Prof. Baregu: Zitto ni mzigo

Prof. Baregu: Zitto ni mzigo

Waswahili husema kuwa majina huumba. Sasa hili jina 'Zito', linabeba maana ambayo waliomwona akiwa mdogo walihisi ndivyo atakavyokuwa.
 
Huyu mzee naye Onchocerca volvulus wamempanda kwenye ubongo,unafiki mbaya sana.

Mbona huwa hawatoi maoni juu ya viongozi waandamizi wa chama hata inapothibitika wamefanya madudu?

Au Baregu anaamini watu wazima hawajambi?

Mbowe alipojipachikia majina yake ya wabunge wa viti maalum,mbona hatukumsikia akisema chochote?

Hata kama mimi ndo ningekuwa Zitto ushauri wa wazee wa aina hii siuchukui hata kwa bakora.

Mungekuwa mnawakemea na hao jamaa tungejua kweli mnamaanisha.

BAREGU ACHA UTOTO you're too old for this bora ukae kimya.

Hawa ndo wazee alowasema jamaa kwamba wanasubiria kurudisha namba kwa muumba.

Jinga wewe,hujui kuwa aliyepewa kazi ya kudivice formular ya kuteuwa wabunge wa viti maalum ni Prof Kitila Mkumbo?
 
Wewe ni mzima? Unajua jinsi wabunge wa kuteuliwa kupitia CHADEMA walivyopatikana? Vigezo na maamuzi ya nani awe mbunge wa kuteuliwa viliandaliwa na Dr. Kitila, na mapendekezo yalipelekwa na Kitila Mkumbo kwa niaba ya kamati.

Huyu binadamu ni wa kuhurumiwa tu,wakati mwingine post zao zinatusaidia kujua uwezo wao wa kufikiri hivyo tunapata kibali cha kuwapuuza!
 
WAACHE NDEGE WAPITE JUU YA KICHWA CHAKO WAONDOKE ZAO USIKUBALI WAJENGE KIOTA JUU YA KICHWA CHAKO MAANA WALIMWENGU NA MUNGU WATAKULAUMU SANA NA KUKUÖNA MBAYA KAMA NDUMILA KUWILI.
WEWE UKITUHUMIWA KUTENDA USALITI AU UOVU WAKATI UNATAKA KUUTENDA AU UMEUTENDA ACHA NA UJUE HILO NI ONYO LAKIN UKAJA UKATENDA YALE UNAYOTUHUMIWA NA YAKBAINIKA HATA KWA FIKRA NA MACHO HAKIKA HUTAWAPONA WALIMWENGU NA MUNGU KWANI WATASEMA MMEÖANA TULIYOSEMA NA NA KUMTUHUM? BAADA YA HAPO KAMA HUKUOMBA MSAMAHA KWA KUAMINI UNAAKILI NYINGI LAANA ITAKUTAFUNA NA UIMARA WAKO UTAKWISHA NA KUITWA DHAIFU,LIMBUKENI,MLAFI wA MADARAKA,MSALITI,NDUMILAKUWILI . Asante



Ndio nini hii? Mbona kila mtu ktk hili suala la zitto anatoa Unabii wake? Why everyOne is trying to tell/show how Zitto was supposed to behave?

Let him be, him. Becouse that's how he is...
 
Huyu mzee naye Onchocerca volvulus wamempanda kwenye ubongo,unafiki mbaya sana.

Mbona huwa hawatoi maoni juu ya viongozi waandamizi wa chama hata inapothibitika wamefanya madudu?

Au Baregu anaamini watu wazima hawajambi?

Mbowe alipojipachikia majina yake ya wabunge wa viti maalum,mbona hatukumsikia akisema chochote?

Hata kama mimi ndo ningekuwa Zitto ushauri wa wazee wa aina hii siuchukui hata kwa bakora.

Mungekuwa mnawakemea na hao jamaa tungejua kweli mnamaanisha.

BAREGU ACHA UTOTO you're too old for this bora ukae kimya.

Hawa ndo wazee alowasema jamaa kwamba wanasubiria kurudisha namba kwa muumba.

Kiongozi acha kumshambulia Baregu. Kwan una uhakika gani kama kayaongea yeye au maneno ya uchonganishi? Kazi ya vijana wa ufipa ya uzushi umeisahau?

Chanzo cha habari hamna. Na video kaweka ya zito kujiuzulu. Hayo maneno Baregu kayaongelea wapi?
 
