Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

SEHEMU 51...
“ Mungu, naomba umpe ushindi Tatiana, Mungu, nakuomba sana ufanye hilo,” alisema Nathan huku akiona washiriki watano wa mwisho wakiwa wamekaa tayari mbele ya ukumbi tayari kwa matokeo kutangazwa. Mapigo yake ya moyo yakaanza kumdunda.
*****

Tatiana hakuamini kile alichokuwa amekisikia kwamba alikuwa ametangazwa na kuwa mshindi wa shindano hilo lililodumu kwa miezi sita. Alisikia vizuri kwamba akitajwa jina lake lakini hakuamini kama alisikia vizuri au alikuwa amesikia jina jingine lililofanana na lake.
Kilichomshtua na kuamini kwamba alikuwa ametajwa yeye ni kelele za watu waliokuwa ukumbini pale ambao walikuwa wakilitaja jina lake kwa shangwe kubwa. Hapo ndipo akaamini kwamba yeye ndiye aliyeibuka mshindi katika shindano lile.
Furaha iliyoje! Alishindwa kuamini, hakuendelea kusimama, akajikuta akichuchumaa chini na kuanza kulia kama mtoto. Kile kiasi cha dola milioni tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni kumi zilikuwa zake.

Majaji wote wakasimama na kuanza kumfuata Tatiana aliyekuwa amezungukwa na washiriki wengine na kisha kumkumbatia kwa fuaraha, walikuwa wakimfariji, aache kulia kwani ule ulikuwa ni ushindi wake, alikuwa amejipatia kiasi kikubwa cha fedha ndani ya siku 180 tu.

Kila mtu aliyekuwa akifuatilia shindano lile alishangilia kwa kuona kweli haki ilitendeka, yule mtu aliyekuwa amestahili kuchukua ushindi ule, aliuchukua kitu kilichompa sifa sana bwana Warren kwa kuonekana kwamba hauwa na shindano lililokuwa na upendeleo.
Hapohapo vyombo vya ahabari vikaanza kutangaza juu ya ushindi ule, kila sehemu, picha za Tatiana akilia jukwaani zilikuwa zikionekana, kwa kipindi cha dakika kadhaa tu, tayari akawa maarufu mkubwa duniani.

“Tattie, don’t cry baby, I told you you are the best ever,” (Tattie, usilie kipenzi, nilikwambia wewe ni bora haijawahi kutokea) alisema Smith huku akimkumbatia Tatiana.

Watu kutoka ukumbini pale tayari walikwishajazana jukwaani na kila mmoja kutaka kumshika Tatiana ambaye kwa kipindi hicho alikuwa msichana mwenye uwezo mkubwa kifedha japokuwa hakuwa bilionea kama wengine.
 
52...
Kwa Smith, hicho ndicho kilikuwa kipindi maalumu cha kuionyesha dunia kwamba msichana yule aliyekuwa bora kwa kuimba duniani, alikuwa mpenzi wake. Pasipo kujiuliza chochote kile, pasipo kuogopa kamera wala kujua kwamba watu wawili waliokuwa wakimpenda sana Tatiana walikuwa wakilifuatilia shindano lile kwenye televisheni, hapohapo akamkumbatia Tatiana kwa nguvu kisha kuanza kubadilishana mate kitu kilichoshangiliwa sana na watu waliokuwa pale ukumbini.
*****

Ilikuwa ni zaidi na kupigiliwa msubali wenye ncha kali moyoni mwake au kuteketezwa na moto huku akijiona, maumivu aliyokuwa ameyapata Peter yalikuwa makubwa yalioufanya mwili wake kuanza kutetemeka na kijasho chembamba kuanza kumtoka.
Hakuamini kile alichokuwa akikiona mahali pale, msichana aliyekuwa akimpenda, aliyempa nafasi kubwa moyoni mwake, alikuwa amesimama jukwaani na mwanaume mwingine kisha kubadilishana mate naye.

Alihisi wivu mkali ukiuchoma moyo wake, hasira zake zikawaka, pasipo kutarajia, machozi yakaanza kububujika mashavuni mwake. Hakuendelea kuangalia kwani kadiri alivyokuwa akiangalia na ndivyo alivyozidi kuumia zaidi, akajikuta akiizima televisheni na kukimbilia chumbani.
Huko hakunyamaza, akaanza kulia kwa sauti ya juu kama mtoto. Wafanyakazi wa nyumba ile wakaogopa kwa kuhisi kwamba inawezekana kulikuwa na msiba, hivyo wakaanza kuelekea chumbani kwa Peter lakini mlango ulifungwa kwa ndani.
Walijaribu kuugonga lakini haukufunguliwa, bado kilio cha Peter kiliendelea kusikika ndani ya chumba kile, kilio kilichochanganyikana na maumivu makali ya moyo wake.

