1
TAARIFA KWA UMMA
ZABUNI YA 4 YA KUNADI VITALU VYA
UTAFITI WA GESI ASILIA
Utangulizi.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo
ya Petroli Tanzania (TPDC), tarehe 25/10/2013 ilizindua rasmi zabuni ya
nne ya vitalu vya utafiti wa mafuta na gesi asilia vilivyoko bahari kuu na
ziwa Tanganyika kaskazini. Uzinduzi wa zabuni hii ulihusisha vitalu 7
vilivyoko bahari kuu (deep offshore blocks) pamoja na kitalu cha ziwa
Tanganyika kaskazini (Lake Tanganyika North). Vitalu vya bahari kuu vipo
katika kina cha maji kati ya mita 2000 na 3000 wakati kitalu cha ziwa
Tanganyika kinafikia kina cha mita 1500. Mchakato wa zabuni utafungwa
rasmi baada ya miezi sita na Zabuni zitakazowasilishwa kabla ya saa nne
asubuhi ya Alhamisi ya tarehe 15 mwezi Mei mwaka 2014. Zabuni
zitafunguliwa kwa uwazi mbele ya washiriki wa mnada watakaopenda
kuwepo ama kuwakilishwa siku ya ufunguzi.
2
Majina ya vitalu vinavyonadiwa ni kama inavyooneka katika jedwali hapa
chini.
Nambari Jina la kitalu Eneo (mita za Mraba)
1 Block 4/2A 3630
2 Block 4/3A 2620.3
3 Block 4/3B 3045.0
4 Block 4/4A 2963.3
5 Block 4/4B 3048.9
6 Block 4/5A 2545.3
7 Block 4/5B 3052.6
8 Lake Tanganyika North 9670.2
Faida za Ugawaji wa Vitalu vya utafiti kwa njia ya Zabuni
Utaratibu huu wa kutoa maeneo kwa kutumia zabuni hutumika sehemu
nyingi duniani zikiwemo nchi nyingi za Bara la Afrika, Asia, Ulaya, Marekani
(kusini na kaskazini). Umuhimu wa kugawa vitalu kwa njia ya zabuni ni
pamoja na:
 kuhakikisha kuwa mchakato mzima unafanyika kwa njia ya uwazi;
 kutoa vitalu kwa utaratibu mzuri ili kuweza kuendeleza rasilimali kwa
gharama nafuu endapo ugunduzi utafanyika;
3
 kupata wawekezaji bora wenye mitaji, utaalamu na uzoefu wa
kufanya utafutaji;
 kutoa nafasi kwa wawekezaji wazalendo kushiriki katika shughuli za
utafutaji wa mafuta na gesi; na
 kutoa fursa kwa makampuni mengi na wataalamu mbalimbali kuona
takwimu (data) zilizopo na hivyo kupata kwa wingi maoni mbali mbali
ya kitaalamu kuhusiana na uwezekano wa kuwepo mafuta na/au
gesi.
Gharama za kushiriki kwenye Zabuni
Gharama za kushiriki kwenye zabuni zinajumuisha ada isiyorejeshwa ya
ushiriki kwenye zabuni, gharama za kununulia kifurushi cha zabuni
yenyewe, gharama za kununulia vifurushi vya data za mitetemo cha lazima
kwa waomba zabuni wa vitalu zilivyopo bahari kuu na ziwa Tanganyika
kaskazini na gharama za kununulia ‘data' za nyongeza za hiari kadri
mshiriki atakavyoona inafaa.
Ada ya ushiriki kwenye zabuni isiyorejeshwa ambayo ni Dola za Marekani
50,000. Gharama halisi ni kama zilivyonyambuliwa hapa chini:
Gharama kwa muombaji wa vitalu vya baharini
i. Gharama za kununulia kifurushi cha lazima cha zabuni za vitalu
vya bahari kuu (Bidding Round Data Package (BRDP) for deep
offshore blocks) ni Dola za Marekani 750,000 kwa kila kifurushi.
