Prof. Baregu: Zitto ni mzigo

Prof. Baregu: Zitto ni mzigo

PROFESA Mwesiga Baregu, mmoja wa watu wanaoheshimika nchini amesema, aliyepata kuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, anaponzwa na kibuli cha kujiona hakuna zaidi ya yeye.

Amesema, Zitto ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tanzania Bara na naibu kiongozi wa upinzani bungeni, anafanya kazi asiyoifahamu na ambayo haina mavuno.

"Ninamfahamu vizuri. Wakati tuhuma hizi za usaliti zilipoanza kuibuka, Kamati Kuu ilinikabidhi jukumu la kumsaidia mama yake mzazi kumlea kijana huyu."

Kauli ya Baregu ilitolewa siku moja baada ya Zitto kujiondoa bungeni na baadaye kujiunga na Chama cha ACT – Tanzania.

Prof. Baregu aliwahi kuwa "mlezi wa Zitto" ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Alikabidhiwa jukumu hilo na Shida Salum, mama mzazi wa Zitto (marehemu), baada ya mama huyo kuiomba Kamati Kuu (CC) ya chama hicho "kusaidia kumlea."

Prof. Baregu ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema anasema, "Zitto hamnazo. Amekuwa anajiona yeye ni zaidi ya chama. Hashauriki."

Anasema wakati ule alipopewa kazi ya kumlea Zitto "katikakati ya migogoro, tulikuwa tunazungumza naye mara kwa mara. Ninamfahamu. Kazi hii ya kumlea tulikabidhiwa mimi na mama yake mzazi, Bi. Shida Salum," anaeleza Baregu.

Mama mzazi wa Zitto, alifariki dunia Juni mwaka jana, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kauli ya Prof. Baregu ilifuatia gazeti hili kutaka maoni yake juu ya mustakabali wa kisiasa wa Zitto baada ya kuwahi kujiondoa ndani ya Chadema.



Huyo ndiye Prof Baregu kwa wale mliodhani eti anaweza kumfuata Zitto.
Aina za maprofesa wanaoweza kumfuata Zitto mbona wanajulikana jamani?!
 
Last edited by a moderator:
Mwl. Kaijage

Hapa tunazungumzia u hamnazo wa Zitto.
Kadawi Limbu ni mtu Makini Kabisa na Mwenyekiti Halali wa ACT- Wazalendo
 
Last edited by a moderator:
Hivi wanaosema Zitto ni kichwa kwa lipi? Kwa GPA ya 3.5?

Kuhusu Prof, moja ya kazi za kipuuzi alizowahi kufanya Baregu ni hii ya kushauri "mzigo".
 
Madhara yatafuatana na madhara, Habari ya shari kwa habari ya shari. Ndivyo itakavyokuwa kwenye nyumba ya wasio jielewa.
 
Baregu nae ni mzigo, hana kazi yoyote anayofanya ya maana ni profesa lakini kichwani hakuna kitu zero brain
 
Naona hadi profesa Baregu kamchoka zitto, sio siri zitto hata mi nimemchoka kwakweli nilikuwa namtetea sana.
 
WAACHE NDEGE WAPITE JUU YA KICHWA CHAKO WAONDOKE ZAO USIKUBALI WAJENGE KIOTA JUU YA KICHWA CHAKO MAANA WALIMWENGU NA MUNGU WATAKULAUMU SANA NA KUKUÖNA MBAYA KAMA NDUMILA KUWILI.
WEWE UKITUHUMIWA KUTENDA USALITI AU UOVU WAKATI UNATAKA KUUTENDA AU UMEUTENDA ACHA NA UJUE HILO NI ONYO LAKIN UKAJA UKATENDA YALE UNAYOTUHUMIWA NA YAKBAINIKA HATA KWA FIKRA NA MACHO HAKIKA HUTAWAPONA WALIMWENGU NA MUNGU KWANI WATASEMA MMEÖANA TULIYOSEMA NA NA KUMTUHUM? BAADA YA HAPO KAMA HUKUOMBA MSAMAHA KWA KUAMINI UNAAKILI NYINGI LAANA ITAKUTAFUNA NA UIMARA WAKO UTAKWISHA NA KUITWA DHAIFU,LIMBUKENI,MLAFI wA MADARAKA,MSALITI,NDUMILAKUWILI . Asante
 