CHAMA cha Alliance for Change and Transparance (ACT-Tanzania) kimefanikiwa kuishawishi kwa hoja mahakama kuu ya Tanzania na kushinda katika maombi ya zuio la muda yaliyoombwa na wanachama wake Kadawi Limbu na wenzake ya kutaka mahakama Kuu itoe amri ya zuio la muda kwamba Samson Mwigamba, Peter Mwambuja na Mohamed Masaga wasijihusishe na shughuli yoyote ya Chama mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa

Kutokana na kutupwa kwa zuio hilo la muda kesi ya msingi namba 21/2015 imepangwa kusikilizwa April 15 mwaka huu, huku Limbu na wenzake wakitakiwa kulipa theluthi moja ya gharama za kesi hiyo

Kabla ya Limbu na wenzake kuomba zuio la muda la kutaka Mwigamba na wenzake wasijishughulishe na kazi za Chama kwa nafasi ya Katibu Mkuu,Naibu katibu Mkuu na mhasibu,walifungua kesi ya msingi iliyokuwa na maombi manne

1 Mahakama kuu ya Tanzania Itamke kuwa Chama cha ACT-Tanzania haina kamati kuu na Halmashauri kuu

2 Mahakama kuu ya Tanzania itamke kuwa kikao halali cha viongozi wa ACT-Tanzania ni kile cha kamati kuu iliyokutana Disemba 31 mwaka jana

3 Mahakama kuu itamke kuwa washitakiwa watatu Mwigamba,Masaga na Mwambuja siyo wanachama halali wa ACT-Tanzania

4 Mahakama kuu iwatake washitakiwa kulipa gharama zote za kesi

Kwa upande wake wake Mwigamba na wenzake waliweka pingamizi la kusikilizwa kwa maombi ya zuio la muda ya Limbu na wenzake kwa hoja zifuatazo

1 Walalamikaji Limbu na wenzke hawakuonyesha ni kanuni gani ya kisheria waliyotumia kuiomba mahakama itoe zuio la awali

2 Kwenye hati ya mlalamikaji katika kesi ya msingi mlalamikaji namba moja ni Kadawi Lucas Limbu,lakini Kwenye hati ya kiapo ya maomb ya zuio la muda mla kiapo namba moja amejitambulisha kuwa ni ACT-Tz

3 Maombi hayo yangeweza kuombwa katika mahakama ya chini badala ya mahakama kuu

Kufuatia hoja hizo tatu za mawakili wanaowawakilisha kina Mwigamba, wakili wa Limbu na wenzake alikiri upungufu katika hati yao ya maombi hivyo mahakama kuu chini ya Jaji J.Mwandambo ikatupilia mbali maombi ya zuio la muda na kumtaka Mlalamikaji Kulipa gharama za kesi.
who cares?
 
Ama kweli nyani haoni kundule. Wewe Baregu ndo mzigo. Professor mzima utakubalije kutumiwa vibaya na kijana mcheza disco? Siyo tu mcheza disco bali pia kijana mwenye eimu ya kidato cha sita mwenye ufaulu wa sifuri? We ndo mzigo siyo zitto

Usikimbilie kumkashifu Prof. Kwan hii habari ipo kimajungu, haina chanzo. Na mleta mada kajua kuwa wengi hapa ni mb8 hivyo hamtajiangaisha kuifungua. Kifupi kilichopo ni hotuba ya Zitto. Kifupi huyo kenge kawashika vizuri na propaganda zake.

Sasa hivi wanafanya chini juu kuhakikisha wanamfitinisha Zito kwa kila mtu japo yeye hana muda nao.

Hiyo habari haina chanzo bshaka ni majungu kama majungu mengne ya siku zote waenezayo chadema dhidi ya wapinzani wao.
 
PROFESA Mwesiga Baregu, mmoja wa watu wanaoheshimika nchini amesema, aliyepata kuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, anaponzwa na kibuli cha kujiona hakuna zaidi ya yeye.

Amesema, Zitto ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tanzania Bara na naibu kiongozi wa upinzani bungeni, anafanya kazi asiyoifahamu na ambayo haina mavuno.

“Ninamfahamu vizuri. Wakati tuhuma hizi za usaliti zilipoanza kuibuka, Kamati Kuu ilinikabidhi jukumu la kumsaidia mama yake mzazi kumlea kijana huyu.”

Kauli ya Baregu ilitolewa siku moja baada ya Zitto kujiondoa bungeni na baadaye kujiunga na Chama cha ACT – Tanzania.

Prof. Baregu aliwahi kuwa “mlezi wa Zitto” ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Alikabidhiwa jukumu hilo na Shida Salum, mama mzazi wa Zitto (marehemu), baada ya mama huyo kuiomba Kamati Kuu (CC) ya chama hicho “kusaidia kumlea.”

Prof. Baregu ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema anasema, “Zitto hamnazo. Amekuwa anajiona yeye ni zaidi ya chama. Hashauriki.”

Anasema wakati ule alipopewa kazi ya kumlea Zitto “katikakati ya migogoro, tulikuwa tunazungumza naye mara kwa mara. Ninamfahamu. Kazi hii ya kumlea tulikabidhiwa mimi na mama yake mzazi, Bi. Shida Salum,” anaeleza Baregu.

Mama mzazi wa Zitto, alifariki dunia Juni mwaka jana, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kauli ya Prof. Baregu ilifuatia gazeti hili kutaka maoni yake juu ya mustakabali wa kisiasa wa Zitto baada ya kuwahi kujiondoa ndani ya Chadema.



