Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

SEHEMU YA 154

Nikola alipoondoka, naye akarudi uwanjani mpaka tamasha lilipoisha saa sita usiku na kisha kuelekea sehemu ya kuegeshea magari kwa ajili ya kuondoka. Muda wote huo, Buffet hakuwa na furaha, alionekana kuwa na hofu kubwa huku kwa kumwangalia tu ungegundua kwamba kulikuwa na kitu alichokuwa akikijua ambacho kilimsumbua moyoni mwake.

Mara baada ya kusaini vitabu vya mashabiki wake, Tatiana akaingia garini huku akiwa na furaha tele, aliwapungua mikono, vioo vikapandishwa na kuanza kuodoka mahali hapo huku akiwa na msafara wa magari matano.

Moyoni alifarijika mno, hakuamini kama alimaliza vizuri kufanya shoo ile iliyokuwa imehudhuriwa na watu wengi. Msafara wa magari hayo ukaanza safari kuelekea hotelini, kila mmoja alikuwa kimya garini, walipofika kwenye makutano ya
Barabara ya Welsing na Bulsberg, hapohapo ukasikika mlio mmoja mkubwa, gari alilopanda Tatiana ambalo lilikuwa katikati ya magari hayo yaliyosimama kwenye mataa, likaanza kubimbilika, watu walioshuhudia tukio lile, wakashika vichwa vyao, vilio vikasikika, kila mtu akabaki ameduwaa, gari alilokuwa amepanda Tatiana, lilikuwa nyang’anyang’a.

“Tatiana.....” alijikuta akiita Buffet, hapohapo akateremka kutoka garini na kuanza kukimbia kule lilipokuwa gari lile alilokuwa Tatiana.
 
SEHEMU YA 155

Ilikuwa ni ajali mbaya mno, gari lile alilokuwa Tatiana lilirushwa kutoka lilipokuwa na kubimbirika kwenda upande mwingine, kila mtu aliyeiona ajali ile, alihuzunika kwani kwa muonekano tu, hakukuwa na mtu yeyote aliyehisi kama kuna mtu alikuwa mzima ndani ya lile gari.

Damu zilitapakaa sehemu yote hiyo, ajali ile ambayo ilionekana ni ya kizembe ikaanza kulaumiwa na kila mtu. Ilikuwaje gari ligongwe wakati lipo katika mataa tayari kwa kuvuka? Dereva aliyeligonga gari lile alikuwa na utaalamu gani wa kuhama kutoka barabara nyingine na kuhamia barabara ile na kuligonga? Kila swali lililoulizwa, hakukuwa na mtu mwenye jibu sahihi.

“Tatiana....” aliita Buffet, alikuwa amefika katika gari lile, alijaribu kuchungulia ndani, damu zilianza kuchurizika kutokea ndani ya gari lile kitu kilichomshtua sana Buffet.
Watu wengine waliokuwa katika magari mengine ambao walikuwa kwenye msafara ule wakateremka na kuelekea kule kulipokuwa na gari lile kisha kuanza kusaidia kufungua milango kwa ajili ya kuwatoa majeruhi wale.
“Mlango haufunguki,” alisema jamaa mmoja.

“Vunja kioo,” alisema jamaa mwingine.
Hakukuwa na cha kufanya zaidi ya kuvunja vioo vya gari lile kisha kuwatoa majeruhi. Vazi alilokuwa amelivaa Tatiana, kwa kuliangalia tu, usingeweza kugundua kama lilikuwa jeupe kwani lilitapakaa damu kila sehemu.
Walichokifanya ni kuwatoa majeruhi hao na kisha kuwaingiza kwenye magari mengine na kuanza kuwapeleka katika Hospitali ya Helios Klinikum Berlin-Buch iliyokuwa umbali wa kilometa moja kutoka hapo walipokuwa.

Ndani ya gari, Buffet alikuwa pembeni ya Tatiana, alikuwa akilia tu kwani kile kilichokuwa kimetokea, kilimuumiza moyo wake. Hakujua afanye nini, alibaki akilia tu kwani kila kitu kilichokuwa kimetokea, alikifahamu na hata mtu aliyepanga ajali ile alimfahamu sana, alikuwa mpenzi wake, Nikola.

Japokuwa Tatiana alikuwa hoi na hakuweza hata kutingisha kiungo chochote kile, lakini bado Buffet alikuwa na mapenzi ya dhati kwa msichana Nikola ingawa kile kilichokuwa kimetokea hakukipenda kabisa.
 
