Adrian Stepp
JF-Expert Member
- Jul 1, 2011
- 2,764
- 2,581
Nimeona niseme neno kuhusu tamko la Lawrence Masha kujitoa CHADEMA, mimi raia ambaye sina chama.
Kwanza, ni muhimu tukumbushane kuwa kwa mujibu wa tangazo la kimataifa la haki za binadamu, ni haki ya kila binadamu kujiunga na wenzake katika kufuatilia au kufanikisha malengo halali, kama vile ya kisiasa. Ni haki ya kila mtu kujiunga na chama cha siasa.
Kujitoa katika chama na kujiunga na kingine ni haki ya kila mtu.
Kwa hivyo, kuwadhalilisha watu wanaojitoa kwenye chama fulani na kuingia kingine ni kuwakosea haki.
Hivi karibuni, kwa mfano, baada ya Lazaro Nyalandu kuhama CCM, tumemsikia Rais Magufuli akitamka kuwa watu hao wanaohama CCM ni mafisadi na majizi.
Kauli hiyo ya Rais inakiuka haki za binadamu, mojawapo ikiwa hiyo niliyotaja hapa juu.
Nyingine ni haki ya kila binadamu ya kutambuliwa kwa utu wake na kuheshimiwa, pasipo kudhalilishwa.
Hakuna mtu anayestahili kuitwa fisadi au jizi bila mahakama kuthibitisha ana hatia.
Hao ambao Rais Magufuli anawaita mafisadi na majizi hawajathibitishwa hivyo na mahakama yoyote.
Rais anakosea kwa hilo, na sherti akosolewe. Azingatie haki za binadamu.
Kwa mujibu wa tangazo la kimataifa la haki za binadamu, na kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, mtu akituhumiwa kwa kosa lolote, ana haki ya kuhesabiwa kuwa hana hatia hadi mahakama ithibitishe kuwa ana hatia.
Mahakama ziko kwa ajili ya kulinda haki, pamoja na haki za watuhumiwa.
Zaidi ya hilo suala la haki za binadamu, barua hii ya Masha ina ujumbe muhimu kwa CCM na CHADEMA.
Inaikumbusha CCM kwamba wapinzani wana wajibu na haki ya kuikosoa serikali inapobidi. Hilo ni fundisho kwa serikali ya awamu ya tano, ambayo inakuwa mbogo dhidi ya wakosoaji.
Tena ni ajabu kuwa serikali inayosemwa kwamba ina wasomi wengi iwe haivumilii kukosolewa. Msomi wa kweli ni mtu anayetambua na kuthamini hoja, zikiwemo hoja kinzani. Anathamini kuhoji, kujihoji, kuhojiana, na malumbano ya hoja. Anathamini kukosoa, kukosolewa, na kukosoana. Wasomi wa serikali ya awamu ya tano ni wasomi wa dizaini ya pekee.
Ni vigumu kuamini kama walizingatia masomo au walipitapitaje vyuoni.
Kwa upande wa CHADEMA, barua ya Masha ina fundisho pia.
Amewakosoa vizuri kwamba wanapaswa waende mbali zaidi ya kutegemea tu madhaifu ya CCM. Wajikite katika kutunga na kufafanua sera.
Binafsi, nimevutiwa na hoja hiyo. Kazi kwao.
Nini maoni yako?
Kwa ufupi:
Prof.Joseph Mbele alifundisha Literature Chuo kikuu cha DSM kuanzia Mwaka 1976 kisha Kuhamia Chuo cha Mt.Olaf Marekani kuanzia 1990 mpaka hivi sasa ambapo ni Mhadhiri Mwandamizi wa Literature!
Ni intake ya Marehemu Mbunda Msokile aliyekua mwalimu wa Kiswahili UDSM!
Kwanza, ni muhimu tukumbushane kuwa kwa mujibu wa tangazo la kimataifa la haki za binadamu, ni haki ya kila binadamu kujiunga na wenzake katika kufuatilia au kufanikisha malengo halali, kama vile ya kisiasa. Ni haki ya kila mtu kujiunga na chama cha siasa.
Kujitoa katika chama na kujiunga na kingine ni haki ya kila mtu.
Kwa hivyo, kuwadhalilisha watu wanaojitoa kwenye chama fulani na kuingia kingine ni kuwakosea haki.
Hivi karibuni, kwa mfano, baada ya Lazaro Nyalandu kuhama CCM, tumemsikia Rais Magufuli akitamka kuwa watu hao wanaohama CCM ni mafisadi na majizi.
Kauli hiyo ya Rais inakiuka haki za binadamu, mojawapo ikiwa hiyo niliyotaja hapa juu.
Nyingine ni haki ya kila binadamu ya kutambuliwa kwa utu wake na kuheshimiwa, pasipo kudhalilishwa.
Hakuna mtu anayestahili kuitwa fisadi au jizi bila mahakama kuthibitisha ana hatia.
Hao ambao Rais Magufuli anawaita mafisadi na majizi hawajathibitishwa hivyo na mahakama yoyote.
Rais anakosea kwa hilo, na sherti akosolewe. Azingatie haki za binadamu.
Kwa mujibu wa tangazo la kimataifa la haki za binadamu, na kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, mtu akituhumiwa kwa kosa lolote, ana haki ya kuhesabiwa kuwa hana hatia hadi mahakama ithibitishe kuwa ana hatia.
Mahakama ziko kwa ajili ya kulinda haki, pamoja na haki za watuhumiwa.
Zaidi ya hilo suala la haki za binadamu, barua hii ya Masha ina ujumbe muhimu kwa CCM na CHADEMA.
Inaikumbusha CCM kwamba wapinzani wana wajibu na haki ya kuikosoa serikali inapobidi. Hilo ni fundisho kwa serikali ya awamu ya tano, ambayo inakuwa mbogo dhidi ya wakosoaji.
Tena ni ajabu kuwa serikali inayosemwa kwamba ina wasomi wengi iwe haivumilii kukosolewa. Msomi wa kweli ni mtu anayetambua na kuthamini hoja, zikiwemo hoja kinzani. Anathamini kuhoji, kujihoji, kuhojiana, na malumbano ya hoja. Anathamini kukosoa, kukosolewa, na kukosoana. Wasomi wa serikali ya awamu ya tano ni wasomi wa dizaini ya pekee.
Ni vigumu kuamini kama walizingatia masomo au walipitapitaje vyuoni.
Kwa upande wa CHADEMA, barua ya Masha ina fundisho pia.
Amewakosoa vizuri kwamba wanapaswa waende mbali zaidi ya kutegemea tu madhaifu ya CCM. Wajikite katika kutunga na kufafanua sera.
Binafsi, nimevutiwa na hoja hiyo. Kazi kwao.
Nini maoni yako?
Kwa ufupi:
Prof.Joseph Mbele alifundisha Literature Chuo kikuu cha DSM kuanzia Mwaka 1976 kisha Kuhamia Chuo cha Mt.Olaf Marekani kuanzia 1990 mpaka hivi sasa ambapo ni Mhadhiri Mwandamizi wa Literature!
Ni intake ya Marehemu Mbunda Msokile aliyekua mwalimu wa Kiswahili UDSM!