kiraia
JF-Expert Member
- Nov 20, 2007
- 1,716
- 999
Sidhani kama kuna binadamu anayeweza kujitenga na binadamu wenzake halafu huyo huyo akaja kuwa kiongozi wa binadamu wenzake, lazima uishi katika dunia, nashangazwa sana na binadamu wanaojaribu kuishi katika dunia ya kusadikika kwamba wao hawana mawaa yoyote, unaweza kuwa na rafiki mtumia kilevi lakini wewe usiwe mtumiaji wa hicho kilevi ukawa unatumia kitu kingine tofauti,
sioni ajabu mtu fulani kupiga picha na fulani, sio lazima wawe washirika katika kila kitu, ni ajabu sana kuanza kuimplicate watu wengine kwa mambo fulani simply kwa picha tu, kama ni hivyo basi watanzania natusibirie rais ajaye atoke mars ambaye huyo hajawahi kuwa na ukaribu na binadamu wengine maana huyo hata kuwa na picha au watu wa kumhusisha nae.
Kwanini hakupiga picha na baba yangu akapiga na Rugemalila kama ni kigezo cha kutokujitenga na watu?