SEHEMU YA 156

Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika hospitali hiyo ambapo manesi waliokuwa nje wakaleta machela na kisha miili ya majeruhi wale kuchukuliwa na kuanza kupelekwa ndani. Buffet hakunyamaza, aliendelea kulia huku akimtaka Tatiana aamke kitandani pale lakini hakuweza kufanya hivyo, aliumizwa vibaya na alikuwa amepoteza fahamu.

“Subirini hapa,” alisema nesi mmoja, walikuwa nje ya mlango ulioandikwa Theatre (chumba cha upasuaji).
“Nataka niwe naye karibu dokta.”
“Hapana! Subirini hapa.”

Hawakuwa na jinsi, kwa sababu waliambiwa wasubiri, wakafanya hivyo. Wakakaa kwenye kiti, Buffet alikuwa akibubujikwa na machozi tu, kile kilichokuwa kimetokea kilimuumiza moyo wake, hakutaka kumkumbuka tena Nikola japokuwa alimpenda sana msichana huyo.
Hapo ndipo alipoanza kujuta kwamba ni bora angemkataa msichana huyo mapema na kuwa na Nikola ili kile kilichokuwa kimetokea kisingetokea, ila huo haukuwa muda wa majuto, ulikuwa ni muda wa kufikiria nini kilitakiwa kufanyika baada ya hapo.

Walikaa pale kwa zaidi ya masaa matatu, hakukuwa na mtu yeyote aliyezungumza nao zaidi ya madaktari kuingia na kutoka kwa kupishana tu. Kila mmoja alionekana kuwa bize kwani kile kilichokuwa kimetokea kiliwatia presha hata wao wenyewe.

Vyombo vya habari havikuwa mbali, mara baada ya kusikia kwamba kulikuwa na ajali mbaya iliyokuwa imetokea, kwa haraka wakaanza kuelekea katika hospitali hiyo ili kupata uhakika juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

Watu wakazidi kuogopa, walijua fika kwamba ajali ile ilikuwa ni ya kupanga kutokana na jinsi ilivyokuwa imetokea, ila mpaka katika kipindi hicho, hawakujua ni nani alikuwa nyuma ya kile kilichokuwa kimetokea.

Watu wakaanza kukusanyika katika hospitali hiyo, walionekana kuchanganyikiwa mno, matukio kadhaa ya nyuma yaliyomtokea mwanamuziki Tatiana, na lile lililokuwa limetokea, yaliwahuzunisha sana kwani hawakuamini kama kungekuwa na mtu aliyekuwa akitafutwa na kifo namna ile.

Masaa matano yalipita, hawakupokea taarifa zozote kutoka ndani ya kile chumba zaidi ya madaktari kupishana kwa zamu tu. Wengine wakashindwa kuvumilia zaidi, wakainuka na kuondoka kwa ahadi kwamba wangerudi hospitalini hapo baadaye.
 
Eeh mungu naomba hadi nifike mwisho wa simulizi hii tatiana awe amekufa kwel,ila peter asijulikane kabisa kama amehusika kwa chochote
 
SEHEMU YA 157

Ingawa wote waliondoka lakini Buffet hakutaka kuondoka, alikuwa hospitalini pale, alikalia kiti huku akiwa amejiinamia chini, machozi hayakukauka, kila alipokuwa akimkumbuka Tatiana, aliendelea kulia.
“Samahani!” aliisikia sauti ya mtu mmoja, alipouinua uso wake, alikuwa daktari.
“Ndiyo dokta!”

“Pole kwa kilichotokea!”
“Asante sana. Niambie nini kinaendelea ndani.”
“Tumejitahidi sana.....”
“Lakini amefariki?”
“Hapana! Bado anapumua, ila kwa kutumia msaada wa mashine,” alijibu dokta yule.
“Atapona?”
“Tuna uhakika huo.”
Majibu ya daktari yule yalimridhisha lakini hakutaka kuyaamini kwa asilimia mia moja kwamba Tatiana ataweza kupona kwani kwa jinsi alivyokuwa amemuona, aliumizwa vibaya mno kichwani.

Hakuwa na jinsi, kwa sababu yeye ndiye aliyesema kwamba mpenzi wake angepona, hakuwa na jinsi zaidi ya kusubiri na kuona kile ambacho kingeendelea. Ilipofika saa kumi na moja alfajiri, Buffet hakuweza kuendelea kukaa hospitalini hapo, alichokifanya ni kurudi hotelini kupumzika kwani usiku mzima hakuwa amelala.