“Peter...fungua mlango,” alisema mfanyakazi mmoja, alikuwa mama mtu mzima.
Peter hakutaka kufungua mlango, bado aliendelea kubaki ndani huku akilia tu. Alishinda ndani asubuhi mpaka mchana.Mchungaji Lazaro aliporudi kutoka kanisani, akaambiwa kile kilichokuwa kimetokea.
“Kisa nini?” aliuliza.

“Hata sisi hatufahamu, tulisikia tu akilia,” alijibu mfanyakazi yule.
Mchungaji Lazario akaelekea chumbani kwa Peter, akajaribu kuufungua mlango lakini ulikuwa umefungwa kwa ndani. Mama Peter akawa na wasiwasi kwamba inawezekana kulikuwa na jambo baya lilikuwa limetokea, hivyo kuendelea kuuliza zaidi.
 
SEHEMU YA 53...
Mchungaji Lazaro na mkewe wakaanza kumuita na kumtaka kuufungua mlango lakini Peter hakufanya hivyo, aliendelea kuufunga mlango ule na hakutaka kuufungua kabisa jambo lililowatia hofu wazazi hao kwa kuhisi kwamba inawezekana Peter alikuwa amejidhuru chumbani, hivyo wakaanza kufanya mchakato wa kuuvunja mlango.
*****

Kilichotokea kwa Peter ndicho kilichotokea kwa nathan pia, hakuamini kile alichokuwa akikiona katika televisheni kipindi kile, hakuamini kama kweli msichana aliyekuwa akimpenda kwa moyo wote, Tatiana alikuwa akibadilishana mate na mwanaume ambaye alikuwa akimuona mara kwa mara wakati walipokuwa wakifanya mazoezi, Smith.

Moyoni aliumia mno na kilichomuumiza zaidi ni kwamba alimuacha msichana Dasy kwa sababu ya Tatiana lakini mwisho wa siku, msichana huyo alikuwa na mwanaume mwingine kabisa. Nathan akashindwa kuvumilia, kile alichokuwa amekiona kwenye televisheni kilimchanganya na kumuumiza mno, akajikuta akianza kububujikwa na machozi.

“Haiwezekani! Tatiana hawezi kufanya hivi,” alisema Nathan huku akionekana kuwa na hasira.
Alionekana kama kichaa, alitembea huku na kule pale sebuleni huku akilia tu, kila alipokuwa akiwaangalia wawili wale kwa jinsi walivyokuwa wamekumbatiana baada ya kubadilishana mate, aliendelea kuumia zaidi.
“Tatiana, nimemuacha Dassy kwa ajili yako! Haiwezekani, lazima ulipe hili,” alisema Nathan huku wakati mwingine akiongea kama kichaa.
*****

Kiasi cha dola milioni tano kikaingizwa ndani ya akaunti ya Tatiana aliyokuwa amefunguliwa na kuunganishwa na benki moja nchini Tanzania. Bwana Warren hakutaka binti huyo akatwe katika fedha zile kama kodi ya serikali, alichokifanya ni kuongeza kiasi kingine ambacho kilikatwa na Tatiana kupata kiasi chote pasipo makato yoyote yale.

Moyo wake ulifurahia, hakuamini kama tangu siku ya kwanza alipokwenda nchini Tanzania kumbe ndiyo alikuwa akimfuata mshindi wa shindano lile. Aliyakumbuka maneno yake ambayo mara kwa mara alikuwa akiwaambia washiriki walipokuwa nchini Tanzania kwamba alikuwa na hisia kabisa kwamba mshindi wa shindano lile angetokea katika nchi hiyo japokuwa hakujua ni nani.
 
SEHEMU YA 54...
Kilichoongeza furaha zaidi kwa bwana Warren ni kile kitendo cha mtoto wake kubusiana na Tatiana, hakuamini kama hali ilikuwa namna ile, akabaki akitabasamu tu kwani hata naye, mbali na upofu aliokuwa nao Tatiana, alivutika na uzuri aliokuwa nao.

Akamfuata binti huyo palepale mbele ya ukumbi ule na kumkumbatia huku akiwa na furaha kubwa. Waandishi wa habari waliendelea na kazi zao za kupiga picha kwani hata hali ile waliyokuwa nayo mahali pale, ilionyesha dhahiri kwamba mzee huyo alifurahishwa na mengi katika ushindi wa Tatiana.

