JokaKuu
Platinum Member
- Jul 31, 2006
- 30,441
- 55,018
Mbona mika 30 kabla ndege hazijanunuliwa hicho kilimo chako kilishindikana? Kwa hiyo trilion mbili ndizo ingeleta mapinduzi ya kilimo? Kama taifa tunazo sababu nyingi tu za kuwa na ndege zetu wenyewe. Tatizo siyo kununua ndege tatizo ni usimaizi na uendeshaji wa shirika letu la ndege. Wakati Julius Nyerere anaondoka madarakani kama miaka 40 iliyopita aliacha shirika la ndege likiwa na ndege 11 na wakati huo hakukuwa na fursa mbalimbali za kibiashara na pia uchumi wetu ulikuwa mdogo sana kuliko hali ilivyo sasa. Sasa kama wakati huo tulikuwa na ndsge 11 leo hii ni kitu gani kinatuzuia tusiwe na ndege idadi kama hiyo au hata na zaidi? Kwanza ilikuwa nia aibu kubwa sana kwa taifa letu kuwa na shirika la ndege ambalo halina hata ndege moja!
..trillion 2 zilizotumika kununua ndege ni sawa na bajeti ya wizara ya kilimo kwa miaka 6.
..Na kilimo ndicho kinachoajiri watu [ 65% + ] wengi hapa Tz. Pia tumekuwa tukiambiwa ndio uti wa mgongo wa taifa letu.
..Kauli mbiu ya serikali ya awamu ya 5 na 6 ni Tanzania ya VIWANDA.
..Na viwanda hivyo vinatakiwa vitumie malighafi zinazotokana na wakulima wetu.
..Kwa msingi huo, ni lazima tukiinue kilimo chetu ili tuweze kuzalisha mazao mengi na yenye ubora wa kuweza kutumika kama malighafi ktk viwanda tunavyotarajia vitaanzishwa.
..Njia ya uhakika ya kuinua kilimo ni kuongeza bajeti inayokwenda ktk sekta hiyo kusaidia ktk huduma za ugani, utafiti wa mbegu bora, upatikanaji wa pembejeo, etc etc.
..Nchi yetu na watu wake ni masikini kwasababu serikali zetu zote hazikuwekeza vya kutosha ktk kilimo, ufugaji, na uvuvi.
..Tatizo la shirika la ndege haliko ktk usimamizi bali liko ktk changamoto na ugumu wa biashara ya usafiri wa anga. Hata tukiweka malaika kuongoza shirika letu la ndege bado tutaingia hasara.