Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Tabia ya polisi wa Tanzania kuwatisha, kuwapiga na kuwaumiza wananchi wanaotumia haki yao ya kuhoji utendaji wa serikali inazidi kuota mizizi na kuibua maswali kuhusu wajibu wa polisi kwa raia wanaotuhumiwa kuvunja sheria.
Kwa hali isiyoeleweka Polisi wa Tanzania wameamua kutoheshimu uhuru wa mikusanyiko na uhuru wa mawazo kama ilivyooanishwa kwenye Katiba kama vile ni uvunjaji wa sheria na hivyo kujipa mamlaka ya kuwaadhibu watuhumiwa kwa vipigo.
Kauli za maafande wa polisi katika miaka ya karibuni imezidi kuwa ya kibabe na ya kiuonevu kiasi cha kutishia amani ya nchi kama wananchi wataamua kujibu mapigo kama invyotokea katika mataifa mengine ndani na nje ya Afrika.
Imekuwa kawaida polisi, ambao jukumu lao la msingi ni kuwalinda raia na mali zao, wamesikika wakitoa kauli za vitisho utadhani muda wote wako vitani na raia ambao kimsingi ndio waajiri wao kupitia serikali yao waliyoichagua wao.
Baadhi ya kauli hizo ni kama ifuatavyo...
Katika ombi langu hapo juu, nimeomba mwenye ushahidi wowote wa raia wa nchi hii kujibu mapigo kama inavyotokea katika nchi nyingine auweke hapa. Binafsi sina, ila naona kila mara polisi wakitoa vipigo kwa raia wasio hata na fimbo.
Hawaishii kupiga tu watu wazima wanaume kwa wanawake, wamethubutu kuwapiga hadi vitoto wa shule na hakuna tamko lolote limewahi kutolewa na vyombo vyenye jukumu la kuhakikisha raia wanatendewa haki.
Watu wanapigwa kabla ya kukamatwa, wanapigwa baada ya kukamatwa, wanapigwa wakiwa mikononi mwa polisi tayari iwe ndani ya gari au kwenye vituo vya polisi kama vile jukumu la polisi kwa sasa ni kupiga, kuumiza na hata kuua.
Watu waliokamatwa wamefikishwa mahakamani wakiwa na majeraha makubwa hadi kutembea wanashindwa lakini sijawahi kuisikia hata Mahakama ikitaka kujua kilichotokea au hata kuhoji kwa nini mtuhumiwa anachechemea.
Wananchi wamekamatwa majumbani wakiwa na afya zao lakini baada ya muda mfupi kwenye kituo cha polisi, wanapelekwa mahakamani wamebebwa hawawezi kutembea. Je ni kitu gani kinawapata hawa raia kwenye vituo vya polisi?
Juzi nimemsikia IGP mwenyewe kwa kauli yake akiwatishia wananchi waliopanga kufika mahakamani kusikiliza kesi ya Mbowe aliyeshtakiwa kwa kosa la ugaidi kwamba wasithubutu la sivyo watakiona cha moto na serikali ya SSH kimyaa!
Na siku hiyo ikafika. Polisi walivyotanda utadhani wanaenda vitani. Kila aina ya silaha ilikuwepo kupambana na maadui waliopanga kuhudhuria kesi. Wakaona hata hiyo hiitoshi wakakumbuka mbinu ya makaburu ya kuwatumia mbwa!
Kweli tumefika huko! Na hata miezi sita haijafika tayari hatuna tofauti na makaburu wa Afrika Kusini miaka karibu sitini enzi za Nelson Mandela na wenzake walipofunguliwa kesi ya ugaidi na serikali ya kibaguzi ya wakati huo.
Je ikitokea wananchi wakachoka na uonevu, wakaamua potelea mbali, kama ni keba keba kama inavyotokea sehemu mbali mbali duniani, je kutakalika? Tumshukuru Mungu aliyetujaalia Watanzania uvumilivu lakini mpaka lini?
