Picha hii ya Lema imenifikirisha sana!

Picha hii ya Lema imenifikirisha sana!

Huyo huko ndiko alikokuzoea..yupo comfortable sana huko kuliko akiishi uraiani..wenzio kina sugu, msigwa, nasari, silinde, prof jay wako bize kuwaletea wananchi wao maendeleo..yeye yupo na vimbari vya mahakama..tehe
 
Kamanda yuko fit, nami naweka nadhiri kuwa siku ya tarehe mosi, 2017 nitafunga kula ili kupaza sauti yangu kwa Mwenyenzi Mungu kwa ajili ya Lema, Ben na wote wanaoonewa na serikali hii isiyoheshimu uhuru wa watu.
Maana ni ajabu na kweli kuwa Mwalimu Nyerere alipigana dhidi ya ukandamizaji wa haki kwa ukanda wote wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, lakini leo nchi yake iliyotukuka kuwa kimbilio la wapigania haki na uhuru kutoka kila kona ya dunia imekuwa ndiyo inatunga sheria za Kikaburu. Eee, Mwenyezi Mungu tuhurumie waja wako.
 
Naamini atarudi inara zaidi na kuonyesha utuuzima zaidi...
 
Constable Isabella haoni ata aibu asee.. 2020 hataamini wana arusha watavomfanya sjui watawanyan'ganya zile tuktuku
 
matukio yote mawili siyo mazuri:
1. Umakini wa Askari, inaonyesha Mh. Lema ahamini kama mahabusu, na Askari analazimika kuwa makini zaidi asije 'akamtoroka'. Ndiyo askari anasikiliza kama Mh. Lema anaweza akawa anaagiza kama ya DrugLord wa Mexico (ni samehe kwa mfano huu lengo ni kutaka kuhakikisha mnaelewa ninachokimaanisha), kumtorosha mahabusu. Huwezi kumlaumu askari katika mazingira haya. Kukosa kuaminiwa hasa kwa vyombo vya usalama si jambo zuri wala la kujisifia.

2.Bado hii inampunguzia Mh. Lema sifa muhimu ya kuaminika kama raia mtiisheria bila shuruti. unajua huyo askari nyota kaipataje? Jibu ni baada ya kukidhi vigezo muhimu sana vya kudhibiti mahabusu ama wafungwa. Sasa kama jeshi la Magereza linalazimiaka kutumia rasilimali watu muhimu kabisa walioiva, maana yake kuna shida mahali. Si vyema kujisifia mambo yanayotupunguzia sifa.

NOTE: Wewe Allen Kilewella na Mimi TUJITEGEMEE, maaelezo yetu juu ya hiyo picha hayana mashiko, hivyo hayatakiwi kutiliwa maani. Sababu kati yetu, hakuna anayejua askari yule anawaza nini, wala hatuji Mh. Lema alikuwa anawaza nini, na mkuu wa magereza aliyempanga huyo askari wa nyota alikuwa anawaza nini! Tusitumie maelezo yetu haya ku'justify' jambo lolote. Kikubwa tuombe wahusika wahakikishe haki inatendeka, na Mh. Lema arudishiwe uhuru wake kwa utaratibu sahihi unaojali haki na utu.
Wewe TUJITEGEMEE, usijitoe ufahamu kudai askari kakidhi vigezo, unakumbuka kipindi kile cha ziara ya Rais Obama hapa nchini jinsi askari mmoja wa kwetu alivyotaka kumzuia Mwandishi yule wa kike kwa ukali tena akiwa na kitambulisho shingoni hadi ikabidi askari wa FBI aingilie kati. Maaskari wa kwetu kwa kawaida hawatumii weledi hata kidogo , wao ni misuli zaidi.
 
Ni ajabu sana pale watu wanapojifanya kukufagilia na kukupa matumaini bandia huku ukiwa ktk mateso gerezani,acheni kumdanganye mwenzenu eti upo ngangari wakat amesota gerezani na nyie mpo huru uswahilini


Mandela alikaa gerezani miaka 27..kuna ambao walikuwa wanamtia moyo na kuna ambayo walikuwa na kauli kama zako. Ila Mwisho wa siku kile alichokua anaamini na kukipigania kilitimia...inawezekana sio kwa kiasi alichotaka ila kilitimia..

Na siku zote wapanda miti ni wachache ila wanaokuja kufurahia kivuli ni wengi..
 
Kisicho weza kukuangamiza kitakuongezea nguvu lema anauthibitisha usemi huo
 
Jaman tuachen uongo pale anamaanisha nimtu aliekua amesimama lakin baada yakuikosa zamana anaegemea meza kwauchovu kama amechoka akili baada yakuambiwa hali sio nzyr bado nakutoka kwass bado nivigum
 
Mtukuka sana Mwalimu alipita,Muungwana Mwinyi vilevile,mzee wa malofa pia kama ilivokuwa kwa maraha,na sasa asiyejaribiwa na atapita,isiyopita ni haki tu,lema atashinda tu hata kama asiyejaribiwa hataki ni muda tu.
 
Inavyoonekana court session imeisha ndio wakili akaenda pale kuongea nae........hapo lazima askari awe karibu maana hakunasessioon......ulinzi wa askari magereza unachukua nafasi
Nani anaondoka wa kwanza kati ya Hakim na mtuhumiwa baada ya Hearing ???
 
Watesi wa Lema aibu inawaandama kama mkia wa fisi, mpaka kaburini watakuwa wakisikia jina "Lema" wanajutia maamuzi yao ya kipambaufu.
 
Nani anaondoka wa kwanza kati ya Hakim na mtuhumiwa baada ya Hearing ???
Hakimu ndio wa kwanza!!! Mnaachwa hapo polisi na magereza wanawazunguka kwa waliokosa dhamana!! Unaendaga mahakamani kweli au ndio akili za mitandao ubishi bila facts?
 
Mkuu pamoja na kusema yote hayo lakini bado hakupunguzi adha za Binadamu kuwa Rumande au Gerezani. Nakuhakikishia kuwa Wewe unaweza labda ukawa unamwona Mheshimiwa Lema yupo ngangari ila nikuambie tu kuna uwezekano mkubwa tu moyoni mwake anaumia mno tena kwa mengi ila anajikaza tu kwa nadharia yao ya Ukamanda.

Kama Wewe unaona Mheshimiwa Lema huko alipo sijui rumande au gerezani anapata raha inayompelekea kutokuwa na hofu basi kaombe kubadilishana nae yeye atoke halafu Wewe ukae huko hata kwa siku tatu ( 3 ) kisha uje utupe mrejesho wako humu.

Namkubali sana Mbunge Lema ila akae akijua kuwa Siku zote sikio halizidi Kichwa na kama ile Kauli tunayoambiwa aliongea jana Mbunge mwenzie Kiukamanda Nassari kuwa yoyote anayepinga yanayofanywa na Serikali ya Rais Dkt. Magufuli ni taahira na akapimwe akili ni ya kweli basi Mheshimiwa Mbunge Lema amejitakia mwenyewe na inabidi tu sasa awe mpole.

Awamu hii ya Mr. Sulphuric Acid siyo ya Ki sport sport jamani Wanasiasa wa Upinzani hivyo nendeni nae kwa akili mno na mahesabu makali otherwise you will all be doomed.
Mmh maccm bhana,hata Farao aliamrisha mzaliwa wa kwanza kiume wa Waisrael wauwawe lkn na yeye alikufa. Kuuwawa na kupotea kwa viongozi wa upinzani si salama kwenu hata nyie mmeshakufiwa na viongozi wenu pia.
 
Back
Top Bottom