STUNTER
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 13,077
- 17,260
- Thread starter
- #241
Ilipoishia..
Niliishiwa nguvu nakujikuta nikiurudishia ule
mlango kama nilivyoukuta nakurudi sebuleni, ile
najigeuza tu nirudi zangu nilipotoka mara tena uso
kwa uso na mke wa Steve na safari hii alikuwa
kabadilika kidogo.....
'
Endelea…
Kadri macho yalivyokuwa yanamtoka huyu mke
wa Steve ndivyo mwili wangu ulizidi kunisisimka na
kunyong’onyea, nilijijaza nguvu za kishujaa
nakutoa mkono wangu taaratibu nakuusogeza
mpaka shingoni mwake kisha nikamkaba kwa
nguvu zangu zote. Macho yake yaliendelea kumbadilika na kwa sasa nilijihisi mikono yangu
kama inazidi kuwa laini huku nikihisi kama shingo
yake inakuwa kama tope tope.
“..Mamaaaa…!! Mamaaaa…!!!”
Uzalendo ulinishinda nakujikuta nikitoa sauti ya juu
huku ule mwili wa yule mwanamke ukizidi kupukutika nakuwa kama tope tope, ikafika
kipindi nikashuhudia mwili wake wote
ukimung’unyika mpaka akayeyuka kabisa. Nguvu
sikuwa nazo tena zaidi yakuendelea kukaa pale
pale chini huku nikitumia mikono yangu
kujikokotea mpaka sebuleni kisha nikapumzika. “..amkaaa…?, amkaaa kumekucha..”
Ilikuwa ni sauti ya Steve akiwa kavalia bukta
yakehuku mkononi akiwa kashikilia mswaki.
“..kumekucha, amka ukapige hata mswaki ili
unywe chai..”
Aliendelea kuongea Steve nakunifanya niendelee kumshangaa tu huku nisiamini yale yote
yalionitokea usiku.
“…Steve, wifi yuko wapi…?”
Nilimuuliza kwa makusudi ili nijue kilichotendeka
usiku ule alikuwa ni yeye au nani?
“..Yupo jikoni anapika chai, akimaliza ataleta hapa sebuleni utamuona tu, kwani vipi ulkuwa
unamuhitaji..?”
“..Hapana, nimemuulizia tu kwa maana sijamuona..”
Nilizuga nakuchukuwa mswaki kisha nikatoka
mpaka nje kwenda kupiga mswaki na nilipomaliza
nilijirudia zangu mpaka ndani ambapo tulikunywa chai kisha Steve akaniambia kuwa anaenda
kuomba ruhusa kazini kwake hivyo niwe tayari
atarudi kunichukuwa. Furaha na amani ya ajabu
iliendelea kunitawala ndani ya moyo wangu
japokuwa Steve alipoondoka tu ile amani
ikatoweka tena ghafla. “..Usiku ulikuwa unataka kufanyaje Malaya
wewe..?”
Aliongea mke wa Steve nakunifanya niingiwe na
uwoga huku mwili wangu ukianza kunisisimka.
“..Si naongea na wewe..? Mimi nilijua tu utakuwa
mchawi kweli na nimethibitisha ilo usiku Malaya mkubwa wewe tena Yule wa waume wa watu, na
umekutana na kisiki hapa nimechanjiwa toka
kwetu Kigoma Malaya mkubwa wewe..?”
Aliendelea kuniambia maneno ya ukali yule Mama
na muda wote sikuongea hata neno zaidi ya
kumtizama tu machoni mwake, Alivyoona nazidi kuwa kimya akanisogelea mpaka karibu
nilipokuwa nimeketi nakunishika shingoni
mwangu, hisia kali nilizipata nakufananisha tukio
kama lile la usiku wake alionifanyia. Sikutaka
kuonekana dhaifu tena hata kidogo kwani tayari
nilishaigundua dhamira yake hivyo nilifanikiwa kuvuta kistuli kilichokuwa karibu yangu pale
sebuleni kisha nikamvaa nacho mpaka kichwani
mwake akadondoka chini nakupoteza fahamu
hapo hapo.
“..huwezi kushindana na mtoto wa mjini..”
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikimtolea fyonyo la dharau nakuingia mpaka chumbani kwake,
nilikagua kagua mpaka nikafanikiwa kuipata pochi
yake ambapo nilitoa kiasi kidogo cha pesa kama
shilingi elfu ishirini, nikachukuwa nguo zake
kwenye kabati lake la nguo nakuvaa. Ndani ya
muda mchache tayari nilikuwa nipo nje natafuta njia ya kuelekea kufika mpaka pale kituo cha polisi
kwa ajili ya kuonana na Steve. Kumbukumbu za
kufika pale kutuo cha polisi sikuwanazo zaidi ya
kukodi bajaji kisha ikanipeleka mpaka makaburini
pale nilipofumaniwa jana yake asubuhi na
nilipofika maeneo ya pale ilikuwa ni rahisi kupakumbuka kituo cha polisi kwani hakikuwa
mbali na mitaa ile ya makaburini.
“… Za sa hizi jamani…!! Samahanini namuulizia Steve
sijui nimemkuta..?”
“.. Ahaa mkuu Steve, yupo msubiri hapo pembeni..”
Aliongea Polisi mmoja aliyekuwa zamu ambapo hata jana sikumuona na ndio maana hata hana
kumbukumbu na mimi. Nilisubiri kidogo tu na
punde Steve alitoka ndani ya kile kituo mpaka
eneo nililopo.
“..OOoooh, Asia umekuja, mbona nilikuahidi
nitakuja kukuchukuwa nyumbani huko huko…” “..Hapana, nimeona kama nachelewa na mimi
kukaa huku kwenu Bagamoyo naogopa sana
yasije yakanitokea kama ya jana..”
“..Acha imani potofu bwana, hii siyo Bagamoyo ya
wachawi wala wanga kuwa na imani tu, utaishi
vizuri na kwa furaha tu, ennheee niambie vipi mke wangu umemuacha au katoka huko..?”
“.. Mkeo ameniacha hapo mtaa wa juu, kwani
alinisindikiza mpaka mitaa ilee, na hata nguo za
kubadilisha alinipa yeye tena asubuhi
ulivyoondoka, nimempenda sana anajua kuishi na
watu na anaonekana ana huruma..?” “..Ni kweli, mke wangu ni mkarimu sana kwa
wageni, anajua matatizo na shida za watu, naishi
naye vizuri sana tangu nimemuooa..”
Niliguna kimya kimya huku nikimtolea Jicho la
kujificha Steve kisha nikauchukuwa mkono yangu
nakuikutanisha mikono yangu na yake bila woga wowote.
“..Sasa Steve? Si umeshaomba ruksa, nakuomba
unirudishe basi Dar es salaam..?”
“..Hilo tu usijari, ila embu ngoja nimeshasahau kitu
ndani mara moja..”
Steve alirudi tena mpaka ndani ya ofisi, ndani ya muda mfupi akarudi na bahasha mkononi.
“..Sasa inatubidi turudi tena mpaka nyumbani
kwani mke wangu sijamuaga na pia kuna hela
natakiwa nimpelekee ili aende kununua vitu
sokoni kwani aliniambia kuwa vitu vimeisha..”
Nilionesha kukataa lakini Steve hakukubaliana na mimi kabisa hivyo nilipanda tena gari yake nakisha
safari ya kurudi nyumbani kwa Steve ikaanza tena.
Njia nzima nilitetemeka mithili ya mtu ambaye
hajawahi kuoga maji ya baridi na yupo sehemu ya
baridi. Niliogopa sana endapo Steve akijua mchezo
nilioufanya kwa mke wake. Kadri tuliyokuwa tunaenda ndivyo na mimi mapigo yangu yamoyo
yalivyokuwa yakinibadilika na kwenda kasi mno.
Hatimaye ndani ya kama dakika kumi tukawa
tumeshafika nje kwa Steve, tulijikuta wote mimi na
Steve tukitoa macho kwa mshangao tulipofika tu
nje ya nyumba yake kwani tulikutana na umati mdogo wakinamama huku kila mmoja akiwa
amejifunika khanga na kwa mbaali tulisikia vilio
kuashiria kuwa kuna msiba.
“..Ulivyoondoka ulikuacha salama huku..?”
Alinigeukia Steve nakuniuliza kwa ukali huku
amenitolea macho na akitafuta kitu mifukoni mwake..
“..Hao wakinamama ndio nawaona sasa hivi lakini..
Nikiwa bado namuelezea Steve kabla sijamalizia
kuongea mara ghafla simu ya Steve ikaita..”
“..Mkuu uko wapi…?”
“..Ndio naingia kwangu lakini kidogo nahisi hali si nzuri kwani vipi..?”
“..Ni kweli na kabla hujafika ni kwamba kuna binti
amonekana hapo kwako ametoka kwa haraka
sana na inasemekana anahusika na kifo cha mkeo
kwani mashuhuda wamemuona akitoka huku
amechanganyikiwa na hali tuliyomkuta nayo marehemu mkeo ni kapigwa na stuli eneo la
nyuma ya kichwa nakusababisha umauti wake…”
Steve alinigeukia huku akitoa machozi na mishipa
ya shingoni mwake ikimtoka vilivyo, alitoa pingu
nakunifunga mkono mmoja na mwingine
akanifunga kwenye msteringi wa gari yake kisha akatoka nakufunga vioo vyote vilivyokuwa na
tinted kisha akaloki milango yote akaelekea ndani
kwake huku akiniacha peke yangu ndani ya gari..
Bado nilikuwa sijielewi elewi pale ndani ya lile gari,
nilijaribu kuangalia huku na kule lakini haikusaidia
kitu, kila nikilipenyeza jicho langu kupitia kioo cha mbele ya gari ndivyo hasira nazo zilikuwa zikinijaa.
“..Najuta kuja huku Bagamoyo na sitorudia tena
eeeh! Mungu niponye tu…”
Nilibaki naongea peke yangu huku nikijihisi koo
langu limeshikwa na kwikwi na siyo kwikwi ya
hasira tu bali kwikwi ya hasira kali niliyokuwa nayo, kwa sasa macho yangu nilijihisi kama
yanatoa machozi tena yale machozi ya hasira kila
nikiona umati wa wakinamama na wakina baba
ukiongozana kuingia mpaka ndani na wengine
wakipishana kwa kutoka nje. Ndani ya muda
mchache tayari nilishuhudia Steve akiongozana na wenzake kuubeba mwili wa marehemu
nakuupeleka mpaka kwenye gari lilokuwa
pembeni yangu. Akili ilianza kunichemka huku
nikiangalia huku na huku ndani ya gari japo
kuambulia chochote niweze kujinusuru katika
hatari niliyokuwanayo. Ndani ya muda mchache nilifanikiwa kugundua funguo zikiwa
mchanganyio na hata muonekano wake ulionesha
wazi hazikuwa funguo za nyumba bali zilikuwa ni
funguo kama za pingu japo sikuzijua sana,
nilizichukua nakuanza kuzijaribisha moja baada ya
nyingine bila ya mafanikio yoyote. Nikiwa bado nashangaa shangaa kuzikagua zile funguo mara
nikahisi mtu anagonga kwenye dirisha la kioo.
“..nani..? nani…?”
Niliongea kwa sauti bila kusikia chochote, nilijijaza
moyo wa kijasiri nakuendelea kuzitafuta funguo za
kuweza kufungua pingu ambazo zilikuwa zimeshikamana na msteringi wa gari hili la Steve.
Nilijitahidi kuzifungua kwa kutumia mdomo
waangu na meno huku nikifungua kwa nguvu
zote. Sikuweza kufanikiwa kufungua lakini
halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi fasta
nakuamua nijiweke vizuri nakuliwasha gari kwa kutumia waya kama wafanyavyo wezi wa magari.
Ndani ya muda mchache niliweza kuliwasha gari
hivyo nikalirudisha nyuma nakuondoka kimya
kimya huku nikiamini kwa asilimia zote Steve
atakuja kugundua baadaye sana ambapo tayari
nitakuwa nimeshafika mbali. Kuwepo kwa barabara nyingi na kona kona za hapa na pale
ndicho kilichonisababisha nisielewe njia ya
kutokea kuelekea Dar es salaam. Sikutaka hata
kufungua vioo zaidi ya kuongoza hivyo hivyo tena
nikiwa nimejibana bana mapaja yangu na msteringi
nimeukumbatia huku nikitoka kwa mwendo wa kawaida tu. Sikuweza kufika mbali sana kutokana
na kuchoka kwanza kwa pingu nilizokuwa nazo
na pili sikuielewa haswa barabara ya kuelekea Dar
es salaam. Niliisimamisha gari baada ya kutembe
kwa mwendo kidogo kutoka lile eneo ambalo
alikuwa akiishi Steve na kwa sasa nilikuwa eneo wanaloziba pancha na kutengeneza magari
mabovu, pale pale nikafungua mlango nakumuita
kijana mmoja.
“..Mambo vipi…?”
“..Poa tu Sister vipi pancha nini…?”
“..Hapana, unaniona hapa mkononi, haya fanya ufanyavyo unitoe hizi pingu sasa hivi na kuhusu
pesa wala hata usijali”
“..Kwa hilo tu Sister!, wala usihofu tena nafanya
mwenyewe, vipi utanipa shilingi elfu kumi na
tano..?”
“..kuhusu pesa ondoa shaka..” Yule kijana hakutaka kabisa kuchelewa zaidi ya
kutoka mbio pale nakurudi na spana mbali mbali
ikiwa ni pamoja na msumeno mkubwa. Zoezi la
kama dakika tanotu lilikuwa tosha kwa huyu
kijana kunitoa pingu ambazo zilishikana na
msteringi wa gari. Amani kubwa iliyoambatana na furaha ya ajabu ilianza kuninyemelea ndani na nje
ya mwili wangu nakutamani sana nifike Dar kwa
muda mfupi. Nilitoa ile pochi ambayo niliichukuwa
kwa mke wa Steve nakutoa noti mbili za shilingi
elfu kumi kumi nakumpatia Yule kijana kisha
akanirudishia chenchi nakuondoka zangu huku nikijidai kuulizia duka maeneo ya pale. Vichochoro
viwili vitatu vilinitosha kabisa kutoroka na
kulitelekeza gari la Steve huku nikiulizia sehemu
ambayo ninaweza japo kupata usafiri wa daladala
au hata bajaji.
“..Mpaka stendi shiingi ngapi..?” “..Utanipa buku mbili tu..”
Nilichukuwa pikipiki kisha nikampatia hela ya
kunifikisha mpaka Dar es salaam kabisa kwani
niliamini endapo nitachukuwa daladala itakuwa
rahisi sana kushikwa na Steve au mapolisi
wenzake. Piki piki ilikuwa iko spidi sana, dereva hakutaka hata kidogo kuchelewa , upepo mkali
uliokuwa ukinipuliza njiani, hatimaye tukafika
maeneo ya bunju ambapo kwa bahati mbaya
pikipiki ikaanza kutoa mlio wa ajabu kuashiria
kuwa kuna itilafu ndani yake. Nilimpatia pesa yake
lakini alioneka kuchukizwa na mimi kumpatia hela . Sikumuelewa hata kidogo anachomaanisha hadi
alipovua kofia na miwani ndipo na mimi
nikamgundua.
“…waaat, ooohh kumbe ni weweeeeee, noooo…!
Noooo…! Noooo…?”
“Masikini nimekwisha Tina mimi…!” Niliropoka kwa sauti ya juu baada ya kumgundua
yule mtu kuwa alikuwa ni yule mzee alionifanya
mpaka nikajikuta nimeamkia makaburini tena uchi
wa mnyama kabisa na kwa muda huu kumbe
alikuw ni dereva pikipiki na alionesha kuchukizwa
baada ya kumlipa pesa yake. “..Ulinitoroka na leo ndioleo na unabahati nilikuwa
nakupeleka mpaka kwa wakuu wa mizimu kwa
babu zangu Tegeta shetani mkubwa tena malaya
usiye na hila wewe”
Aliendelea kufoka Yule kijana nakunishika mkono
huku akiiacha pikipiki yake nakuniburuta nilijitahidi japo kugoma lakini nilipata makofi na
ngumi huku akiniburuta kwa nguvu zake zote tena
eneo ambalo hata sikulijua. Kadri alivyokuwa akinivuta ndivyo na mimi
nikaanza kupata nguvu za ajabu huku nikijihisi lile
eneo la usoni ambalo nilichanjwa kipindi kilee
likiniuma sana.
“..Hunijui..? leo ndio utanijua vizuri..”
Nilijikuta naropoka tena kwa ujasiri wa hali ya juu. Sasa nilishindwa kuelewa kuwa ni nguvu za
kichawi alizokwa nazo huyu mzee au la kwani hali
ya hewa ilibadilika ghafla kiasi kwamba nikaanza
kunyeshewa na mvua tena ile mvua ya mawe,
niliendelea kuvutana na Yule mzee japo sikupata
msaada wowote kwani sikuweza kumuona mtu yeyote zaidi ya kuwa sisi wawili tu tukisumbuana.
“..Sema mwenyewe..?, unataka tukuue au ujiunge
na kundi letu..?”
“..niacheni jamani.., mie sitaki choc…”
Kabla sijamalizia tu kuongea nilishangaa napokea
bonge la kibao kutoka kwa mtu ambaye sikumuona lakini sauti tu za watu wengi ndizo
nilizisikia zikinihoji. Mwili wangu kwa sasa ulikuwa
kama sugu kwani hata yale maumivu sikuyasikia
zaidi ya kuhisi tu nimepigwa na mtu nisiyemuona. ******** Maumivu ya kichwa yaliochanganyikana na
uchovu huku upepo ukivuma sana nakujikunyata
kwa kuhisi baridi kali. Kila nikiendelea kutoa
macho nakuliangalia hili eneo bado nilikuwa
sipajui ni sehemu gani japo palikuwa ni kama
jangwa kumbwa lililojaa michanga tupu, akili yangu yote ilikuwa imenivurugika na kusababisha
kumbukumbu zote kunipotea.
“..hapa ni wapi..? Nirudisheni kwetu.., Baba yangu
yuko wapi..?”
Niliuliza kwa sauti ya ukali huku nikimfuata Bibi
mmoja aliyekuwa pembeni yangu na kwa muda huu alionesha kuwa yuko ‘busy’ sana, alikuwa
peke yake tu, nilimsogelea mpaka karibu na kwa
hasira nilizokuwa nazo ukichangia na
kutokujitambua vizuri, nilimshika kitenge chake
alichokuwa amekivaa nakukivuta kwa nguvu
mpaka nikahakikisha amebaki uchi wa mnyama. “..nani aliyenileta huku..? si nakuuliza wewe
kibibi..?”
Alinitolea macho tu bila kunijibu chochote.
“..sasa leo mie nataka mnirudishe kwa wazazi
wangu, wapumbavu sana nyie..?”
Nilijikuta nachota mchanga kwa hasira huku nikimwagia nao Yule Bibi na mwingine nikimlisha
mdomoni, kadri nilivyokuwa nikimtesa huyu Bibi ili
japo anioneshe kwa wazazi wangu ndivyo alikuwa
akibadilika nakuwa kama ule mchanga niliokuwa
nikimwagia. Maskini Tina mimi, nguvu zilianza
kunilegea na ule woga ukaanza kunitanda tena katika lile eneo, mara nikahisi kama kuna umati wa
watu umetanda japo sikuwaona lakini sauti za
watu wakicheka na kujibizana ambao sikuweza
kuwaona ndizo zilikuwa zikichochea hisia zangu
kwa haraka zaidi. KESHO YAKE ASUBUHI “…Tinaaaa…? Tinaaaa weweeee…? Enheee vipi..?
Umekuja saa ngapi shosti..?”
Bado nilitoa macho huku na kule huku nisielewe
elewe kabisa nimefikaje fikaje hapa chuoni CBE,
marafiki zangu walitanda kunishangaa kitandani
mwangu wakiongozwa na rafiki yangu kipenzi Aisha.
“..Shosti kwani vipi ulifiwa nini..? Pole na umekuja
saa ngapi..?”
“..Hapana mbona wala hata sikufiwa jamani kwani
vipi..?”
“..Shosti yani na lijiupara lote hilo bado unatudanganya..? Pole bwana, kwani umefiwa na
mzazi yupi..?”
Niliona kama wananizungua, niliamka pale
kitandani mpaka kwenye kabati langu la vipodozi
ambapo kuna kioo kikubwa nikajiangalia. Mchozi
ulianza kunidondoka taratibu baada yakujigundua nimenyolewa upara huku uso wangu ukiwa na
chanjo chanjo kama kabila lile la wamakonde
kutoka Mtwara. Niliumia sana moyoni nabado
nilikuwa sina kumbukumbu za kutosha ilikuwaje
kuwaje zaidi ya kukumbuka tu nilienda Bagamoyo
na huko nilifanikiwa kumuona Steve halafu akanipa hadi nauli nikarudi zangu Dar..
“..nani aliyenichanja…?, nauliza nyie, nani humu
bwenini amenifanyia hivi..?”
Niliwageukiwa marafiki zangu pale bwenini
nakuwauliza kwa hasira zote nakuwafanya
waanze kuniogopa tena siyo kwa ukali tu bali kwa sura yangu ilivyokuwa inatisha.
“..kuna niliyemchukulia bwana wake humu
ndani...? kwanini mnifanyie hivi..? Aisha rafiki
yangu nani aliyenifanyia mchezo huu, heee..? Na
kwanini mimi tu jamani mnanifanyia hivi..,
nimewafanya nini jamani.., au kwakuwa siingiagi darasani mara kwa mara eeenh..?”
Niliongea kwa jazba huku nikibubujikwa na
machozi, kadri nilivyokuwa nikiongea ndivyo na
umati wa wanafunzi wenzangu kutoka mabweni
mengine ulikuwa ukijaa ndani ya chumba chetu
kuja kunishangaa, hasira zilinizidia zaidi ya pale mpaka nikajikuta nachukuwa nguo zangu kabatini
na nyingine nikizitoa kwenye begi pamoja na viatu
vyangu vyote huku nakuzikusanya pamoja
nakutoka mpaka nje, nikarudi tena mpaka bwenini
tena nakukukusanya vipodozi vyangu vyote
pamoja na kiberiti nakutoka navyo mpaka nje, nakuanza kuvichoma moto kwa hasira kali
niliokuwa nayo.
“..Tinaaa, Tinaa rafiki yetu umekuwaje lakini..?”
“..Niacheni, si ndiyo mlivyotaka mfurahi haya
furahini sasa..?, furahini na mpige na vigele gele
kabisa..?” Walinifuata marafiki zangu mpaka nje nakunizuia
lakini haikusaidia chochote zaidi ya ule moto
kuongezeka kasi huku vipodozi vyangu
vikiendelea kuharibika. Niliuacha ule moto
ukiendelea kuwaka pale nakutoka mpaka dukani
ambapo nilinunua viwembe kama viwili nakurudi tena mpaka bwenini, sikujali makelele ya wanaume
wa hapa chuo tena wale waliokuwa wananifuata
nyuma nyuma nakunicheka huku wengine
wakinizomea. Niliongoza mpaka bwenini na
nilipofika nilifungua vile viwembe nakuanza
kujichanja zaidi ya nilivyoukuwa mwanzo. “..Hapana Tina usifanye hivyoo, usifanye hivyo..?”
“..Embu niacheni, nyie si ndio mmeyataka haya yote
nakunifanya hivi.., niacheni nijimalizie mpendwe
nyinyi, acha niwe mbaya si mlinichanja niwe mbaya
wacha nijiendeleze mwenyewe..?”
Tayari niikuwa kama nusu chizi kwa kuchanganyikiwa, walimu wa chuo walikuja
mpaka bwenini kuingilia kati swala langu,
walinishika lakini nilikuwa na nguvu za ajabu sana,
iliwachukuwa muda mpaka kufanikiwa kunifunga
kamba mikononi.
“..mpelekeni ofisini huyu..?” Nilisikia sauti ya mwalimu mmoja akiwambia
wanafunzi wa kiume wanipeleke mpaka ofisini
kwake, wanafunzi walikuwa ni wengi sana
wakinishangaa kwa jinsi nilivyokuwa nimebadilika
ghafla nakuwa Tina kichaa, kadri walivyokuwa
wananivuta nakunipeleka huko ofisini ndivyo na mimi nguvu zilikuwaa zikiniongezeka mara mbili ya
pale nakujikuta niking’ata zile kamba mkononi
kwa kutumia meno kisha kila mwanafunzi
aliyenisogelea alikuwa akiambulia meno tu, nilikuw
peku kabisa huku zile nguo nilizokuwa nimezivaa
zikawa zimetapakaa damu kidogo, hilo sikulihofia nikakimbia nakuongoza bara bara yakuelekea
Buguruni. Kundi kubwa la wanafunzi
likichanganyikana na watu wa mitaani na walimu
walikuwa nyuma yangu wakinifukuza kwa nia ya
kunikamata, nilishindwa hata kujielewa nguvu za
kukimbia nilipozitolea kwani nilikuwa na spidi ya hatari. Ndani ya muda mchache nilikuwa
nimeshakatisha vichochoro zaidi ya kumi na kwa
muda huu sikumuona hata mtu aliyeendelea
kunifuatilia kwa nyuma. Nilipofika tu Buguruni
nikaingia kwenye daladala ziendazo Gongo la
mboto, lengo langu likiwa nikushuka pale uwanja wa ndege ili niende kwa wazazi wangu Mwanza.
“..dada nauli yetu ipo wapi..?”
Aliongea kondakta baada ya kunishusha uwanja
wa ndege.
“..unataka nauli tu..? hii hapa chukuwa..?”
Nilivua nguo yangu ya ndani nakumfunulia naniii yangu kisha nikavaa nakukimbia zangu kuelekea
uwanja wa ndege huu abiria wote nikiwaacha
wakicheka kwenye daladala nakuondoka zao.
Nilipofika tu uwanja wa ndege, sikuwa na nauli
yeyote lakini nilijikuta na imani tofauti huku asilimia
zote nikiamini kwa njia yeyote lazima nitapanda ndege na nitafika mpaka nyumbani kwetu
Mwanza. Nikiwa bado naangaza huku na kule
kuangalia abiria mara..
“..Tinaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa….?”
Maskini mwili wangu wote ulininyong’onyea ghafla
baada ya kumuona Jerry, na nilishajisahau kama Jerry anafanya kazi uwanja wa ndege…
******* **
nini hatma ya Tina mikononi mwa Jerry..?
**
Inamaana Tina hajapata kumbukumbu kwa yale
aliyofanyiwa Bagamoyo..?
**
wazazi wa Tina wakijua itakuwaje..?
**
Je unaweza kutabiri Play gal itaishaje?
**
Utamu ndio kwaaanza unaanza na kumbuka hii
ndiyo Play gal (This is it..) kweli kweli, usikubali
ikupite inayokuja..
