Play Gal ( Tina zoa zoa)

Play Gal ( Tina zoa zoa)

Ilipoishia…
Nilihuzunika sana nakuanza kuilaumu nafsi yangu
kwa kutokufikiria. Nikiwa bado kwenye mawazo
huku watu wakinishangaa mimi na huyu Mama.
Mara huyu Mama akatoa sauti ya kuamuru kitu.
“.. jamani mapolisi binti mwenyewe ndio huyu
hapa..!!, mchukuweni tumpeleke kituoni..” Kumbe na mapolisi walikuwa wamenizunguka
eneo lote nililokuwa nimezungukwa na watu
ambapo walikuwa wamevalia nguo za kiraia.
Walinichukuwa nakunipiga pingu huku umati wa
watu ukinisikitikia kwa kitendo nilichokifanya cha
kumuua mchungaji wao mchungaji James..
'
Sasa endelea…
“..inuka twende hukoo..!!, husikii..?”
Machozi yangu hayakuwa mbali na uso wangu.
Yalianza kunibubujika huku nikijifanya mbishi na
king’ang’anizi wa kutokuinuka pale kwenye
benchi. Ule umati wa watu ukazidi kuongezeka
mara mbili yake nakuanza kupiga makelele ya kuwachochea wale mapolisi huku baadhi yao
wakiangua vicheko vya hapa na pale. Sasa Tina
mimi nikawa sina ujanja zaidi yakuendelea
kushikilia benchi lile la kukalia wageni nikibakiwa
na butwaa.
“..jamani, sio mimi niacheni..?, mmenifananisha jamani..?”
“..akufananishe nani mshenzi mkubwa wewe..? na
leo ndio utaenda kuozea jela Malaya wewe..?”
Nilijikuta mwili wangu wote unakosa nguvu huku
mapolisi wakinibeba juu juu kama vile mzoga wa
mnyama tena mnyama mkubwa. Walinipiga kwa ubishi wangu wakugoma kunyanyuka kisha
wakaniingiza ndani ya gari yao ya kipolisi huku ule
umati wa watu pale stendi ukiwa pamoja nao
kunisindikiza kwa makelele na vicheko na baadhi
kuhuzunika na nadhani walikuwa wakimpenda
sana mchungaji James. “..kama kufa wacha nife leo leo tu..! Sitapenda
nikaozee jela angali bado kijana hivi..?”
Nilijisemea kwa sauti ya chini chini nikiwa ndani ya
ile gari ndogo ya polisi huku baadhi ya polisi
wakiwa wamenizunguka chini ya ulinzi mkali na
mikono yangu ikishikamana vya kutosha na pingu. Zile nguo zangu zote nilizokuwa nimezivaa nilihisi
kama zimelowa tena chapa chapa na si kwa maji
bali kwa jasho na kojo lililokuwa likinitoka ovyo
kwa woga wa hali ya juu likiendelea kupenyeza
ndani ya nguo zangu zoote.
Kila mtu alikuwa akiendelea na shuguli zake. Hakukuwa na baridi sana na wala jua lilichelewa
kutoka. Mawingu yaliendelea kuvutana
nakuashiria dalili zote za kushuka kwa mvua lakini
upepo mkali uliokuwa ukivuma kutoka mashariki
kwenda magharibi ndio uliosababisha kukatisha
mvua. Makaratasi pamoja na risiti za mabasi zote zilikuwa zimejaa mavumbi yaliosababisha na huu
upepo uliojaa vumbi. Milango pamoja na madirisha
navyo havikuwa mbali katika kupiga makelele.
Kwa sasa macho yangu yalikuwa yamenitoka na
niliangaza huku na huku ilikuvuta japo
kumbukumbu kujua ni sehemu gani hapa nilipo. Nilijiangalia tena mara mbilimbili nguo zangu kama
zimelowa lakini ndio kwanza zilikuwa kavu tena
zilizojaa ubaridi.
“..Dada..?, basi limeshafika vipi huendi tena..? basi
hilo hapo mbele yako limetokea Kigoma..”
Amani na furaha tele iliniingia ndani ya moyo wangu nakuanza kuamini kuwa kumbe vyote vile
nilivyonitokea muda si mrefu haikuwa kweli bali
ilikuwa ni ndoto. Eti mpaka mmama mmoja akanijia
tena pamoja na mapolisi wakanichukuwa
nakuacha umati wa watu ukipiga makelele kwa
vicheko. Nilijisachi vizuri mifukoni mwangu kuangalia kama zile hela nilizochukuwa kwa
mchungaji James bado zipo. Kwa bahati nzuri zote
zilikuwepo. Nilitoa shilingi elfu thelathini
nakumkabidhi konda kisha akanikatia tiketi ya
kuelekea Dar es salaam.
Njia nzima hadi tunafika Singida bado nilikuwa sijiamini amini Tina mimi. Ndoto niliyokuwa
nimeiota ilishanijenga tena vibaya ndani ya
halmashauri ya ubongo wangu nakuona sasa nipo
katika wakati mgumu. Sikutaka tena kufumba
macho kwani niliamini nitaanza tena kuziota zilie
zile ndoto mbaya na nitaumbuka humu kwenye basi Tina mie. Siti niliyopata ilikuwa ni ya dirishani
na tena nilikuwa peke yangu kutokea Mwanza
mpaka tulipofika Dodoma ndipo abiria mwingine
akapanda na kukaa pembeni yangu. Alikuwa ni
Mmama tu na tena alikuwa na mtoto mdogo
anamyonyesha. Mwili wangu wote ukaanza kunisisimka kila nikimwangalia yule mtoto.
Alikuwa ni mzuri sana kuanzia macho yake,
masikio na hata mdomo wake. Kila mama yake
alivyokuwa anambembeleza ndivyo na mie
nilikuwa nazidi kusisimka mwili. Hisia kali zilinivuta
mpaka nikakumbuka kwa jinsi nilivyoathirika na ukimwi na tena kuhusu kupata mtoto nisahau
kabisa milele yote kama alivyoniambia dokta.
“…Jerry..?? Jerry..?? Kwanini Jerry umenifanyia hivi
mie..?? Kwanini..?”
Taaratibu wimbi la matone ya machozi likaanza
kunidondoka huku nikiendelea kumwangalia Yule mtoto. Ni Jerry ndio alioaharibu maisha yangu yote
japo ni tamaa zangu za mwili ila amechangia kwa
kiasi kikubwa kuniharibu kimaisha na kimasomo
kwa ujumla. Kwanza yeye ndie alieniambukiza
ukimwi. Pili ndio alionisababisha mpaka kwa hasira
niache masomo nakuanza kudili na ndugu zake nao kuaambukiza.
“..alaaniwe Jerry huko alipo..!! Na ole wake nikifika
Dar..?”
Nilijikuta uzalendo umenishinda nakuanza
kuropoka ndani ya basi. Kitendo changu cha
