Picha: Mengi akigawa utajiri wake

Picha: Mengi akigawa utajiri wake

idoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2013
Posts
3,051
Reaction score
1,423
FaizaFoxy, Lizaboni, gsu, Chabruma, mjepo, Simiyu Yetu & co. mpo?
Dr.Mengi-27Jan2015.jpg


Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi, akiwapatia chakula watu wenye ulemavu na wasaidizi wao wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam juzi. Kila mwaka, Dk. Mengi huandaa chakula cha mchana kwa watu hao ambapo mwaka huu jumla ya watu 4,000 walihudhuria. PICHA: KHALFAN SAID
 
Mh!! ila binadamu kuishi naye kazi zilipoibiwa za escrow tulilalamika sana haya sasa wenye nazo wakiwagawia mnalalamika. Jamani kazi ipo
 
Sioni km ni unafiki kuwafsnya walemavu nao walau kwa siku moja wafurahi.
Wenzetu wa upande wa pili huwa wanagawa misaada sehemu zao za ibada2...kwetu sisi ni tofauti sanw, binadamu wote ni sawa bila.kujali imanj. Keep up Mengi.
 
Hapo anawatumia vilema kujitafutia umaarufu.

Jaribu kutumia hekima japo kidogo tu,vitabu vyote vitakatifu vinasisitiza umuhimu wa kuwajali wasiojiweza,ni jukumu letu sote kuwasaidia wasiojiweza.Nani asiyetambua mchango wa Mh. Reginald MENGI kwenye sekta ya elimu,watoto wa kike,vijana,madini n.k. Kutoa siyo utajiri ni moyo wa mtu mwenyewe
 
Last edited by a moderator:
kabisa...kumpa mtu chakula haimsaidii chochote
Katika jitihada zake za kuendelea kuwawezesha watu wenye ulemavu, Dk. Mengi alitangaza shindano la kubuni wazo la biashara huku kila mmoja miongoni mwa washindi kumi watakuwa wakizawadiwa Sh. milioni 10 kwa ajili ya kuwasaidia kuinua hali zao kiuchumi.
Kwa upande wake, kampuni ya Kamal Group, iliahidi miguu ya bandia 200 wiki hii kwa ajili ya kuwasaisaidia watu walioko kwenye kundi hilo.
soma zaidi hapa
 
Nasikia kila mwaka hutumia zaidi ya milioni 50 kuandaa shughuri hizo, ingekuwa jambo la maana zaidi kama hiyo pesa kila mwaka angekuwa anaitumia kuwalipia gharama za shule hao walemavu, Kwani wengi wao wanasoma shule za msingi na waliobahatika kuendelea ni ktk shule za kata, ambapo kwa kiwango hicho angewasaidia walemavu wengi sana kuliko kuwaita na kuwafariji kwa chakula na mziki wa masaa machache tu, huku wakikabiliwa na changamoto nyingi za kimaisha??? Mi nadhani washauri wake walione hili japo anajitahidi ila aangalie njia bora ya kuwasaidia zaidi ambayo itakuwa ya kudumu kwa wahusika nayo ni kupitia elimu.
 
Back
Top Bottom