Ilipoishia... .
..nikachukuwa simu yangu
nakutuma meseji kwa John..
'...John mpenzi, angalia chini ya
uvungu wa kitanda chako,
Kama ulidhani umenitoa bikra
hapa umechemsha, nakifupi tu, NIMESHAATHIRIKA...
'
Endelea... Nilipomaliza kuituma tu, nikaizima simu yangu
nakuirudishia kwenye kipochi huku nikifurahia
kitendo nilichomfanyia John,
"..hapa na bado, nitahakikisha nimeumaliza ukoo
wao wote...!"
Nilijisemea peke yangu huku nikipanda daladala ya kuelekea posta kwa usiku ule..
Sikuumia moyoni kisa John ameniacha bali
nilikuwa nafuraha ya kumuambukiza ukimwi..
"..mh huenda sina hata huo ukimwi, halafu najisifu
sifu, embu ngoja kesho nikitoka kwenye kipindi
asubuhi niingie hospitali.." Bado nilikuwa nikijiuliza nakujijibu mwenyewe
huku daladala ikikatiza maeneo ya magomeni
kuelekea posta..
Mwendo wa kama dakika 20 ulitosheleza
kunifikisha pale chuoni 'Cbe ndani kabisa ambapo
ndipo hosteli zetu zilipo, Nilipofika tu kwenye 'rumu' yangu sikumkukuta
Aisha hivyo niliamini tu atakuwa kaenda kujirusha
viwanja hivyo breki ya kwanza nikabadilisha nguo
zangu nakuvaa kanga kisha nikaingia bafuni
nakujisafisha zile 'tomato sauce' bandia zilizokuwa
kwenye ile bikini yangu pia kwenye naniii yangu, Nilipomaliza nikarudi mpaka rumu nakuiwasha ile
simu yangu.
Meseji kama 5 ziliingia mfululizo na zote zilikuwa
zimetokea kwa John, alikuwa akinitukana na
kulaani kitendo nilichomfanyia nakunihakikishia
ama zangu ama zake siku akinishika, nilizisoma zile meseji kisha nikafyonza kwa dharau nakuzifutilia
mbali,
"..akijifanya mjanja namfanya kama nilivyomfanya
kaka yake 'Jerry..' eti anataka kuoa bikra..?, bikra
aende huko kwao Pemba tena vijijini na umalaya
wake ndio atapata mabikra.." Nilizungumza kimoyo moyo huku hasira kali
iliyoambatana na dukuduku rohoni vikinishika
nakutamani nimrudie usiku huu huu.. ~ Baada ya wiki 2 ~ Nilivalia nguo ya 'baibui' huku nikijifunika mpaka
eneo la paji la uso, kama muislamu vile sikutaka
kusindikizwa na mtu yeyote zaidi ya kubeba
kamkoba changu nakuelekea hospitali ya mnazi
mmoja tena kwa kujiamini...
Niliingia mpaka ofisi ya dokta niliyokuwa nikimfahamu nilimweleza nia yangu yakuja kupima
kisha akanichukuwa damu nakwenda kuipima.
Haikupita muda akarudi,
"..enh niambie dokta imekuwaje mzima.."
"...unaweza kuniambia huyo mtu mara ya mwisho
kukutana naye kimwili ni lini..?" "..dokta zimeshapita kama wiki mbili sasa.."
"...matokeo yako haya hapa hauna tatizo lo..."
"..kweli dokta..?"
"..yeah ni kweli kabisa haujaathirika ila sasa we leo
rudi nyumbani halafu njoo baada ya wiki mbili,
kwani magonjwa kama ukimwi ni mpaka mwezi upite ndipo vijidudu vionekane.."
Nilichukuwa yale majibu yangu japokuwa bado
nilikuwa kishingo upande nakutokumuamini
kabisa dokta japo huwa ananitibia mara nyingi
niumwapo..
Nilienda tena hospitali nyingine lakini majibu yalinionesha nimeshaathirika,
Njia nzima nilikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa,
akili, ukichanganya na hasira kali ilinituma niende
mpaka hospitali ile aliyokuwa amelazwa Jerry pale
'Ocean road' napo nilipofika ile wodi sikumkuta na
alikuwa amesharuhusiwa kama siku mbili zilizopita..
