Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
- Thread starter
- #321
SEHEMU YA 170
Siku hiyo walizungumza mengi na kisha kulala. Siku iliyofuata, wakafuatwa na gari kutoka ubalozini ambapo wakachukuliwa na kupelekwa katika hospitali hiyo ambapo baada ya kufika, moja kwa moja wakapelekwa katika chumba alicholazwa Tatiana.
Japokuwa kulikuwa na watu wengi waliotaka kumuona msichana huyo lakini wao waliruhiswa kutokana na kibali maalumu walichokuwa nacho. Walipofika chumbani humo, macho yao yakatua kwa wazazi wa Tatiana na balozi aliyekuwa na familia yake.
Wakasalimiana. Peter akaanza kupiga hatua kukifuata kitanda alicholazwa Tatiana. Alipofika, akaanza kumwangalia msichana huyo, hapohapo kumbukumbu za maisha yake ya nyuma aliyopitia na msichana huyo yakaanza kujirudia kama mkanda wa filamu, ghafla machozi yakaanza kujikusanya mashavuni mwake.
“Tatiana....amka,” alisema Peter huku akimwangalia. Watu wote walikuwa kimya.
“Peter,” aliita mzee Sangiwa.
“Ndiyo!”
“Hii ni laana Peter, yote yametokea baada ya kukuacha wewe,” alisema mzee Sangiwa.
“Hakuna, nahisi Mungu anataka kuzungumza nami kuhusu yeye. Hebu subiri,” alisema Peter.
Akayarudisha macho yake kwa Tatiana, akamshika mkono na kuyafumba macho yake. Wote wakabaki kimya, walimwangalia Peter, hawakujua alifanya nini, ila alibaki kimya kabisa. Ghafla, machozi yakaanza kububujika mashavuni mwake, moyo wake ukaumizwa mno.
Akamwachia mkono Tatiana na kisha kuelekea pembeni, aliisikia sauti ikimwambia kitu, ilimhuzunisha sana, alibaki akilia peke yake kiasi kwamba watu wengine wakaanza kuogopa.
“Mchungaji, tuambie kuna nini,” alisema mzee Sangiwa.
“Tatiana atapona,” alisema Peter.
“Asante Mungu!”
“Ila...”
“Kuna kuna nini?”
“Hatoweza kuona tena,” alisema Peter huku akiyafuta machozi yake, mama Tatiana, bi Frida akaanza kulia kwa sauti kubwa, kile alichoambiwa kwamba binti yake asingeweza kuona tena, kiliuchoma moyo wake.
Siku hiyo walizungumza mengi na kisha kulala. Siku iliyofuata, wakafuatwa na gari kutoka ubalozini ambapo wakachukuliwa na kupelekwa katika hospitali hiyo ambapo baada ya kufika, moja kwa moja wakapelekwa katika chumba alicholazwa Tatiana.
Japokuwa kulikuwa na watu wengi waliotaka kumuona msichana huyo lakini wao waliruhiswa kutokana na kibali maalumu walichokuwa nacho. Walipofika chumbani humo, macho yao yakatua kwa wazazi wa Tatiana na balozi aliyekuwa na familia yake.
Wakasalimiana. Peter akaanza kupiga hatua kukifuata kitanda alicholazwa Tatiana. Alipofika, akaanza kumwangalia msichana huyo, hapohapo kumbukumbu za maisha yake ya nyuma aliyopitia na msichana huyo yakaanza kujirudia kama mkanda wa filamu, ghafla machozi yakaanza kujikusanya mashavuni mwake.
“Tatiana....amka,” alisema Peter huku akimwangalia. Watu wote walikuwa kimya.
“Peter,” aliita mzee Sangiwa.
“Ndiyo!”
“Hii ni laana Peter, yote yametokea baada ya kukuacha wewe,” alisema mzee Sangiwa.
“Hakuna, nahisi Mungu anataka kuzungumza nami kuhusu yeye. Hebu subiri,” alisema Peter.
Akayarudisha macho yake kwa Tatiana, akamshika mkono na kuyafumba macho yake. Wote wakabaki kimya, walimwangalia Peter, hawakujua alifanya nini, ila alibaki kimya kabisa. Ghafla, machozi yakaanza kububujika mashavuni mwake, moyo wake ukaumizwa mno.
Akamwachia mkono Tatiana na kisha kuelekea pembeni, aliisikia sauti ikimwambia kitu, ilimhuzunisha sana, alibaki akilia peke yake kiasi kwamba watu wengine wakaanza kuogopa.
“Mchungaji, tuambie kuna nini,” alisema mzee Sangiwa.
“Tatiana atapona,” alisema Peter.
“Asante Mungu!”
“Ila...”
“Kuna kuna nini?”
“Hatoweza kuona tena,” alisema Peter huku akiyafuta machozi yake, mama Tatiana, bi Frida akaanza kulia kwa sauti kubwa, kile alichoambiwa kwamba binti yake asingeweza kuona tena, kiliuchoma moyo wake.