Pepo la kupinga linaiangamiza CHADEMA, sasa wanapinga yale waliokuwa wanataka yawe kwenye bajeti

Anayetekeleza yaliyokuwa yanasemwa na CHADEMA ana imani nao ndiyo maana anafanya waliyoyasema,msiojua CHADEMA walipokuwa wanayasema ndio muliokuwa wapinzani wa kubwa wa mambo yaliyokuwayanasemwa.

Kwa kuwa mumeamua kucheza muziki wa CHADEMA,CHADEMA wataendelea kuwatazama jinsi mnavyo serebuka na kukata viuno wakati mnacheza muziki wao,wanachofanya na watakachoendelea kukifanya ni kuwasahihisha makosa yenu mnayoyafanya wakati mnacheza muziki wao na hapo ndipo mnapokuja na hoja zenu za kusema kuwa CHADEMA wanapinga kila kitu.
kwanini wanapinga walioyasema?
 
We jamaa ina maana huwezi kuanzisha uzi ambao Chadema haihusiani? Mbona una akili mgando sana kias hicho? Kila kukicha ni Chadema tu? TANZANIA ina mambo mengi mkuu
Ni kweli yapo mengi lkn ni yapi yasiyokuwa kwnye siasa?? Siasa ndio inaongoza maisha yetu ya kila siku.ni kweli hata shetani kz ake ni kupinga mazuri yoote anayofanya mungu.yeye shetani hakuna jema lolote litokalo kw mungu.yoote ni mabaya.Na huyo roho wa shetani akikupanda wewe ytapinga kila kitu
 
Fikiri nje ya box, kila siku wewe na chadema tu tena unaiandika kwa mabaya, binadamu mwenye akili kama yako ni hatari kwenye jamii, ya nini kusumbuka na asie kuhusu?! Unatia kichefuchefu sasa kila ukiandika chadema, si lazima uanzishe mada soma za wengine huna upeo mkubwa wa kufikiri.
Wewe mwenye upeo wa kufikiri.kitu gn kinachofanyika tz kisichomhusu mtz? Duu machiz kumbe tupo wengi.
 
Hili tatizo la kupinga kila kitu sasa limegeuka sumu, Chadema ilianza kama Chama chenye mawazo mbadala, baadaye kama chama/serikali mbadala huku wakiwaainisha maadui wa nchi kwa uaminifu mkuu. Baadaye wakanunuliwa na wale waliowaita maadui wa nchi na hapa ndipo balaa likaanza. Tukashuhudia pepo la kupinga kila jema likiwavaa.

mambo mengi waliyowahi kuyapendekeza ikiwamo kufuta ushuru kwenye mazao,kutambuliwa kwa wamachinga na kudhibiti mapato na kodi kwenye madini pamoja na udhibiti wa matumizi sasa wamegeuka kuwa wapingaji wa mambo hayo na kibaya zaidi siku hizi hawaji na hoja mbadala,utasikia tu 'hakuna kitu', 'wanakosea', 'mpinzani hutakiwi kuunga mkono hoja' nk..nk..nk.

Niseme tu, kupinga mfululizo husababisha sumu mwilini na baadaye mpingaji hugeuka sumu, ni pepo..na ngumu kuaminika tena. Mfano mdogo ni jinsi ambavyo Tundu lissu alivyogeuka sumu kwa nchi yake na kila dalili zipo atakuwa sumu kali kwa chama chake. Kilichobaki ni kutafunana wenyewe kwa wenyewe.

Nawasilisha.
Na nasikia kasema huko kwa Machadema menzake,wote hawana sifa za kugombea urais zaidi yake!
 
Wewe mbunge wa viti maalum CCM na uko bungeni now, hebu weka hapa ushahidi wa audio au video ya mbunge wa upinzani akisimama na kusema hayo maneno unayoyaandika.
 
Hii ina mazuri yake lakini sio kwamba haina cha kukosa au kukipinga.

Ujinga huu wa baadhi ya wanaCCM wa kuunga mkono kila kitu umeligharimu sana taifa hili.
Kuanzia uhuru mpaka leo tumekwama kwa sababu ya kuunga mkono kila kitu halafu baadae akija Rais mwingine tunasoma upepo wake na kubadilika huku tukiwa tumeshapata hasara kubwa.