kuropoka japo kwa sauti ya chini chini kilinifanya nianze kujishtukia lakini kumbe hakukuwa na mtu
yeyote aliyeniangalia ama kunishtukia. Hata yule
mama ndio kwanza aliendelea kupekuwa pekuwa
vitu vya mtoto wake vizuri nakuvipanga. Mwendo
wa masaa matano na nusu tulikuwa tumeshapapita
Morogoro na kwa muda huu tulikuwa tukiitafuta Chalinze. Akili yangu yote sasa nilikuwa
nimeielekeza kwa Jerry ambaye ndio chanzo cha
kuharibu maisha yangu kwa ujumla.
”..nitahakikisha nimemuua mmoja mmoja kama
nilivyomuua mchungaji James..”
Niliongea kimoyo moyo huku nikiikaza sura yangu kwa hasira ya hali ya juu. Kwa muda huu yule
mtoto mchanga aliyekuwa akilia alikuwa
ameshapitiwa na usingizi mkali. Yule mama alikuwa
kimya akijisomea kitabu chake huku akihuziunika
na kucheka hapo hapo kwa alichokuwa
akikisoma. “..mmhh kwa kweli hii hadithi ni nzuri sana sijawahi
kuona..”
Alinigeukia nakuniongelesha huku akiwa
kaendelea kushikilia kitabu kile cha hadithi.
“..kwani kikoje..”
“..kinaitwa ‘SITAKI TENA’ yaani hadithi ya humu ndani mhh..”
“..ikoje kama za shigongo..”
“..hapana hii ina muundo fulani hivi lakini inavutia
na kuteka hisia zangu. Tangu nimeanza kuisoma
nyumbani Dar es salaam bado sijaimaliza na haipiti
muda naendelea kuisoma tena, nimekuja huku Dodoma njia nzima bado naendelea tu kuisoma na
ndio kwanza bado kurasa kama arobaini ndio
niimalize.
“..inaonekana ni ndefu eenhh..?”
“..anhh ndefu sana..!!, ni ‘novo’ kabisa hii. Yaani
kuna binti humu ndani anaitwa Levina. Maskini amepata shida toka mdogo mpaka amekuwa bado
anaishi katika mazingira magumu tu..”
Kuanzia Chalinze njia nzima ikawa ni yule mama
ananihadithia ile hadithi ya Sitaki Tena. Nilianza
kutekwa hisia zangu kwani baadhi ya matukio
aliyokuwa amefanya yameendana na mimi kabisa. “..enhee ikawaje sasa huyo Levina..”
“..yaani hadithi inavyoanza Levina akiwa bado
mdogo sana anacheza rede na wenzake na kwa
bahati mbaya na haraka haraka kimchezo, Levina
anaokota jiwe nakumrushia mwenzake huku
akidhania ni mpira. Basi lile jiwe linamfikia mwenzake kwa nguvu nakujikuta mwenzake
akikata roho pale pale. Sasa hapo ndio hadithi
inaanza sasa..”
“ennhh, nipe uhondo japo kidogo..”
“..mkasa unaanzia anapelekwa rumande. Huko
mapolisi wa zamu wanambaka na kuharibu usichana wake. Kesi yake ilikuwa inasua sua kwani
baba yake alipoteza nguvu ubavu mzima kwa
mshtuko hivyo kitendo cha kufuatilia kesi kikawa
chini ya mama yake na baadhi ya mawakili
waliokuwa wanamsaidia. Mwisho wa siku levina
akatumikia kifungo cha maisha gerezani..” “..Mungu wangu..!!, ikawaje sasa..?”
“..hakukuwa na ujanja tena ikabidi asafilishwe
mpaka kwenye gereza la watoto watukutu la
mbeya amabapo ndipo maisha yake yakaanza
upya..”
“..pliiz..!! pliiz..!!, nakuomba uniazime niendelee kupata uhondo halafu tukifika Dar es salaam
nitakuachia, wewe si cha kwako,?..”
“..usijali..!!, chukuwa, endelea hapa nilipomaliza
kukuhadithia..”
Akili yangu yote ikawa imebadilika vya kutosha.
Mawazo yangu yote nikayahamishia kwenye hii hadithi ya ‘SITAKI TENA’ iliyokuwa imetungwa na
mwandishi maarufu na ninayempendaga siku zote
‘’ Nilishawahi kusomaga hadithi zake
kipindi cha nyuma facebook ila hii sijawahi
kuisoma. Mwendo wa masaa mawili na nusu
ulinitosha sana kuisoma hadithi robo nzima ya kile kitabu huku nikitamani kujua mbeleni. Sikuwa na
ujanja tena kwani tulikuwa tumeshaingia ndani ya
hili jiji la Dar es salaam. Giza lilikuwa limeshatanda
muda mrefu tu kuashiria kuwa ni usiku japo
sikufahamu ni usiku wa saa ngapi. Nilimkabidhi
yule mama kitabu chake. Alikuwa na mizigo mingi chini ya basi hivyo akaniomba nimshikie mtoto
wake na mkoba wakati wakushuka ili ahakikishe
mizigo yake asije akaibiwa. Kwa upande wangu
sikuwa na mzigo wowote hivyo nikamsaidia
kubebelea mkoba wake na mtoto wake
nikambeba kifuani kama mwanangu vile kisha nikaongozana na huyu mama kushuka.
Kitendo cha kutangulia kushuka yule mama
akapokelewa na mwanaume huku akikumbatiwa.
Halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi haraka
haraka nakutambua kuwa inawezekana akawa
ndio mumewe. Sikumuona vizuri usoni kwa sasabu ya kukumbatiana na yule mama pia giza giza na
mwanga ulikuwepo kidogo tena ile wa ndani ya
basi japo kwa sauti zao ndizo ziliweza kupenyeza
ndani ya ngome ya masikio yangu.
“..mwanangu Brayan yuko wapi..?”
“..Si huyo hapo amembeba huyo dada..?” Aliongea yule mwanaume kwa sauti ya ukali naya
nguvu akimuuliza mkewe huku akiacha
kumkumbatia nakuangaza huku na kule ndipo
jicho lake likakutana moja kwa moja na langu.
“…Tinaaa..? wewe si Tina wewe..?”
Alikuwa ni yule yule mvulana niliokuwa nikimchukia maishani mwangu na ndio yule
aliyenipotezea malengo yangu ya kimaisha yote. Si
mwingine bali alikuwa ni Jerry. Na kumbe huyu
alikuwa ni mtoto wake. Nilijiuliza maswali mengi
papo hapo japo sikupata jibu kwani
ninavyokumbuka kuwa Jerry aliambiwa kuwa hawezi kumzalisha mwanamke kutokana na
kwanza kuathirika na ukimwi na pili tulishawahi
kumkata kata nanii yake na viwembe mimi na rafiki
yangu Aisha na tulihakikisha tumeikata mirija yake
