johnmashilatu
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 718
- 703
Jeshi la Polisi wilayani Ngara mkoani Kagera linadaiwa kumuua kwa kumpiga risasi mkazi wa eneo ya Nyamiaga wilayani humo aliyewatisha kwa shoka askari waliokwenda kumkamata.
Katika tukio hilo la Jumatatu jioni, askari sita wanadaiwa kumuua Philbert Protas ( 30) kwa kumpiga risasi kadhaa mwili baada ya kuwatisha kwa shoka askari hao waliokwenda kumkamata akituhumiwa kumshambulia mwanamke mmoja mkazi wa mtaa huo.
Mwenyekiti wa mtaa wa Nyamiaga Robert Choya anasema aliwaita askari hao baada ya kutokea vurugu kwenye eneo lake na walipofika, mtu hyo alikataa kutoa ushirikiano kwa polisi na kuwatisha kuwashambulia kwa shoka ambapo walimpiga risasi na kufariki muda mfupi baada ya kufikishwa katika hositali ya wilaya hiyo, Nyamiaga.
Hata hivyo, Baba mdogo wa marehemu, Posian Apolinary amesikitishwa na kitendo cha polisi kumpiga risasi mtoto wake na kupelekea kifo wakati wangeweza kutumia njia nyingine kumdhibiti kwani inadaiwa awali alipigwa risasi mguuni na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kujisalimisha.
Diwani wa kata ya Nyamiaga, James Bazisa amesema maziko ya mtu huyo yanafanyika leo nyumbani kwao eneo la Nyamiaga.
Katika tukio hilo la Jumatatu jioni, askari sita wanadaiwa kumuua Philbert Protas ( 30) kwa kumpiga risasi kadhaa mwili baada ya kuwatisha kwa shoka askari hao waliokwenda kumkamata akituhumiwa kumshambulia mwanamke mmoja mkazi wa mtaa huo.
Mwenyekiti wa mtaa wa Nyamiaga Robert Choya anasema aliwaita askari hao baada ya kutokea vurugu kwenye eneo lake na walipofika, mtu hyo alikataa kutoa ushirikiano kwa polisi na kuwatisha kuwashambulia kwa shoka ambapo walimpiga risasi na kufariki muda mfupi baada ya kufikishwa katika hositali ya wilaya hiyo, Nyamiaga.
Hata hivyo, Baba mdogo wa marehemu, Posian Apolinary amesikitishwa na kitendo cha polisi kumpiga risasi mtoto wake na kupelekea kifo wakati wangeweza kutumia njia nyingine kumdhibiti kwani inadaiwa awali alipigwa risasi mguuni na kunyoosha mikono juu kama ishara ya kujisalimisha.
Diwani wa kata ya Nyamiaga, James Bazisa amesema maziko ya mtu huyo yanafanyika leo nyumbani kwao eneo la Nyamiaga.