tuelezee kwa uchache tu kwanini unatumia hiyo avatar.
Binafsi avatar yangu ni GOLDEN RECORD,hii avatar niliipenda kwasababu zaidi napendelea mambo ya sayansi ya anga kwa kifupi hii golden record ni disk ambayo iliwekwa kwenye kifaa cha kisayansi kilichorushwa miaka ya zamani sana. Kifaa kilichobeba hii golden record kinaitwa Voyager 1,mpaka hivi sasa kifaa hichi kimeshapita mbali sana I mean kimeshatoka nje ya solar system yetu!. Nini kipo kwenye golden record..?
View attachment 1988481
Disk hii imetengenezwa kwa dhahabu ili iweze kutunza ujumbe uliomo kwa muda mrefu na disk hii inarekodi za sauti nyingi kutoka hapa duniani Kama mvua,sauti za wanyama,picha na salamu za lugha mbalimbali pia inaonyesha ramani ya sisi tulipo(dunia yetu).
Lengo lilikuwa ni kujulisha viumbe wengine(Kama wapo na wakibahatika kukipata kifaa husika).. ukiangalia pichani Kuna michoro kila mchoro ktk golden record unamaana yake nimeelezea kiufupi ila nishasikiliza kilichowekwa humo ni record ambayo inamasaa takribani matano!.. sikumaliza yote Kuna miziki n.k hi yote ni kututambulisha sisi kwa hao viumbe wengine.
Kwanini hiyo picha..? Kwasababu kwanza napenda "HUMANITY" pia napenda "ULIMWENGU" na sifa zake zote napenda Sana kuufahamu ulimwengu zaidi ya hivi ninavyoufahamu!. So hii picha kwangu inamaana kubwa Sana kutokana na kiu cha kupenda sayansi ya anga, kupenda kuujua ulimwengu pia napenda humanity yani jinsi tulivyo ndio maana hata ktk profile banner yangu nimeweka picha ya Adam na Eva hii ikielezea jinsi navyopenda uutu wetu na mazingira yetu kiujumla!.
Nisiwachoshe yangu ni hayo machache wewe je, profile picture yako inazungumza nini..??
Dah! Wapiga dili walianza kitambo so nawewe ni mpiga dili mkuu..?Mimi natumia picha ya Chifu Mbelwa wa Tanga alieingia mkataba na mwakilishi wa Ujerumani kumpa sehemu ya Tanganyika 1884View attachment 1988858