...kwa maana hiyo, 'inakuwa rahisi' kujirusha nje ya ndoa iwapo utaivua hiyo pete?
Kwa wanandoa inamaanisha kuwa ninyi ni wenzi halali kwa kipindi chote mtakapokuwa pamoja. Uhalali huu hutakiwa kwenda sambamba na kiapo cha uaminifu mlichokitoa na kuhakikisha mnakifuata.
Kwa wanajamii- Ina maanisha kuwa fulani (mwenye pete) hayuko available ni mali ya mtu tayari na hivyo vishanshuda na mangurumbene wakae mbali na kifaa hicho.
Kwa siku hizi inamaanisha : Hata mie nshatoa nuksi (kwa wanawake) na wanaume inaonyesha uwezo alionao wa kutunza familia (hata kama hatunzi)
...kwahiyo mamsap akiiacha pete nyumbani ujue ndoa ipo mashakani?
ina maana kwamba upendo wenu hauna mwisho.Mtapendana Forever and ever, endlessness love na kwamba love lenu halitavunjika.
Lakini cha ajabu watu wana ndoa na bado kucheat kama kawaida, tena mtu anaamua kuvua kabisa hiyo pete, hasa wanaume, ukichunguza asilimia kubwa ya wanaume hawapendi kuvaa pete za ndoa ukilinganisha na wamama. Utamkuta mama kabebesha pete zote engagement na wedding rings.
Ndo maanake...ukikuta mamsap havai ujue hata njemba haivai.
Babylonnyemba haivai ndio nini tena jamani ?makubwa haya!!!.
Babylon
Penny kaandika Njemba akimaanisha mwanaume/mume siyo nyemba.. Yaani kama mamsap havai pete ya ndoa ujue na njemba hana na yeye kabisaa.
Mbu!
Swali: Je kwa wasabato imekaaje? Maana katika suala la kufunga ndoa hamna kuvalishana pete kanisani labda baadae kwa wakati wenu mvalishane maana ni kama fasheni. Ina maana usipokuwa na pete wakati umeoa/kuolewa unaonekanaje kwenye jamii?
Twaib sheikh twaib...kwahiyo mamsap akiiacha pete nyumbani ujue ndoa ipo mashakani?
Hata mie pia dalili n'shaziona. Na si ajabu ya'shatendeka. Yote heri!Hali inavyokwenda humu ndani ya JFkuna uwezekano wa wanachama wake kuazisha Blind date siku moja kwa kutumia vijineno vya ujanja ujanja
Ndo maanake...ukikuta mamsap havai ujue hata njemba haivai.