4
ii. Gharama za kununulia kifurushi cha lazima cha taarifa za
mitetemo ya ‘Mandatory 2D SPAN' ni Dola za Marekani milioni
3.375 kwa kila kifurushi.
iii. Gharama za kununulia taarifa za hiari za mitetemo ya ‘Optional 2D
SPAN data' ni Dola za Marekani 750 kwa kila kilomita moja ya
urefu.
Gharama kwa muombaji wa kitalu cha kaskazini ya ziwa
Tanganyika
i. Gharama za kununulia kifurushi cha lazima cha zabuni ya kitalu
cha ziwa Tanganyika kaskazini (BRDP for Lake Tanganyika North)
ni Dola za Marekani 350,000 kwa kila kifurushi
ii. Gharama za kununulia taarifa za hiari za mitetemo ya ‘Optional
Phase I and Phase II data' ni Dola za Marekani 220 kwa kila
kilomita moja ya urefu.
Waomba zabuni ni lazima waoneshe ushahidi wa kununua taarifa (data)
kwa kuambatisha risiti ya manunuzi pamoja na mkataba wa kutunza siri
waliosaini katika zabuni watakazo rejesha.
Kabla ya kushiriki katika uombaji zabuni, makampuni yote ni lazima
yaweze kutimiza masharti ya zabuni yaliyowekwa. Makampuni inabidi
yanunue kifurushi cha zabuni husika (Bid Round Data Package – BRDP).
5
Kifurushi cha zabuni (Bid Round Data Package – BRDP)
Katika kifurushi hiki kuna vitabu vya zabuni pamoja na maelekezo ya
taratibu za kushiriki na kuwasilisha zabuni [Bidding Instructions]; maelezo
ya jinsi ya kutathini zabuni [Evaluation Criteria]; vipengele vya tathmini ya
uwezo kifedha [Fiscal Terms]; mfano wa mkataba wa kugawana mapato
wa 2013 [Model Production Sharing Agreement]; Sheria inayosimamia
utafiti na uzalishaji ya mwaka 1980 [Petroleum (Exploration and
Production) Act 1980]; Sheria ya Hifadhi ya Mazingira [Environmental
Management Act 2004]; Sera ya Nishati ya 2003 [Energy Policy of 2003];
na Sera ya Gesi Asilia ya 2013 [Natural Gas Policy].
Sababu za kuuza data
Data za utafutaji mafuta na gesi huuzwa kwa sababu gharama za
kukusanya data ni kubwa sana, hivyo mauzo hufidia gharama za
ukusanyaji data hizo za awali na kufanya miradi ya ukusanyaji data kuwa
endelevu.
Kwa upande wa baharini inabidi kukodi meli maalumu zenye mitambo ya
kukusanyia data. Meli hizi zinabeba mitambo na kompyuta maalumu
zinazotumia teknolojia ya hali ya juu kurekodi tabia za miamba za kuakisi
mawimbi ya sauti chini ya ardhi (reflection seismic methods). Meli hizi
huweza kukaa baharini kwa hadi miezi mitatu au zaidi zikifanya shughuli za
ukusanyaji data na zinahudumiwa kimahitaji kwa kutumia helikopta na meli
6
ndogo za kutoa huduma. Ulinzi pia kujikinga na maharamia huhitajika.
TPDC na wabia wake hugharamia zoezi la ukusanyaji data. Ni wazi kwamba
gharama hizi huwa ni kubwa sana, hivyo inabidi data zinazopatikana
ziuzwe ili mwekezaji na TPDC waweze kurejesha gharama zao.
Kwa upande wa nchi kavu napo pia gharama ni kubwa. Gharama huanza
kwa kutengeneza mikuza, kulipa fidia, kulipa makandarasi wa kipima
mikuza, kusafisha mikuza na kurekodi tabia za miamba za kuakisi mawimbi
data za mitetemo.