yote inayopitisha mbegu za uzazi na hadi akazimia
na kuwahishwa hospitali kipindi cha nyuma. “..Tina mlete mwanangu nimesema..?”
Kwa sasa Jerry alikuwa amebadilika nakuwa mkali
sana huku akinisogelea karibu. Mke wake alikuwa
akimvuta kana kwamba aniachIe nakuwa mimi ni
mtu mzuri tu tangu nimetoka naye safarini. Kila
wakijibizana Jerry na mkewe ndipo na mimi nikapata nafasi ya kuwazunguka mpaka kwenye
basi jingine nikalizunguka tena basi jingine
nakuwatoroka pale pale pale huku nikiwa
nimemshikiria mtoto wao.
“..ama nife mimi Tina..!, au Jerry..! sitamrudisha
huyu motto kamwe..!!” Nilijisemea kwa sauti ya chini chini huku
nikitokomea mpaka kwenye geti la nje kabisa na
nilipofika nje kabisa ndipo kwa mbaali nikasikia
tangazo kuwa kuna dada ametoroka na mtoto na
amevaa suruali ya jinsi akiwa na mkoba mweupe.
Eti akamatwe popote alipo humu ndani ya stendi.. “..It’s too late Jerry..!! (Jerry umeshachelewa..!!)”
Niliongea kwa kujidai huku nikipanda dalaladala
yakuelekea Mbagala na nisijue naenda kwa nani na
wala itakuwaje huko nieandapo na huyu mtoto..
Ile hali ya woga na kutetemeka ilishaanza
kutoweka ndani ya akili na mwili wangu kwa ujumla. Na sasa akili yote nilikuwa nimeielekeza ni
jinsi gani nitaishi na huyu mtoto huko niendako.
Nilijiona mtu tofauti sana kutokana na kuwa na
mtoto japo si wakwangu lakini kwa jinsi
nilivyokuwa nambembeleza akilia hata akicheka.
Nilikuwa nacheka naye kila abiria allikuwa akinishangaa nakuona ni jinsi gani nilivyokuwa na
kipenzi na mtoto wangu japo ukweli si mtoto wa
kumzaa mimi. Ilinichukuwa kama lisaa mpaka
kufika Temeke. Japo daladala ilikuwa inaelekea
mbagala lakini kwa upande wangu kutokana na
kuchoka sana mwili na pia mtoto alikuwa kashajisaidia hivyo nilitakiwa nimbadilishe nguo
nikaamua kushukia Temeke nakutafuta gesti ya
bei nafuu uswahilini. ******* ‘Mji mwema guest house’ ndio gesti niliokuwa
nimefikia Tina mimi na huyu mtoto wa Jerry
niliomuiba. Kwa sasa alikuwa amelala hivyo
nilipoingia tu chumbani nilimvua nguo zote kisha
nikaifungasha vizuri ile pampasi yake iliyokuwa
imejaa kinyesi pamoja na mkojo nakuiweka katika mfuko wa rambo nakuvitupia kwa pembeni.
Nilipomaliza kumsafisha nilichukuwa pampasi ya
akiba ambayo ilikuwa katika huu mkoba mkubwa
niliouchukuwa kwa mama yake na huyu mtoto.
Usingizi ulikuwa wa shida sana kwangu nadhani
hii yote ni kutokana na kuchoka sana mwili na hata akili yangu. Mawazo mengi niliokuwa nayo na
mipangilio yangu ya baadaye kuhusu huyu mtoto
ni kati ya vitu ambavyo bado vilisumbua sana
katika halmashauri ya kichwa changu. Nilifanikiwa
kuupata usingizi kwa tabu sana na nilipokuja
kushtuka usiku wa manane napo sikuwa na saa wala simu hivyo sikuweza kugundua imetimia
muda gani lakini giza bado lilikuwa ni tororo. Mtoto
alikuwa anakoroma kuashiria kuwa alikuwa na
usingizi sana. Nilitamani japo kupata tena usingizi
kwa mara ya pili lakini bado kichwa changu
kikaendelea kuwa na mawazo mgando ya kumuwaza Jerry kwa vitendo alivyowahi
kunifanyia kipindi cha nyuma.
“..Piga ua.! Lazima nije kumtafuta Jerry na nimuue
kabisa kwani adhabu ya kumchukulia huyu mtoto
wake haitoshi.. yeye ndio aliofanya mpaka
nimepoteza ramani ya maisha yangu kwa ujumla..” Nilijikuta naropoka mwenyewe kitandani
nakufanya mpaka mtoto ashtuke nakuanza kulia.
Nilimtoa pale kitandani nakuanza kumbembekleza
lakini haikusaidia kitu zaidi ya kuzidisha kulia zaidi.
Nilimchukulia japo ile nyonyo yake ya kunyonyea
maziwa ambapo ilibakiwa na vimaziwa kidogo alivyokuwa amevihifadhi mama yake kwenye
mkoba lakini bado haikusaidia kitu chochote.
Machozi yalikuwa mengi sana nakunisisimua mwili
mzima kila nilipokuwa nikimwangalia huyu mtoto.
Alibadilika mwili nakuwa mwekundu kutokana na
kulia kwa muda mrefu. Nilijitahidi kumbembeleza hata kwa kutoa maziwa yangu nakumdanganyish
ia kama namnyonyesha ndipo akanyamaza
nakuanza kunyonya maziwa yangu ambayo
kiukweli hayakuwa yakitoa chochote.
“..Sasa huuuuyu mtoto nimuite jina gani..?”
Nilibaki nimeduwaa mwenyewe huku nikijisikia raha kwa kunyonywa maziwa yasiotoka na kale
katoto mpaka akapitiwa tena na usingizi. Nilijiuliza
maswali mengi sana juu ya jina la huyu mtoto
kwani Jerry mara ya mwisho alimuita Mama yake
na huyu mtoto ‘Mama Brayan’ hivyo moja kwa moja
huyu mtoto ndio atakuwa ‘Brayan’. Lakini kwa upande wangu inanibidi nimbadilishe jina huyu
motto haraka iwezekanavyo.
“..Adrian..!!, Adrian..!! yeees..! nitamwita Adrian tu
haina hata ulazima wa kumuita jina la nyumbani
kwetu kwani mtoto si damu yangu..?”
Niliongea kimoyomoyo huku nikijitandikia vizuri shuka nakujilaza tena kitandani tayari kwa
kuutafuta usingizi kwa mara ya pili. ~ BAADA YA WIKI TATU ~ Mtoto Adrian nilishamzoea na nilishamchukulia
kama moja ya mtoto wangu wa kumzaa. Pale gesti
wahudumu wote wakajua ni mtoto wangu na hata
wakanipa jina la Mama Adrian. Uchangamfu wangu
wa kuongea na kila mtu ni kati ya vitu ambavyo
viliwavutia wengi. Zile hela ambazo nilizichukuwa kwa Mchungaji James nilipomuua kwa sasa zikawa
zimeniishia, si kwa kula tu bali hata kwa matumizi
ya huyu Adrian. Ilifika kipindi natumia hadi elfu
kumi na tano kwa ajili ya matumizi ya mtoto tu.
Ilinibidi kila siku niwe na pampasi tatu hadi nne na
kopo zima la maziwa ya ng’ombe kwa ajili ya kumnywesha. Sikutaka kujihusisha na marafiki wa
mbali nahii gesti kwani niliamini ndipo kujulikana
kwangu mpaka kwa Jerry. Habari za nyumbani
kwa Baba na Mama yangu sasa nikawa
nimezisahau kabisa. Nilianza maisha ya
kujitegemea mimi kama mimi tena bila ya kuwa na msaada wowote huku asililimia mia nikiamini
endapo baba au mama yangu akagundua kuwa
sipo chuoni muda mrefu ataumia sana. Sasa akili
yangu yote nikaielekeza katika kufanya mapenzi
na watu tofauti tofauti ili tu nipate chochote cha
kuniwezesha kujikimu mimi na huyu Adrian. Kuna kipindi nilikubali hata kuingiliwa kinyume na
maumbile ili mradi tu nipate chochote na hata
wanaume wengine walikuwa wananiingia hivi hivi
bila hata ya kutumia kondomu na hata kunilipa.
Siri kubwa tatu ndizo zilikuwa zimekaa kichwani
mwangu kama sheria na kiapo cha kutokumwambia mtu yeyote mpaka mwisho wa
uhai wangu. Siri ya kwanza ni juu ya huyu mtoto si
wangu ila wote wanatambua kuwa ni wangu. Siri
ya pili ni kuwa hapa nilipo nimejificha na
nilishawahi kufanya mauaji hivyo ni wazi natafutwa
huko Mwanza na pia natafutwa na Jerry na mkewe juu ya huyu mtoto wao niliotoroka naye. Na siri ya
mwisho inayoniumiza sana akili yangu ni juu ya
ugonjwa huu wa ukimwi. Ni kweli nimeathirika
japokuwa dalili zake sijazipata bado lakini mara ya
mwisho niliambiwa hospitali kuwa nimeathirika. Na
ndio siri iliyonifanya hata nishindwe kuendelea na masomo kwa kuchanganyikiwa na pia hata
niwafiche ndugu, wazazi hata na marafiki zangu
wote wanaonifahamu.
“..Binti leo nina buku tano tu..”
“..Twende tu haina shida ila tunatumia kondomu..”
“..aanhaa..!!, kondomu ya nini..?” “..hheee..!!, we vipi..? basi niongezee ziwe elfu kumi
twende bila kondomu..”
Alikuwa ni mzee mzima kabisa ambaye ana uwezo
hata wa kunizaa, na kwa muda huu alikuwa
meshazoea kuja kufanya mapenzi na mimi kwa
kutumia kondomu sasa leo naona kaja kivingine kabisa na anataka twende naye bila kutumia kinga.
Tulikubaliana naye nakuelekea mpaka chumbani
kwangu nilipopanga ambapo nilimchukuwa
Brayani nakumlaza chini kisha nikapanda
kitandani nakuvua nguo zangu zote nakubakiwa
na shanga tu kiuononi kwa ajili ya kuwadanganyishia wanaume wapenda ngono.
“.. haya nipe changu kabla..?, huna navaa nguo
hakuna kufanya chochote..?”
“..hilo tu..! ondoa shaka..!!”
Yule mzee hakuwa mbishi, alichomoa noti ya
shilingi elfu kumi nakunipatia. Niliichukuwa nakuiweka kwenye nguo za Adriani pale chini
kisha nikamfuata huyu mzee mpaka kitandani.
Nilianza kwa kumchezea kifuani kwake. Hakutaka
kuchezewa sana kwani haja yake nikufanya tu
mapenzi na mimi hivyo akajiandaa tayari kwa
kufanya mapenzi. Akiwa kishavua nguo zote mara tukasikia mlio wa simu yake ikiita..
“.embu naomba simu yangu hapo kwenye
suruali..”
Alinituma nimtolee simu yake. Haraka haraka
nikainuka na kwenda kumtolea na kisha
kumkabidhi.. ile nampa tu simu ikakatika. Akaiangalia namba nakuizima kabisa kisha
akanigeukia kwa tabasamu nakuanza kufanya
mapenzi na mimi. Nilimuonea huruma sana
kwakuwa nimeshaathirika hivyo nilimuona kuwa
naye anapoelekea ni huko huko. Kutokana na
tamaa zangu za pesa hata sikutaka kumzuia alifanya atakavyo na alipomaliza tu cha kwanza.
“..unataka kuongeza..?”
Nilimwambia kwa sauti ya taratibu na ya kimahaba
huku nikimrembulia macho. Yule mzee alitaka tena
hivyo akachukuwa suruali yake akaniongeza elfu
kumi nyingine napo tukaanza tena kufanya mapenzi kwa mara ya pili. Tukiwa katikati ya
mapenzi mara mwanangu Adrian akaanza kulia
kwa sauti yake ya juu. Sikutaka kumbembeleza
mpaka nimalizane kwanza na huyu mzee. Hivyo
tukaendelea tena lakini kwa safari hii mwanangu
Adriani ni kama alikuwa amezidisha kulia kwa sauti ya juu. Bado sikutaka kwenda kumbembeleza.
Tukiwa tupo katikati ya mahaba mara tukasikia
hodi inapigwa Mlangoni kwangu. Ilipiga kwa
nguvu kuashiria kuwa mtu anahasira au anataka
kitu cha haraka. Hakukuwa na sauti nyingine
yeyote zaidi ya kulia sana kwa mwanangu Adrian na yule mtu kuendelea kupiga hodi kwa nguvu.
Nilichokifanya nilimfanyia yule mzee ishara ya
kumnyamazisha kwa kutumia kidole changu
kukiweka mdomoni, kisha nikamchukua
mwanangu Adriani hivyo hivyo akiwa analia
nakumtupia uvunguni mwa kitanda na baada ya hapo nikaelekea moja kwa moja mpaka mlangoni
tena kwa kujiamini huku nimejifunika khanga
nakuufungua mlangu nusu.
“eenhe unasemaje..?”
Uso wangu kwa sasa ukawa umekutana moja kwa
moja na Mmama ambaye sura yake si ngeni kabisa machoni mwangu huku akibubujikwa na machozi
yalioambatana na kwikwi na nilipomuuliza tu kuwa
anasemaje. Pale pale alinisukuma nakuingia mpaka
chumbani kwangu kwa nguvu…
************************************* ***
Unavyodhani huyo Mama nii yupi..? Na Tina
atafanyaje..?
***
Nini hatma ya Tina kimaisha..?
***
Usithubutu kusimuliwa story hii ndio kwanza
imeanza kunoga kwani mwisho wa hii ya 40 .
**
Jiandae kujua kilichompata Tina ndani ya Play
gal
 
