Hongera sana CCM kwa mchakato wa kura za maoni

Amani Msumari

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
1,830
976
Ndugu zangu, salamu.

Napenda kuchukua fursa hii kukishukuru chama changu kwa kuendesha vizuri mchakato wa kura za maoni kwa ngazi ya majimbo na viti maalumu. Ni imani yangu kuwa michakato mingine itaendelea vyema kwa ngazi zinazofuatia.

Ninajua zipo changamoto ndogondogo za madai ya rushwa, ukiukwaji wa taratibu n.k ila kwa leo sio lengo langu kujadili changamoto hizo. Itoshe kusema kuwa CCM imejiwekea utaratibu mzuri wa kushughulikia changamoto hizo na ndio maana mchakato utaenda mpaka ngazi ya taifa. Hongera sana CCM.

Sisi wote ni mashahidi wa utitiri wa watia nia ya ubunge kwa tiketi ya CCM. Ona mafukara, matajiri, wasanii, wasomi na wasio wasomi ukimiminika majimboni. Wavivu wa kufikiri wanaweza kumchukulia kirahisi, wenyewe wanasema poa hali hi ila kwa watu werevu hili ni jambo fikirishi. Usione vyaelea, vimeundwa.

CCM ipo, itaendelea kuwepo na kushinda chaguzi kwasababu ni chama kilichopo mioyoni mwa watanzania. Hi ni kwasababu moja tuu, CCM ni chama kinachojifanyia tathimini na kukumbatia mabadiliko chanya kutokana na wakati.

Ilikuwa vigumu sana hapa juzi Kati kwa mwanaCCM wa kawaida, asiye na pesa kupata fomu na kutia nia ya ubunge. CCM ikakaa na kutathimini, ikaja na utaratibu wa sasa na motokeo tumeyaona. CCM imeonesha kuwa inapendwa na makundi yote. Wakati Kuna vyama vinatafuta wagombea, hali ni tofauti kwa CCM. Makumi kwa mamia walijitokeza.

Hi sio bahati mbaya, uongozi mzuri umeleta haya. Hongera mwenyekiti wa CCM taifa na Rais wa JMT Dr. ndugu John Magufuli na viongozi wote akiwemo mzee Mangula, komredi Dr Bashiru, ndugu Polepole, ndugu Heri n.k. CCM imeimarika zaidi katika uongozi wenu.

Tunawatakia heri na fanaka katika kazi iliyo mbele yenu. Tutashiriki kwa hali na mali katika kampeni na kuhakikisha CCM sio tuu inapata ushindi bali inapata ushindi wa kishindo kizito.

Vijana, wazee na akina mama ambao sio wanaCCM, karibuni CCM, karibuni sehemu salama

#tukutanekwenyekampeni
 
We ni mpuuzi mkuu ccm unaipaje hongera wakati uchaguzi karibu 90% ulikuwa ni Rushwa pekee. Halafu unaropoka eti changamoto ndogondogo kama rushwa.
Ndugu yangu acha hasira, tulia na utulize kichwa, akili na moyo wako.

Tofautisha rushwa na madai ya rushwa. Halafu naanzaje kuacha kukisimu chama changu kwa mazuri inayofanya? Kama wewe unashida na mambo mema basi unahitaji maombi.

Kuropoka na kuongea ni vitu viwili tofauti. Tafuta Pepsi, umeshalipiwa. 90% umeiripoti wapi? Uko wapi uzalendo wako? Kumbuka sisi wote tunawajibu was kupambana na rushwa, hivyo nakushauri katoe ripoti kwenye vyombo husika.

Pia nakukaribisha kwenye ofisi yoyote ya CCM ukatoe hayo malalamiko. Tambua tuna vikao vitaendelea soon baada ya kumpumzisha mzee wetu. Karibu utoe taarifa, itafanyiwa kazi.
 
Ila mlungula ulitawala aisee kila mahali yaani. chama chetu inabidi tujitathimini kwa kweli vinginevyo ni sawa na kuziba nyufa kwa makaratasi.

Kina Madaraka waliambulia kura namba ya kiatu imagine!
 
Mbona umetoka bilabila Kama jina lako? Rudia kusoma kwa utulivu kwani inaonekana una hasira na jazba. Nukuu hicho kipande nikupe ufafanuzi. Dawa itawaingia tuu
Kama unasema Rushwa ni "changamoto ndogo ndogo" unadhani nani wa kuendelea kusikiliza mpambaji!?
 
ila mlungula ulitawala aisee... kila mahali yaani. chama chetu inabidi tujitathimini kwa kweli vinginevyo ni sawa na kuziba nyufa kwa makaratasi.

kina Madaraka waliambulia kura namba ya kiatu imagine!
Madaraka Kama Madaraka ni mtanzania kama walivyowengine. Wajumbe wanahaki ya kumchagua yule wamtakaye.

Kama mwanaCCM nakushauri upeleke hizo tuhuma kwa ngazi husika za chama na Takukuru kwa eneo uliopo
 
Hapa ndipo mnapokosea. Tafuta muda wa kumfahamu mtu kabla ya kuongea.

CCM inaendeshwa kwa ruzuku, michango ya wanachama na wasio kuwa wanachama (wenye nia njema) na miradi yake mbalimbali.

Kwataarifa tuu, namba yangu ipo na inafahamika kuliko unavyodhani wewe. Aidha mimi sio wa kujiuliza CCM itanifanyia nini. Mimi nahakikisha nafanya kwa CCM kwa hali na mali.

Pokea taarifa hiyo

Hiki kitu wanakisahau sana, bora umemkumbusha.
 
We ni mpuuzi mkuu ccm unaipaje hongera wakati uchaguzi karibu 90% ulikuwa ni Rushwa pekee,
Halafu unaropoka eti changamoto ndogondogo kama rushwa.
Weka ushahidi hapa wa asilimia hiyo 90% kuwa kura za maoni ziligubikwa na rushwa.

Kama mgombea wako hakupata kura ulizozitaka haimaanishi hakubaliki bali alibugi kwenye ushawishi.

Jambo lingine ni kwamba mchakato ulikuwa wa uwazi na bado taratibu za kupata wagombea zinaendelea
 
Back
Top Bottom