Najiuliza tatizo hasa linakua ni nini?
Kuna mapungufu kwenye kila bajeti tangu uhuru na ndio maana bado nchi yetu ni maskini sana.
Tatizo ni kwamba hatujadili na kubishana kwa kiwango cha juu kuhusu mapungufu na namna ya kuyaondoa. Kukaa na kusisfia tu usahihi wa jambo ni kupoteza muda.
Kwani hata usiposifia litafanyika na matokeo yake yatalifanya lisifiwe.

Mapungufu ni lazima yakosolewe na kupingwa ili usahihi upatikane. Wanachofanya wapinzani ni kudeal na mapungufu ambayo ndiyo yatakayowaumiza watanzania wasio na hatatia. Hakuna waziri anayeumizwa na mikataba mibovu kwani wanaifanya kwa kunufaika wao na familia zao ba marafiki zao wanaotumika kuzima hoja za kukosoa ili waonekane wapo sahihi kwa muda wanaokuwa madarakani.
Ni dhahiri kuwa nia njema bila kuiweka ikajadiliawa na kuonyesha makaosa na kusahihisha hua haiwezi kudumu.
Mfano ni Sera ya ujamaa na vijji vya ujamaa. Kama ingepata mjadala wa kutosha na kushirikisha mawazo mbadala ingelikomboa taifa. Lakini ilifanyika kishabiki na kisiasa matokeo yake haikuleta mabadiliko chanya.

Huwezi kusifia ujenzi wa nyumba ambao tayari kuna nyufa kwenye msingi na unapojaribu kulosoa ujenzi huo unaambiwa kuwa kaa pembeni wewe hufai mana unapinga kila kitu.

Ni lazima kila mwenye akili na maarifa afahamu kuwa nyufa kwenye nyumba ndiyo hatari kuliko kukamilisha nyumba na kupaka rangi kwa lengo la kusifiwa kuwa umejenga nyumba kwa haraka.

Kila mwenye maarifa atafahamu kuwa wapinzani hawapingani na SHERIA bali wanapingana na MATAMKO ambayo hayana misingi ya kisheria.

Kama CCM wana nia ya dhati ya kuleta mabadiliko ya kudumu na sio ya kutafuta kura basi wajenge mifumo ya kisheria kwanza pale wanapoona kosa.

Mfano kwa sasa uhalifu wa kimitandao na matumizi mabaya ya mitandao umepungua sana kutokana na sheria na sio matamko. Sheria ilitungwa na kila mtu anajikuta anaifuata kwa lazima au vinginevyo anaenda jela.

Leo hii tunalalamika na mikataba inayowapa upendeleo wawekezaji na kuwapa fursa ya kutuibia lakini tunasahau kuwa tumempa waziri mamlaka ya kujifungia ndani peke yake na kujadili na mwekezaji bila kupeleka matokeo ya mjadala wake bungeni ili maslahi ya wananchi yaangaliwe kwa kina kabla ya kusaini mlataba. Matokeo yake uwekezaji umekua ni vichochoro vya ufisadi na kulihujumu taifa huku waliouza rasilimali zetu wakiwa wamejipanga kipropaganda na kutudanganya kwa orodha ndefu ya faida tutakazo zipata kwa kujengewa madarasa mawili ya sh. Mil. 50 huku tukiibiwa mabilioni ya fedha.

Hapa ndipo wenye akili,maarifa na werevu wanapopingana na wanufaika wakuu na wapiga debe wao.

Wapinzani waendelee kupinga na kukosoa yale yasiyofaa hata kama Wabunge wa CCM watasifia mana haijawahi kutokea CCM wakakubali kuwa wamekosea wakati rais akiwa bado madarakani.

Tangu mwanzo wakati wa mikataba hiyo mibovu CCM walikua wanasema kuwa wapinzani ni wanasiasa uchwara wasio na hoja huku meza zikigongwa na wabunge na mawaziri wakajinufaisha na mikataba mibovu.
Akaja Kikwete hali ikawa hiyo hiyo. Wakasema rais ana nia njema lakini wanaomwangusha ni watendaji wake. Mikataba ikaendelea kuwekwa kama mashindano ya kuuza rasilimali kwa kasi.