CHAMA cha Alliance for Change and Transparance (ACT-Tanzania) kimefanikiwa kuishawishi kwa hoja mahakama kuu ya Tanzania na kushinda katika maombi ya zuio la muda yaliyoombwa na wanachama wake Kadawi Limbu na wenzake ya kutaka mahakama Kuu itoe amri ya zuio la muda kwamba Samson Mwigamba, Peter Mwambuja na Mohamed Masaga wasijihusishe na shughuli yoyote ya Chama mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwaKutokana na kutupwa kwa zuio hilo la muda kesi ya msingi namba 21/2015 imepangwa kusikilizwa April 15 mwaka huu, huku Limbu na wenzake wakitakiwa kulipa theluthi moja ya gharama za kesi hiyoKabla ya Limbu na wenzake kuomba zuio la muda la kutaka Mwigamba na wenzake wasijishughulishe na kazi za Chama kwa nafasi ya Katibu Mkuu,Naibu katibu Mkuu na mhasibu,walifungua kesi ya msingi iliyokuwa na maombi manne1 Mahakama kuu ya Tanzania Itamke kuwa Chama cha ACT-Tanzania haina kamati kuu na Halmashauri kuu2 Mahakama kuu ya Tanzania itamke kuwa kikao halali cha viongozi wa ACT-Tanzania ni kile cha kamati kuu iliyokutana Disemba 31 mwaka jana3 Mahakama kuu itamke kuwa washitakiwa watatu Mwigamba,Masaga na Mwambuja siyo wanachama halali wa ACT-Tanzania4 Mahakama kuu iwatake washitakiwa kulipa gharama zote za kesiKwa upande wake wake Mwigamba na wenzake waliweka pingamizi la kusikilizwa kwa maombi ya zuio la muda ya Limbu na wenzake kwa hoja zifuatazo1 Walalamikaji Limbu na wenzke hawakuonyesha ni kanuni gani ya kisheria waliyotumia kuiomba mahakama itoe zuio la awali2 Kwenye hati ya mlalamikaji katika kesi ya msingi mlalamikaji namba moja ni Kadawi Lucas Limbu,lakini Kwenye hati ya kiapo ya maomb ya zuio la muda mla kiapo namba moja amejitambulisha kuwa ni ACT-Tz3 Maombi hayo yangeweza kuombwa katika mahakama ya chini badala ya mahakama kuuKufuatia hoja hizo tatu za mawakili wanaowawakilisha kina Mwigamba, wakili wa Limbu na wenzake alikiri upungufu katika hati yao ya maombi hivyo mahakama kuu chini ya Jaji J.Mwandambo ikatupilia mbali maombi ya zuio la muda na kumtaka Mlalamikaji Kulipa gharama za kesi.
Kama mnasiaga kichaa hamjamuona mmoja ni huyu hapa.
 
Hii porojo yako inahusiana nini na mjadala hapa!
CHAMA cha Alliance for Change and Transparance (ACT-Tanzania) kimefanikiwa kuishawishi kwa hoja mahakama kuu ya Tanzania na kushinda katika maombi ya zuio la muda yaliyoombwa na wanachama wake Kadawi Limbu na wenzake ya kutaka mahakama Kuu itoe amri ya zuio la muda kwamba Samson Mwigamba, Peter Mwambuja na Mohamed Masaga wasijihusishe na shughuli yoyote ya Chama mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa

Kutokana na kutupwa kwa zuio hilo la muda kesi ya msingi namba 21/2015 imepangwa kusikilizwa April 15 mwaka huu, huku Limbu na wenzake wakitakiwa kulipa theluthi moja ya gharama za kesi hiyo

Kabla ya Limbu na wenzake kuomba zuio la muda la kutaka Mwigamba na wenzake wasijishughulishe na kazi za Chama kwa nafasi ya Katibu Mkuu,Naibu katibu Mkuu na mhasibu,walifungua kesi ya msingi iliyokuwa na maombi manne

1 Mahakama kuu ya Tanzania Itamke kuwa Chama cha ACT-Tanzania haina kamati kuu na Halmashauri kuu

2 Mahakama kuu ya Tanzania itamke kuwa kikao halali cha viongozi wa ACT-Tanzania ni kile cha kamati kuu iliyokutana Disemba 31 mwaka jana

3 Mahakama kuu itamke kuwa washitakiwa watatu Mwigamba,Masaga na Mwambuja siyo wanachama halali wa ACT-Tanzania

4 Mahakama kuu iwatake washitakiwa kulipa gharama zote za kesi

Kwa upande wake wake Mwigamba na wenzake waliweka pingamizi la kusikilizwa kwa maombi ya zuio la muda ya Limbu na wenzake kwa hoja zifuatazo

1 Walalamikaji Limbu na wenzke hawakuonyesha ni kanuni gani ya kisheria waliyotumia kuiomba mahakama itoe zuio la awali

2 Kwenye hati ya mlalamikaji katika kesi ya msingi mlalamikaji namba moja ni Kadawi Lucas Limbu,lakini Kwenye hati ya kiapo ya maomb ya zuio la muda mla kiapo namba moja amejitambulisha kuwa ni ACT-Tz

3 Maombi hayo yangeweza kuombwa katika mahakama ya chini badala ya mahakama kuu

Kufuatia hoja hizo tatu za mawakili wanaowawakilisha kina Mwigamba, wakili wa Limbu na wenzake alikiri upungufu katika hati yao ya maombi hivyo mahakama kuu chini ya Jaji J.Mwandambo ikatupilia mbali maombi ya zuio la muda na kumtaka Mlalamikaji Kulipa gharama za kesi.
 
Back
Top Bottom