Uchaguzi 2020 Polepole: CCM inawataka wagombea wote waliofeli kura za maoni kuwapigia kampeni washindi watakaokaidi kukosa teuzi!

Katibu wa uenezi wa CCM ndugu Polepole amewataka wagombea waliofeli kwenye kura za maoni wawapigie kampeni walioshinda pindi kampeni zitakapofunguliwa.

Polepole amesema CCM ni chama kikubwa tena ni taasisi ya Umma hivyo ina vyeo na fursa nyingi kwahiyo wale watakaokaidi kukampenia wenzao watakosa teuzi siku za usoni.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Haka kajamaa kamejishushia heshima sana, sasa ndio nini icho kaongea. Mbona ni kama anajipaka kinyesi usoni. Wewe mtu kashinda kura za maoni mkamkata sababu m'memuona hafai sasa teuzi gani atakayofit mtu wa aina iyo..? Halafu kwani yeye Mungu kiasi awe na uhakika watashinda mpaka anafikia hatua ya kuwatisha wenzie tena wengine kiumri ni sawa na baba yake?? Hizo teuzi hazitolewi kwa kugawa kama maandazi.
Inatosha watuachie nchi yetu, wasituvuruge kabisa.
 
Anawataka au anawaomba......

Kwa hiyo anawafokea sio..... Ngoja wamwonyeshe muziki kwamba wao sio watu wa hovyo km yy
 
Nani alisema ni kigezo cha rushwa tu ndicho kilitumika kupata wateuliwa. Kulikuwa na vigezo vingi vya kutumia kumpata anayestahili kuwakilisha wanaCCM kwenye uchaguzi wa mwaka huu. Kutotumia rushwa kupa kura za wajumbe, kuwa na uwezo wa kuwakilisha vema na kwa umakini wananchi, uzalendo usio tiliwa shaka na mambo mengine kama hayo, ndiyo yalitumika kupata nafasi kuwakilisha CCM katika uchaguzi wa 28.10.2020. Kwa hiyo si kutotumia rushwa pekee kilikuwa kigezo cha kupata nafasi ya uwakilishi kwenye uchaguzi. Upo!?

Duuuu kweli ccm kazi ipo. Hiyo inaonyesha utii huko ccm sio kwa ajili ya imani kwa chama na misingi yake, bali unatakiwa utii ili uzawadiwe cheo! Huwa mara nyingi nasema huko ccm hakuna nidhamu, bali kuna unafiki ili kupata cheo. Hii ndio inayosababisha ccm kufanya ukatili, ufedhuli, uhayawani na ushenzi wa wazi kwenye chaguzi zetu, ili kubaki madarakani kwa ajili vya vyeo.
 
Katibu wa uenezi wa CCM ndugu Polepole amewataka wagombea waliofeli kwenye kura za maoni wawapigie kampeni walioshinda pindi kampeni zitakapofunguliwa.

Polepole amesema CCM ni chama kikubwa tena ni taasisi ya Umma hivyo ina vyeo na fursa nyingi kwahiyo wale watakaokaidi kukampenia wenzao watakosa teuzi siku za usoni.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Mwambieni Polepole wenu HASITUFOKEE.
 
Katibu wa uenezi wa CCM ndugu Polepole amewataka wagombea waliofeli kwenye kura za maoni wawapigie kampeni walioshinda pindi kampeni zitakapofunguliwa.

Polepole amesema CCM ni chama kikubwa tena ni taasisi ya Umma hivyo ina vyeo na fursa nyingi kwahiyo wale watakaokaidi kukampenia wenzao watakosa teuzi siku za usoni.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Mzee naona anatangaza Teuzi kipindi hiki ambacho tunaweka kusema ni Rushwa!! yaani ukishiriki kampeni unapata UTEUZI ukigoma HUPATI.

Mambo ya kutishana!!
 
Mwambie Polepole keshaanza Serukamba kule Kigoma kahamia ACT na keshachukua fomu ya kugombea ubunge.................. pia mwambieni Membe kawaita wote waliokatwa waende ACT watapata nafasi upo wewe Polepole? akili ndogo kama kidonge cha priton
 
Katibu wa uenezi wa CCM ndugu Polepole amewataka wagombea waliofeli kwenye kura za maoni wawapigie kampeni walioshinda pindi kampeni zitakapofunguliwa.

Polepole amesema CCM ni chama kikubwa tena ni taasisi ya Umma hivyo ina vyeo na fursa nyingi kwahiyo wale watakaokaidi kukampenia wenzao watakosa teuzi siku za usoni.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Ukumbuke wagombea wengi waliofeli ni watumishi wa Umma na hapo walipo July na August 2020 mishahara hawana. Kisa waliogombea uongozi wa kisiasa ndani ya CCM. Leo unakuja na gia nyingine wakawasaidie kampeni umesahau wameponea kufukuzwa kazi? Na mishahara imechukuliwa na serikali hiyo hiyo ya chama tawala?
 
Katibu wa uenezi wa CCM ndugu Polepole amewataka wagombea waliofeli kwenye kura za maoni wawapigie kampeni walioshinda pindi kampeni zitakapofunguliwa.

Polepole amesema CCM ni chama kikubwa tena ni taasisi ya Umma hivyo ina vyeo na fursa nyingi kwahiyo wale watakaokaidi kukampenia wenzao watakosa teuzi siku za usoni.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Watumishi wa umma,kugombea uongozi ndani ya CCM mwaka 2020 imekuwa Kama janga la ugonjwa wa covid-19 kwao na familia zao. Kuwatambua waende Tena kusaidia kampeni ni kuwatonesha kidonda moyoni mwao.wakati wanasubiri October 28,wafanya Yao.
 
Hii ni kutwika mtu gunia la misumari. Sisi wajumbe tumemchagua mtu kwa kura nyingi, mkatuletea wa kura 5 kisa kaunga juhudi Mkono. Mkaacha anayetekeleza ilani na kusababisha juhudi kuonekana. Wanachama wetu hawamtaki, alitutesa katika uchaguzi uliopita, hatukulala, kutwa kucha tuko kwenye kampeni kumtetea mbunge na Rais wetu, yeye anatukana na kukashifu. Leo kawa mzuri kuliko wafia chama? Wakati huohuo wwapinzani hawamtaki, kasaliti chama Chao. Leo tuambiwe tukapige kampeni la sivo hakuna uteuzi! Hizo teuzi za kutosha waliokatwa wote zitatoka wapi? Au tutaunda taifa jipya? Hiyo siyo rushwa ya teuzi? Hiki Ni chama au kambi ya jeshi, au shule na polepole ni mwalimu Mkuu?
Wajumbe si mulionekana mkila kuku kwa mrija? Mnanyonya supu, mko na roho ngumu,
Sisi huku tumetumia kipengele cha UZALENDO uliotukuka. Mpo.
Kapigeni kampeni
 
Katibu wa uenezi wa CCM ndugu Polepole amewataka wagombea waliofeli kwenye kura za maoni wawapigie kampeni walioshinda pindi kampeni zitakapofunguliwa.

Polepole amesema CCM ni chama kikubwa tena ni taasisi ya Umma hivyo ina vyeo na fursa nyingi kwahiyo wale watakaokaidi kukampenia wenzao watakosa teuzi siku za usoni.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Mwambie polepole ajiandae tu kuwa Katibu Uenezi wa Chama Pinzani baada ya uchaguzi mkuu wa hapo October 2020
 
Back
Top Bottom