Picha: Mbowe akagua Red brigade Mwanza

Picha: Mbowe akagua Red brigade Mwanza

Ulinzi kwa ndugu zetu albino ni mdogo sana.Maisha yao yapo hatarini sana hususani kipindi hiki watu wanapotafuta uongozi kwa njia za giza.

Mbaya zaidi mpaka na dau la kiungo cha albino kimetangazwa kama si kosei na B.B.,C. Hizo hela ni nyingi na zinaweza kuendelea kuwashawishi wanaotaka utajiri wa haraka haraka. Vyombo vya ulinzi na usalama havijachukua hatau ya kuridhisha ya kuwalinda albino.

Wanaishi kwa wasiwasi. unatambua kuwa CHADEMA hawana jeshi.Tunatambua kuwa wanakikundi cha vijana kwa ajili ya kulinda kura,mali za chama pamoja na viongozi wa chama.

Tumewaona wakila kiapo Mwanza na tuliwaona Mbeya. Wanaonekana wana nidhamu na ari kubwa. Kwa ari na nidhamu yao,hawa vijana wanaweza kuisaidia nchi kutoa ulinzi kwa ndugu zetu albino.

Chama kifanye upembuzi wa kuwatambua albino popote pale walipo,halafu wawape kazi redbrigade kuhakikisha wanakua salama.Hapa mbinu za ulinzi watafundishwa ili kusiwatenge na pia wasijisikie kunyanyapaliwa.

Hili litakuwa ni jukumu la kijamii muhimu ambalo CHADEMA kupitia red brigade watakuwa wamelifanya kwa watanzania kupitia ndugu zetu albino.

Nawasilisha.
 
Daaaaaaaaaaahhh mawazo yamegongana namimi nilikuwa nawaza hivyohivyo.uwezi amini hawajamaaa wapo vizuri sana
 
Wakati mwingine acheni utani, suala la ulinzi wa taifa sio km kujifunza udereva, red brigade tz nzima hawazd hata 5000, mafunzo yao ni Yale ya kupiga Nondo/Kunyanyua vyuma uswaz wataezea wapi, suala la ulinzi ni taaluma ambayo kwa utashi wako ujikute tu ni ndoto, tupiganie nchi kwa ujumla wasimame kidete kuwalinda ndg zetu vngnevo tunatwanga maji kwny kinu
 
Naona mnataka kuanzisha makundi ya ujambazi, REDBRIGADE ni wahuni waliokata tamaa waliokotezwaokotezwa leo uwape kulinda ALBINO?
 
....red brigate ina uwezo wa kuwalinda albino kabisa
 
Wapelekwe polisi waache alama za vidole gumba na taarifa zao za nyuma ziwekwe sawa ili isijesumbua baadae kuwakamata. Magenge kama haya ndio yanabadilika kuwa waasi. Msela hata ukimvalisha suti bado anaonekana tu!

....

red%2Bbrigade2.jpg


mbowe_Red%2BBrigade.jpg


Lwakatare.jpg


red_brigade1.jpg
 
Yap itakuwa poa maana naona ulinzi wa taifa hili upo kwa ajili ya kuzuia maandamano ya wapinzani tu
 
Wakati mwingine acheni utani, suala la ulinzi wa taifa sio km kujifunza udereva, red brigade tz nzima hawazd hata 5000, mafunzo yao ni Yale ya kupiga Nondo/Kunyanyua vyuma uswaz wataezea wapi, suala la ulinzi ni taaluma ambayo kwa utashi wako ujikute tu ni ndoto, tupiganie nchi kwa ujumla wasimame kidete kuwalinda ndg zetu vngnevo tunatwanga maji kwny kinu

La kuzingatia ni kuwa wana watu wengi nyuma yao na bado hawajaingia katika mfumo CCM wa rushwa. Kwa hiyo uwezekano wa kuzuia matukio kabla ya kutokea ni mkubwa kuliko walio katika mfumo rasmi na wanachukiwa na wananchi kwa kutetea na kulinda CCM.
 
Mh, nakazi ya police ninini? kilamtu na jukum lake wanapewa mipesa ya nini? kama wameshindwa wananchi tunapaswa kufanya mabadiliko na sikuwapa ulinzi kikundi cha chama, ambao si jukum lao
 
Back
Top Bottom