Mkuu Azimio Jipya naona umekasirika mpaka umesahau ku-edit ulichoandika.... Nimekuelewa. Hizi bluu nilizopaka ndio ulichokisema kwa uchungu nami nakubaliana nawe kwa kiasi kikubwa. Kimsingi Civil War ya Tanzania inatengenezwa na wanaofikiri watabaki salama kwa civil war hiyo. Kwa mfano, salamu za Red Guard na Blue Guard ilikuwa ni kujibu Green Guard. Hivyo, huhitaji kuumiza sana kichwa kuelewa ni kwa nini Green Guard haikemewi na watawala wakati inatumika kuumiza watu. Matokeo yake ndio haya, na reaction ya serikali imekuwa kama ulivyoandika.
Binafsi sifurahii hali ya uvunjifu wa amani, kinachotokea Tanzania ni watu kutumia fikra zao ili kuendelea kuhifadhi amani yao. Pengine ndio inabidi tujadili hii namna mpya ya kujilinda kuanzia sababu zilizotufikisha hapa, matokeo yake na namna gani tutarejea kwenye misingi yetu mizuri tuliyoipoteza kutokana na uongozi wa serikali kama ulivyoelezea.