Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,869
- Thread starter
- #361
Karibu ndani kabisa yaan mpaka huku kwa sarafinaunikaribishage mpaka ndani sio naishia nje tu![]()
![]()
Sarafina - Mtunzi Nyemo Chilongani
Karibu ndani kabisa yaan mpaka huku kwa sarafinaunikaribishage mpaka ndani sio naishia nje tu![]()
![]()
asanteeeeeee nishafika.siku nyingine uwe unaniita kwenye mambo mazuri kama haya.me pia ni mhitaji wa hivi vitu.Karibu ndani kabisa yaan mpaka huku kwa sarafina
Sarafina - Mtunzi Nyemo Chilongani
Ahahhh sijajua najua we mambo zako ni kulee jukwaa la chini![]()
kote kote ni pogo ukinikose kule ujue nipo huku.ukinikosa huko ujue nipo tech mara chache sana nipo siasani japo sina chama.Nitaitafuta niisomeNimeweka nyingine itafute inaitwa sarafina
Ahahh usiniambie umeingia kwenye ulimwengu wa story hajanitumia mm jaman Sarafina - Mtunzi Nyemo ChilonganiNitaitafuta niisome
Bila kusahau mimi na Davent jmosi tumempiga muhindi mimi mkeka mmoja yeye miwili hajakutumia ya Heinken?
Ukimuona mgande maana amekula bata mno great park hapoAhahh usiniambie umeingia kwenye ulimwengu wa story hajanitumia mm jaman Sarafina - Mtunzi Nyemo Chilongani
mimi nahisi Peter ndio atamfanyia MaombiEeh mungu naomba hadi nifike mwisho wa simulizi hii tatiana awe amekufa kwel,ila peter asijulikane kabisa kama amehusika kwa chochote
Ila ana roho ya pakaDhambi ya usaliti itamtesa huyo malaya Tatiana.. Bado Smith hajaanza kulipiza kisasi!!!
doh Peter ana competition ya hatari inabidi afunge na kuomba papuchi ya Tatiana ibaki salama
mkuu unawazia papuchi tu na sio uaminifu duuuuhhh mbona zipo papuchi zilizokwisha wahi pitiwa sana hapo zamani ila baada ya kuwa mtu mpya uaminifu unaukuta tuNzuriSEHEMU YA 01...- NYEMO CHILONGANI
“Sijui atazaliwa mtoto gani.”
“Labda wa kiume.”
“Mmmh! Mimi napenda awe mtoto wa kike ili na sisi tujivunie kwa mara nyingine.”
“Ila yeye mwenyewe si alitaka wa kiume?”
“Nani?”
“Sangiwa!”
“Ndivyo alivyosema?”
“Ndivyo nilivyosikia, eti kwa sababu ana watoto wengi wa kike, hivyo anataka apate na mwingine wa kiume!”
“Mmmh! Nafikiri hizo ni tetesi tu.”
Yalikuwa ni mazungumzo ya wanawake wawili miongoni mwa watu wengi waliokuwa wamekusanyika nje ya nyumba pekee iliyokuwa imeezekwa bati na kujengwa kwa matofali, nyumba ya mzee aliyeaminika kuwa na fedha nyingi katika Kijiji cha Chibe kilichokuwa mkoani Shinyanga.
Kila mtu alitaka kujua ni mtoto gani ambaye angezaliwa na mke wa Sangiwa aliyekuwa na fedha nyingi kijijini hapo. Watu walimpenda Sangiwa kwa kuwa hakuwa mtu wa majivuno, kile alichokuwa nacho, alitamani wengine pia wakipate.
Kipindi cha nyuma alikuwa na maisha magumu, masikini kama watu wengine, alidharaulika sana kijiji hapo, hakuwa na nyumba kwani wazazi wake walipofariki, hata ile nyumba aliyokuwa akiishi, akafukuzwa.
Alipitia maisha magumu, hakuona afadhali ya maisha hata siku moja, kila siku alikuwa mtu wa kuomba misaada tu, wapo waliokuwa wakimsaidia lakini pia kulikuwepo na wale waliokuwa wakimnyima.
Alipoona kijijini Chibe maisha yalikuwa magumu, hapo ndipo alipoamua kuhama na kuhamia kijiji cha jirani cha Beda. Maisha hayakubadilika, bado aliendelea kuishi kwenye maisha ya kimasikini hali iliyomfanya kwenda kuomba kazi kwa mzee Mwiku aliyekuwa kijijini hapo.
Kwa kuwa mzee huyo alikuwa na ng’ombe wengi, akampa Sangiwa kazi ya kuwa mchungaji wa mifugo yake. Hilo halikuwa tatizo kwa Sangiwa, kwa kuwa alikuwa na shida, hakuwa na fedha, akakubaliana naye na hivyo kuanza kazi hiyo.
Ilikuwa kazi ngumu mno, kitendo cha kuchunga zaidi ya ng’ombe elfu kumi huku akiwa na wenzake wawili tu ilikuwa kazi kubwa. Kuna kipindi wanyama hao walikuwa wakiingia katika mashamba ya watu, waliwafukuza na hata wakati mwingine kusemwa sana huku wakipokea vitisho vya kila aina.
Itaendelea.
NzuriSEHEMU YA 17...
Peter alikuwa amedhamiria kumwandikia barua msichana huyo pasipo kukumbuka kwamba alikuwa kipofu. Siku iliyofuata, akaandika barua ndefu iliyojaza maneno matamu ambapo moja kwa moja akaelekea mjini ambapo huko akaituma kwa njia ya posta tena huku akiwa ameinyunyizia na manukato yaliyokuwa yakinukia vizuri.
Hakutaka kupoteza muda mjini, alichokifanya ni kurudi nyumbani huku akionekana kuwa na furaha tele. Katika kila alilokuwa akilifanya, bado kichwa chake kilimkumbuka msichana huyo ambaye alionekana kuwa kila kitu.
Usiku, usingizi wake ulikuwa wa mang’amung’amu, hakulala hata mara moja kutokana na mawazo mazito aliyokuwa nayo juu ya msichana huyo mrembo.
“Mmmh!” Peter alitoa mguno.
Hapo ndipo alipokumbuka kwamba msichana aliyekuwa amemtumia barua ile, Tatiana hakuwa mzima wa macho, alikuwa kipofu kwa asilimia mia moja, akaanza kujiuliza ni kwa namna gani ujumbe ule ungeweza kumfikia na kuusoma.
Barua ilijaza maneno mengi ya kimapenzi, alifahamu kwamba Tatiana aliheshimika sana kijijini kwa kuwa alikuwa mtu wa dini sana, lakini kitendo cha kumwandikia barua ile kilimaanisha kwamba ni lazima barua ile apewe mtu fulani na kumsomea, je hilo lisingekuwa tatizo kwake?
Tayari akaanza kupata mawazo mengine, hayakuwa mawazo mazuri bali yalikuwa mabaya ambayo aliona kwa namna moja au nyingine ingeweza kumuharibia msichana huyo aliyeaminika sana katika suala zima la dini.
Hakutaka kujali sana, kama kosa alikwishafanya hivyo alichokuwa akikisubiri kwa wakati huo ni kuona kitu gani kingetokea, kama lingekuwa tatizo kwake, basi alikuwa tayari kukabiliana nalo.
****
Tatiana aliendelea kumtumikia Mungu kupitia uimbaji wake kanisani. Moyo wake ulikuwa ukifarijika mno kila alipokuwa akikumbuka kwamba pamoja na kuwa msichana kipofu lakini bado Mungu alikuwa na mipango mingi na maisha yake.
Hali aliyokuwa nayo ilikuwa imekwishazoeleka maishani mwake. Tangu azaliwe, hakuwahi kumuona mtu yeyote zaidi ya kusikia sauti zao huku akiwa na hisia kali kwamba mtu aliyesimama mbele yake alikuwa nani na katika umati wa watu uliokuwa mbele yake, kulikuwa na watu wangapi.
Itaendelea.
We umepotelea wapi