Picha: Bodaboda na Simba uso kwa uso

Picha: Bodaboda na Simba uso kwa uso

Hapa ningekuwa mimi ningezimia aisee maana muoga kinyama, mnyama mwenyewe simba!! Nilishawahi kukutana na kitimoto pori asubuhi asubuhi saa 12 wakati nakusanya kuni za kupika chai,

siku hiyo nakumbuka miguu iliishiwa nguvu nikaanguka chini bahati nzuri nilikuwa na ba'mdogo wangu akapiga ukunga ndio noah akasepa.

Imebidi nicheke tu, mweeeeeeee
 
Khaaa.. mbele ya simba utatoa mkono? Si ajabu hata waliokuwemo kwenye hilo gari hali ya hewa ilichafuka...Kukutana na simba maeneo ambayo hukutegemea sio mchezo. hao jamaa wa bodaboda unawafahamu au unawasikia? Wana akili zinazowatosha wao tu, kama hawajali trafic light itakuwa taa za gari?

Hewa ilichafuka?walitoa hewa ya ukaa?
 
Ashukuru huyo simba pengine ni mzee au ni mgonjwa, angepata cha mtema kuni.

Huyo simba ni kijana angekuwa Mzee au magonjwa asingemchelewa! Maana simba wazee hawawezi kufukuzia mawindo hivyo huwa wanavizia witu!
 
Haaaahaaaahaah!!Vipando hivi bhana yan kila wakat huwa unafikiria ku_overtake sasa maeneo mengine si ya kufanya masihara.Hatar san
 
Wachangiaji wengi wameangalia tu upande hasi wa mwendesha bodaboda, upande chanya unaonyesha kuwa huyu kijana ni jasiri na anamudu vyema pikipiki yake. Hebu angalia, amesimama kwa breki zake vizuri, akateremka kwenye pikipiki yake, akaingia mbuga za wanyama kwa sekunde chache kumuangalia mfalme wa pori na kumpa mtalii ndani ya gari kupata picha nzuri, halafu akamheshimu mfalme kwa kumpisha apite kwanza. Wengi wameeleza vile ambavyo ingekuwa kwao kama ingewawatokea, wangekojoa, kunya, kuzirai, nk.

Mungu alituumba tutawale wanyama na mazingira yanayotuzunguka. Huyu bodaboda husafiri barabara hii mara kwa mara na hukutana na wanyama wa kila aina.
 
Siku zote bodaboda huwa wanaharaka sasa sijui kwa nn hapo aligeuza na kurud mbio.
 
Alivaa 'jezi' za msimbazi akidhani simba atamuelewa kama ndugu!
 
Picha ya kutengeneza hakuna ukweli wowote mpiga picha alikuwa kwenye ford xlt angalia wiper zinapoishia eti napikipiki imeonekana na engine gari liko juu angemuona kwa chini sasa wapo kima kimoja na gari....zakuambiwa changanya na zako..Jkikwete.
 
ilitokea ghafla katika barabara ya makongolosi kuelekea rungwa mkoani mbeya. Ghafla kwenye kona mnyama simba kakutwa kajipumzisha katikati ya barabara eneo la pori la simba.

Wakati magari yakiwa yamesimama, mara bodaboda akatokea na bila kujua akataka kuyapita kwa kasi (kuchepuka) ndipo alipokutana uso kwa uso na mnyama huyo hatari. Hata hivyo aliweza kugeuka na kukimbia wakati na simba naye akanyanyuka na kuingia porini.


View attachment 227826View attachment 227827View attachment 227828

siku nyingine watajiju
 
Da nimecheka sana kwi kwi kwi kwi kwi na hapo inaonekana hawa jamaa kwenye gari walimuonya asimame ila kwa akili za boda boda angejalibu kupita hapa alafu mziki wake angeuona.

Kuna siku tulikua ngorongoro sasa simba walikua wamelala barabarani jamaa mmoja na landcruiser yake alamkanyaga mkia simba mmoja da chamoto alikiona cruiser ilipigwa kofi moja mlango wote kwisha ha ha ha ha

mkuu hio cruiser ilkua ya mfinyanzi ama?
 
huyu jamaa atokatiza njia hiyo na boda boda tena ,kupenya Penya kutakuwa sio sehemu ya udereva wake tena.umezikosa rip hapa jamvin bodaboda .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom