ilipoishia...
"..Lucyyyyyyy.....??? Lucccccccccy...??"
Shebby aliita kwa sauti ya ukali, sikutaka kuinuka
pale sebuleni, nilikaa kimya kama simsikii akiniita.
Nikiwa bado nipo pale sebuleni nimezubaa
nakumsubiri Shebby aniletee simu yangu mara
nikaanza kuuona moshi mweupe ukitanda kwa juu huku ukija kwa kasi. Mapigo yangu ya moyo
yakaishiwa nguvu nakwenda taratibu sana
nakuusababisha mwili wangu unilegee kwa
kukosa nguvu huku macho pia yakinilegea. Kwa
mbali nilisikia mlio wa pikipiki ukiondoka,
nilijitahidi kutoa sauti lakini haikuwa na nguvu hivyo nikataka kuinuka ili nikimbie nakutokomea
nje lakini nguvu sikuwa nazo zaidi yakuendelea
kukaa kwenye kochi pale sebuleni nikiwa hoi....
'
endelea.....
Kila nikijitahidi kusimama bado nilikuwa hoi, ule
moshi uliokuwa unatanda ukatoweka ghafla na
kwa muda huu kimyaa kilitanda, kila nikijitahidi
kutoa sauti ilikuwa haitoki mithili ya television
iliyozuiliwa sauti isitoke. Akili yangu ikawa haifanyi
kazi tena, niliweza kutambaa chini chini, kila nikijaribu kutoka upande wa nje nilikuwa
nashindwa hivyo nikajikuta nikiranda randa pale
pale senuleni. Harufu kali na nzuri ya marashi tena
yale marashi ya karafuu nzuri inayotengenezwa
Zanzibari ndio ilikuwa ikinivuta bila ya mimi
kujitambua ambapo nilijikuta nikitambaa mpaka kwenye chumba kilichokuwa wazi.
"..siiiiiiimmmmuuu yako.., sssiiiimmmmuuu
yyaaakkkooo hhhhiiii ccchhuukkkuuuwa..,
cchhhuukkuuwa...?"
Sauti mbili mbili zilikuwa zikipishana katika masikio
yangu hali ambayo ilinijaza hofu kubwa huku mwili ukinitetemeka sambamba na mkojo kunimwagika.
Niijaribu tena kwa mara ya pili kutoa sauti ya juu
lakini nilishindwa zaidi ya kutomuona mtu yeyote
bali kusikia sauti tu.
"...kweli nimeamini hii ndio bagamoyo.."
Niliusemea moyo huku nimejipumzikia zangu pembeni ya ukuta nikisubiri hatma yangu ndani ya
hiki chumba. Machozi mfululizo yaliokuwa
yananidondoka kuanzia usoni mpaka tumboni
mwangu nakuufanya mwili wote usisimke si kwa
furaha bali kwa mateso ya ghafla niliyopata humu
ndani. Ile arufu ilizidi kuwa kali zaidi huku ikisababisha moshi ujae tena na safari hii haukuwa
moshi wa kawida bali ulikuwa moshi ule wa kijani
kama ule wa sehemu za disco na haukunidhuru
zaidi ya kujaa ndani ya chumba mpaka nikajikuta
sioni kitu.
"..njooo..?, njooo mpenzi..?" Sauti ya taratibu na yakuvutia tena ile iliyokuwa
imechanganyikana na ya Biggy, Jerry, Vonso na
Steve ndio iliyokuwa inakonga masikio yangu
nakuyatekenya. Kila nikijaribu kuutoa mkono
wangu bado niliendelea kushikwa na mtu
nisiyemwona wala kumtambua. Kutokana na sauti yangu kushindwa kufanya kazi nilijikuta sina nguo
huku nikiendelea kutekenywa karibu mwili mzima,
nguvu yakuutoa mkono sikuwa nayo kwani
nilikuwa kama mlemavu aliyepooza mikono au
kukatwa kabisa.
"..hapa hapa.., lala, lala mpenzi.." Zile sauti mbili mbili bado zilikuwa zinaranda ndani
ya masikio yangu, na kwa muda huu niijikuta
nimelala sehemu ambayo sikuiona kwa macho
kutokana nakujaaa sana moshi, ila nilijihisi niko
kwenye manyoya manyoya tena yale malaiiini.