Huyu mzee atakuwa Profesa wa mizizi na sio kufikiria, ukiwa Counselor wa mtu hutakiwi kutoa siri zake, kidogo tu kaanza kuropoka, zero kabisa naanza kumdharau. Ukiwa mleI haimaanishi kumchunguza mtu ili ukaseme magazetini. Zero kabisa na ndio maana anaongozwa na form four failure bila kujijua
 
Last edited by a moderator:
Kwani kuhama chadema ndiyo zitto amekuwa hamnazo kwa nn asiseme kuwa zitto ni mzigo pindi yupo cdm that shame
 
Wewe ni mzima? Unajua jinsi wabunge wa kuteuliwa kupitia CHADEMA walivyopatikana? Vigezo na maamuzi ya nani awe mbunge wa kuteuliwa viliandaliwa na Dr. Kitila, na mapendekezo yalipelekwa na Kitila Mkumbo kwa niaba ya kamati.

Acheni kukanusha vitu msivyovijua mbona hata kipengele cha ukomo wa uenyekiti kilitolewa kinyemela hatukumsikia huyo profesa wenu akitoa maoni?

Tafuteni waraka wa Chacha Wangwe muusome ndo mje kuutetea upuuzi wenu hapa mtapingaje ilihali Wangwe kayaandika hayo akitokea kuwa Makamu mwenyekiti wa chama.

Kwa hiyo na suala la kukiuzia chama vifaa used kwa bei ya juu nalo hamlijui na huyo mzee wenu?

Hiyo report ya CAG mbona hajasikika akitoa maoni tuone kama uprofesa wake hajauweka mfukoni kwa wenye chama?

Punguzeni unafiki mazee maana haubadili ukweli inshort Baregu aanze kwa kumkosoa Mbowe kwanza ndo tujue anachokisimamia.
 
CHAMA cha Alliance for Change and Transparance (ACT-Tanzania) kimefanikiwa kuishawishi kwa hoja mahakama kuu ya Tanzania na kushinda katika maombi ya zuio la muda yaliyoombwa na wanachama wake Kadawi Limbu na wenzake ya kutaka mahakama Kuu itoe amri ya zuio la muda kwamba Samson Mwigamba, Peter Mwambuja na Mohamed Masaga wasijihusishe na shughuli yoyote ya Chama mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa

Kutokana na kutupwa kwa zuio hilo la muda kesi ya msingi namba 21/2015 imepangwa kusikilizwa April 15 mwaka huu, huku Limbu na wenzake wakitakiwa kulipa theluthi moja ya gharama za kesi hiyo

Kabla ya Limbu na wenzake kuomba zuio la muda la kutaka Mwigamba na wenzake wasijishughulishe na kazi za Chama kwa nafasi ya Katibu Mkuu,Naibu katibu Mkuu na mhasibu,walifungua kesi ya msingi iliyokuwa na maombi manne

1 Mahakama kuu ya Tanzania Itamke kuwa Chama cha ACT-Tanzania haina kamati kuu na Halmashauri kuu

2 Mahakama kuu ya Tanzania itamke kuwa kikao halali cha viongozi wa ACT-Tanzania ni kile cha kamati kuu iliyokutana Disemba 31 mwaka jana

3 Mahakama kuu itamke kuwa washitakiwa watatu Mwigamba,Masaga na Mwambuja siyo wanachama halali wa ACT-Tanzania

4 Mahakama kuu iwatake washitakiwa kulipa gharama zote za kesi

Kwa upande wake wake Mwigamba na wenzake waliweka pingamizi la kusikilizwa kwa maombi ya zuio la muda ya Limbu na wenzake kwa hoja zifuatazo

1 Walalamikaji Limbu na wenzke hawakuonyesha ni kanuni gani ya kisheria waliyotumia kuiomba mahakama itoe zuio la awali

2 Kwenye hati ya mlalamikaji katika kesi ya msingi mlalamikaji namba moja ni Kadawi Lucas Limbu,lakini Kwenye hati ya kiapo ya maomb ya zuio la muda mla kiapo namba moja amejitambulisha kuwa ni ACT-Tz

3 Maombi hayo yangeweza kuombwa katika mahakama ya chini badala ya mahakama kuu

Kufuatia hoja hizo tatu za mawakili wanaowawakilisha kina Mwigamba, wakili wa Limbu na wenzake alikiri upungufu katika hati yao ya maombi hivyo mahakama kuu chini ya Jaji J.Mwandambo ikatupilia mbali maombi ya zuio la muda na kumtaka Mlalamikaji Kulipa gharama za kesi.

Hii ni nyingine kabisa na inahitaji uzi wake!
 
Chadema kinazidi kujichanganya juu ya hili la Zitto, kama mwanamke umeachana naye unaacha hata kumzungumzia, unamwacha akahangaike na dunia sio kila saa ooh ana kiburi, hashauriki, ana hiki na kile.

Kama mnamaanisha Zitto si kitu, mwacheni aendelee na maisha yake.
 
Mwenye Enzi Mungu atujalie afya njema na pumzi tuweze kuishi na kushuhudia safari ya Zitto Kabwe huko ACT-Wazalendo ili hatimaye atuthibitishie alikotoka walikuwa wanamchelewesha.
Zitto yupo kambi ya Act-wavamizi,na siyo Act-wazalendo,naona unafanya makusudi.
 
Back
Top Bottom