Ilipoishia….

Nilichokifanya nilimfanyia yule mzee ishara ya
kumnyamazisha kwa kutumia kidole changu
kukiweka mdomoni, kisha nikamchukua
mwanangu Adriani hivyo hivyo akiwa analia
nakumtupia uvunguni mwa kitanda na baada ya
hapo nikaelekea moja kwa moja mpaka mlangoni tena kwa kujiamini huku nimejifunika khanga
nakuufungua mlangu nusu.
“eenhe unasemaje..?”
Uso wangu kwa sasa ukawa umekutana moja kwa
moja na Mmama ambaye sura yake si ngeni kabisa
machoni mwangu huku akibubujikwa na machozi yalioambatana na kwikwi na nilipomuuliza tu kuwa
anasemaje. Pale pale alinisukuma nakuingia mpaka
chumbani kwangu kwa nguvu…
'
Sasa endelea….
“...Hivi jamani nikupe nini ili uridhike mwanaume
wewe..? eti Baba Jose..? Kwanini unanifanyia mimi
hivi..? kitu gani hujaridhika kutoka kwangu..? kitu
gani sikupi mie..?”
Nilishusha pumzi chini huku macho yangu
nikiyatoa kwa tahamaki nikiendelea kumshuhudia yule Mama akilalama. Kumbe yule mzee niliokuwa
nafanya nae mapenzi alikuwa ni mume wake wa
ndoa. Na kwa sasa alikuwa kama kishamfumania
akiwa na mimi. Aliendelea kumlalamikia sana
mume wake huku akimshika shingoni vilivyo.
“..Lakini mama Jose..?” “..lakini nini..? hivi kweli baba Jose ndio mchezo
wako huo unaofanyaga..? lini utakuwa mume
wangu..? kama ni watoto tunao wanne, badala
tupange ni jinsi gani tutawatunza na kuwasomesha
we ndio kwanza unahangaika nakutangatanga na
visichana vidogo.. embu inuka twende nyumbani huko..?”
Bado yule Mama alionekana kuwa na hasira
iliyoambatana na kwikwi kali kwani kila muda
alikuwa akihema kwa shida huku akiishiwa pumzi
kwa hasira ambayo alikuwa nayo ya kumfumania
mume wake. Akiwa bado anagombana na mume wake mara mwanangu Adrian akaanza kulia pale
chini yao.
“..tobaa..!!!, na tena kumbe binti mwenyewe ana
mtoto mchanga..? wewe baba Jose nini unafanya
jamani..? twende..!!, twende..!!, twende nyumbani
nimesema..? Nilisogea mpaka karibu yao kiuwoga woga huku
nanyata mithili ya simba anaponyemelea kitoweo
nakumchukuwa mwananagu Adrian nakuanza
kumbembeleza huku nikiwaacha yule Mama na
mumewe wakiendelea kuvutana. Waliendelea
kuzozana tena kwa sauti ya juu nakusababisha watu waanze kuchungulia madirishanai huku
wakipiga kelele za uchochezi. Baada ya muda
kama wa dakika tano nzima za ugomvi na
kuvutana huku na kule ndipo wakaondoka zao
wakiniacha nikiendelea kumbembeleza
mwanangu Adrian ambaye kwa muda huu ni kama alikuwa akizidisha kulia.
Baada ya muda kama wa dakika kumi ndipo
mwanangu Adrian akaanza kunyamaza
nakunifanya nijisikie faraja tele moyoni. Tabasamu
aliokuwa akiendelea kulitoa ni wazi kuwa alikuwa
mtoto msikivu anapobembelezwa. Niliinua mkono wangu wa kulia nakuanza kumpapasa maeneo ya
shingoni, mpaka usoni mwake. Alinishtua sana
kwani mwili wake ulionekana wamoto sana.
Kamasi za majimaji zilizokuwa zinamtiririka kupitia
puani mwake ni wazi zilionesha kuwa anaumwa.
Nilimvua nguo zake haraka haraka nakuanza kumuogesha. Nikiwa bado namuogesha mara tena
nikasikia kama mtu anabisha hodi. Mwanzo
nilionesha kusita lakini kadri nilivyokuwa
naendelea kumuogesha mwanangu Adrian ndivyo
na yule mtu alizidi kupiga hodi. Nilimtoa kwenye
beseni lake la kuogea nakumuweka kitandani nakuelekea mlangoni kujua ni nani alikuwa
anapiga hodi.
“Mama Adrian..? Mambo..? Samahani unahitajika na
meneja yupo mapokezi..?”
“..sawa Salma.., mwambie nakuja sasa hivi..?”
Alikuwa ni rafiki yangu wa humu ndani ambaye nayeye ni mfanyakazi na yupo mapokezi na kwa
muda huu alikuwa amekuja kuniiita kuwa
nahitajika na meneja. Ile hali yangu ya uwoga
ilianza kunitawala tena, mwili wangu wote
uliishiwa nguvu nakujihisi kama ile hali ya
kutetemeka imenianza tena kwani safari hii nilikuwa natetemeka sana maeneo ya mdomoni na
nywele kunisisimka. Nilichokifanya nilivaa nguo
zangu haraka haraka na kisha kumchukuwa
mwanangu Adrian nakuelekea mpaka mapokezi
ambapo ndipo alipokuwa meneja akiniita.
“..naam bosi wangu nasikia unaniita..?” “..ndio nakuita, hivi mama Adrian kwanini unataka
kutuchafulia jina hapa mtaani..?”
“..kwani vipi meneja..?”
“ina maana hujui kitu ulichofanya muda si mrefu..?”
“..anhh..!!, unajua meneja ni kwamba..”
Kabla sijaanza kumsimulia meneja. Alinikatiza kuendelea kuongea neno lolote. Sura yake ilikuwa
imembadilika na hakuwa kama meneja yule wa
awali niliomzoea kwani alionekana dhahiri
kuchukizwa na kile kitendo cha mimi kufumaniwa
na yule Mzee.
“..sitaweza kuvumilia ujinga unaoendelea kufanya kila siku humu ndani. Katafute gesti nyingine za
kufanya huo ujinga hapa kuanzia sasa hatukuitaji
na mambo yako ibilisi we..?”
“..Jaribu kunisikiliza na mimi basi meneja..?”
“..hapana..?, hapana nimesema siwezi kukusikiliza
tena wala kukuelewa kwa namna yeyote zaidi ya kukuona umeenda huko chumbani nakutoa kila
kilicho chako na ufunguo wangu nauhitaji ndani
ya dakika kumi, umenisikia na kunielewa..??”
Nilikuwa sina tena ujanja Tina mimi kwani pamoja
nakumpigia magoti meneja huku nikitoa machozi
ya hapa na pale lakini haikusaidia chochote wala kunielewa. Inaonekana kile kitendo cha mimi
kufumaniwa kilimuuma sana nakuona kuwa
amechafuliwa jina na atakosa wateja. Sikuwa na
jinsi zaidi ya kuelekea tena chumbani nakukusanya
kila kilichokuwa changu. Sikuwa na begi
lakuwekea nguo hivyo nilichukuwa nguo zangu na za mwanangu Adrian kisha nikaziweka kwenye
fuko kubwa la lambo, na vitu vidogo vidogo kama
chupa ya maziwa na vijipodozi niliviweka kwenye
ule mkoba wa kipindi kile nilioondoka nao kutoka
kwa mama yake na huyu mtoto. Nilirudi mpaka
pale eneo la mapokezi nilipomuacha Meneja. “..funguo wenu huu hapa..?”
“…Nenda huko hatukuhitaji tena hapa Malaya
uliokubuhu wee..?”
Niliumia sana moyoni kwa maneno aliokuwa
akinitolea yule meneja nakujiona kuwa sifai na sina
hata haja ya kuishi hapa duniani. “..Adrian..? najua wewe huna hatia lakini sina jinsi
inabidi nikuhifadhi nakukulea mpaka
utakapokuwa kwa hali yeyote ile. Kubali vitu vyote
utakavyokutana navyo ukiwa na mimi mpaka
utakapokuwa mkubwa..?”
“Nilijikuta naongea na mwanangu Adrian japo alikuwa haelewi ninachokiongea kwakuwa bado
mchanga sana lakini alitoa tabasamu nakunifanya
nimbusu paji la usoni mwake nakuelekea kituo cha
dala dala huku nisielewe ninapoelekea.
“..nitaishi tu, Mungu ndio ajuaye..!”
Nilijikuta naongea peke yangu huku mwanangu Adrian nikimuweka vizuri kwani alikuwa
ameshalala. Ilinichukuwa zaidi ya dakika karibu
kumi nzima nikiwa nimezubaa peke yangu kituo
cha daladala huku nikifikiria nitaelekea wapi na
huyu mtoto. Akili yangu ikawa si ya Tina yule wa
zamani bali ni ya Tina mlezi tena yule wa mlezi wa katoto kachanga ‘Adrian. Hatimaye nikaingia
kwenye daladala iendayo mwananyamala na bado
nilikuwa sijielewielewi.
“…Sitakuacha na wala sintokuwa msaliti kwako
mwanangu Adrian..!!”
Bado niliongea peke yangu nilipoingia kwenye daladala. Baadhi ya abiria karibu wote ndani ya
daladala walikuwa wakinishangaa sana na
nadhani nikutokana na kuonesha sura ya huzuni
na kuchanganyikiwa kwa mawazo juu ya
mwanangu Adrian. Safari ya kutokea Temeke na
kuelekea Mwananyamala ilianza. Njia nzima nilikuwa mtu wa mawazo tu haswa ni jinsi gani
nitaishi huko niendako. Kuna wakati nilifikiria hata
kwenda pale chuo kwa rafiki yangu Aisha japo
anipe ushauri wa huyu mtoto na maisha yangu
kwa ujumla lakini nikaogopa kwanza kuchekwa
na pili mara ya mwisho nilipata uchizi nikiwa pale chuo hivyo kama wataniona na mtoto mdogo
watanishangaaa sana na kunicheka kwa dharau.
“ahh..!! liwalo na liwe bwana…!!, konda nishushe
hapo magomeni hospitali..?”
Nilijikuta naghairi kufika Mwananyamala ambapo
ndio mwisho wa daladala hii na ndio malengo yangu kwa ujumla japo sikujua naenda kwa nani.
Hivyo akili na mwawazo yangu ya ghafla
yakabadilisha mwelekeo mzima wa safari yangu.
Na kwa sasa nikashuka pale magomeni hospitali
na mizigo yangu kisha nikaelekea upande wa pili
nakupanda daladala ziendazo Posta kwa lengo la kushukia pale chuo cha biashara CBE ambapo
ndipo nilipokuwa nasoma chuo na rafiki yangu
kipenzi Aisha. Saa ya kwenye daladala ilikuwa jibu
tosha kuwa inaelekea saa kumi na moja ya jioni.
Haikunichukuwa muda sana kwani mwendo wa
kutoka Magomeni hospitali mpaka chuo cha biashara CBE ni kama dakika saba hivyo nilishuka
huku nambembeleza mwanangu Adrian
mgongoni.
“..twende mwanangu.., hapa ndipo nilipokuwa
nasoma..??”
Tayari akili yangu ilikuwa ni sawa na ya mwanangu Adrian kwani kuna kipindi nilikuwa nikiongea
naye utadhani kuwa ananielewa nakunisikia kwa
ninachokiongea. Mshipa wangu wa aibu niliuweka
pembeni kwa muda nakuvaa sura ya mbuzi tena
yule beberu kabisa. Nilijitwisha fuko langu la lambo
kichwani huku kwenye kwapa nikiuweka mkoba wangu vilivyo na mgongoni nikimbeba mwanangu
Adrian tena akiwa amepitiwa na usingizi.
“..embuuu…!! embuu…!!, hivi tulikuwa tunakaa nae
bweni lipi tena..?? ok..!! ok, nimeshakumbuka
ghorofa G namba 13..”
Chuo chote cha biashara CBE kilikuwa kimya sana na najua tu ikiwa hali kama hii ni dhahiri kuwa
wanafunzi wote wanakuwa katika mitihani tena ile
ya kumaliza chuo. Pale getini hakukuwa na mlinzi
yeyote hivyo niliingia bila ya kuulizwa na mtu
yeyote. Nilipishana na baadhi ya wanafunzi
wachache sana tena wale masista duu na wengine mabrazameni bila ya kujali wala kujiogopa
nilipishana nao huku akili yangu yote nikulifikia
jengo G namba 13.
“..samahani Anti.. eti namba 13 kuna watu…”
Nilimuuliza mdada mmoja alioonesha sura yake ni
ngeni kabisa machoni mwangu kwanza hata alikuwa hanifahamu kwani hakuonesha mshtuko
wowote..
“..kwani wewe unamtaka nani..? Maana wanafunzi
karibu wote wanafanya mitihani kasoro wale wa
mwaka wa kwanza walioingia juzi juzi ndio wapo
wapo humu mabwenini..” “..sawa..!!, unamfahamu Aisha.., anakaa chumba
hicho hapo juu namba 13..?”
“..Aisha..? Aisha..??, mhhh..!! Namfahamu wewe ni
nani yake labda..?”
“..rafiki yake wakaribu na nimesoma naye hapa
hapa chuoni..” “””haloooo…!!! Eti rafiki yake wa karibu nimesoma
naye..??, unahadhi wewe yakutembea na Aisha..?
mwenye hipsi.., shepu shepu sio la mchina..
wakutembea na ‘Verosa’ sio daladala, bajaji wala
teksi..?
Alinitolea maneno ya umbea na yakuumiza sana roho tena kwa pozi huku mdomo akiyumbisha
kana kwamba sina hadhi yakuongea naye yeye
wala huyo Aisha.
“..subiri hapo hapo nikakuangalizie maana nahisi
utakuwa umekosea njia kwani Aisha nimjuaye
mimi hawezi kuwa na mtu kama wewe ambaye hujui hata kujipodoa wala kuoga, mwenye kunuka
makwapa na hilo toto sijui ndio kojo au lijimavi
limeshajinyea..?”
Aliondoka huku akiendelea kuongea maneno
yake machafu na kwenda kumuita Aisha. Niliumia
sana moyoni nakutamani hata kumrukia na kumpiga lakini niiliogopa kufanya vurugu yeyote
katika maeneo ya hapa chuoni. Kwani niliamini
nitakamatwa na tena ikijulikana nilikuwa nasoma
hapa ndio nitaharibu kila kitu.hivyo nikawa mpole
tena mjinga haswaa huku nimejibanza
nakumsubiri huyo alieenda kumuita Aisha. Ilinichukuwa dakika kama nne nzima peke yangu.
Harufu kali ya marashi ya ‘adorable’ ilioambatana
na sauti ya viatu ndio ilinifanya nianze kutoa
mchozi kwani ndio marashi niliokuwa nayapenda
kutumia na rafiki yangu kipenzi Aisha tulipokuwa
wote chuo kipindi kile. “..Aishaaaaa..?? Aisha rafiki yangu..?”
Nilishusha fuko langu chini nakumkimbilia aisha
huku nikitaka kumkumbatia lakini nilipofika karibu
yake tu akanikwepa nakunifyonza huku macho
akiyatoa vilivyo.
“..wee chizi vipi..?” “..jamani Aisha embu niangalie vizuri..?
umeshanikumbuka rafiki yangu kipenzi..?”
“..sauti siyo ngeni.., embu nikumbushe unatokea
wapi wewe..?”
Maskini Aisha alikuwa ameshanisahau kabisa japo
mimi nilishamtambua. Kuharibika kwangu sura na nyele zangu za kipindi kile vilitosha kunibadilisha
nakuwa Tina feki. Hata nilipomwambia Aisha kuwa
naitwa Christina ama Tina bado alikataa nakusema
kuwa Tina yule wazamani alishakuwaga chizi wa
mitaani na siwezi kuwa mimi. Nilitumia dakika
kama kumi nzima za kumulelewesha hadi akanitambua.
“..niwewe Tina..? hata bado siamini kipenzi changu
kwanini umekuwa hivyo jamani..??, shetani gani
aliokutembelea Tina ukabadilika kiasi kile..?? Ona
sasa mwenzako nimetoka kumalizia mtihani wa
mwisho.., si tungekuwa tumemaliza wote sasa hivi Tina..?”
Aisha aliongea na mimi kwa uchungu wa hali ya
juu huku akitaoa machozi kama vile mtoto mdogo.
Alinitoa mule chuoni ndani nakunipeleka mpaka
nje. Tukatafuta sehemu nzuri ya baa nakukaa kisha
nikaanza kumsimulia yote yalionikuta kipindi sipo naye. Aliona na kufananisha maisha yangu kama
vile sinema tena ile ya tamthiliya ambayo ya muda
mrefu sana. Nilimuelezea kuanzia tulipoanza naye
mpaka nilipomucha chuo nakuanza kufanya
umalaya wangu tena kwa kumficha mambo mengi.
Kuhusu kuathirika kwangu nilimficha lakini kuhusu huyu mtoto nilimdanganya kuwa ni mtoto
wangu ambaye nilizaa na mchungaji yupo Mwanza
kaniacha na kunitelekeza na mtoto.
“..pole sana rafiki yangu Tina, ndio maisha jinsi
yalivyo. Enhee kwa hiyo unaishi wapi kwa sasa..?”
“Aisha..? hapa unaponiona sina mbele wala nyuma na naishi peke yangu na huyu mtoto wangu tena
kwa kutangatanga..”
Tukiwa bado tunaongea mara mwanangu Adrian
akashtuka kutoka usingizini nakuanza kulia kwa
sauti ya juu. Nilimfunua vizuri nakuanza
kumbembeleza huku nikimtolea maziwa kwenye chupa..
“..mtoto wako mzuri sana Tina.., anaitwa nani..?”
“..anaitwa Adrian. Kwa hiyo sasa hivi Aisha
umeolewa au maana nakuona na pete ya uchumba
shosti..?”
Nilimbadilishia mada asiendelee kuniuliza juu ya huyu mtoto. Alikuwa amevalishwa pete lakini
hakuniweka wazi kuhusu bwana anayeishi naye
ila aliniambia tu ni mfanyabiashara tena
wakimataifa hivyo si mtu wakukaa sana nayeye
hivyo ni kama anaishi yeye na mfanyakazi tu.
Alinichukuwa pale nakuelekea mpaka eneo aliokuwa amepaki gari lake na safari ya kuelekea
kwake ikaanza kwani aliniahidi kuishi na mie
mpaka mtoto atakapokuwa mkubwa ama mimi
nitakapopata kazi yakueleweka nakujitegemea
mwenyewe.
“..Aisha..?, wewe ni rafiki wangu wa milele.., na sina rafiki kama wewe..?”
Niliongea kwa kusisimka huku uso wangu
ukitawaliwa kwa machozi ya furaha. Gari lake
lilikuwa zuri sana na lenye vioo vyeusi vya
kumfanya mtu wanje asiweze kuwaona.
Mwanangu Adrian nilikuwa nimeshamshusha mgongoni nakumlaza siti ya pembeni yangu. Muda
wote Aisha alikuwa akitabasamu nakucheka na
mimi karibu njia nzima na hata tulipofika kwenye
foleni alikuwa akinipigisha stori za chuo
nilivyoacha gumzo kwa kila anayenijua na hata
kitendo cha wazazi wangu kuja kunitafuta chuoni. Kifupi nilifarijika sana nakujiona mtu mwenye
bahati ya mara nyingine tena bahati ya mtende.
“..kumbe Aisha unaishi mbali hiivi…??, enhee..!! ni
wapi hivi shosti maana hiyo safari hatufiki tu..”
“..weee unafikiri mbali basi..?? ni hapo bunju tu..,
tukivuka aka kapori tu tumeshafika..” Gari ilitembea kama alivyoniahidi kuwa tukivuka tu
kapori tumeshafika. Giza nalo lilikuwa
limeshatanda. Nilihakikisha mwanagu Adriani
nimemfunika vizuri kwa ajili ya baridi ya mule ndani
ya gari. Tukiwa bado tupo eneo la kale kapori mara
Aisha akasimamisha gari kisha akaanza kufungua droo za mbele ya gari yake kana kwamba kuna
kitu amekisahau au anakitafuta amekikumbuka.
Ghafla akatoa bastola ndogo nakunielekezea
kichwani mwangu..
“..hapo hapo ulipo Tina..??, usitingishike wala
kuongea chochote na nitakufyatua usipotii amri hii..??”
Mapigo yangu ya moyo yakabadilika nakuanza
kutemeka huku kojo likichukuwa nafasi yake
kunitiririka. Nikawa siamini kwa kilichonitokea.
Nilibaki kimya kama alivyoniambia Aisha huku ile
bastola iking’ang’ana katika paji langu la uso vilivyo tayari kwa kufyatuka. Sikuweza kujipindua
zaidi ya kusikia tu Aisha akiongea na mtu kwenye
simu.
“..kazi yenu tayari haya sasa mko wapi mnipe
changu..?”
Aisha aliongea kwenye simu kwa sauti ya ukali na yakikatili kisha ndani ya dakika chache mlango wa
gari kwa upande wangu ukafunguliwa. Tochi
zilinimulika kisha nikashikwa na watu
nisiowafahamu halafu kwenye gari nikamshuhudia
Jerry kiingia kisha akambeba yule mtoto na
kuondoka zao na Aisha huku wakiniacha nimekumbatiwa na watu nisiowafahamu.
“..mnampeleka wapi mwanangu..??,
mrudisheni..??”
Nilitoa makelele ya nguvu lakini haikusaidia
chochote zaidi ya ile gari kutokomea huku wale
wavulana waliokuwa wamenishika kwa kunikumbatia wakianza kunivua nguo zangu na
zao tayari kwa kunibaka kwa zamu…

