Picha: Rais Kikwete ashiriki maombolezo ya Regia Mtema

RIP dada Regia...

Kikwete ni muungwana sana yanapokuja masuala ya kijamii, I like him. Ila kwa usahihi ungesema Mbowe aongoza maombolezo, Kikwete ahudhuria. Kumbuka Dr Kikwete alishatoa salam za rambirambi kwa Mh Mbowe. Hapa wale mnaochukulia mambo ya siasa personal mna nafasi nzuri kujifunza hapa kuwa nje ya siasa sisi wote ni ndugu.
 

Haujapenda nini sasa mkuu?mbona hizo ni picha za kawaida sana?kumbuka Regia mpaka anaondoka alikua anasimamia na kutekeleza itikadi za chadema katika kuhakikisha watanzania wenzake wananeemeka na rasilimali zao,na ndio maana hata mh rais alipotuma salamu za maombelezo alimtumia MWENYEKITI WA CHADEMA na akaomba azifikishe kwa familia ya mpendwa wetu Regia,hizo picha hazina madhara yeyote na suala zima la msiba,na utamaduni huo si kua ndio chadema wa kwanza kuutumia duniani!sitashangaa na nitafarijika sana nikiona dada yetu anazikwa na bendera ya chama ambacho mpaka umauti wake aliamini kua kingewakomboa watanzania katika matatizo yao lukuki!watanzania ni wamoja,tunatofautiana kiitikadi tu jinsi ya ukombozi wetu kiuchumi!kapumzike kwa amani dada yetu,mwana Morogoro mwenzangu Regia E Mtema!tutaonana tena paradiso
 

Picha hazina ubaya kama ulivyosema, nakubaliana nawe kabisa kimtazamo. Ila nichoongelea kuona mbali zaidi katika nafasi kama hii kwenye misiba tuwe na mazoea ya kuweka kando itikadi za kichama ingawa mhusika ni wa kutoka chama hicho. Walioendelea na uungwana wakiongozwa na ustaarabu ndivyo wanavyofanya. Sisi bado tungali na matabaka ya kushabikia chama badala ya hoja za kiitikadi. Ndio utaona watu wanaenda hadi makaburini kwa itikadi wakati msiba hauhusiki na itikadi ambao umetokea katika mazingira ya kawaida. Yale yaliyotokea Arusha okay, lakini hii hapana.
 
Hojatete acha hizo. Kumbuka Hayati Regia alikuwa mbunge kupitia tiketi ya chadema hivyo nafikiri ni sahihi tu kuonekana kwa bendera ya chama. Sioni kama kuna tatizo sana hapo. Pia nashukuru sana kwa mdau aliyetuwekea picha tukaona kilichokuwa kinaendelea.
 

Watu kutoa maoni ni jambo la kawaida, na tujue tupo watu tufauti kimtazamo, kifikra nk, cha msingi niliyoongelea ni mambo ya kawaida yanayotendwa na wastaarabu wenye kujali watu tuwapo pamoja katika matukio yanayotukutanisha watu wa itikadi tofauti tuonyeshi ili kutoa ile khali ya wengine kushikwa na kwikwi fulani. Ni maoni wala yasiwaumize vichwa.
 

mkuu hapo nilipo bold bado unaendelea kumkomalia Dr Slaa kuhusu mavazi?
 
Suala la mavazi sidhani kama ni tatizo wao Chadema kuweka mabango yao ni sawa kwa kuwa alikuwa mwakilishi kupitia chama chao, mavazi yao ni sehemu ya maombolezo kwao, hujawahi kuona wanachama wa nyama vingine pia wanazikwa wakati jeneza limefunikwa na bendera ya chama, na hiyo inatokea kokote kule duniani.
 
Kwa mwendo huu Slaa hafai kuwa na nafasi kubwa kwenye serikali yetu.
Mtu asiyependa madiliko hafai. Inabidi ajifunze kubadilika na kuendana na mazingira.

kakufanya nini unaanza kumkashifu Slaa wa watu? Subiri msiba uishe mkuu
 
Katika nafasi kama hizi tunatanguliza wakuu kwamba wanaongoza maombolezo, ni kitu cha kawaidfa kutafsirika vizuri tu. Asante Geza Ulole
Hii tafsiri si sahihi Rais anapewa mamlaka hata yaliyo nje ya katiba na yaliyo ya binafsi, huongozi maombolezo kama hujashiriki kujayaandaa na bila ridhaa ya wahusika! Naomba hiki kichwa cha habari kibadilishwe kiwa Rais JK ashiriki kwenye maombolezo au aongoza serikali yake kwenye maombolezo! Ni hayo tuu....
 


Pichani Heche mwenyekiti wa umoja wa vijana Chadema na sare za chama msibani

Chadema ni chama makini, tunataka kuchangia mawazo kuongeza kiwango cha umakini zaidi, hivyo maoni yetu si kukiua chama ila ni kukifanya kiwe makini na mtazamo mpana na mwono mpana zaidi. Chadema kimejaa wasomi tunataka kifanye shughuli zaki kisomi kwa viongizi kuwa vinara wa kutoa mifano na wengine watafuta.
 

umeanza vizuri, kumbe ulikuwa unamtafuta Dr Slaa? vazi la Dr Slaa lipo kotekote, ofisini, kanisani, msibani, hotelini, hata kuchimba mtaro linafaa huhitaji kubadilisha.
 

Mkuu nchi haijengwi kwa kukutana misibani. kuhudhuria kwao ni moja ya jukumu lao kwani aliyekufa ni kiongozi mwenzao wa umma, hata kama ni kutokea upinzani. na haya ni mambo ya kawaida kwa taratibu zetu za kijamii za kiafrika, hasa tz. Hili halimaanishi kwamba serikali ya ccm italeta ushirikiano na wapinzani katika kujenga nchi, hakuna dalili hizo. Kumbuka kauli ya jk alipokutana na cdm juu ya kusaini mswada wa kuundwa kamati ya mabadiliko ya katiba. alisema asingesaini wenzake kwenye chama wangemchukuliaje?

Pia angalia umuhimu wa Prf Lipumba na watu wanavyomtumia huko duniani, na angalia hapa kwetu anavyodharaulika na kuachwa bila kutumika ipasavyo
 
Hamad Rashid Mohamed alikuwepo,nadhani cuf wengine wamesusa,lakini ni mapema mno ku conclude,tusubiri
 
Kweli nimekubali ule utabili wa mrithi wa Shekhe Yahya,kwamba umaarufu utaongeza kwa JK mwaka huu,hapo tayari naona umeshaongezeka, R.I.P REGIA.
 
maalim seif na hivi pale ni mapambio mwanzo mwisho kwa baba askofu sijui kama sio kumkutanisha mbwa na paka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…