Tatizo ni moja kuweka ushabiki wa kushangilia chenga huko timu ikiendelea kufungwa magoli.
 
Umeyaona hayo unayosema kwenye hoja ya mleta mada?Hebu soma content ya kilichoandikwa,kuna hata kimoja alichokibainisha mleta mada katika kujenga hoja yake???
Kaandika upuuzi!
Pole sana kaka wale maadui watatu wa maendelleo aliosema Nyerere wakati tuna pata uhuru Maradhi, ujinga na umasikini. Alisahau tatizo moja angekuwa hai lazima ange update hiyo list na kuongeza la nne ambalo ni CCM.
 
Hili tatizo la kupinga kila kitu sasa limegeuka sumu, Chadema ilianza kama Chama chenye mawazo mbadala, baadaye kama chama/serikali mbadala huku wakiwaainisha maadui wa nchi kwa uaminifu mkuu. Baadaye wakanunuliwa na wale waliowaita maadui wa nchi na hapa ndipo balaa likaanza. Tukashuhudia pepo la kupinga kila jema likiwavaa.

mambo mengi waliyowahi kuyapendekeza ikiwamo kufuta ushuru kwenye mazao,kutambuliwa kwa wamachinga na kudhibiti mapato na kodi kwenye madini pamoja na udhibiti wa matumizi sasa wamegeuka kuwa wapingaji wa mambo hayo na kibaya zaidi siku hizi hawaji na hoja mbadala,utasikia tu 'hakuna kitu', 'wanakosea', 'mpinzani hutakiwi kuunga mkono hoja' nk..nk..nk.

Niseme tu, kupinga mfululizo husababisha sumu mwilini na baadaye mpingaji hugeuka sumu, ni pepo..na ngumu kuaminika tena. Mfano mdogo ni jinsi ambavyo Tundu lissu alivyogeuka sumu kwa nchi yake na kila dalili zipo atakuwa sumu kali kwa chama chake. Kilichobaki ni kutafunana wenyewe kwa wenyewe.

Nawasilisha.
Binti hivi huwa unapata wapi muda wa kumpikia mmeo kama kila wakati uko Jamii Forums kushangilia uchafu wa nzi wa kijani wa Lumumba?
 
umewasilisha kitugani? Mbona mlipinga waliposhauri haya mnayofanya? Je,mlijiuliza au kuwauliza namna ya kuyafanya au mlikurupukia tuu. Tatizo hapa Ni uslow learner...mtakuja kuyaelewa haya wanayoshauri after 10 years! Kijani Ni rangi nzuri lkn nimeichukia sababu ya masisiemu...can't u be so serious?? Nikujichekesha na kujisifia vitu vya ujinga ili wapinzani waumie bila ya kujali wananchi na Taifa linadorora kwaujeuri wakiujinga mnaofanya...
 
wanapinga kuwa kengeza hajazama kwenye kisima cha huba cha dege la jeshi madame mwizi wa damu na pesa taslimu...
 
Hakuna pepo wala shetani.
Kile kinachoitwa pepo ni kasoro za mifumo mikuu ya fahamu.

Shetani ni kitu cha kufikirika ambacho kimebuniwa kama (scapegoat) kisingizio cha uwepo wa uovu hapa duniani.

Narudia. Hakuna pepo la kupinga wala la kuunga mkono.
Ni akili zenu tu.
 
Kama huna hoja si lazima kuchangia, Wakudadavua ametoa hoja nzuri kwa mwelekeo wa vyama vyetu mbadala wanapinga hata yale yaliyokuwa wanapendekeza kweli wanafaa kuongoza nchi?
Si wanatoa hoja mbadala jumatatu ama??? Ssa wamepinga lini??? Wakati jumatatu ndio "wanapinga" kwa hoja mbadala na kushauri mambo machache yanayotakiwa kufanyiwa mabadiliko!!!!

Sasa hizi kejeli sahvi mapema ni za nni?? Afu wwe unasupport
 
jenga hoja na si kubweka dogo.
Maoni ni jumatatu sasa hiyo kupinga kila kitu umeitoa wapi?? Au maoni ya mtu mmoja moja humu Jf Ndio msimamo wa upinzani wote???

Maoni ni jumatatu utaona hoja zikipanguliwa kwa hoja haraka ya nni mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom