Polisi Kuwasaka Waliompa JK Siku 100

Polisi Kuwasaka Waliompa JK Siku 100

Status
Not open for further replies.
Haaaaaa kumbe waheshimiwa wanapitiaga JF nimemuona Nahodha anasema wao wametumwa wawatafute hao watu wanaosambaza ujumbe,makampuni yamemgomea kumpa details kwa ajili ya kulinda mteja na kutopoteza wateja wao...

Safi kabisa
 
waziri wa mambo ya ndani mh vuai amesema selikali kupitia jeshi la polisi wameanza uchunguzi kubaini ni nani aliyesambaza waraka kwenye mtandao unaomtaka jk kujiuzulu ndani ya siku 100 na pia amewataka wananchi kutoa ushiriano kwa jeshi la polisi
 
Tukumbuke kuwa na makampuni ya simu yanawajibu wakulinda wateja wao "protect customer privacy" na wao wakienda kinyume na sheria hiyo basi mtu unawashtaki; unahakikisha ukipata msukosuko (wekwa ndani) familia yako nayo inafidiwa na kampuni ya simu. Ni lazima hizi kampuni za simu ziheshimu makubaliano yao na wateja.

uhuru na haki haya maneno tunapenda sana kuyatumia lakini tunasahau kitu mambo muhimu yanayoambatana nayo:
uhuru lazima uwe na mipaka.
Hakuna haki bila wajibu.
Kuhusiana na makampuni ya simu kulinda taarifa za wateja wao, wajibu una ukomo kama maslahi ya taifa yatakuwa hatarini, lakini kwakuwa ni jambo la kisheria basi ni lazima utoaji wa taarifa za mteja uhizinishwe na mahakama
 
Yule mmiliki wa Ze Utamu inasemekana amesha-gaddafiwa zamani sana sasa nyie mnaojifanya kusambaza viujumbe vyenu vya kipuuzi endeleeni tu. Kwa taarifa yenu, JK ndiye anajulikana kama Rais anayeongoza kuua maadui zake kuliko Rais yeyote aliyewahi kuongoza Tz. Achilia mbali maadui zake aliowaweka gerezani kama kina Babu Seya kutokana na tofauti ndogondogo.
 
walikuwa wanacheza na serikali hao watu ... watakamatwa TU ...
 
Yule mmiliki wa Ze Utamu inasemekana amesha-gaddafiwa zamani sana sasa nyie mnaojifanya kusambaza viujumbe vyenu vya kipuuzi endeleeni tu. Kwa taarifa yenu, JK ndiye anajulikana kama Rais anayeongoza kuua maadui zake kuliko Rais yeyote aliyewahi kuongoza Tz. Achilia mbali maadui zake aliowaweka gerezani kama kina Babu Seya kutokana na tofauti ndogondogo.

sijakupata mkuu, Gaddaf alifanywa mambo mawili, wewe una maanisha vp? Moja kati ya hayo mawili? Au jumla kuu?
 
Niliwai pata hbr kuwa ze utamu owner ni mtoto wa mze CHELA,
Yule mmiliki wa Ze Utamu inasemekana amesha-gaddafiwa zamani sana sasa nyie mnaojifanya kusambaza viujumbe vyenu vya kipuuzi endeleeni tu. Kwa taarifa yenu, JK ndiye anajulikana kama Rais anayeongoza kuua maadui zake kuliko Rais yeyote aliyewahi kuongoza Tz. Achilia mbali maadui zake aliowaweka gerezani kama kina Babu Seya kutokana na tofauti ndogondogo.
 
Njia pekee ya kuondokana na vitisho ni kutekeleza matakwa ya wananchi kwa kuacha kuwa mtawala na kuwa kiongozi. Ndo maana tunahitaji katiba mpya itakayo tupa pamoja na mambo mengine. nafasi ya kutoa mawazo yetu bila kuhofia kukamatwa.
 
Mkuu,

Hakuna kujificha katika net kuna vichwa dunia hii acha tu ze utamu yuko wapi ananyea ndoo segerea. Think before you post anything katika internet.

Acha kutisha watu wewe nani amekuambia ze utamu yupo segerea? Kwa taarifa yako tu ni kwamba ze utamu ni member hapa na kila siku anaingia humu...

Ni ukweli kabisa ukiwa kwenye net ni rahisi sana kutambulika ila siyo kirahisi kama una vyodhania wewe.
 
....inanikumbusha utotoni, mtu akikutania na ukionyesha kukasirika basi utani unazidi.
Wangeyafanya haya kimya kimya. Wamefanya hata wale wasiokuwa na taarifa kuzipata au kuanza kutafuta zaidi.
 
Haaaaaa kumbe waheshimiwa wanapitiaga JF nimemuona Nahodha anasema wao wametumwa wawatafute hao watu wanaosambaza ujumbe,makampuni yamemgomea kumpa details kwa ajili ya kulinda mteja na kutopoteza wateja wao...

na wakifanya hivyo nadhani itakuwa imekula kwa hayo makampuni ya simu. jamaa anadhani huku ni kama zanzibar, ngoja yamkute yalomkuta mapuri
 
hapo chadema hawajatajwa wakuu hebu tujuzeni wengine
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom