KWELI Picha hii ilipigwa mwaka 2012 nchini Korea Kaskazini

KWELI Picha hii ilipigwa mwaka 2012 nchini Korea Kaskazini

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
1775999363128.png
MJB PYONG 2.jpg
MJB PYONG 3.jpg
MJB PYONG 4.jpg
 
Tunachokijua
Wadau mbalimbali wa JamiiCheck kupitia mitandao ya kijamii na Jukwaa la JamiiCheck wameshiriki kubainisha uhalisia wa picha iliyowasilishwa na mdau akitaka kupata uhalisia wa mahali ilipopigwa na ilikuwa kwenye tukio gani.

Wengi wameeleza kuwa picha hiyo imepigwa nchini Korea Kaskazini kwenye moja ya matukio yaliyofanyika nchini humo.

JamiiCheck imefuatilia na kujirirdhsiha kuwa picha hiyo ilipigwa na mpiga picha kutoka Urusi Ilya Pitalev (Photojournalist), April 2012 wakati wa maadhimisho ya miaka 100 tangu kuzaliwa kwa mwanzilishi wa Korea Kaskazini, Kim Il Sung, yaliyofanyika Pyongyang.

Mpiga picha huyo alishinda tuzo ya Sony World Photography ya picha bora kwenye kundi la masuala yanayoendelea (Current affairs), iliyotolewa mwaka 2013. Pitalev alipata picha za kuvutia zinazoonyesha maisha ya kisasa ya Korea Kaskazini mwaka 2012, wakati nchi hiyo ilipofungua milango yake kwa kundi maalum la wapiga picha kwa muda wa siku chache tu, katika maadhimisho ya miaka 100 tangu kuzaliwa kwa mwanzilishi wake, Kim Il Sung.
Ilikuwa ni show ya cheka tu ya kubwa kuliko ya huko korea, ilikuwa mwaka 1927
Haya majibu ni ya Facebook,kule Facebook majibu ya kipuuzi kama haya huwa mnapata likes sana wapuuzi wengine wanapenda huu ujinga wenu..Lakini jamiiforums ukiendekeza majibu kama haya sanasana utaonekana mpumbavu tu
 
Kwa msaada wa Google, reverse image search:

Picha hiyo inaonyesha umati wa wanajeshi wa Jeshi la Korea Kaskazini na raia wakiwa katika majukwaa ya Uwanja wa Kim Il Sung huko Pyongyang.


Picha hii ilipigwa na mpiga picha Ilya Pitalev wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 100 ya kuzaliwa kwa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Il Sung.

Ilichaguliwa kama mshindi wa fainali katika kipengele cha Masuala ya sasa (Current Affairs) kwenye tuzo za Sony World Photography Awards za mwaka 2013.

Mandhari haya yanaonyesha utofauti mkubwa wa mwonekano kati ya wanajeshi waliovalia sare na raia waliovalia mavazi ya kitamaduni yenye rangi za kuvutia (choson-ot).

Picha hii mara nyingi huangaziwa kama picha mashuhuri iliyopigwa bila kutumia mbinu za kidijitali au programu ya Photoshop.
 
Back
Top Bottom