Tunahitaji makampuni yatumie data hizi kutathmini sehemu ambazo
zinaweza kuwa na hifadhi za mafuta na gesi asilia. Tathmini hizo zitatumika
kusaidia wataalamu kupima uwezo wa makampuni na kuchagua kampuni
stahili kupewa vitalu.
Utazamaji wa Takwimu/ Taarifa - Data Viewing
Utazamaji wa taarifa za kijiofizikia na kijiolojia (data viewing) unaweza
kufanywa kwenye ofisi za Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC).
Mtazamaji anapaswa kuweka miadi ‘appointment' ya kutembelea chumba
chenye hizo taarifa kupitia:
Shirika la Mendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)
Tower A, Benjamin William Mkapa, Pension Towers Building,
Plot 23/90-23/92 Azikiwe/Jamhuri Streets,
Dar Es Salaam,
Tanzania.
7
Mkurugenzi Mkuu, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania
Simu ya mezani : +25522 2200103/4
Barua pepe :tpdc4thround@tpdc-tz.com
Tovuti :
Tanzania Petroleum Development Corporation
Mtazamaji atapata nafasi ya kuona taarifa zilizomo kwenye kifurushi cha
zabuni cha vitalu vya bahari kuu (BRDP), kifurushi cha zabuni cha ziwa
Tanganyika, ‘data' za lazima za mitetemo zenye jumla ya kilometa 4500 za
urefu, na taarifa nyinginezo za mitetemo kama zitahitajika na pamoja na
seti ya ‘data' za zamani zilizoboreshwa.
SEHEMU A: USHIRIKI WA WAZAWA
Maelezo kuhusu fursa sawa katika kushiriki kwenye mnada wa vitalu vya
utafiti wa mafuta na gesi ni kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma
ya mwaka 2004 (Public Procurement Act, 2002).
Ingawa Zabuni iko wazi kwa makampuni ya ndani na ya nje kushiriki,
Utaratibu umewekwa utakaotoa upendeleo kwa makampuni ya ndani
yaliyosajiliwa kwa sheria za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na
kumilikiwa na wazawa kwa asilimia zisizopungua 50 ikiwa yatatimiza vigezo
vilivyowekwa kuviwezesha kupata huo upendeleo. Vilevile ushirikiano wa
ubia kwa makampuni yanayomilikiwa na wazawa na yale ya nje utapewa
upendeleo ikiwa utatimiza vigezo vilivyowekwa ambavyo vinataka pamoja
8
na mambo mengine; kuthibitisha kuwa atafanya kazi zenye thamani
isiyopungua asilimia 10 ya gharama ya kazi na kuwa atapata mgawo
usiopungua asilimia 20 ya faida itakayopatikana.
Mambo ya kufanya ili kushiriki kwenye Zabuni
Kampuni inayotaka kununua data na kushiriki kwenye zabuni inaweza
kuwasiliana na:
Mkurugenzi Mtendaji,
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania,
Tower A, Benjamin William Mkapa Pension Towers Building, Plot 23/90-
23/92 Azikiwe/Jamhuri Streets,
S.L.P. 2774,
Tel: +25522 2200103/4
Dar Es Salaam, TANZANIA
Barua pepe:
tpdc4thround@tpdc-tz.com
Wazabuni watarajiwa wanaweza kutuma maswali ya ufafanuzi kuhusiana
na zoezi la zabuni.
Muombaji anapaswa kurejesha kwa mkono nakala 2 pamoja na nakala
halisi vikiwa vimefungwa na kuviweka katika sanduku la zabuni lililopo
katika ofisi kuu za Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, (Tower "A")
chumba numbari 401 kilichopo gorofa ya nne, jengo la Benjamin William
Mkapa Pension Towers, Kitalu nambari 23/90-23/92, Azikiwe/Jamhuri
9
Streets, Dar es Salaam, au itumwe kwa huduma ya kutuma vifurushi
vilivyoandikishwa (registered post/mail) kwenda kwa:
Katibu wa Bodi ya Zabuni ya Shirika la Maendeleo ya Petroli
Tanzania S.L.P. 2774, Dar-es-Salaam.
