kyarluta
Member
- Oct 28, 2019
- 24
- 12
Nawapongeza akina mama na vijana wajasiriamali wa stendi ya Chato. Napongeza hasa wale wanaouza maziwa.
Ni hivi majuzi 19/4/2020, nilipita na basi Fikosh nikitokea Mwanza kuelekea Bukoba, muda wa saa 6 mchana. Nilishawishika kununua maziwa ya mgando baada ya kuwa na hamu nayo. Yalikuwa yako kwenye chupa kubwa ya maji ya lita moja na nusu. Maziwa hayo nilikuja kuyanywa saa nne usiku.
Ama kwa hakika maziwa hayo yalikuwa matamu, hayakuwa yamekatika kwa maana ya kujitenga na maji, hayakuwa machachu na harufu yake ilikuwa original. Hayakuniumiza tumbo. PONGEZI SANA.
Nawashauri wauza maziwa wa Bukoba stendi, Karagwe Kihanga ( kwa Wachina) Kyaka na wale wa Muhoro (njia ya Lindi) kuwaiga wajasiriamali hawa wa Chato stendi.
Kwa wana Chato, kamwe msije mkashawishika kuongeza maji, wala kugandisha maziwa kwa kulazimisha na chachu ili yagande haraka. Mtaharibu soko la maziwa yenu.
Ni hivi majuzi 19/4/2020, nilipita na basi Fikosh nikitokea Mwanza kuelekea Bukoba, muda wa saa 6 mchana. Nilishawishika kununua maziwa ya mgando baada ya kuwa na hamu nayo. Yalikuwa yako kwenye chupa kubwa ya maji ya lita moja na nusu. Maziwa hayo nilikuja kuyanywa saa nne usiku.
Ama kwa hakika maziwa hayo yalikuwa matamu, hayakuwa yamekatika kwa maana ya kujitenga na maji, hayakuwa machachu na harufu yake ilikuwa original. Hayakuniumiza tumbo. PONGEZI SANA.
Nawashauri wauza maziwa wa Bukoba stendi, Karagwe Kihanga ( kwa Wachina) Kyaka na wale wa Muhoro (njia ya Lindi) kuwaiga wajasiriamali hawa wa Chato stendi.
Kwa wana Chato, kamwe msije mkashawishika kuongeza maji, wala kugandisha maziwa kwa kulazimisha na chachu ili yagande haraka. Mtaharibu soko la maziwa yenu.