“Do you remember what I told you six months ago?” (Unakumbuka nilichowaambia miezi sita iliyopita?) aliuliza bwana Warren.
“I do remember,” (Nakumbuka) alisema Tatiana huku akiyafuta machozi yaliyokuwa yakimbubujika.
“This is God’s plan, He wants you to move from poverty to wealth,” (Huu ndiyo mpango wa Mungu, hutaka wewe utoke kwenye umasikini mpaka utajiri) alisema bwana Warren huku akiachia tabasamu pana.

Kila kitu kikakamilishwa siku hiyo, baada ya hapo, ikapangwa sherehe ya kumpongeza Tatiana kutokana na ushindi aliokuwa ameupata na wenzake walioingia kwenye tano bora, hivyo tarehe ikawekwa wazi, ilikuwa ni wiki mbili kuanzia siku hiyo.
Akachukuliwa chumba katika moja ya hoteli ya nyota saba jijini New York, huko akakaa na wenzake wanne huku wakiisubiria hiyo sherehe ya kuwapongeza huku kwa bwana Warren, akianza kufanya mikakati wazazi wa washindi walioingia tano bora waweze kufika nchini Marekani kusherehekea na ndugu zao.

“Kwa hiyo wazazi wangu watakuja huku?” aliuliza Tatiana.
“Ndiyo! Mipango inaanza kupangwa. Tatiana, unaanza kuelekea kwenye utajiri mkubwa endapo utafanya mipango madhubuti juu ya fedha zako,” alisema Smith.

“Nitajitahidi kufanya kila liwezekanalo mpaka niwe bilionea, ila itawezekana?” aliuliza Tatiana.
“Kwa nini ishindikane?”
“Huoni jinsi nilivyo?”
“Tatiana, nikwambie kitu?”
“Niambie.”
“Tabasamu kwanza,” alisema Smith, Tatiana akaachia tabasamu pana lililotoka moyoni.
“Nimewasiliana na Dk. Stephen Buffet kutoka Denver, Colorado kwa ajili yako.”
“Ndiye nani?”
 
SEHEMU YA 55...
“Ni mtaalamu wa magonjwa ya macho, nimezungumza naye na ni kwamba utatakiwa kuelekea huko kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa macho yako ili uweze kuona kwa mara ya kwanza,” alisema Smith.
“Nione?”
“Ndiyo!”
“Itawezekana vipi? Nimezaliwa hivihivi Smith.”

“Tatiana! Kuna wengi walizaliwa hivyo lakini mwisho wa siku wakapona kabisa. Gharama yake ni kubwa lakini nitagharamia mimi mwenyewe, ninataka uone, upo tayari?” aliuliza Smith.
“Nipo tayari mpenzi.”
“Sawa. Sherehe ikishakwisha, tutakwenda huko,” alisema Smith na kisha kukumbatiana. Huo ndiyo ukawa usiku wa kwanza kwa wawili hao kufanya mapenzi na Tatiana kutolewa usichana wake.

“Nitakupenda milele kwa hii zawadi uliyonipa,” alisema Smith, hakuamini kumkuta Tatiana akiwa bado hajaingiliwa na mwanaume yeyote yule.
“Nitakupenda pia mpenzi,” alisema Tatiana na kukumbatiana kwa furaha.
 
Ayaaa imeniuma sana mzungu kumla sista etu daaaaah imeniuma sana saaaaana yan hapa nilipo nalia tu daaaaah kweli penzi maumivu sijui tu washikaji zangu peter na nathan huko waliko km mm tu imeniuma hivi daaaaah imeniuma sana .
.
Shunie usiishie hapa tu please ifike mwisho kama kuleeeee Gosheni maaana naona damu tu huko mbele watu wamechafukwa.
 
Ayaaa imeniuma sana mzungu kumla sista etu daaaaah imeniuma sana saaaaana yan hapa nilipo nalia tu daaaaah kweli penzi maumivu sijui tu washikaji zangu peter na nathan huko waliko km mm tu imeniuma hivi daaaaah imeniuma sana .
.
Shunie usiishie hapa tu please ifike mwisho kama kuleeeee Gosheni maaana naona damu tu huko mbele watu wamechafukwa.
Aargghh mnaniudhi nyie wa isiishie hapa naletaje story nusu
 
Aargghh mnaniudhi nyie wa isiishie hapa naletaje story nusu
Nakujua huletagi nusu best but tuvumilie si unajua vile inauma story ikipotea tunajihami tu usituarostishe jamaani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom