Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,358
- 153,996
SUALA la Muungano limeibuka karibu katika kila mkutano wa Tume ya Kukusanya Maoni ya Mabadiliko ya Katiba, ambapo juzi askari Polisi Josephat Mwamunyange, alijitambulisha mbele ya mabosi wake, kuwa yeye ni Mtanganyika.
Akitoa maoni mbele ya wajumbe hao kwenye kambi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, ya 411 KJ, Ruhuwiko, wilayani hapa, Mwamunyange alisema yeye si Mtanzania bali Mtanganyika.
"Mimi ni Mtanganyika, si Mtanzania … Muungano unanufaisha wakubwa na kutuacha sisi masikini. Zanzibar wanatubagua, niliwahi kwenda katika safari ya mafunzo nikiwa kidato cha tatu, hata namba ya mpirani sikupewa, kwa kuwa natoka Bara," alisema Mwamunyange.
Polisi huyo wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), alitaka Muungano uvunjwe na kuongeza kuwa wakati Wabara wanabaguliwa wakiwa Zanzibar, Tanzania Bara, Wazanzibari wamegeuza kuwa ‘shamba la bibi' bila kufafanua, lakini akaongeza kuwa kwa bibi ndiko hata ukirudi nyumbani saa saba usiku, hasemi neno.
Akitoa maoni mbele ya wajumbe hao kwenye kambi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, ya 411 KJ, Ruhuwiko, wilayani hapa, Mwamunyange alisema yeye si Mtanzania bali Mtanganyika.
"Mimi ni Mtanganyika, si Mtanzania … Muungano unanufaisha wakubwa na kutuacha sisi masikini. Zanzibar wanatubagua, niliwahi kwenda katika safari ya mafunzo nikiwa kidato cha tatu, hata namba ya mpirani sikupewa, kwa kuwa natoka Bara," alisema Mwamunyange.
Polisi huyo wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), alitaka Muungano uvunjwe na kuongeza kuwa wakati Wabara wanabaguliwa wakiwa Zanzibar, Tanzania Bara, Wazanzibari wamegeuza kuwa ‘shamba la bibi' bila kufafanua, lakini akaongeza kuwa kwa bibi ndiko hata ukirudi nyumbani saa saba usiku, hasemi neno.