Nilianza kuhisi kama sehemu zangu za siri zinavuja maji maji tena yale yanayoteleza, mara nikahisi tena
yale maji maji kama yanarudishwa ndani kwa
nguvu huku nikijihisi mumivu si yakawaida,
nilijaribu kuinua mkono wangu tena kwa mara
nyingine lakini hali ikawa ni ile ile sikuweza kuinua
mkono wangu. Mara ule moshi ukayeyuka na macho yangu yakakutana uso kwa uso na Shebby
huku pembeni yake wakiwa mabaunsa tena
wakiwa uchi kabisa na nanii zao zikiwa
zimesimama sana. ule moshi ukaanza kutanda tena
kwa kasi nakusababisha nisiweze kuona tena
mbele na safari hii nilihisi kama nachapwa na fimbo mgongoni na tumboni kwani maumivu niliyasikia
mara mbili mbili, nilishikwa maziwa yangu kwa
nguvu huku nikihisi tena kama maji maji yanatoka
kupitia sehemu angu za siri nakurudishwa kwa
nguvu sana hali ambayo ilinipelekea kupoteza
kabisa fahamu zangu.. ********* Kelele za watu zilizoambatana na vigelegele mithili
ya harusi ndio zilizoamsha hisia zangu toka
usingizini nakujikuta niko peke yangu uchi wa
mnyama tena makaburini, ndio kwanza kulikuwa
kunakucha, woga ulinitanda sambamba
nakusisimka mwili wangu, nguo zangu zilikuwa zimerushwa juu ya misalaba ya makaburi na
mkoba wangu pia. Bila kuhofia chochote nilitoka
pale nakukusanya nguo zangu moja baada ya
nyingine ile nataka kuvaa tu..
"..mwanga huyooo...??, mwangaaa...?, jamani
mchawi huyo nayetuwangia....?" Kelele za watu zilianzaa kusikika kila upande
nakusababisha watu wajae pale makaburini
nilipokuwa huku baadhi yao wakitaka kunitupia
mawe.
"..unatoka wapi? na umetumwa na nani..?"
Mzee mmoja wa makamo aliniuliza kwa sauti ya ukali nakunifanya niendelee kuwa nakigugumizi
huku mchozi ukinitoka kwa aibu iliyonipata Tina
mie. Ule umati wa watu haukuridhika na mie kuwa
kimya hivyo mmoja wapo akaja na kamba na
kunifunga.
"..dawa yake tunamfanya kama tulivyomfanya bibi Mwajabu, tutamtembeza mitaa yote hivi hivi uchi
kisha tunampeleka polisi akanyee debe, ndio dawa
yao hawa wachawi.."
Kila nikijitahidi kujitetea haikuwezekana zaidi
yakuambuliwa kupigwa makofi huku
wakizigombania nguo zangu nakuzichana chana vipande mithili ya ile picha ya Yesu kisha
wakachukuwa mkoba wangu. Aibu kubwa
ilinishika haswa nilipotembezwa mtaa mzima,
watoto, wazee sambamba na vijana ndio
waliokuwa mstari wa mbele kupiga makofi na
kunicheka, kila nikijitahidi kuuficha uso wangu ndo kwanza nilikuwa nikiambulia makofi na
wananchi wenye hasira kali.
"..tumpitisheni na mtaa wa shekhe Juma?"
Aliropoka mzee mmoja, watoto walinisogelea
karibu yangu huku wakishika shika matiti yangu
na hata watu wazima wengine wakinishika makalio yangu, kuna kipindi niliteleza kwa bahati
mbaya mpaka chini nikaambulia kuchezewa
sehemu zangu za siri huku wengine wakizipiga
piga kwa kutumia fimbo na mawe.
"..mnisamehe jamani..!, mnisamehe mie sio
mchawi..?" "..usistutanie hata kidogo...? na makaburini ulifuata
nini tena ukiwa uchi kabisa?"
Waliniinua juu nakunitembeza tena huku
wakiifungua mikono yangu kamba nakuitanua
huku na kule, mwili wangu sasa ukawa
hautamaniki kwa kupigwa pigwa, damu zilianza kuniganda mwilini kuanzia usoni mpaka maeneo
ya sehemu zangu za siri. Umati wa watu ulizidi
kuwa mkubwa sana mara tatu ya ulivokuwa huku
madererva teksi na boda boda wakipiga honi zao.
Niliendelea kuumia mwili wangu wote na akili
yangu ikawa imenivurugikaa kabisaa, nikiwa bado katika hali ya mshangao wa ule umati mara uso
wangu moja kwa moja ukakutana na mtu kama
Steve...
Bado niliendelea kuangua kilio huku nikimtazama
yule mtu aliyefanania kama Steve. Maumivu
niliyokuwa nimeendelea kuyapata ndio yalikuwa yamenivuruga kichwa changu na akilli kwa ujumla
huku zile kelele za madereva taksi na boda boda
zikiharibu kabisa halmashauri ya ubongo wangu
nakujikuta sijielewe elewi..
"..Steve..? Steve..?"
Nilimwita yule mtu niliokuwa nimemfananisha na Steve, hakunijibu chochote zaidi ya yeye
kuchukuwa kipande cha fimbo pembeni kwa
mwenzake kisha akanivaa na kuanza kunichapa
kwa nguvu zote.
"..Kituoni palee, tumpelekeni tu, mpumbavu
mkubwa, yaani usiku tulale yeye atukoseshe usingizi wetu kwa kutuwangia, tena fala kabisa.."
Aliendelea kuongea yule mtu niliokuwa
nimemfananisha na Steve na kweli hakuwa Steve
niliyemdhania, kwani huyu alikuwa mweupe sana
pili hata ile ongea yake ilikuwa tofauti na Steve
ninayemjua mimi. Maskini baada ya kunidhalilisha Tina mie hatimaye wakaniburuta mpaka kituo cha
polisi.
"Afande Adrian, huyu asiingie kwanza ndani, hiyo
midamu yake kuanzia kichwani mpaka miguuni
inabidi tuitoe.."
Aliongea askari mmojawapo tena kwa ukali huku ule umati wa watu uliokuwa umenizunguka na
kunipiga ukitawanyika, na sasa ilikuwa ni vita
yangu mie na mapolisi hapa kituoni.
"...afande embu changamka na kalete ndoo mbili
za maji pamoja na viwembe viwili.."
Yule afande aliendelea kuamrisha na punde, yule aliyekuwa ametumwa akawa amesharudi na ndoo
mbili huku mkononi mwake akiwa kashikilia
viembe. Zile ndoo mbili zote ziliishia kwenye mwili
wangu huku mabaki ya damu damu
yaliochanganyika na vumbi vumbi yakichukuwa
nafasi yake kutoka katika mwili wangu, na baada ya hapo nilipewa lishuka chafu chafu lililonuka
mikojo nijistiri. Ndani ya muda mfupi nikawa sio
Tina yule unayemjua kwani nilinyolewa kichwa
changu chote nakubakiwa na upara tena ule
uliojaa madonda donda yaliokuwa
yamegandishwa na damu damu. Niliingizwa ndani nakuchanganyika na wahalifu mbali mbali tena
mwanamke nilikuwa peke yangu..
"..utakaa apo kwa mda na usiku tutaliamisha na
kulipeleka kulee.."
Alionge askari, akimwambia mwenzake kuhusiana
na mimi. Woga uliokuwa umenijaa tena ule uiochanganyika na kutetemeka mwili mzima huku
nikiwa kama mtu aliyepigwa na ganzi kwa
maumivu yake. Hata ile hamu ya kula sikuwa nayo
tena, na mpaka inaingia jioni hakuna hata polisi
aliyetaka kuchukuwa maelezo yangu hivyo
nikajipa maswali mengi kichwani nakuona huenda hakunaga maelezo kwenye kesi kama hizi za
kichawi. Taa zilizokuwa zimewashwa ndani ya
kituo hiki cha polisi ilidhihirisha wazi umeshawadia
usiku. Hata askari yule aliyekuwa akinifokea
mchana naye aliondoka nakuja maaskari wengine
wakakabidhiana zamu pale huku nawasikiliza. Nikiwa bado katika dimbwi la mawazo mara..