Kwakuwa nilivalia 'baibui' ilikuwa ni vigumu
kuonekana hivyo nikapanda daladala mpaka
msasani alipokuwa anaishi Jerry, nilibadilisha sauti
nakuwa nyembamba sana hivyo mlinzi
akaniruhusu nikapita pale getini mpaka sebuleni, nikamkuta Jerry yupo kwenye kibaiskeli spesho
kwa wagonjwa huku akiwa na wanaume wanne
na wanawake kama sita hivi lakini John
hakuwepo,
Sikuwa muongeaji wala kuonesha mapepe yeyote,
niliwadanganya kuwa mie ni jirani yao japokuwa sijaamia muda mrefu maeneo haya huku nikijitahidi
kuizuia hasira kila nikimwangalia Jerry na
nikikumbuka nilivyopima ukimwi nakukutwa nao,
"..haya yote umeyataka wewe Jerry.."
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikimkazia Jerry
macho ya hasira.. "..nimeanza na Jerry na sasa hivi ni zamu ya
mmojawapo kati ya hawa.."
Niliongea mwenyewe huku nikiwatolea macho
wale wanaume waliokuwa wanamuuguza Jerry..
Haraka haraka nikaaga nakutoka nje, ile namuaga
mlinzi, akatoka ndani mzee mmoja wa makamu huku mkononi kamshika mwanae..
"..bado hujaondoka tu.."
Yule mzee aliniambia kiutani huku akiwa na lafudhi
ya ki pemba,
",mie mbona nimeshafika, nyumbani kweu jirani tu
hapo, sema naifikiria safari yakulekea kariakoo sasa hivi.."
Nilimtega maksudi kumwambia hivyo kwani
alikuwa na gari lake,
"..ok, mie kwangu magomeni, twende nitakuacha
magomeni uchukue daladala,"
Niliingia siti ya pembeni yake na mtoto wake alikuwa siti ya nyuma kabisa, huku nikijidai na
kujishembendua ovyo..
"..mtoto wako mzuri, anaitwa nani..?"
nilianza uchokozi taratibu bila ya yeye kujijua
"..anaitwa Latifah.."
"..ohh anajina zuri, hivi we na Jerry mpoje..?" "..Jerry ni mdogo wangu anayenifuata akitoka
Jerry anafuata John na ndio mtoto wa mwisho
kwenye familia yetu..
"..kazi imekwisha, sasa hapa ndio simwachi ng'o,
haijalishi ameoa au hajaoa au anamtoto sijui
anajiheshimu.., hapa kwangu kaisha...." NJia nzima nilikuwa nikimwangalia kwa jicho la
kuibia ibia huku matamanio yangu yakichukuwa
nafasi yake, mpaka alipofika magomeni pale
usalama, akapaki gari yake pembeni,
"...mie naishi hapo kituo cha mbele 'magomeni
mwembe chai' lakini natumai utapanda daladala pale za kwenda kariakoo.."
"..wala usijari, kuna kitu naenda kununua mara
moja halafu nakurudi kwangu 'Ilala'.."
Nilimdanganya tena kwa kujiamini, ile hali ya ujasiri
nilikuwa nayo bila hata kuwa na mshipa wa aibu..
"..amh nimesahau kujitambulisha, mie naitwa Grace ni mfanyakazi mwenzake na Jerry.."
"..ahaa, ni vizuri binti, mimi kama unavyomwona
mwanangu hapa pembeni, naitwa Baba Latifah au
ukipenda niite Ustadhi Juma..."
"...ok, usijali labda kwa hapa sina 'business card'
zimeniishia, labda ungenipa namba yako ya simu na mimi nikupe yangu.."
"..ooh, wala usijari Grace, namba yangu ni
0713133633.."
Niliichukuwa nakumpa namba yangu huku
nikiondoka na uhakika wa hali ya juu mpaka
kwenye daladala ziendazo posta na siyo tena kariakoo kama nilivyokuwa nimemdanganya hapo
awali,
"..na hivi leo sijaingia darasani, lakini Aisha
atanielekeza walichofundishwa leo.."
Niliendelea kuongea mwenyewe huku nikiwa
ndani ya daladala maeneo ya 'fire' karibu na kituo cha 'akiba' ambapo ndipo ninaposhukia kwenda
chuoni kwetu 'cbe'.
Nilipofika tu 'hostel' breki ya kwanza ilikuwa
nikuvua ile mi nguo ya baibui kwani ilikuwa
imenijazia joto sana,
"..shosti kwa mishemishe, hata hutulii..?" Alikuwa Aisha akiongea na mimi.
"..nitulie wapi wakati mjini kuna mambo mengi!
Haya embu niambie mlichofundishwa leo..?"
"..leo tumefundishwa somo moja tu.."
"..lipi hilo"
"..Entreprenuer.." "..na mwalimu wa 'Law' hakuingia..?"
"..yule katuambie mpaka wiki ijayo hivyo tujiandae
kwa 'test' kutoka kwake.." **** Usiku wote akili ilikuwa ikimuwaza Baba Latifah,
kila muda nilipotaka kumtumia meseji nilikuwa
nasita nakuhisi huenda akaipokea mke wake
nikaharibu kila kitu nakumkosa kabisa, hivyo
nikajilalia zangu mpaka asubuhi..
Nilikuwa nakipindi asubuhi hivyo nilitumia masaa mawili nikawa sina tena kipindi,
"..kwa muda huu kama hayupo ofisini sijui.."
Niliichukuwa simu yangu nakumpigia baba Latifah,
lakini iliita tu nakukatwa hapo hapo,
Woga ulianza kuchukuwa nafasi yake katika mwili
wangu huku akili ikinituma kuwa huenda ameshajua mchezo wote ninaoufanyaga..
Nikiwa ndani ya dimbwi la mawazo kwa muda
mfupi mara simu yangu ikaita, harakaharaka
nikaangalia jina lilikuwa ni baba Latifah, nikaipokea
kwa pozi na tabasamu zito,
"..hallow," "..yeah, nani Grace?"
"..ndio unaongea na Grace.."
"..nisamehe binti, nilikuwa naendesha gari ndio
maana niliikata simu yako lakini usijari, nimeshafika
na kwasasa nipo hapa hapa ofisini kwenu.."
"..uko wapi baba Latifah..?" Niko hapa 'aiport' unapofanyia kazi na mdogo
wangu Jerry, na nimekuja kufuatilia pesa zake kwa
ajili ya matibabu, wewe uko kwa wapi..?"
Nilijihisi mdogo ghafla kama kidonge cha 'piriton'
huku nikiamini kwa asilimia zote nitakuwa
nimeshaharibu haswa akiulizia jina la Grace akaambiwa hamna jina hilo nitakuwa simpati tena.
Hapo hapo akili yangu ikachemka ghafla nakupata
wazo nakumjibu..
"..nimetoka ofisini na nipo posta kuna bidhaa
tumeleta hivyo kwa leo sintoweza kurudi ofisini
mpaka kesho, lakini nahitaji kukuona leo jioni kuna vitu ninavyo nataka umpelekee mgonjwa
'Jerry' mie nimebanwa sana.."
"..wala usijari binti, wewe niambie nikukute
wapi..?"
"...kwa sababu nitakuwepo posta mpaka jioni
sana, nitakutafuta kwenye mida ya saa kumi na mbili, samahani kwa usumbufu lakini.."
"..kuwa na amani kabisa binti yangu.."
Nilimaliza kuongea na simu huku furaha kubwa
nikiwa nayo, nikatafuta nguo ya kuvaa ambayo
itaendana na zile za wafanyakazi wa 'airport'
Hatimaye nikapata kisketi cha bluu na shati jeupe lililonipana na nikachukuwa kikoti cha Aisha cha
bluu nachenyewe chakubana na kisha nikafunga
funga mtandio wa bluu ndio ikawa kama tai..
Saa kumi na mbili kasoro nilikuwa nipo 'Subway'
posta nikiwa nimeifunga kanga yangu ndani ya
karatasi la kuhifadhia zawadi na juu yake nikiandika maneno 'Get well soon Jerry' (ugua pole
Jerry) huku nikimsubiri baba Latifah...
Nilimpigia simu kujua amefika wapi,
"..hallow, nipo hapa 'subway' posta nakusubiri.."
"..nami nakaribia nipe dakika kama kumi.."
Sikusubiria sana akawa ameshafika, nilijifanya ninaharaka sana na nimechoka na mizunguko
toka asubuhi nilipotoka na wenzangu kumbe wote
uongo..
"...pole sana na kazi, ndio majukumu yalivyo.."
"..chukuwa hii ni zawadi kwa Jerry ataifurahia sana
akiifungua na utamwambia kuwa imetoka kwa wafanyakazi wenzake.."
Aliichukuwa,
"..ok, kwakuwa umechoka sana wacha
nikusogeze mpaka karibia na kwako, uliniambia
unaishi wapi tena..?"
"..Ilala boma.." Giza lilikuwa limeshatanda, tukaingia ndani ya gari
lake, Nikamuwahi kabla hajaliwasha nikamshika
mkono, akashangaa..!!
"...najua umeoa na una mtoto, ningependa leo
nikucheleweshe kidoogo kurudi kwako.."
Baba Latifah alikaa kimya huku akihema juu, hapo hapo nikavua kikoti changu nakusingizia joto..
Akiwa bado ananishangaa nikaanza kuvua
vishikizo vya shati huku kisketi nikikipandisha kwa
juu nakuachia mapaja wazi... Inaendelea saa 4 usiku………