Mshiriki katika zabuni pia anaweza kushiriki katika zabuni kwa kuwasilisha
zabuni yake siku ya ufunguzi kabla ya saa nne asubuhi kwa masaa ya
Tanzania siku ya Alhamisi tarehe 15 mwezi Mei mwaka 2014 kama
ilivyoelekezwa kwenye muongozo wa zabuni uliokwishatolewa na unaweza
kuuona kwenye tovuti maalumu iliyoandaliwa kwa ajili ya zabuni ya
ugawaji wa vitalu:
The 4th Tanzania Offshore Licensing Round
Tathimini za Zabuni za vitalu zilizopokelewa
Zabuni za vitalu ni zabuni za kimataifa na za wazi kwa makampuni yenye
nia ya kufanya shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia. Zabuni hizo
hazibagui asili ya makampuni, kampuni yaweza kuwa ya kitaifa au ya
kimataifa. Utoaji wa zabuni huzingatia mambo makuu matatu;
 uwezo wa kampuni kifedha;
 uwezo wa kampuni kitaalamu; na
 mgawo wa rasilimali kwa Taifa endapo gesi na mafuta vitagunduliwa.
10
Zabuni zitakazopokelewa zitafanyiwa tathimini kufuatana na vigezo
vilivyowekwa kulingana na kazi za kitaalamu ambazo muomba zabuni
atakuwa ameahidi kuzitekeleza kwa vipindi vyenye jumla ya miaka 11
(4/4/3) ya utafiti kama vilivyo kwenye sheria inayosimamia shughuli za
utafiti na uzalishaji wa mafuta na gesi Tanzania. Mkurugenzi Mtendaji wa
Shirika ataunda Kamati ya kufanya tathimini kwa mujibu wa sheria
inayosimamia manunuzi ya umma.
Mapendekezo ya Kamati ya tathimini hupitiwa na Bodi ya Manunuzi ya
Shirika ambapo mapendekezo ya Bodi ya Manunuzi huwasilishwa kwa
Mkurugenzi Mtendaji ambaye naye huyawasilisha kwenye Bodi ya
Wakurugenzi wa Shirika ili kuandaa mapendekezo yatakayopelekwa kwa
Waziri kwani ndiye mwenye dhamana ya kutoa leseni za utafiti. Kama
Waziri atakubaliana na mapendekezo aliyoletewa ataiagiza kampuni
iliyoshinda itaarifiwe na kujiandaa kwa mazungumzo na timu ya washauri
wa serikali kuanza kwa nia ya kusaini mkataba wa kugawana mapato.
Mkataba huu pindi unaposainiwa pamoja na majukumu hutoa haki za
kipekee kwa kampuni iliyoshinda zabuni kufanya shughuli za kutafuta
mafuta na gesi asilia kwa kipindi kilichowekwa katika eneo husika.
Kampuni iliyoshinda hupewa kuendesha leseni ya utafutaji na Waziri wa
Nishati na Madini kwa niaba ya TPDC kama mkandarasi. Kampuni hiyo
itapaswa kufanya kiasi cha kazi za kitaalamu za kitafiti zitakazo husisha
shughuli za kijiofizikia, kijiolojia na kijiochemia kama ilivyo kwenye
mkataba.
11
Kazi hizo huhusisha uchukuajia wa data za mitetemo za 2D na 3D,
uchimbaji wa visima vya utafiti, uchimbaji wa visima vya kuthibitisha kiasi
ya hazina ya gesi au mafuta iliyopatikana na pia uchimbaji wa visima vya
uendelezaji wa maeneo hazina ilipogunduliwa.
