Picha za Green Guard, Red Brigade na Blue Guard

Picha za Green Guard, Red Brigade na Blue Guard

Iliwahi kuvumishwa kuwa Kikwete anashauriwa vibaya, halafu washauri wake wakalaumiwa sana. Sasa alipokurupuka kuilalamikia chadema ati isithubutu kuanzisha Red Brigade napo alishauriwa vibaya ama ni mwendelezo wa majanga!

hapa ni sawa na wachawi kugongana uso kwa uso kwenye safari zao.

inabidi tukubali kuwa siasa za CCM ni cha mtoto kwa siasa za CHADEMA...chadema noma1
 
7+Nape+na+viongozi+waliompokea+wakiwasili+kwenye+kambi+ya+Baraza+la+Vijana+wilaya+ya+Missenyi.jpg
 
Kwa ufupi ni kwamba tamko la CHADEMA litakuwa ama chanzo cha kufungwa kwa biashara hii ya kuwatumia vijana na watoto ndivyo sivyo, au si ajabu ukawa ndio mwanzo wa 'kuviimarisha' kabisa vikosi hivi, maana vyama vitaanza kushindana nani ana jeshi kali zaidi.

Pengine pia tumepeta hoja ya nyongeza kwenye ibara ya katiba mpya inayohusu vyama vya siasa. Iwe "marufuku kwa vyama vya siasa kuonesha kusudio la kuanzisha, au kuazisha jeshi au kikundi chochote chenye kufanana kwa namna yoyote ile na jeshi"
Waridi, Mimi naona kwa vyovyote vile GUARDS zote ni mali ya Rais chini ya serekali yake. Kwani haziko juu ya sheria za kuvipa nguvu zaidi ya jeshia la Polisi na la Ulinzi!!

Kama political guards zinakuwa na nguvu hadi kufanya viongozi wa polisi na Rais aanze kuzitolea matamko that means ... Polisi, JWTZ na vyombo vingine vya ulinzi .... Viko wapi? Ikimaanisha Credibility ya serekali ichukuliweje?

Sisiti kusema kuwa safari ya kuwa na Umoja wa Kitaifa chini ya vyama vingi kwa nchi nyingi za Africa ni safari ndefu.

Kwani vyama badala kuimarisha UTAIFA kwa manufaa ya Maendeleo ya jamii vinaimarairhs UCHAMA na JESHI LA ULINZI la kila Chama ... Kama huo sio Ujinga na Ujuha ni nini? Kama huo sio mwito wa kumuita Mkoloni aje atukomboe tusije uuana na kumalizana kwa majeshi ndani ya majeshi ni nini?

Nani kakumabia tuko tayari Kutuwwa Uhuru wa Kitaifa?
 
Last edited by a moderator:
Hawa nao ni Green Guard?

22.jpg
 
Kwani vyama badala kuimarisha UTAIFA kwa manufaa ya Maendeleo ya jamii vinaimarairhs UCHAMA na JESHI LA ULINZI la kila Chama ... Kama huo sio Ujinga na Ujuha ni nini?

Juzi tuu tuliambiwa na wafuasi wengi wa Chadema na CCM hapa hapa jamvini kuwa kwa mwenyekiti wa Chadema kwenda kunywa togwa Ikulu na Rais ndiyo utaifa.
 
Iliwahi kuvumishwa kuwa Kikwete anashauriwa vibaya, halafu washauri wake wakalaumiwa sana. Sasa alipokurupuka kuilalamikia chadema ati isithubutu kuanzisha Red Brigade napo alishauriwa vibaya ama ni mwendelezo wa majanga!

hapa ni sawa na wachawi kugongana uso kwa uso kwenye safari zao.

inabidi tukubali kuwa siasa za CCM ni cha mtoto kwa siasa za CHADEMA...chadema noma1

Mimi naagalia swala zima kwa picha kubwa zaidi! Rais kasema aliyosema, washauri wake wamempotosha au wao ndio walipotoshwa hiyo sio hoja kubwa!

Hoja ya msingi hapa ni kuwa kuna Guards TATU ndani ya nchi ambazo ni dhibitisho kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vinahitaji kujaziliwa kwa kuwa na mapungufu. Kibaya zaidi ni kuona serekali ambavyo haijielewi wala haijajipanga katika ku manage hizi guards kwa haki. Kila Mtu kwenye serekali anaibuka na kusema jambo lake kuhusu guards, sereakali na viogozi wake ndio wanajichanganya kabisa hawana mtizamo mmoja wa kuvisemea vyobo hivyo nayo inaigia kwenye malumbano yasiyo na msingi hasa ikitetea Guard yake!-

Guards Tatu kwa vyama vitatu vya siasa, kwani imekuwa sawa na Nchi tatu ndani ya nchi moja kila moja na jeshi lake? Yet serekali nayo inaiigia kwenye mvutano wa kitoto kama huu ...? Lets be-serious do you real know what is a civil war?

Watanzania tuamke tuache mzaha wa kisiasa kwa maisha yetu ...!!!
 
Mimi naagalia swala zima kwa picha kubwa zaidi! Rais kasema aliyosema, washauri wake wamempotosha au wao ndio walipotoshwa hiyo sio hoja kubwa!

Hoja ya msingi hapa ni kuwa kuna Guards TATU ndani ya nchi ambazo ni dhibitisho kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vinahitaji kujaziliwa kwa kuwa na mapungufu. Kibaya zaidi ni kuona serekali ambavyo haijielewi wala haijajipanga katika ku manage hizi guards kwa haki. Kila Mtu kwenye serekali anaibuka na kusema jambo lake kuhusu guards, sereakali na viogozi wake ndio wanajichanganya kabisa hawana mtizamo mmoja wa kuvisemea vyobo hivyo nayo inaigia kwenye malumbano yasiyo na msingi hasa ikitetea Guard yake!-

Guards Tatu kwa vyama vitatu vya siasa, kwani imekuwa sawa na Nchi tatu ndani ya nchi moja kila moja na jeshi lake? Yet serekali nayo inaiigia kwenye mvutano wa kitoto kama huu ...? Lets be-serious do you real know what is a civil war?

Watanzania tuamke tuache mzaha wa kisiasa kwa maisha yetu ...!!!

Mkuu Azimio Jipya naona umekasirika mpaka umesahau ku-edit ulichoandika.... Nimekuelewa. Hizi bluu nilizopaka ndio ulichokisema kwa uchungu nami nakubaliana nawe kwa kiasi kikubwa. Kimsingi Civil War ya Tanzania inatengenezwa na wanaofikiri watabaki salama kwa civil war hiyo. Kwa mfano, salamu za Red Guard na Blue Guard ilikuwa ni kujibu Green Guard. Hivyo, huhitaji kuumiza sana kichwa kuelewa ni kwa nini Green Guard haikemewi na watawala wakati inatumika kuumiza watu. Matokeo yake ndio haya, na reaction ya serikali imekuwa kama ulivyoandika.

Binafsi sifurahii hali ya uvunjifu wa amani, kinachotokea Tanzania ni watu kutumia fikra zao ili kuendelea kuhifadhi amani yao. Pengine ndio inabidi tujadili hii namna mpya ya kujilinda kuanzia sababu zilizotufikisha hapa, matokeo yake na namna gani tutarejea kwenye misingi yetu mizuri tuliyoipoteza kutokana na uongozi wa serikali kama ulivyoelezea.
 
Back
Top Bottom