".. wee mchawi..?, mchawi...?"
Aliniita polisi mmoja huku akija kunitoa
nakunipeleka hadi kwenye meza kubwa kisha
akachukuwa kitabu kikubwa nakuanza kunihoji
huku akiandika kitu. "..embu niambie jina lako kamili, na unaishi mtaa
gani hapa Bagamoyo..?"
"..naitwa Lucy Andrew na natokea Dar es salaam.."
"..Lucy Andrew, huku Bagamoyo ndio ulikuja
kuwanga..? wenzako wako wapi..?"
"...Afande ni vigumu kuniamini lakini ukweli bado upo pale pale, tangu nimezaliwa mie nausikiaga tu
uchawi na sijui hata huwa wanafanyaje fanyaje, na
nilikuja kwa ndugu yangu anaitwa Ste...."
Kabla sijamalizia kuongea chochote nilishangaa
kumuona Steve akiingia ndani ya kituo cha polisi
tena huku sura yake kaikunja. "..Steve..?, Steve..?"
Nilijikuta nongea kwa sauti ya chini chini huku
nikijihisi mate yamenikauka kwa sauti yangu
ilivyokuwa ndogo. Steve alinisogelea mpaka pale
kwenye meza kuu tulipokuwa tumesimama.
"..jambo afande..?" Walisalimiana na hapo hapo halmashauri yangu ya
kichwa ikafanya kazi wa urahisi zaidi nakujua
haraka kumbe Steve ni polisi tena yule
anayeheshimika. Baada yakusalimiana pale kumbe
Steve hakugundua kuwa aliyekuwa anahojiwa ni
mimi hivyo ile anataka kujiweka sawa hapo hapo nikaropoka kwa nguvu.
".Steve ni mimi Lucy hujanijua jamani..?"
"..kelele...?, shiiiiiiii....!!! huruhusiwi kuongea
chochote mpumbavu weeeee....?"
Alidakia yule polisi aliyekuwa ananihoji mwanzoni
na nilivyoongea tu hivyo Steve alinigeukia taratibu huku akiusogeza uso wake karibu yangu
nakuniangalia vizuri..
"..umejuaje jina langu na wewe ni Lucy wa wapi..?"
Ni vigumu kuamini Steve kwakuwa
nimeshaharibiwa sura na hata nywele sina embu
niangalie vizuri, mie ni Lucy yule wa Dar es salaam na hii yote nikukufuata mpaka huku na ona
nlichofanyiwa na watu wenye roho mbaya..,
ningeuliwa Steve..!! ningeuliwa tena kwa ajili
yako..!!"
"..unasemaje...? Lucy sasa hapa umefikaje..?"
"...ndio maana nikakwambia ni stori ndefu ila kifupi nimefanyiwa vibaya na mtu ambaye nilipanda naye
daaladala mpaka hapa Bagamoyo ambapo aliniibia
simu yangu kwenye daladala niliposhuka tu
sikumuona, nilielekezwa mpaka anapoishi na
nilipofika kwake akinifanyia madawa yake
nakuniharibu sehemu zangu za siri na nilipokuja kuzinduka asubuhi nilijikuta nipo makaburini tena
huku nguo zangu zikiwa imetapakaa kwenye
misalaba ya makaburi na hapo hapo ndipo watu
wenye hasira kali wakaniona nakunifuata
nakuniita mchawi huku wakinitembeza mitaa ya
huku karibu yote tena nikiwa uchi kama nilivyozaliwa..."
"..pole sana Lucy, Afande..? huyu binti namjua na
hata nilivyokuwa kwenye msiba wa kaka yangu
kule Dar huyu alitusaidia sana nakuwa karibu yetu
katka kipindi chote cha majonzi.."