Makadirio ya gharama za mfano kwa kiwango cha chini kufanikisha
shughuli za utafiti mpaka uendelezaji zinaweza kuwa kama zilivyoainishwa
hapa chini:
12
Dola za
Marekani
Tathimini za kijiofizikia na kijiolojia 10 milioni
Ukusanyaji wa takwimu za 2D na 3D 5 - 25 milioni
Jumla kwa Tathmini zote za kimazingira (EIAs) 12 milioni
Uchimbaji wa visima 3 vya utafiti (@ 170 mill) 510 milioni
Uchimbaji wa visima 6 vya tathmini (@ 150 mill) 900 milioni
Uchimbaji wa visima 10 vya uendelezaji (@ 100 mill) 1000 milioni
Jumla ya gharama isiyohusisha miundombinu Dola za Marekani
milioni 2437 (2.4 Bn)
Makadirio haya hayahusishi gharama za kuweka miundombinu ya
kuwezesha uzalishaji, usafishaji, uchakataji, uuzaji na gharama zinginezo.
Gharama hizi zinaonesha makadirio ya gharama za awali za shughuli za
utafutaji wa mafuta na gesi asilia. Gharama za uendelezaji kuweka
miundombinu hadi kufikisha gesi kwa mtumiaji huweza kufikia hadi Dola za
Marekani bilioni 15 (US$ 15Bn).
Baada ya kusainiwa kwa mkataba, mshindi wa zabuni atatakiwa kutekeleza
mambo aliyoahidi wakati wa vipindi vya utafiti.
13
Akichimba kisima na kugundua mafuta au gesi, atapaswa kufanya utafiti
zaidi ili kujiridhisha kuwa kiasi kilichogunduliwa kinaweza kuzalishwa kwa
faida. Katika utafiti huo, mwenye leseni analazimika kuchimba visima zaidi
pamoja na kufanya thathmini za kijiofizikia na kijiolojia zaidi.
Akijiridhisha, kuwa hazina iliyogunduliwa inaweza kuzalishwa kwa faida,
anapaswa kuomba leseni ya uzalishaji ambao hutakiwa kuambatanisha
maombi yake na mpango kabambe wa kuendeleza hazina iliyopo (mafuta
au gesi). Waziri akiridhika na mpango uliowasilishwa na kampuni, huipa
hiyo kampuni leseni ya uendelezaji inayompa haki mwenye leseni
kuendeleza na kuizalisha hazina aliyoipata kwa kipindi cha miaka 25 na
inaweza kuongezwa kwa kipindi kingine cha miaka 20.
Mauzo ya kinachozalishwa hutumika kurudishia gharama zilizowekezwa
kwenye shughuli zote za mradi na faida hugawanywa kwa namna
iliyokubalika katika mkataba wa kugawana mapato.
Taarifa hii inatolewa ili kuelimisha umma kuhusiana na zabuni za ugawaji
wa vitalu iliyozinduliwa tarehe 25/10/2013 na haipaswi kuchukuliwa kama
maelekezo kwa wanaotaka kushiriki kwenye zabuni (Invitation to Bid).
Maelekezo ya namna ya kushiriki kwenye zabuni yanapatikana kwenye
mtandao ufuatao:
(
http://www.tz-licensinground.
com/pdf/Invitation%20for%20Bids%2031%20Oct%202013.pdf).
14
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linayaalika makampuni ya
wazawa yenye uwezo wa kifedha na kitaalamu kushiriki katika zabuni
iliyotangazwa ya kutafuta wawekezaji wa vitalu vya utafiti sambamba na
makampuni ya nje.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na:
Idara ya Utafutaji, Uzalishaji na Huduma za Kiufundi,
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania
Tower A, 9th Floor; BWM Pension Tower
Azikiwe/Jamhuri Street
P.O. Box 2774
Dar es Salaam, Tanzania
simu: +255 22 2200103/4, 2200112
fax: +255 22 2200113
Barua pepe:
tpdc4thround@tpdc-tz.com