Alipofika hotelini, akaingia chumbani kwake na kujilaza. Wala hazikupita dakika nyingi, akaona simu yake ikiita, alipokiangalia kioo cha simu ile na kuona jina la Nikola, akajikuta akiiweka simu ile pembeni.

Mapenzi mapenzi tu, kichwa chake kikaanza kumfikiria Nikola pia, hakuweza kuuzia moyo wake kuacha kumfikiria msichana huyo kwani bado aliuteka mno moyo wake, akajikuta akiiangalia simu yake na kisha kuichukua. Kwa kuwa simu ilikuwa imekwishakata, akaamua kupiga yeye.
 
SEHEMU YA 158

“Unasemaje?” aliuliza Buffet hata kabla ya salamu.
“Nini kinafuata?” ilisikika sauti ya Nikola ikiuliza swali.
“Kuhusu nini?”
“Kwani tulipanga nini? Au bado unampenda?” aliuliza Nikola kwa sauti ya kiburi.

“Hapana! Ulichokifanya sijakipenda, ni bora ungeacha niachane naye kwa usalama,” alisema Buffet.
“Nimekupa masaa mangapi ufanye hivyo? Mbona hukufanya maamuzi?”
“Hata kama Nikola, vitu vingine si vya kufanya harakaharaka.”
“Sasa ninataka uniambie, nini kinafuata!”

“Nikola, naomba muda.”
“Muda zaidi! Wa nini?”
“Kwanza apone.”
“Haiwezekani Buffet! Yaani hapo haiwezekani kabisa. Hebu niambie kwanza nijue, unanipenda?”
“Nakupenda lakini.....”
“Lakini nini?”

“Ngoja ap...” alisema Buffet lakin hata kabla hajamaliza sentensi yake, Nikola akakata simu.
Buffet akachanganyikiwa, kitendo cha kukatiwa simu kikamfanya kufikiri kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wa kuwasiliana na msichana huyo. Hakutaka kumuacha, hakutaka kuona akiondoka zake, alikuwa akimuhitaji mno hivyo alichokifanya ni kumpigia simu, mbaya zaidi, simu ilikuwa ikiita pasipo kupokelewa kitu kilichozidi kumchanganya na kumuumiza moyo wake.

“Pokea simu Nikola,” alisema Buffet huku akiwa na presha kubwa, simu haikupokelewa, iliendelea kuita na hata alipojaribu baadae, haikuwa hewani, ilizimwa jambo lililomchanganya sana Buffet.
 
SEHEMU YA 159

Watu hawakuamini kile kilichokuwa kimetokea, kila mtu aliyesikia kuhusu ajali aliyokuwa ameipata Tatiana, alisikitika mno kwani kulionekana kuwa na mpango kabambe wa watu fulani waliotaka kumuua msichana huyo.
Maandamano yakaanza kufanyika shemu mbalimbali duniani, watu wakaingia barabarani na kushika mabango na kulaani juu ya kile kilichokuwa kikiendelea kwamba wahusika walitakiwa kuacha kwani kile alichokuwa akikifanya Tatiana kilikuwa ni kipaji chake na hakutakiwa kushambuliwa.

Maandamano yale yakawasukuma viongozi mbalimbali wa serikali ya Tanzania na Marekani, wakawasiliana na hapo ndipo walipoanza kufanya upelelezi wa chini kwa chini kwa kutumia shirika la upelelezi la CIA kwa nchini Marekani na Interpool kwa ajili ya kuhakikisha mtu aliyefanya hilo anajulikana haraka iwezekanavyo.

Kitu cha kwanza kabisa, wapelelezi kutoka nchini Marekani wakasafiri mpaka nchini Tanzania, huko, walikuwa wakienda kufuatilia kile walichokuwa wakihitaji kukifahamu juu ya Tatiana kwani walikuwa na wasiwasi kwamba inawezekana chimbuko la mambo hayo yote lilianzia nchini Tanzania.

Walipofika huko, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuonana na wazazi wake, wakazungumza nao kisha kuwauliza maswali kadhaa kuhusu Tatiana. Mzee Sangiwa na mkewe walikuwa kwenye maumivu makali na hapo walikuwa wakijiandaa kwa ajili ya kuelekea nchini Ujerumani.

