Elections 2010 Pingamizi la CHADEMA latupwa

Tanzania inamhitaji mtu atakayesimama katika falsafa za Hayati Luck Dube, kama utahitaji kusimama katika haki na kweli, kubali kusimama peke yako. Utegemezi ni mdudu atakayetumaliza. Anyway all ears are upon the media kujua hatma.
 
hahahaha

tendwa katendwa jamani!

ushahid wa ccm hauna mashiko wameelekezwa namna ya kuandika upya then wampe tendwa
 
Kwa walio Jijini Dar es salaam, Msajili wa vyama vya siasa Ndg, J. Tendwa alitegemewa kuzungumza na vyombo vya Habari leo kutoa maamuzi juu ya Pingamizi la CHADEMA dhidi ya JK wa CCM, je maamuzi yashatoka, tunaomba mwenye updates atujuze

walisema NEC ndiyo inatoa pingamizi lakini Tendwa ndiye anapaswa kushauri kutokana na maelezo ya wahusika na pia atatoa copy ya ushauri wake kwa vyama husika
 
Yaani wewe post ya kwanza unaanza na kuomba updates kuna mtu humu ulimtuma be serious mpigie simu Tendwa atakuwa nazo
Ringmaster
Join Date Mon Sep 2010
Posts 1
Thanks : 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power 0


acha hizo bwana, we kata issue

ss wazoefu tunajua watu wan id zaidi ya moja na hatushangai kuona mtu kajiunga saa hii na akauliza au kuchangia kitu ambacho tulizungumza miaka mingi nyuma

na huu upumbavu wa kufatiliana nani kaingia lini inasidia nn ?
 
Huyu Msajili nadhani kaenda nyumbani kwa Rais... well hajapewa Tsh 60Million? na ahadi za Ukuu wa wilaya kwenye new established Wilaya's uh ni maporini... atapotea...

CCM hakuna haki so Msajili hatatoa haki...
Demokrasia sio haki?
 
walisema NEC ndiyo inatoa pingamizi lakini Tendwa ndiye anapaswa kushauri kutokana na maelezo ya wahusika na pia atatoa copy ya ushauri wake kwa vyama husika

Cha msingi, Tendwa hana maamuzi. Akikubali pingamizi tu ni kwamba kazi hana kwa hiyo tusitegemee jipya sana. Pia Kungekua na TUME huru, Msajili huru hapo sawa. Kami ni msajili wa vyama, kwa nini ateuliwe na chama kimoja tu ili hali kuna vyama vingi? CCM wangejua hii sheria ingekua hivi basi, wangeisubirisha hii sheria waliipitisha fasta sana.
 
Cha msingi, Tendwa hana maamuzi. Akikubali pingamizi tu ni kwamba kazi hana kwa hiyo tusitegemee jipya sana. Pia Kungekua na TUME huru, Msajili huru hapo sawa. Kami ni msajili wa vyama, kwa nini ateuliwe na chama kimoja tu ili hali kuna vyama vingi? CCM wangejua hii sheria ingekua hivi basi, wangeisubirisha hii sheria waliipitisha fasta sana.


acheni double standard kule nyamagana, yule alipambana na masha kakata rufaa na kashinda na kampeni zimeanza ooh wako makini na uamuzi uko sawa, ila wakiamua hukumu dhidi yenu hawako fair wamechaguliwa na rais.


hivi wanapotoa haki kwa upande wenu wanakuwa wamechaguliwa na mbowe ?
 
Haha, wadau hii ni ile nchi ya kichaa, inayoongozwa na mfalme Juha... Hakuna haki hapa.., na kipimo cha maamuzi ni RATILI MOJA=PESA MOJA!! Sahau Tendwa kufuata kanuni nyengine! Sahau kabisa!!
 
Source: JIACHIE

Sina taarifa yoyote ya kutoa kuhusiana na pingamizi la CHADEMA dhidi ya mgombea urais wa CCM-Tendwa
Monday, September 6, 2010

Msajili wa vyama vya siasa nchini,John Tendwa amesema leo hana taarifa yoyote ya kutoa kuhusiana na pingamizi la CHADEMA dhidi ya mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa aliahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi bila kuhusisha Bunge kitu ambacho kinaenda kinyume na sheria ya Fedha za Uchaguzi.

Bw. John Tendwa alikuwa ameahidi kutoa taarifa baada ya siku tano, hata hivyo leo waandishi wa habari walipokwenda ofisini kwake kwa ajili kutaka kujua hatma ya suala hilo, alisema kuwa leo ana mkutano mwingine, na kuhusu pingamizi la CHADEMA tayari ameshavijibu vyama na pia taarifa ipo Tume ya Uchaguzi ya Taifa . Hivyo akashauri Waandishi hao waende kwa vyama husika na kuwauliza, aidha akaongeza kuwa vyama hivyo pia bado vitalazimika kuwa na muda wa kutosha kupitia kwa kina majibu hayo.
 
Source: JIACHIE

sina taarifa yoyote ya kutoa kuhusiana na pingamizi la chadema dhidi ya mgombea urais wa ccm-tendwa
Monday, September 6, 2010

Msajili wa vyama vya siasa nchini,John Tendwa amesema leo hana taarifa yoyote ya kutoa kuhusiana na pingamizi la CHADEMA dhidi ya mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa aliahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi bila kuhusisha Bunge kitu ambacho kinaenda kinyume na sheria ya Fedha za Uchaguzi.

Bw. John Tendwa alikuwa ameahidi kutoa taarifa baada ya siku tano, hata hivyo leo waandishi wa habari walipokwenda ofisini kwake kwa ajili kutaka kujua hatma ya suala hilo, alisema kuwa leo ana mkutano mwingine, na kuhusu pingamizi la CHADEMA tayari ameshavijibu vyama na pia taarifa ipo Tume ya Uchaguzi ya Taifa . Hivyo akashauri Waandishi hao waende kwa vyama husika na kuwauliza, aidha akaongeza kuwa vyama hivyo pia bado vitalazimika kuwa na muda wa kutosha kupitia kwa kina majibu hayo.


wawafate CHADEMA period
 
Sasa hivi imekaribia saa 12 jioni..Ok, sisi wote ni mabwege, si ndiyo bwana Tendwa, well and good!!
Mind you, this gonna cost you and your superiors! time will tell
 
Aliahidi statement within siku tano au baada ya siku tano? Kuna tofauti kubwa hapo.
 
Msajili wa vyama vya siansa amelitupa rasmi pingamizi la chadema dhidi ya mgombea urais wa CCM. Makamba amelizungumzia hilo kutokana na barua aliyoipata toka kwa msajili

Msajili amesema hana mamlaka ya kutangaza bali kuwatumia barua wahusika yaani CCM na CHADEMA
 
hahahaaaaa!!! Walewale. Natamani kuihama Tanzania!! Pweza Paolo nielekeze pa kwenda...:mad2:
 
Back
Top Bottom