Picha ya Marafiki wa Lowassa

Picha ya Marafiki wa Lowassa

ukiona mtu anatabasamu kwenye kuzika ujue ni psychopath au kwa tafsiri nyingine anafurahia, angalia picha ...
"Mwaka 1995 siku moja asubuhi nikapokea ugeni mtoto akaja chumbani kuniambia baba kuna ugeni nikawakuta marafiki zangu watatu, Samwel Sitta, Edward Lowassa na Rostam Aziz, wakaja kuniambia kwamba tunataka muende na Edward Dodoma mkachukue fomu ya kugombea urais mimi nikasema jambo hilo halipo kwenye mawazo yangu, kama yeye lipo kwenye mawazo basi aende, naye akasema siendi bila ya wewe,"- @jmkikwete


"Basi tukabishana mpaka tukakubaliana kwamba wacha twende, tukaenda kuchukua fomu zile tukazijaza zikarudishwa, michakato ndani ya chama mwenzangu hakubahatika mimi nikabahatika kuwemo kati ya wale watano na baadaye tukapiga kura kwenye NEC nikawemo katika wale watatu, tukaenda mkutano mkuu nikawemo katika wawili, lakini kura zangu hazikutosha akapata Mzee Mkapa nikaja kuwa Waziri wake wa Mambo ya Nje na mwenzangu akaja kuwa Waziri," - Jakaya Kikwete, Rais Mstaafu


#RIPLowassa
 
Dah huyu Mzee tulimuita Fisadi pale Mwembe Yanga tukamuweka kwenye list of shame.

Baadaye akatubu akawa mgombea Urais wetu na tukakesha usiku na mchana tukimshangilia na kuzungusha mikono akawa shujaa wetu huku tukimsafisha na kumuimba tena sio mwizi.

Kuna siku kumbe RA au JK wanaweza kuwa wagombea wetu Urais na kuwasafisha kila mahala.

ndani ya viunga vya Hodeidah Yemen.
 
Ulichelewa sana kufaham hili mkuu, huyu ni mwanamtandao mahiri sana na alipendwa sana na lowasa ndio nguvu ya Jk ikatumika kuigawa nzega iwe na majimbo mawili kwaajili ya kumzawadia bashe
Aiseee!
Kumbe ndio maana!!
 
Gazeti la Rai ( nguvu ya hoja ) lilitumika kumpeleka Jakaya ikulu kwa kuwachafua wagombea wengine kwa kashfa mbalimbali ( salvation rweyemamu ) aliongoza mapambano.
Bashe alikuja kuwa CEO wa HC
Hii issue ya rweyemamu niliwahi kuisikia, hawa jamaa wa mtandao si wa jana wala juzi aisee!
 
Ilikuwa serious,
Kwa jinsi Lowassa alivyokuwa amejipanga kuutwaa Urais.
Hakuwa anatania.
Nadharia njama (conspiracies theories) zipo nyingi sana kuhusu kundi hili... Lakini kwa mtazamo wangu nathani kiunganishi hapo cha hao watu (Gravity force) ni Rostam Azizi.

Nadhani yeye ndiye anaweza kukaa na kila mmoja wa kwenye kundi lao hata kama wenyewe kwa wenyewe wamegombana!
 
Bashe ni kada loyal wa EL then connect dot to RA
 
Nadharia njama (conspiracies theories) zipo nyingi sana kuhusu kundi hili... Lakini kwa mtazamo wangu nathani kiunganishi hapo cha hao watu (Gravity force) ni Rostam Azizi.

Nadhani yeye ndiye anaweza kukaa na kila mmoja wa kwenye kundi lao hata kama wenyewe kwa wenyewe wamegombana!
Pole pole alisema wale hawagombani, ukiona ugomvi au kiashiria chochote cha kugombana ujue ndio wakati wapo close sana
 
Ilikuwa serious,
Kwa jinsi Lowassa alivyokuwa amejipanga kuutwaa Urais.
Hakuwa anatania.
Napata shaka kidogo maana Jk alikua ana maliza isingekuwa hatari kwake kumuachia kiti , labda kwenye chama.

Au hapo kati kati ilikua haziivi tena maana binadamu hata muwe wamoja kiasi gani hamta kosa kuhitalafiana
 
Back
Top Bottom