*********************** ***
kila siku stori inazidi kunoga je Tina atalipizaje
kisasi kwa Aisha..?
***
Inamaana Jerry alishampanga Aisha kuwa
kama Tina atatokea chuoni basi wamchukue mtoto
halafu watalipana pesa..?? nini hatma ya Tina..?

*******
hii ndio play gal (Revenge).., usithubutu
kuhadithiwa hata inayofuata kwani ni kali sana
zaidi ya hapa.
***
endelea kuwa nami kwa msisimko zaidi wa
hadithi hii yenye ukweli ndani yake ya play gal
 
duuh nimekosa hata chakuandika, hongera sana mkuu kwa kipaji
 
Sasa Stunter wakati mwingine uwe na kumbu kumbu
Tina ametolewa kule ufukweni na Vonso ule usiku akiwa uchi coz nguo zake zote alivuliwa na pia waliondoka nazo!

Vonso amemuijia na tax wameenda mwananyamala kwa Vonso coz mkewe na watoto hawapo hivyo huwa yupo peke yake

Vonso anampatia kanga mbili
Hivyo hakuwa na nguo nyingine zaidi ya hizo kanga mbili

Sasa hiyo blauzi na bra zilitokea wapi tena?

Hahahaah uwe makini
wengine huwa tunasoma nukta kwa nukta, neno kwa neno!
 
Sasa Stunter wakati mwingine uwe na kumbu kumbu
Tina ametolewa kule ufukweni na Vonso ule usiku akiwa uchi coz nguo zake zote alivuliwa na pia waliondoka nazo!

Vonso amemuijia na tax wameenda mwananyamala kwa Vonso coz mkewe na watoto hawapo hivyo huwa yupo peke yake

Vonso anampatia kanga mbili
Hivyo hakuwa na nguo nyingine zaidi ya hizo kanga mbili

Sasa hiyo blauzi na bra zilitokea wapi tena?

Hahahaah uwe makini
wengine huwa tunasoma nukta kwa nukta, neno kwa neno!
Hahahahaa kumbe na we umeona!!!! twendeni hivyo hivyo mkuu vitu vingine tutajiongeza wenyewe mbele ya safari
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom