UCL
Member
- Aug 18, 2020
- 8
- 6
Ukweli watumishi hawa wanaumia sana. Yawezekana waliotoa adhabu wakaona kawaida tena sana lakini kwa kifupi wanyonge hawa na familia zao wanalilia mioyoni.Hiyo ni ngumu sana na asahau hilo jambo.
Yaani Watumishi wa Umma ambao ni makada wa CCM zaidi ya elfu 7 waliojitokeza kukipigania chama huko majimboni - Serikali hii hii ya CCM imewanyima mishahara ya miezi miwili ( mwezi wa saba na huu wa nane), leo hii eti waende wakakipigie kampeni CCM huko majimboni, hao makada anawaona ni wajinga enhee?
Sasa subiri waone kitachotokea. Mtu atoke Dar aende Mbeya kukipigia kampeni CCM wakati Mshahara hana, nguvu hiyo ataitoa wapi?
Mwambie pole pole aache ufala ! Wao wasubiri maana dharau zao sasa zitawatokea puani.