Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Jeshi la Polisi limezuia kufanyika Mkutano wa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche na waandishi wa habari ulokuwa ufanyike leo Juni 17, 2025 katika hotel ya Seashells Millennium Hotel, iliyopo Makumbusho Dar es salaam, kwa maelezo kwamba chama hicho kimezuiwa na Mahakama kufanya shughuli za Siasa.
Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa Chadema, Brenda Rupia amesema wa wakati wakiandaa kwa mkutano huo, walifika watu waliojitambulisha kuwa ni maofisa wa polisi na kuzuia ufifanyike.
"Walikuja maofisa wa polisi wakasema CHADEMA imezuiwa kufanya kazi hivyo tusifanye mkutano. Lakini huu mkutano nimeuitisha mimi kama Brenda, sio wa chama," amesema.
Alipoulizwa kuhusu zuio hilo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amehoji, "wanalalamika nini? Basi tunafuatilia wasichokijua na ambacho wanakilalamikia."
Taarifa ya Chama cha Demokrasia na Maendeleoa (CHADEMA)
Jeshi la Polisi limezingira hotel ya Seashells Millennium Hotel na kuwaamuru waandishi wa habari kuondoka, Makamu Mwenyekiti - Tanganyika John Heche alitarajia kufanya Mkutano na Waandishi wa Habari hotelini hapo leo tarehe 17 Juni 2025. Jeshi hilo limedai kuwa Chadema wamezuiliwa kujishughulisha na shughuli yoyote ya kisiasa.
POSTPONED (PP): John Heche anazungumza na Watanzania kupitia Waandishi wa Habari, Dar es Salaam, Julai 17, 2025
Polisi alivamia press na kuamuru Waandishi wa Habari wazime Kamera zote.
Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa Chadema, Brenda Rupia amesema wa wakati wakiandaa kwa mkutano huo, walifika watu waliojitambulisha kuwa ni maofisa wa polisi na kuzuia ufifanyike.
"Walikuja maofisa wa polisi wakasema CHADEMA imezuiwa kufanya kazi hivyo tusifanye mkutano. Lakini huu mkutano nimeuitisha mimi kama Brenda, sio wa chama," amesema.
Alipoulizwa kuhusu zuio hilo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amehoji, "wanalalamika nini? Basi tunafuatilia wasichokijua na ambacho wanakilalamikia."
Taarifa ya Chama cha Demokrasia na Maendeleoa (CHADEMA)
Jeshi la Polisi limezingira hotel ya Seashells Millennium Hotel na kuwaamuru waandishi wa habari kuondoka, Makamu Mwenyekiti - Tanganyika John Heche alitarajia kufanya Mkutano na Waandishi wa Habari hotelini hapo leo tarehe 17 Juni 2025. Jeshi hilo limedai kuwa Chadema wamezuiliwa kujishughulisha na shughuli yoyote ya kisiasa.
POSTPONED (PP): John Heche anazungumza na Watanzania kupitia Waandishi wa Habari, Dar es Salaam, Julai 17, 2025
Polisi alivamia press na kuamuru Waandishi wa Habari wazime Kamera zote.