Polisi Dar wamvamia Mbowe usiku wa manane

Polisi Dar wamvamia Mbowe usiku wa manane

Polisi wana haki ya kumkamata mtu muda wowote wanaopenda.
Kasome vizuri katiba ya nchi ili ujue kutofautisha maana ya haki na wajibu.

Na zaidi ya yote, si sawa kwa mtu kufuatwa usiku wa manane kama si jambazi sugu, muuaji, gaidi au mhaini! Uhalifu mwingine wote unatoa nafasi kwa mhalifu kupewa taarifa ya kuitwa kituo cha polisi kwenda kutoa maelezo. Kutokana na maelezo anaweza kuruhusiwa kurudi au kubakizwa kituoni na kubaki chini ya ulinzi wa polisi.

Inashangaza sana kwa level ya mwenyekiti wa chama cha siasa kikubwa kama CHADEMA kufuatwa usiku na polisi kama jambazi. Hivi angepigiwa simu akarepoti kituo cha polisi asingeenda? Kama polisi hawa wanampigia simu Magid Mjengwa kumuomba afike kituoni kutoa maelezo kuhusiana na tukio la ugaidi, kweli wameshindwa kumpigia simu Mbowe?

Naona CCM wamechoka sana amani ya nchi hii na sasa wanafanya kila jitihada kuivuruga.
 
Mkuu Polisi wanatumika tu kutekeleza matukio ya wakubwa zao, pamoja na hayo wao pia wanastahili lawama. Haya yote yanayoendelea DHAIFU atakuwa anayafahamu hivyo yeye ndio anastahili lawama nyingi zaidi. Nchi iko katika njia panda bila hekima na busara za hali ya juu inaweza kutumbukia kwenye machafuko ya kutisha.
Au ndo washauza nchi kwa makubaliano ya kuiingiza kwenye vita nn???Mbona valuvalu sana??Au ndo?Mh!HATARI TUPU,MAJANGA WALAH.
 
Hii inadhilisha kuwa polis ndio waliohusika kuwatesa Dr Ulimboka na Mwandish Kibanda.. Pili inaonyesha polis wenyewe hawazijui sheria za nchi ndo mana wanatumika ovyo na kwa kukurupuka, ni aibu sana kwa jeshi hili... Kwa sasa hakuna kiongoz yoyote wa polis anaeheshimika, pamoja na IGP mwenyewe, ovyo kabissaa. NAKEREKA SANA NCHI KUFIKIA HATUA HII KIZEMBEZEMBE....
 
Kama taarifa za uharifu wamezipata usiku unategemea wasubiri mpaka mchana ili iweje tumia upeo wako vizuri.
Sasa mbona wanarukana hakuna aliewatuma,mnajua nyie hamko njema kabisa,mnaenda kama mkasi,nchi inaongozwa na kipuuzi.
 
Imekaa kiuchochezi zaidi.. "Silaha nzito", usiku wa manane!!

Mleta maada anaweza aisiwe na kosa ila aliyetoa hii mada ndie mwenye matatizo!!
Polisi wanawahaki kutimiza wajibu wao muda wowote kwa mtu yeyote wanayehitaji ushirikiano nae!!

Pili huyo mtoa maada anatumia umbumbu wa raia kuwahadaa juu ya sheria za kiutendaji za polisi pamoja na maswala ya haki za binadamu! Sioni huo unyama anaousema, ni nacho kiona ni kujenga chuki kati ya polisi na raia.
Kwanza atwambie silaha nzito ni zipi,kama ni SMG ni silaha ya kawaida kwa polisi.

aseme silaha hizo nzito ni zipi ni mabomu ya kivita au ndege za kivita.
 
Kukiwa na Intelligence, au mtu akiona unafanya uhalifu, akataarifu polisi, utakamatwa na kuhojiwa bila kuhitaji warrant.
Kwa mfano, ukimbaka mwanamke kwa kumshika matiti mbele ya hadhara, polisi wakatonywa, basi hawahitaji warrant kukukamata.

Nadhani Mbowe anajua kuwa anawindwa, kutokana na msemo wake kuwa ana ushahidi wa video ... he's got to be under surveillance, hilo lazima. Huo wala si udikteta thats just policing, it's normal ni lazima atakuwa spied.

Uzuri wake, ni kwamba security walijua.

Maana ya warrant ni kuipunguzia jeshi la polisi nguvu ya kuingilia uhuru wa raia ambao upo ki katiba....kuhusu
kufanyiwa upelelezi siyo kweli mbona Mwigulu alisema anazovideo zaidi za kuonyesha Ugaidi wa CDM anadai muda ukifika atazitoa kwa polisi...mbona hafuatwi usiku? Inamaana polisi wana double standard?
 
Polisi wana haki ya kumkamata mtu muda wowote wanaopenda.

Mmmh, siku yakikukuta kama yaliyowapata wapiga kura wa kaka yako jimboni Bumbuli ndipo utakapoelewa kuwa si kila kitu ni cha kushabikia bila kuangalia athari za matukio kama haya kwenye amani ya nchi.
 
Sasa mbona wanarukana hakuna aliewatuma,mnajua nyie hamko njema kabisa,mnaenda kama mkasi,nchi inaongozwa na kipuuzi.
Basi mleta post muongo labda katunga habari sisi tutamwaminije kama upande wa pili wanakataa.
 
Basi mleta post muongo labda katunga habari sisi tutamwaminije kama upande wa pili wanakataa.
Kamuulize kamanda wenu iyo agenda ya siri wametumwa na Koti au Mwigulu Kamishna Mkuu wa Grean Guard..
 
Hivi wale polisi waliokamatwa na magunia yenye bangi walipelekwa wapi, isijekuwa ni hao?
 
Polisi wana haki ya kumkamata mtu muda wowote wanaopenda.
Ujinga ni kile unachosema sio unachofikiria, HAKI ISIYO NA KIKOMO NI UTUMWA, nchi inaendeshwe kwa taratibu na katiba, usiku kumfuata mtu akueleze jambo lolote sio kawaida wala utaratibu wa nchi hii. SASA HARAKA IKO WAPI MBONA WALIPOKUTA HAYUPO HAKUNA IMPACT YOYOTE NI SAWA TU WANGEENDA ASUBUHI KESHO YAKE, kosa ni kwa watu waliofeli kuwapa silaha, tutakoma
 
Back
Top Bottom