Pro-LOWASSA's where are you?

Wapi Pasco??wapi yule aliyetueleza kwamba Mzee Lowasa yupo German mzima wa afya!!
CDM kweli kiboko yao.Naamini mpaka 2014,huyu Mzee kama akigombea urais atakuwa na uwakika wa kula za Monduli tu.


mzee mamvi anacheza karata na Kanisa wakati mmoja wa waumini wa Kanisa ni mimi.

akacheze karata na mafisadi wenzake.
 
arumeru kumewamaliza..pasco hajalipwa ujira wake miezi miwili sasa ameamua bora kudili na fani yake inayomjengea heshima.
 
Anguko la CCM arumeru ni anguko la Lowasa. kwa sasa amegundua kuwa yule mchawi TB JOSHUA anamlia pesa zake kwa kumtabiria uongo.
 
wapi pasco??wapi yule aliyetueleza kwamba mzee lowasa yupo german mzima wa afya!!
Cdm kweli kiboko yao.naamini mpaka 2014,huyu mzee kama akigombea urais atakuwa na uwakika wa kula za monduli tu.

They have retreated in order to advance!!!!! Wanajipanga upya baada ya kipigo cha mbwa mwizi kule Arumeru.
 
Jamaa alipoona NEC imemkalia kimya akadhani safari yake ya kwenda kunyweshwa mwavi kule Nigeria ndo kila kitu. Sasa aendelee na therapy yake ya presha huku akijua kwamba masika hayajaanza!
 
Mbopo naona unashangilia sana huu ushindi wa Arumeru kuliko hata CHADEMA wenyewe walioshinda Ubunge.

Ha ha ha Huyo Jamaa anahisi kuanguka kwa CCM Arusha ni Kuanguka kwa Lowasa? Anahisi jamaa yake Membe atatokea hapo.

CCM Wote ni Wezi
 
mzee mamvi anacheza karata na Kanisa wakati mmoja wa waumini wa Kanisa ni mimi.

akacheze karata na mafisadi wenzake.

Hata huko Kanisani anakocheza karata zake, sio viongozi wote wa makanisa wanamfagilia, yawezekana wanafagilia hela zake tu. Wakati wa kuomba kura ukifika, sijui hata kama watakuja kumpigia debe. Unajua kwa hali ilivyo sasa hivi hata makanisa yanaona aibu sana kujihusisha na CCM kwa kuwa yanaweza kuonekana yanafagilia wananchi waendelee kuwa na hali ngumu ya maisha.

Askofu mzima anasimama madhabahuni akihubiri kwamba ufisadi ni mbaya sana na ndio unadidimiza maisha ya waumini wake kiasi kwamba wamepigika sana, halafu huyo huyo aje kurudi kwa waumini wake kwamba anampigia debe fisadi awe Rais? Hao waumini kama watakubali, basi lazima na wao wawe na matatizo kichwani!

Habari kwamba Askofu wa Lutheran - Dayosisi ya Meru, alikataa katakata kupiga debe la Siyoi [nilisoma kwenye Raia Mwema] ilinifariji sana na kuonyesha kwamba bado tuna viongozi wa dini ambao wana akili timamu. Yule Mzee alimuuliza Lowassa maswali ya maana sana na kama Lowassa ana busara, lile lilikuwa ni darasa tosha sana na labda atapunguza kasi ya michango kwenye makanisa.
 
Mbopo naona unashangilia sana huu ushindi wa Arumeru kuliko hata CHADEMA wenyewe walioshinda Ubunge.

Akili yako inavyokutuma CDM ni mbowe,zitto,slaa,mnyika na viongozi wengne waandamizi.CDM ni yakila mtu,uwe msomi,maskini,mwanajeshi,magereza,mtumishi wa serikali n.k.Kwahyo hata sisi ni wadau wakubwa wa CDM.
PEOPLES.... POWEEER...
 
Ha ha ha Huyo Jamaa anahisi kuanguka kwa CCM Arusha ni Kuanguka kwa Lowasa? Anahisi jamaa yake Membe atatokea hapo.

CCM Wote ni Wezi

Hiyo BOLD ndo ukweli wenyewe ... ndio maana hapo juu nilisema viongozi wa dini wanaona noma kujihusisha na CCM, period!

It doesn't matter, whether ni Sitta, Membe au Lowassa, yeyote atakayegombea kupitia CCM lazima awe na wakati mgumu sana. Ndio maana wamepoteza udiwani kata ya Lizaboni - Songea ambako walimtuma Nchimbi na makada wenzake na udiwani wa kata ya Kiwira - Mbeya ambako walimtuma "mpambanaji" Mana Anne Kilango na Mzee Sitta alikuwa Mwanza akashindwa kukomboa Kata ya Kirumba. CCM ina hali mbaya, huo ndo ukweli.

Nimeangalia majibu ya Mwigulu Nchemba kwenye thread fulani, sikuamini kama ni yeye, maana yale majigambo na majibu ya kejeri yameisha. Sasa amekuja na CD mpya inatwa Tanzania kwanza. Huwezi kusema Tanzania kwanza wakati ukiingia mjengoni [Bungeni] unaenda kupitisha utumbo ambao hauna maslahi kwa wananchi. Sema "Tanzania Kwanza" au "Taifa Kwanza" kwa maneno na vitendo. Wabunge wa CCM kila kukicha ni vijembe na mipasho Bungeni.
 
Mwacheni pasco amkamue pesa yule mzee.
Hata pasco anajua fika kuwa mzee huyu hata ubunge 2015 hatapata.
OTIS
 
Mwacheni pasco amkamue pesa yule mzee.
Hata pasco anajua fika kuwa mzee huyu hata ubunge 2015 hatapata.
OTIS

Pasco alisema atamwambia Mamvi abadili uwamuzi wa kugombea 2015!sasa sijui tayari kumshauri au bado!mkuu Pasco tupe update bana.
 
Akili yako inavyokutuma CDM ni mbowe,zitto,slaa,mnyika na viongozi wengne waandamizi.CDM ni yakila mtu, uwe msomi,maskini,mwanajeshi,magereza,mtumishi wa serikali n.k. Kwahyo hata sisi ni wadau wakubwa wa CDM.
PEOPLES.... POWEEER...

Taratibu Mzee wa SUP,

Ulielewa vyema post yangu? Sikuwa ninai-address kwako, post yangu imeelekezwa kwa Bwana Mbopo ambaye ni shabiki na mpiga debe wa Membe kwenye kinyang'anyiro cha kuomba tiketi ya kugombea urais kupitia CCM.

Membe na Lowassa wote wanafikiria kuomba kugombea kupitia CCM. Jamii imeaminishwa kwamba hakuna kinachomshinda Lowassa iwapo akiamua. Lakini anguko lake la Arumeru ni furaha ya Mbopo pamoja na wana CCM wengine wote ambao wanaumuona hafai kuwa Rais kupitia CCM

Ndio maana nikamwambia anashangilia kuliko hata wana CHADEMA wenyewe.

Kabla huja-quote na kujibu post mtu isome vizuri kama inakuhusu au la.
 
Inasikitisha sana pale unapoona watu wanaojiita makini upeo wao wa kila jambo mwisho ni kwa Lowassa! Simtetei ila ni kitu kibaya kuwa na dhana ya GREAT MAN THEORY kuwa kila kitu Tanzania kinaanzia kwa Lowassa na kinaishia kwa Lowassa, that is purely the poverty of intelect!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom