Mkuu NasDaz,
Kama nilivyosema, nakubaliana na wewe kwa mengi ila kwa uzoefu wangu nilioupata na kukaa na Wadhungu, hizo njia tunazotumia siyo sahihi hata kidogo.
Kwanza lazima ujuwe kuwa ili hao WADHUNGU waje kuwekeza, ni lazima wapate kibali cha Serikali yao na hapo Waziri wa Uchumi mara nyingi muhusika mkuu. Sasa kwangu mie, hata kama ni mtu wa TIC, akiongea na Balozi na Balozi akaandaa mkutano huo kwa kupitia Waziri wa uchumi na kuwaita matajiri kadhaa, basi utafanikiwa zaidi. Wale jamaa wakiitwa na Waziri basi watakuja tu na kumsikilza hata kama atakuwa ni mtu wa chini. Kwa hili unaweza kuniamini au usiamini ila ndiyo best way ya kuwaingia hawa watu. Bila ya Serikali yao kukubali basi wewe unahangaika tu. Ndiyo maana nikasema, LOBBYING ina nguvu zaidi kuliko hata Rais. Huhitaji hata Waziri kama una mtu anayejua kujieleza kwa ufasaha kwa hao matajiri na kwa muda mfupi. Na ukitaka kuwamaliza zaidi, peleka mtu anayeongea lugha yao na kujua mila na tabia zao. Haki ya nani utashangaa wanavyokenua meno siku hiyo kwa kuona Kijana wao MWEUSI.
Kuhusu kutangaza nchi, njia rahisi sana ni kwenye MICHEZO. Ingelikuwa miaka ya 70, unamchukua Filbert Bay au Shahanga na wanakutangazia hilo tangazo lako. Kwa USA, nimeshasema mara nyingi sana kuwa tuna mtu anayefaa kututangazia nchi huko USA ila hatumtumii. Huyu ni Mkulima wa Kahawa huko Mbeya ila ni mtoto wa Legend Jack Robinson ambaye mwaka huu kama sikosei wamecheza hadi film kuhusu huyu Mzee:
Jackie Robinson - Wikipedia, the free encyclopedia
Jamaa anaitwa David Robinson.... huyu angeliuza zaidi Tanzania USA kuliko viongozi wote wa Tanzania.
Angalia akiwa USA anavyopokelewa kwa heshima kwenye TV kubwa......
Ndiyo maana nasema, kama kweli tunataka ifahamike, tutumie njia ambazo kweli tutatangaza kwa muda mrefu. Kwa mfano kama CNN wangelikubali kumfanyia kipindi huyu jamaa, wangi walijua kuzidi hata kufanya tangazo.
Sijui kama umenielewa. Kwamba kuna njia fupi na bei nafuu na zitafanya impact kubwa.
Hata Katanga sasa wapo juu sana kwa sababu ya Team ya TP Mazembe. sisi hata kukimbia hatushindi - SHAME.
Hata kama hatutaki, lakini ukweli utabaki pale pale kwamba tunahitaji PR ya nguvu kuitangaza hii nchi! Unapojenga awareness na business executives ni njia moja wapo ya kujenga awareness about the country as the whole!