Niliishiwa nguvu nakujikuta nikiurudishia ule
mlango kama nilivyoukuta nakurudi sebuleni, ile
najigeuza tu nirudi zangu nilipotoka mara tena uso
kwa uso na mke wa Steve na safari hii alikuwa
kabadilika kidogo.....
'
Endelea…
Kadri macho yalivyokuwa yanamtoka huyu mke
wa Steve ndivyo mwili wangu ulizidi kunisisimka na
kunyong’onyea, nilijijaza nguvu za kishujaa
nakutoa mkono wangu taaratibu nakuusogeza
mpaka shingoni mwake kisha nikamkaba kwa
nguvu zangu zote. Macho yake yaliendelea kumbadilika na kwa sasa nilijihisi mikono yangu
kama inazidi kuwa laini huku nikihisi kama shingo
yake inakuwa kama tope tope.
“..Mamaaaa…!! Mamaaaa…!!!”
Uzalendo ulinishinda nakujikuta nikitoa sauti ya juu
huku ule mwili wa yule mwanamke ukizidi kupukutika nakuwa kama tope tope, ikafika
kipindi nikashuhudia mwili wake wote
ukimung’unyika mpaka akayeyuka kabisa. Nguvu
sikuwa nazo tena zaidi yakuendelea kukaa pale
pale chini huku nikitumia mikono yangu
kujikokotea mpaka sebuleni kisha nikapumzika. “..amkaaa…?, amkaaa kumekucha..”
Ilikuwa ni sauti ya Steve akiwa kavalia bukta
yakehuku mkononi akiwa kashikilia mswaki.
“..kumekucha, amka ukapige hata mswaki ili
unywe chai..”
Aliendelea kuongea Steve nakunifanya niendelee kumshangaa tu huku nisiamini yale yote
yalionitokea usiku.
“…Steve, wifi yuko wapi…?”
Nilimuuliza kwa makusudi ili nijue kilichotendeka
usiku ule alikuwa ni yeye au nani?
“..Yupo jikoni anapika chai, akimaliza ataleta hapa sebuleni utamuona tu, kwani vipi ulkuwa
unamuhitaji..?”
“..Hapana, nimemuulizia tu kwa maana sijamuona..”
Nilizuga nakuchukuwa mswaki kisha nikatoka
mpaka nje kwenda kupiga mswaki na nilipomaliza
nilijirudia zangu mpaka ndani ambapo tulikunywa chai kisha Steve akaniambia kuwa anaenda
kuomba ruhusa kazini kwake hivyo niwe tayari
atarudi kunichukuwa. Furaha na amani ya ajabu
iliendelea kunitawala ndani ya moyo wangu
japokuwa Steve alipoondoka tu ile amani
ikatoweka tena ghafla. “..Usiku ulikuwa unataka kufanyaje Malaya
wewe..?”
Aliongea mke wa Steve nakunifanya niingiwe na
uwoga huku mwili wangu ukianza kunisisimka.
“..Si naongea na wewe..? Mimi nilijua tu utakuwa
mchawi kweli na nimethibitisha ilo usiku Malaya mkubwa wewe tena Yule wa waume wa watu, na
umekutana na kisiki hapa nimechanjiwa toka
kwetu Kigoma Malaya mkubwa wewe..?”
Aliendelea kuniambia maneno ya ukali yule Mama
na muda wote sikuongea hata neno zaidi ya
kumtizama tu machoni mwake, Alivyoona nazidi kuwa kimya akanisogelea mpaka karibu
nilipokuwa nimeketi nakunishika shingoni
mwangu, hisia kali nilizipata nakufananisha tukio
kama lile la usiku wake alionifanyia. Sikutaka
kuonekana dhaifu tena hata kidogo kwani tayari
nilishaigundua dhamira yake hivyo nilifanikiwa kuvuta kistuli kilichokuwa karibu yangu pale
sebuleni kisha nikamvaa nacho mpaka kichwani
mwake akadondoka chini nakupoteza fahamu
hapo hapo.
“..huwezi kushindana na mtoto wa mjini..”
Nilijisemea kimoyo moyo huku nikimtolea fyonyo la dharau nakuingia mpaka chumbani kwake,
nilikagua kagua mpaka nikafanikiwa kuipata pochi
yake ambapo nilitoa kiasi kidogo cha pesa kama
shilingi elfu ishirini, nikachukuwa nguo zake
kwenye kabati lake la nguo nakuvaa. Ndani ya
muda mchache tayari nilikuwa nipo nje natafuta njia ya kuelekea kufika mpaka pale kituo cha polisi
kwa ajili ya kuonana na Steve. Kumbukumbu za
kufika pale kutuo cha polisi sikuwanazo zaidi ya
kukodi bajaji kisha ikanipeleka mpaka makaburini
pale nilipofumaniwa jana yake asubuhi na
nilipofika maeneo ya pale ilikuwa ni rahisi kupakumbuka kituo cha polisi kwani hakikuwa
mbali na mitaa ile ya makaburini.
“… Za sa hizi jamani…!! Samahanini namuulizia Steve
sijui nimemkuta..?”
“.. Ahaa mkuu Steve, yupo msubiri hapo pembeni..”
Aliongea Polisi mmoja aliyekuwa zamu ambapo hata jana sikumuona na ndio maana hata hana
kumbukumbu na mimi. Nilisubiri kidogo tu na
punde Steve alitoka ndani ya kile kituo mpaka
eneo nililopo.
“..OOoooh, Asia umekuja, mbona nilikuahidi
nitakuja kukuchukuwa nyumbani huko huko…” “..Hapana, nimeona kama nachelewa na mimi
kukaa huku kwenu Bagamoyo naogopa sana
yasije yakanitokea kama ya jana..”
“..Acha imani potofu bwana, hii siyo Bagamoyo ya
wachawi wala wanga kuwa na imani tu, utaishi
vizuri na kwa furaha tu, ennheee niambie vipi mke wangu umemuacha au katoka huko..?”
“.. Mkeo ameniacha hapo mtaa wa juu, kwani
alinisindikiza mpaka mitaa ilee, na hata nguo za
kubadilisha alinipa yeye tena asubuhi
ulivyoondoka, nimempenda sana anajua kuishi na
watu na anaonekana ana huruma..?” “..Ni kweli, mke wangu ni mkarimu sana kwa
wageni, anajua matatizo na shida za watu, naishi
naye vizuri sana tangu nimemuooa..”
Niliguna kimya kimya huku nikimtolea Jicho la
kujificha Steve kisha nikauchukuwa mkono yangu
nakuikutanisha mikono yangu na yake bila woga wowote.
“..Sasa Steve? Si umeshaomba ruksa, nakuomba
unirudishe basi Dar es salaam..?”
“..Hilo tu usijari, ila embu ngoja nimeshasahau kitu
ndani mara moja..”
Steve alirudi tena mpaka ndani ya ofisi, ndani ya muda mfupi akarudi na bahasha mkononi.
“..Sasa inatubidi turudi tena mpaka nyumbani
kwani mke wangu sijamuaga na pia kuna hela
natakiwa nimpelekee ili aende kununua vitu
sokoni kwani aliniambia kuwa vitu vimeisha..”
Nilionesha kukataa lakini Steve hakukubaliana na mimi kabisa hivyo nilipanda tena gari yake nakisha
safari ya kurudi nyumbani kwa Steve ikaanza tena.
Njia nzima nilitetemeka mithili ya mtu ambaye
hajawahi kuoga maji ya baridi na yupo sehemu ya
baridi. Niliogopa sana endapo Steve akijua mchezo
nilioufanya kwa mke wake. Kadri tuliyokuwa tunaenda ndivyo na mimi mapigo yangu yamoyo
yalivyokuwa yakinibadilika na kwenda kasi mno.
Hatimaye ndani ya kama dakika kumi tukawa
tumeshafika nje kwa Steve, tulijikuta wote mimi na
Steve tukitoa macho kwa mshangao tulipofika tu
nje ya nyumba yake kwani tulikutana na umati mdogo wakinamama huku kila mmoja akiwa
amejifunika khanga na kwa mbaali tulisikia vilio
kuashiria kuwa kuna msiba.
“..Ulivyoondoka ulikuacha salama huku..?”
Alinigeukia Steve nakuniuliza kwa ukali huku
amenitolea macho na akitafuta kitu mifukoni mwake..
“..Hao wakinamama ndio nawaona sasa hivi lakini..
Nikiwa bado namuelezea Steve kabla sijamalizia
kuongea mara ghafla simu ya Steve ikaita..”
“..Mkuu uko wapi…?”
“..Ndio naingia kwangu lakini kidogo nahisi hali si nzuri kwani vipi..?”
“..Ni kweli na kabla hujafika ni kwamba kuna binti
amonekana hapo kwako ametoka kwa haraka
sana na inasemekana anahusika na kifo cha mkeo
kwani mashuhuda wamemuona akitoka huku
amechanganyikiwa na hali tuliyomkuta nayo marehemu mkeo ni kapigwa na stuli eneo la
nyuma ya kichwa nakusababisha umauti wake…”
Steve alinigeukia huku akitoa machozi na mishipa
ya shingoni mwake ikimtoka vilivyo, alitoa pingu
nakunifunga mkono mmoja na mwingine
akanifunga kwenye msteringi wa gari yake kisha akatoka nakufunga vioo vyote vilivyokuwa na
tinted kisha akaloki milango yote akaelekea ndani
kwake huku akiniacha peke yangu ndani ya gari..
Bado nilikuwa sijielewi elewi pale ndani ya lile gari,
nilijaribu kuangalia huku na kule lakini haikusaidia
kitu, kila nikilipenyeza jicho langu kupitia kioo cha mbele ya gari ndivyo hasira nazo zilikuwa zikinijaa.
“..Najuta kuja huku Bagamoyo na sitorudia tena
eeeh! Mungu niponye tu…”
Nilibaki naongea peke yangu huku nikijihisi koo
langu limeshikwa na kwikwi na siyo kwikwi ya
hasira tu bali kwikwi ya hasira kali niliyokuwa nayo, kwa sasa macho yangu nilijihisi kama
yanatoa machozi tena yale machozi ya hasira kila
nikiona umati wa wakinamama na wakina baba
ukiongozana kuingia mpaka ndani na wengine
wakipishana kwa kutoka nje. Ndani ya muda
mchache tayari nilishuhudia Steve akiongozana na wenzake kuubeba mwili wa marehemu
nakuupeleka mpaka kwenye gari lilokuwa
pembeni yangu. Akili ilianza kunichemka huku
nikiangalia huku na huku ndani ya gari japo
kuambulia chochote niweze kujinusuru katika
hatari niliyokuwanayo. Ndani ya muda mchache nilifanikiwa kugundua funguo zikiwa
mchanganyio na hata muonekano wake ulionesha
wazi hazikuwa funguo za nyumba bali zilikuwa ni
funguo kama za pingu japo sikuzijua sana,
nilizichukua nakuanza kuzijaribisha moja baada ya
nyingine bila ya mafanikio yoyote. Nikiwa bado nashangaa shangaa kuzikagua zile funguo mara
nikahisi mtu anagonga kwenye dirisha la kioo.
“..nani..? nani…?”
Niliongea kwa sauti bila kusikia chochote, nilijijaza
moyo wa kijasiri nakuendelea kuzitafuta funguo za
kuweza kufungua pingu ambazo zilikuwa zimeshikamana na msteringi wa gari hili la Steve.
Nilijitahidi kuzifungua kwa kutumia mdomo
waangu na meno huku nikifungua kwa nguvu
zote. Sikuweza kufanikiwa kufungua lakini
halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi fasta
nakuamua nijiweke vizuri nakuliwasha gari kwa kutumia waya kama wafanyavyo wezi wa magari.
Ndani ya muda mchache niliweza kuliwasha gari
hivyo nikalirudisha nyuma nakuondoka kimya
kimya huku nikiamini kwa asilimia zote Steve
atakuja kugundua baadaye sana ambapo tayari
nitakuwa nimeshafika mbali. Kuwepo kwa barabara nyingi na kona kona za hapa na pale
ndicho kilichonisababisha nisielewe njia ya
kutokea kuelekea Dar es salaam. Sikutaka hata
kufungua vioo zaidi ya kuongoza hivyo hivyo tena
nikiwa nimejibana bana mapaja yangu na msteringi
nimeukumbatia huku nikitoka kwa mwendo wa kawaida tu. Sikuweza kufika mbali sana kutokana
na kuchoka kwanza kwa pingu nilizokuwa nazo
na pili sikuielewa haswa barabara ya kuelekea Dar
es salaam. Niliisimamisha gari baada ya kutembe
kwa mwendo kidogo kutoka lile eneo ambalo
alikuwa akiishi Steve na kwa sasa nilikuwa eneo wanaloziba pancha na kutengeneza magari
mabovu, pale pale nikafungua mlango nakumuita
kijana mmoja.
“..Mambo vipi…?”
“..Poa tu Sister vipi pancha nini…?”
“..Hapana, unaniona hapa mkononi, haya fanya ufanyavyo unitoe hizi pingu sasa hivi na kuhusu
pesa wala hata usijali”
“..Kwa hilo tu Sister!, wala usihofu tena nafanya
mwenyewe, vipi utanipa shilingi elfu kumi na
tano..?”
“..kuhusu pesa ondoa shaka..” Yule kijana hakutaka kabisa kuchelewa zaidi ya
kutoka mbio pale nakurudi na spana mbali mbali
ikiwa ni pamoja na msumeno mkubwa. Zoezi la
kama dakika tanotu lilikuwa tosha kwa huyu
kijana kunitoa pingu ambazo zilishikana na
msteringi wa gari. Amani kubwa iliyoambatana na furaha ya ajabu ilianza kuninyemelea ndani na nje
ya mwili wangu nakutamani sana nifike Dar kwa
muda mfupi. Nilitoa ile pochi ambayo niliichukuwa
kwa mke wa Steve nakutoa noti mbili za shilingi
elfu kumi kumi nakumpatia Yule kijana kisha
akanirudishia chenchi nakuondoka zangu huku nikijidai kuulizia duka maeneo ya pale. Vichochoro
viwili vitatu vilinitosha kabisa kutoroka na
kulitelekeza gari la Steve huku nikiulizia sehemu
ambayo ninaweza japo kupata usafiri wa daladala
au hata bajaji.
“..Mpaka stendi shiingi ngapi..?” “..Utanipa buku mbili tu..”
Nilichukuwa pikipiki kisha nikampatia hela ya
kunifikisha mpaka Dar es salaam kabisa kwani
niliamini endapo nitachukuwa daladala itakuwa
rahisi sana kushikwa na Steve au mapolisi
wenzake. Piki piki ilikuwa iko spidi sana, dereva hakutaka hata kidogo kuchelewa , upepo mkali
uliokuwa ukinipuliza njiani, hatimaye tukafika
maeneo ya bunju ambapo kwa bahati mbaya
pikipiki ikaanza kutoa mlio wa ajabu kuashiria
kuwa kuna itilafu ndani yake. Nilimpatia pesa yake
lakini alioneka kuchukizwa na mimi kumpatia hela . Sikumuelewa hata kidogo anachomaanisha hadi
alipovua kofia na miwani ndipo na mimi
nikamgundua.
“…waaat, ooohh kumbe ni weweeeeee, noooo…!
Noooo…! Noooo…?”
“Masikini nimekwisha Tina mimi…!” Niliropoka kwa sauti ya juu baada ya kumgundua
yule mtu kuwa alikuwa ni yule mzee alionifanya
mpaka nikajikuta nimeamkia makaburini tena uchi
wa mnyama kabisa na kwa muda huu kumbe
alikuw ni dereva pikipiki na alionesha kuchukizwa
baada ya kumlipa pesa yake. “..Ulinitoroka na leo ndioleo na unabahati nilikuwa
nakupeleka mpaka kwa wakuu wa mizimu kwa
babu zangu Tegeta shetani mkubwa tena malaya
usiye na hila wewe”
Aliendelea kufoka Yule kijana nakunishika mkono
huku akiiacha pikipiki yake nakuniburuta nilijitahidi japo kugoma lakini nilipata makofi na
ngumi huku akiniburuta kwa nguvu zake zote tena
eneo ambalo hata sikulijua. Kadri alivyokuwa akinivuta ndivyo na mimi
nikaanza kupata nguvu za ajabu huku nikijihisi lile
eneo la usoni ambalo nilichanjwa kipindi kilee
likiniuma sana.
“..Hunijui..? leo ndio utanijua vizuri..”
Nilijikuta naropoka tena kwa ujasiri wa hali ya juu. Sasa nilishindwa kuelewa kuwa ni nguvu za
kichawi alizokwa nazo huyu mzee au la kwani hali
ya hewa ilibadilika ghafla kiasi kwamba nikaanza
kunyeshewa na mvua tena ile mvua ya mawe,
niliendelea kuvutana na Yule mzee japo sikupata
msaada wowote kwani sikuweza kumuona mtu yeyote zaidi ya kuwa sisi wawili tu tukisumbuana.
“..Sema mwenyewe..?, unataka tukuue au ujiunge
na kundi letu..?”
“..niacheni jamani.., mie sitaki choc…”
Kabla sijamalizia tu kuongea nilishangaa napokea
bonge la kibao kutoka kwa mtu ambaye sikumuona lakini sauti tu za watu wengi ndizo
nilizisikia zikinihoji. Mwili wangu kwa sasa ulikuwa
kama sugu kwani hata yale maumivu sikuyasikia
zaidi ya kuhisi tu nimepigwa na mtu nisiyemuona. ******** Maumivu ya kichwa yaliochanganyikana na
uchovu huku upepo ukivuma sana nakujikunyata
kwa kuhisi baridi kali. Kila nikiendelea kutoa
macho nakuliangalia hili eneo bado nilikuwa
sipajui ni sehemu gani japo palikuwa ni kama
jangwa kumbwa lililojaa michanga tupu, akili yangu yote ilikuwa imenivurugika na kusababisha
kumbukumbu zote kunipotea.
“..hapa ni wapi..? Nirudisheni kwetu.., Baba yangu
yuko wapi..?”
Niliuliza kwa sauti ya ukali huku nikimfuata Bibi
mmoja aliyekuwa pembeni yangu na kwa muda huu alionesha kuwa yuko ‘busy’ sana, alikuwa
peke yake tu, nilimsogelea mpaka karibu na kwa
hasira nilizokuwa nazo ukichangia na
kutokujitambua vizuri, nilimshika kitenge chake
alichokuwa amekivaa nakukivuta kwa nguvu
mpaka nikahakikisha amebaki uchi wa mnyama. “..nani aliyenileta huku..? si nakuuliza wewe
kibibi..?”
Alinitolea macho tu bila kunijibu chochote.
“..sasa leo mie nataka mnirudishe kwa wazazi
wangu, wapumbavu sana nyie..?”
Nilijikuta nachota mchanga kwa hasira huku nikimwagia nao Yule Bibi na mwingine nikimlisha
mdomoni, kadri nilivyokuwa nikimtesa huyu Bibi ili
japo anioneshe kwa wazazi wangu ndivyo alikuwa
akibadilika nakuwa kama ule mchanga niliokuwa
nikimwagia. Maskini Tina mimi, nguvu zilianza
kunilegea na ule woga ukaanza kunitanda tena katika lile eneo, mara nikahisi kama kuna umati wa
watu umetanda japo sikuwaona lakini sauti za
watu wakicheka na kujibizana ambao sikuweza
kuwaona ndizo zilikuwa zikichochea hisia zangu
kwa haraka zaidi. KESHO YAKE ASUBUHI “…Tinaaaa…? Tinaaaa weweeee…? Enheee vipi..?
Umekuja saa ngapi shosti..?”
Bado nilitoa macho huku na kule huku nisielewe
elewe kabisa nimefikaje fikaje hapa chuoni CBE,
marafiki zangu walitanda kunishangaa kitandani
mwangu wakiongozwa na rafiki yangu kipenzi Aisha.
“..Shosti kwani vipi ulifiwa nini..? Pole na umekuja
saa ngapi..?”
“..Hapana mbona wala hata sikufiwa jamani kwani
vipi..?”