Nilihisi moyo wangu kujaa na barafu tena ile ya baridi kwa furaja ya ajabu huku mwili wangu
ukinisisimka nakuona mtetezi wangu sasa
amepatikana, ile hamu yakuwa kicheche sikuwa
nayo tena zaidi yakufikiria nirudishwe zangu Dar tu
nikajisomee.. Ndani ya muda mfupi Steve aliongea
na askari mwenzake kisha wakanichukuwa mpaka kwenye gari huku nikijikunyata na lile shuka
nililopewa kipindi nimemwagiwa maji na
kunyolewa nywele zangu. Nilifikishwa mpaka
nyumba aliyokuwa akiishi Steve, ilikuwa ni nyumba
kubwa na tulimkuta mke wake ambapo nilipofika
tu alinishangaa sana lakini baada ya Steve kumuambia kilichonikuta alinionea huruma
nakuingia chumbani kwake kisha akatoka na
gauni na khanga halafu akanipeleka mpaka jikoni
nikavaa nakurudi sebuleni.. Hakukuwa na chumba
cha wageni lakini kulikuwa na godoro la akiba
ambapo nilitandikiwa vizuri pale sebuleni kisha nikapewa shuka la kujifunika nikalala zangu.
Ndoto za ajabu ajabu ndizo zilininyima kabisa
usingizi wangu, usiku wote nilikuwa mtu wa
mawazo huku machozi yakijitokea peke yake,
nilijikuta hata kwanini sikuingia darasani nikatulia,
nilimuonea huruma baba yangu aliyekuwa akinitumia ada na hata hela ya matumizi kila baada
ya wiki mbili ambapo alikuwa akinitumia hela
nyingi sana tu.
"..kweli dunia tambala bovu..."
Niliusemea moyo huku nikiufuta mchozi wangu
nakujifunika vizuri. Kutokana na kukosa usingizi ukijumlisha mawazo niliyokuwa nayo na ubaridi
uliokuwa unausumbua mwili wangu hatimaye
nikaanza kuhisi hisia za ajabu zinatawala ndani ya
mwili wangu huku akili ya kishetani ikinituma
nimfuate Steve chumbani kwake akanifanye..
"..Hapana...? hapana..? nimesema nooo...?, noooooooooo...? Sitakiiiii....?"
Hisia zilishindwa kabisa kuuzuia mwili wangu hivyo
nikajikuta nimetupa shuka pembeni nakuinuka
huku nikiongoza mpaka chumbani kwa Steve, ile
nakaribia tu kufika mara mlango wachumbani
kwake ukafunguliwa kisha akatoka mkewe aliyekuwa amevalia nguo ya kulalia, kabla
hajaongea kitu nilishangaa macho yake
yanabadilika rangi nakuwa kama yakijani tena
yenye mwanga mkali na meno yake yakichomoza
mithili ya zile picha za kutisha za mazombi. Nikiwa
bado kwenye mshangao ghafla nikahisi kama yule mke wa Steve kayeyuka, niligeuka haraka haraka
nyuma sikumuona, nikaangalia na mbele
sikumuona hivyo nikajijaza moyo wa kijasiri
nakufungua kitasa cha mlango wao taaratibu huku
nikiamini kabisa atakuwepo Steve na watoto tena
wamelala kwa usiku huu. Kila nikifungua kitasa ndivyo kilizidi kuwa kilaini huku kikipitiliza mpaka
nikafanikiwa kuingia, taa ilikuwa imewashwa
ambapo nilimshuhudia Steve akiwa amemkumbatia
mke wake. Niliishiwa nguvu nakujikuta
nikiurudishia ule mlango kama nilivyoukuta
nakurudi sebuleni, ile najigeuza tu nirudi zangu nilipotoka mara tena uso kwa uso na mke wa Steve
na safari hii alikuwa kabadilika kidogo.....
***
Kwa hali kama hii kweli Tina atakuja kuachana
na u play gal..?
***
Hiyo ndio Bagamoyo aliyoivamia Tina kwa
pupa, Tina atafanikiwa ku sex na Steve..?
***
Unavyodhani Tina atatoka salama tena? na
kwanini Tina hatumii akili?
***
Huu ni mwanzo tu, huko tunapoelekea ndio
balaa ni zaidi yakutisha, kusisimua, kukuliza na
hata kukuondolea stress kama ulikuwa na
mawazo...
-
Siku hizi naona LIKE zimepungua..