Kwa hali isiyoeleweka Polisi wa Tanzania wameamua kutoheshimu uhuru wa mikusanyiko na uhuru wa mawazo kama ilivyooanishwa kwenye Katiba kama vile ni uvunjaji wa sheria na hivyo kujipa mamlaka ya kuwaadhibu watuhumiwa kwa vipigo.
Kauli za maafande wa polisi katika miaka ya karibuni imezidi kuwa ya kibabe na ya kiuonevu kiasi cha kutishia amani ya nchi kama wananchi wataamua kujibu mapigo kama invyotokea katika mataifa mengine ndani na nje ya Afrika.
Imekuwa kawaida polisi, ambao jukumu lao la msingi ni kuwalinda raia na mali zao, wamesikika wakitoa kauli za vitisho utadhani muda wote wako vitani na raia ambao kimsingi ndio waajiri wao kupitia serikali yao waliyoichagua wao.
Baadhi ya kauli hizo ni kama ifuatavyo...
- Wanaopanga kuandamana kesho watakiona cha moto
- Wakiandamana watapigwa kama mbwa koko.
- Watu watakaoandamana kwa amani watapigwa hadi wachakae
Katika ombi langu hapo juu, nimeomba mwenye ushahidi wowote wa raia wa nchi hii kujibu mapigo kama inavyotokea katika nchi nyingine auweke hapa. Binafsi sina, ila naona kila mara polisi wakitoa vipigo kwa raia wasio hata na fimbo.
Hawaishii kupiga tu watu wazima wanaume kwa wanawake, wamethubutu kuwapiga hadi vitoto wa shule na hakuna tamko lolote limewahi kutolewa na vyombo vyenye jukumu la kuhakikisha raia wanatendewa haki.
Watu wanapigwa kabla ya kukamatwa, wanapigwa baada ya kukamatwa, wanapigwa wakiwa mikononi mwa polisi tayari iwe ndani ya gari au kwenye vituo vya polisi kama vile jukumu la polisi kwa sasa ni kupiga, kuumiza na hata kuua.
Watu waliokamatwa wamefikishwa mahakamani wakiwa na majeraha makubwa hadi kutembea wanashindwa lakini sijawahi kuisikia hata Mahakama ikitaka kujua kilichotokea au hata kuhoji kwa nini mtuhumiwa anachechemea.
Wananchi wamekamatwa majumbani wakiwa na afya zao lakini baada ya muda mfupi kwenye kituo cha polisi, wanapelekwa mahakamani wamebebwa hawawezi kutembea. Je ni kitu gani kinawapata hawa raia kwenye vituo vya polisi?
Juzi nimemsikia IGP mwenyewe kwa kauli yake akiwatishia wananchi waliopanga kufika mahakamani kusikiliza kesi ya Mbowe aliyeshtakiwa kwa kosa la ugaidi kwamba wasithubutu la sivyo watakiona cha moto na serikali ya SSH kimyaa!
Na siku hiyo ikafika. Polisi walivyotanda utadhani wanaenda vitani. Kila aina ya silaha ilikuwepo kupambana na maadui waliopanga kuhudhuria kesi. Wakaona hata hiyo hiitoshi wakakumbuka mbinu ya makaburu ya kuwatumia mbwa!
Kweli tumefika huko! Na hata miezi sita haijafika tayari hatuna tofauti na makaburu wa Afrika Kusini miaka karibu sitini enzi za Nelson Mandela na wenzake walipofunguliwa kesi ya ugaidi na serikali ya kibaguzi ya wakati huo.
Je ikitokea wananchi wakachoka na uonevu, wakaamua potelea mbali, kama ni keba keba kama inavyotokea sehemu mbali mbali duniani, je kutakalika? Tumshukuru Mungu aliyetujaalia Watanzania uvumilivu lakini mpaka lini?