“..Shosti yani na lijiupara lote hilo bado unatudanganya..? Pole bwana, kwani umefiwa na
mzazi yupi..?”
Niliona kama wananizungua, niliamka pale
kitandani mpaka kwenye kabati langu la vipodozi
ambapo kuna kioo kikubwa nikajiangalia. Mchozi
ulianza kunidondoka taratibu baada yakujigundua nimenyolewa upara huku uso wangu ukiwa na
chanjo chanjo kama kabila lile la wamakonde
kutoka Mtwara. Niliumia sana moyoni nabado
nilikuwa sina kumbukumbu za kutosha ilikuwaje
kuwaje zaidi ya kukumbuka tu nilienda Bagamoyo
na huko nilifanikiwa kumuona Steve halafu akanipa hadi nauli nikarudi zangu Dar..
“..nani aliyenichanja…?, nauliza nyie, nani humu
bwenini amenifanyia hivi..?”
Niliwageukiwa marafiki zangu pale bwenini
nakuwauliza kwa hasira zote nakuwafanya
waanze kuniogopa tena siyo kwa ukali tu bali kwa sura yangu ilivyokuwa inatisha.
“..kuna niliyemchukulia bwana wake humu
ndani...? kwanini mnifanyie hivi..? Aisha rafiki
yangu nani aliyenifanyia mchezo huu, heee..? Na
kwanini mimi tu jamani mnanifanyia hivi..,
nimewafanya nini jamani.., au kwakuwa siingiagi darasani mara kwa mara eeenh..?”
Niliongea kwa jazba huku nikibubujikwa na
machozi, kadri nilivyokuwa nikiongea ndivyo na
umati wa wanafunzi wenzangu kutoka mabweni
mengine ulikuwa ukijaa ndani ya chumba chetu
kuja kunishangaa, hasira zilinizidia zaidi ya pale mpaka nikajikuta nachukuwa nguo zangu kabatini
na nyingine nikizitoa kwenye begi pamoja na viatu
vyangu vyote huku nakuzikusanya pamoja
nakutoka mpaka nje, nikarudi tena mpaka bwenini
tena nakukukusanya vipodozi vyangu vyote
pamoja na kiberiti nakutoka navyo mpaka nje, nakuanza kuvichoma moto kwa hasira kali
niliokuwa nayo.
“..Tinaaa, Tinaa rafiki yetu umekuwaje lakini..?”
“..Niacheni, si ndiyo mlivyotaka mfurahi haya
furahini sasa..?, furahini na mpige na vigele gele
kabisa..?” Walinifuata marafiki zangu mpaka nje nakunizuia
lakini haikusaidia chochote zaidi ya ule moto
kuongezeka kasi huku vipodozi vyangu
vikiendelea kuharibika. Niliuacha ule moto
ukiendelea kuwaka pale nakutoka mpaka dukani
ambapo nilinunua viwembe kama viwili nakurudi tena mpaka bwenini, sikujali makelele ya wanaume
wa hapa chuo tena wale waliokuwa wananifuata
nyuma nyuma nakunicheka huku wengine
wakinizomea. Niliongoza mpaka bwenini na
nilipofika nilifungua vile viwembe nakuanza
kujichanja zaidi ya nilivyoukuwa mwanzo. “..Hapana Tina usifanye hivyoo, usifanye hivyo..?”
“..Embu niacheni, nyie si ndio mmeyataka haya yote
nakunifanya hivi.., niacheni nijimalizie mpendwe
nyinyi, acha niwe mbaya si mlinichanja niwe mbaya
wacha nijiendeleze mwenyewe..?”
Tayari niikuwa kama nusu chizi kwa kuchanganyikiwa, walimu wa chuo walikuja
mpaka bwenini kuingilia kati swala langu,
walinishika lakini nilikuwa na nguvu za ajabu sana,
iliwachukuwa muda mpaka kufanikiwa kunifunga
kamba mikononi.
“..mpelekeni ofisini huyu..?” Nilisikia sauti ya mwalimu mmoja akiwambia
wanafunzi wa kiume wanipeleke mpaka ofisini
kwake, wanafunzi walikuwa ni wengi sana
wakinishangaa kwa jinsi nilivyokuwa nimebadilika
ghafla nakuwa Tina kichaa, kadri walivyokuwa
wananivuta nakunipeleka huko ofisini ndivyo na mimi nguvu zilikuwaa zikiniongezeka mara mbili ya
pale nakujikuta niking’ata zile kamba mkononi
kwa kutumia meno kisha kila mwanafunzi
aliyenisogelea alikuwa akiambulia meno tu, nilikuw
peku kabisa huku zile nguo nilizokuwa nimezivaa
zikawa zimetapakaa damu kidogo, hilo sikulihofia nikakimbia nakuongoza bara bara yakuelekea
Buguruni. Kundi kubwa la wanafunzi
likichanganyikana na watu wa mitaani na walimu
walikuwa nyuma yangu wakinifukuza kwa nia ya
kunikamata, nilishindwa hata kujielewa nguvu za
kukimbia nilipozitolea kwani nilikuwa na spidi ya hatari. Ndani ya muda mchache nilikuwa
nimeshakatisha vichochoro zaidi ya kumi na kwa
muda huu sikumuona hata mtu aliyeendelea
kunifuatilia kwa nyuma. Nilipofika tu Buguruni
nikaingia kwenye daladala ziendazo Gongo la
mboto, lengo langu likiwa nikushuka pale uwanja wa ndege ili niende kwa wazazi wangu Mwanza.
“..dada nauli yetu ipo wapi..?”
Aliongea kondakta baada ya kunishusha uwanja
wa ndege.
“..unataka nauli tu..? hii hapa chukuwa..?”
Nilivua nguo yangu ya ndani nakumfunulia naniii yangu kisha nikavaa nakukimbia zangu kuelekea
uwanja wa ndege huu abiria wote nikiwaacha
wakicheka kwenye daladala nakuondoka zao.
Nilipofika tu uwanja wa ndege, sikuwa na nauli
yeyote lakini nilijikuta na imani tofauti huku asilimia
zote nikiamini kwa njia yeyote lazima nitapanda ndege na nitafika mpaka nyumbani kwetu
Mwanza. Nikiwa bado naangaza huku na kule
kuangalia abiria mara..
“..Tinaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa….?”
Maskini mwili wangu wote ulininyong’onyea ghafla
baada ya kumuona Jerry, na nilishajisahau kama Jerry anafanya kazi uwanja wa ndege…
******* **
nini hatma ya Tina mikononi mwa Jerry..?
**
Inamaana Tina hajapata kumbukumbu kwa yale
aliyofanyiwa Bagamoyo..?
**
wazazi wa Tina wakijua itakuwaje..?
**
Je unaweza kutabiri Play gal itaishaje?
**
Utamu ndio kwaaanza unaanza na kumbuka hii
ndiyo Play gal (This is it..) kweli kweli, usikubali
ikupite inayokuja..
