Polepole ya Kobe ujenzi wa Miundombinu ya Kutolea Huduma za Afya Yamkwaza Naibu Waziri Dkt. Dugange

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,898
942

Polepole ya Kobe ujenzi wa Miundombinu ya Kutolea Huduma za Afya Yamkwaza Naibu Waziri Dkt. Dugange​

Naibu Waziri (Afya) Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI Dkt. Festo Dugange, amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri kusimamia miradi ya ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya ili vikamilike kwa wakati, kwa ubora na kwa kuzingatia thamani ya fedha na kuanza kutoa huduma za afya kwa wananchi haraka iwezekanavyo.

Naibu Waziri Dkt. Dugange ametoa agizo hilo wakati wa kikao kazi baina yake na watendaji wa Idara ya Afya Ofisi ya R ais TAMISEMI kilichofanyika Jijini Dodoma kikiwashirikisha pia watendaji wa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Serikali, Wizara ya Afya pamoja na Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya nchi nzima kwa njia ya mtandao.

Katika kikao hicho Dkt. Dugange amesema ni lazima watendaji katika sekta ya afya wakiri kuwa bado hawajafanya vizuri kiasi cha kutosha katika usimamizi wa ujenzi wa miundimbinu ya huduma za afya licha ya serikali kuwekeza fedha nyingi katika sekta hiyo.

“Kasi ya ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na ukarabati wa hospitali zetu za wilaya katika mikoa yetu yote 26 ya Tanzania Bara na katika halmashauri zetu zote 184, kwa kweli bado hairidhishi” Alisema Dkt. Dugange.

Aliongeza kuwa “Tuna miradi mingi na ya muda mrefu lakini bado haijakamilika licha ya kwamba imepokea fedha zote kwa mujibu wa BOQ na kwa bahati mbaya baadhi ya miradi haina mipango mikakati ya kuikamilisha, hivyo naomba sote kwa pamoja tufanye tathmini ya ufanisi wa ukamilishaji wa miradi ya ujenzi wa miradi hiyo.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Dkt. Dugange amewataka watendaji hao kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa bidhaa za afya kwenye vituo vya kutolea huduma za afya katika maeneo yao, ili kubaini mapungufu yaliyopo na kuchukua hatua za utatuzi kwa haraka na kwa wakati.

Awali akizungumza katika kikao hicho Naibu Katibu Mkuu (Afya) Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Charles Mahera amesema kikao hicho ni mwanzo wa vikao vya aina hiyo na vingi vitakuwa vikifanyika kwa njia ya mtandao ili kurahisisha ufuatiliaji wa utekelezaji wa maelekezo ya viongozi wa ngazi za juu katika kuboresha huduma za afya kote nchini.
 

Attachments

  • GDGAAwTX0AAuPG3.jpg
    GDGAAwTX0AAuPG3.jpg
    43.9 KB · Views: 1
  • GDGABquWYAA_-fI.jpg
    GDGABquWYAA_-fI.jpg
    244.5 KB · Views: 1
  • GDGABqtWsAAZQ0E.jpg
    GDGABqtWsAAZQ0E.jpg
    320.4 KB · Views: 1
  • GDGABqwXEAA7pIs.jpg
    GDGABqwXEAA7pIs.jpg
    281.6 KB · Views: 1
  • GDGABqyWIAAMMTQ.jpg
    GDGABqyWIAAMMTQ.jpg
    288.9 KB · Views: 1
Mbona haensi Rukwa miradi yote ya Afya kuanzia hospital ya Mkoa Hadi Vituo vya Afya imekwama na pesa zimeisha.
 
Tatizo sio pesa ila usimamizi,pesa zimeisha na miradi imeishia njiani
Ndo hivyo kama sio kuiba ni nini, maana kama miradi ilipelekewa pesa kwa Mjibu wa BOQ why pesa kuisha kabla ya Miradi kuisha , kwamba walipiga makadirio ya ujenzi wakiwa wapo usingizini hasa hawa wakandarasi wa iyo miradi,

Ukiona hivyo jua 10% imetembea sana na kusahau kwamba izo pesa zipo calculated katika miradi husika
 
Back
Top Bottom