Prof. Mark Mwandosya Amlipua Apson Mwang'onda Bungeni

Prof. Mark Mwandosya Amlipua Apson Mwang'onda Bungeni

Ccm na siasa zake za majitaka, sisi yetu macho, tunasubiri muanze kutuonga fedha mlizoipora nchi.
 
Riz one kuwa mwanasheria wa kawaida tu ametoa wapi utajiri kiasi hicho? kabla hujauliza swali jiangalie kwanza na angalia wanaokuzunguka ndio uje na swali tena.
Mkuu mie mwana CCM mchapa lapa, sina uhusiano wowote na hao wakubwa.
Lakini ukweli uko pale pale, mali ya wizi kutokana na fedha ya umma huwajengea watu kiburi kisicho na kawaida.
 
quote_icon.png
By CHAZA

Mi nadhani iwe fundisho kwa viongoz wandamiz wa vyombo.vya Ulinzi.na Usalam kujiepusha na mambo ya siasa. Sasa unaona, ex Inteligency jina linatajwa tajwa tu kiholela, inabidi wahusika walijue hilo. Matokeo yake jina linakuwa tarnished kwa mambo ambayo hayana maana kabisa.

Ushauri wako umejaa busara ya hali ya juu sana. Kama wahusika watasikia na kuuzingatia, itakuwa jambo jema sana


Mkuu Lizaboni. Heshima yako na nikupongeze kwa kuongea point leo maana toka nakujua kupitia mabango yako hapa jf sijawahi kusikia au kuona umeandika point. Hongera unabadilika now days.
 
Hao jamaa wa TISS huwa wanastaafu wakiwa na umri gani?ninavyojua kazi zao hufanya kwa siri kwa maana kuwa huwa kazi yao rasmi haijulikani (ukiacha wale wa ngazi za juu), maana yake ni kuwa hata wakiwa bado kazini wanaweza wakaingia kwenye siasa. Je, kuna tofauti gani anapoingia kwenye siasa akiwa kazini na akiwa amestaafu?
 
Mwandosiya anaweweseka tu...Apson ni msitaafu anahaki ya kufanya siasa kama mtu mwingine yeyote!
 
Ujumbe wa Mwandosya ungekuwa muafaka kwenye nchi inayoendeshwa kwa kanuni, maadili na miiko. Hizo tunu zilishatupiliwa mbali siku nyingi na kubakiza utashi wa rais aliye madarakani na maswahiba zake kuongoza nchi. Halafu, nafasi za kisiasa ndio zimefanywa kila kitu. Nje ya hapo, you're nothing! Akina Apson wana nini cha kuwaongoza hivi leo? Mwandosya atoe mawaidha mapana zaidi ya kurejesha tunu za Taifa kabla ya kutaka kuasa watu na vikundi binafsi. Yeye mwenyewe ni mhanga wa mengi tu katika serikali na chama chake. Au anajikomba kwa watu fulani - tena ambao wameshamhujumu hata afya yake? Ayaseme yote; hasa yale ya msingi ili yasaidie taifa sio mtazamo finyu anaotuletea hapa.
 
Wadau, akitoa mchango wake wakati wa mjadala wa sura za Rasimu ya Katiba, Waziri Prof Mark Mwandosya amewataka wakuu wa vyombo vya dola kujiepusha na siasa pindi wanapostahafu kwenye utumishi. Anasema kuwa wakuu hao wa vyombo vya dola hususan Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mkuu wa Majeshi na Mkuu wa Polisi wakiwa wakiwa kwenye nyadhifa zao wanamiliki mafaili, Dossier za wanasiasa wote. Hali hiyo inawaweka kwenye position ya kuwajua in and out wanasiasa wote hususan wale wanaotarajia kugombea nafasi za juu hasa ya Urais.

Mwandosya anasema kuwa kitendo cha Wakuu hao baada ya kustahafu kujihusisha na siasa kwa kuamua kugombea nafasi za kisiasa au kuwaunga mkono baadhi ya wanasiasa wanaogombea nafasi za kisiasa kunawaweka kwenye nafasi ya kukiuka maadili ya kazi zao. Anasema kuwa ijapokuwa wanapostahafu wanaacha mafaili ofisini, wanaondoka na kumbukumbu moyoni.


Mwandosya asiweweseke leo, wakati vyama vya upinzani, hususani CDM walipolalamika kuwa idara hiyo ya usalama inatumiwa na CCM kuihujumu CDM, wanaCCM walikuwa wanacheka. Sasa imekuwa mkuki kwa nguruwe. Walikuwa wakiwatumia TISS kuwahujumu CDM, sasa yale mabomu waliyoyatumia kulipua wengine yanawalipukia wao wenyewe na kuwadhuru. Viongozi wa juu wa CCM kama Mwandosya hawapaswi kuyasema hayo leo hii kwa sababu madhara ya hayo wanayoyalalamikia yalipokuwa yanasikika kwa CDM waliona kuwa CDM wameishiwa. WanaCCM mnavuna mlichopanda
 
Mimi nilisema tangu mwanzo kuwa Apson amekosea sana kujiingiza kwenye siasa ametia aibu heshima yote aliyokuwa nayo itapotea ngoja kampeni zianze mtaniambia wenyewe,mwandosya kafanya vema.

Chabruma amepost thread yake saa sita kamili, wewe ndani ya dakika tatu umefungua, kuisoma yote, kuandika na kupost ndani ya dakika tatu...what a clever 'lady'!!!

Hata ninyi mpo kwenye kambi nyingine, hakuna tofauti kubwa sana na akina Lowassa. Hata matumizi ya pesa hayako tofauti sana!

Acheni kuichanganya 'system'
 
Kwa akili hii ya Mwandosya, sishangazwi na ccm walipomuuwa Kombe kwasababu ya kushirkiana na Mrema.

Wakati huo Mrema akigombea urais kupitia NCCR Mgeuzi mwaka 1995. Mrema alikuwa akilipuwa mabomu ya kashfa na siri za ufisadi. Hii ilikuwa baada ya Kombe kustaafu ukuu wa usalama wa Taifa kama ilivyo kwa Mwang'onda!

Wakaona kuwa siri hizo Mrema anazitoa kwa Kombe!

Huyu Mwang'onda hawamwezi kwasababu anamsapoti gamba mwenzao mwenye nguvu kubwa waliyeshindwa kumvua gamba!

Je Mwandosya alisapoti kitendo kile dhidi ya Abdulrahman Kombe?

Msimamo wake huu dhidi ya Mwang'onda, hauna tofauti na msimamo wao dhidi ya Kombe!
 
Mwandosya asiweweseke leo, wakati vyama vya upinzani, hususani CDM walipolalamika kuwa idara hiyo ya usalama inatumiwa na CCM kuihujumu CDM, wanaCCM walikuwa wanacheka. Sasa imekuwa mkuki kwa nguruwe. Walikuwa wakiwatumia TISS kuwahujumu CDM, sasa yale mabomu waliyoyatumia kulipua wengine yanawalipukia wao wenyewe na kuwadhuru. Viongozi wa juu wa CCM kama Mwandosya hawapaswi kuyasema hayo leo hii kwa sababu madhara ya hayo wanayoyalalamikia yalipokuwa yanasikika kwa CDM waliona kuwa CDM wameishiwa. WanaCCM mnavuna mlichopanda

Mkuu, kwanza siamini kuwa TISS inakihujumu chadema. Hayo ni mawazo finyu kabisa. Naamini kuwa kama TISS inahusika na hujuma dhidi ya chama cha upinzani ni wazi kuwa Dr Slaa na Mbowe wasingekuwa hai mana kila kukicha wanaitukana Idara na viongozi wake
 
Kwa akiki hii, sishangazwi na ccm walipomuuwa Kombe kwa kushirkiana na Mrema baada ya kustaafu ukuu wa usalama wa Taifa!

Huyu hawewezi kwasababu anamsapoti gamba mwenzao mwenye nguvu kubwa waliyeshindwa kumvua gamba!

aliyemuua Kombe ni huyu Apson. Alihofia haya anayofanya yeye. Kwa hiyo kama Kombe aliuawa kutokana na kumsupport Mrema, huyu Apson mbona anafanya yaleyale ya Kombe?
 
Hakumtaja jina lakini naona umbea wake ulilenga huko. Ila ni lazima tukubaliane kwamba kama umestaafu kusiwe na mizengwr ya kuwafumba watu mdom. Apson ana kaki na maamuzi binafsi kama raia yeyote wa nchi hii. Kuchagua, kuchaguliwa na kuamua new haki yake ya kikatiba. Mwandosya ambae hana anachofanya serikalini zaidi ya kulipwa bure mbona watu hatumsemi??
 
aliyemuua Kombe ni huyu Apson. Alihofia haya anayofanya yeye. Kwa hiyo kama Kombe aliuawa kutokana na kumsupport Mrema, huyu Apson mbona anafanya yaleyale ya Kombe?
Kwamba alishiriki hilo la Kombe, sina details zozote hapo. Nafahamu tu mafisadi wa ccm walishiriki.

Hapo kwenye kufanya alichofanya Kombe, tofauti yake ni kwamba Mwang'onda yeye anamsapoti kigogo wa ccm na si upinzani kama Ilivyokuwa kwa Kombe.

Je kama Mwang'onda angekuwepo kwenye kambi yake Mwandosya, angelalamika?

Je ana nini cha kuhofia kwenye mafaili yake yaliyoko usalama wa Taifa?!

Pia nakutaarifu, twende mdogomdogo maana maswali yangu huwa magumu sana tu!
 
CCM ni chama changu lazima nikiri, lakini kwa kuchezeana faulu hakuna wa kumnyoshea mwenzake kidole wote wanacheza rafu tena mbaya. ukiona mwandosya analalama ujue kazidiwa na nguvu ya upande wa pili. kuhusu wastaafu wa vyombo vya dola kutojihusisha na siasa CCM ndio tulibariki ilo suala, mpaka baadhi yao wakawa mawaziri. anachotakiwa kufanya mwanosya ni kupeleka hoja yake ndani ya nec ili ijadiliwe huko ambako najua pia hatafaulu kwani chanzo cha haya yote ni sisi ccm wenyewe, huwa tunawaahidi hawa kuwa wakistaafu tutawapa nafasi
 
Hivi mbona hakumlalamikia general Shimbo?

Double srandard nyingine bana!
 
Back
Top Bottom