“Taarifa zinasema kwamba Tatiana alikuwa kipofu tangu alipozaliwa, kweli?” aliuliza mpelelezi mmoja, kutokana na kuwa wa kimataifa, hata lugha ya Kiswahili haikuwasumbua, walikuwa wakizungumza zaidi ya lugha saba, tena kwa ufasaha.
“Ndiyo!”

“Unamfahamu mtu wa kwanza kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi?” aliuliza Kim.
“Ndiyo! Alikuwa mchungaji Peter Lazaro.”
“Sawa. Hakuna tatizo,” alisema Kim na kisha yeye na wenzake kuondoka mahali hapo pasipo kuuliza huyo Peter alikuwa nani na aliishi wapi.

Walikuwa na kila kitu mikononi mwao, walichokuwa wakikihitaji ni mahali watu hao walipokuwa. Walifuatilia kwa kipindi kichache na wakagundua kwamba Peter ndiye alikuwa mpenzi wa kwanza wa Tatiana.
 
SEHEMU YA 160

Umakini wao wa kutafuta wahusika, pia walifanikiwa kuingia katika simu ya Tatiana na kuangalia mawasiliano yake kwa ujumla, tangu siku ya kwanza alipoanza kutumia simu mpaka siku hiyo.
Mbali na hiyo, pia walipitia mawasiliano yake na barua pepe, kulikuwa na watu wengi waliokuwa na wasiwasi nao, ila kubwa zaidi Peter. Wakaondoka Shinyanga na kuelekea Mwanza ambapo huko wakakutana na mwinjilisti Peter na kuanza kuzungumza naye.
“Unamfahamu Tatiana?”

“Ndiyo! Nyie ni wakina nani?”
“Usijali, sisi ni watu tunaofanya naye muziki.”
“Sawa!”
“Unafahamu nini kuhusu yeye?”
“Ni mwanamuziki.”
“Alikwishawahi kuwa mpenzi wako?”
“Ndiyo! Ila aliniacha.”
“Kwa nini?”

“Sijajua, ila nahisi kwa sababu alimpata mwanaume mwingine,” alisema Peter.
“Ulijisikiaje ulipoachwa, ulikasirika?”
“Ndiyo lakini kila kitu kimepita.”
“Ulisoma wapi ulipofikia elimu ya chuo?”
“Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.”

“Mwaka gani?” Yalikuwa ni maswali mfululizo, watu wale waliokuwa mbele yake walionekana kuwa makini mno, wakati akiulizwa maswali na Kim, mpelelezi mwingine alikuwa bize na simu yake. Mwingine alikuwa wakimwangalia kwa umakini machoni.

Pembeni yao, kama umbali wa hatua thelathini walilisimamisha gari lao lililokuwa na vioo vilivyowekwa tinted nzito. Ndani ya gari lile, kulikuwa na watu ambao kazi yao ilikuwa ni kucheza na sura tu.

Walikuwa na kamera zenye uwezo mkubwa, walikuwa wakiurekodi uso wa Peter huku wakiwa na picha kadhaa zilizokuwa zikionyesha sura zilizokuwa na muonekano tofautitofauti hali iliyowafanya kugundua mwanaume huyo alikuwa akifikiria vipi.
“Anaonekanaje?”

“Sura yake inafanana na hii hapa,” alisema mpelelezi mmoja garini huku akiionyesha sura fulani kwenye kompyuta.
“Na picha hiyo inasemaje?”
“Mtu mwenye huzuni, aliyeumizwa, nahisi kuna kitu,” alisema jamaa huyo.
“Kingine?”

“Wakati mwingine sura yake inafanana na hii hapa.”
“Inasemaje?”
“Mtu mwenye hasira.”
Wapelelezi walitumia zaidi sura kusoma hisia za mtu alizokuwa nazo moyoni mwake, waliamini kwamba kama mtu angeweza ishara fulani usoni mwake, ilimaanisha kitu fulani, hivyo ndivyo ilivyokuwa.
 
SEHEMU YA 161

Katika aina ya sura alizokuwa akiziweka Peter zilionyesha ni jinsi gani aliumia alipokuwa ameulizwa kuhusu Tatiana na ni kwa jinsi gani alikuwa na hasira. Wapelelezi wale aliokuwa akizungumza nao hawakutaka kukaa sana mahali hapo, wakaaga na kuondoka.

Hawakusihia hapo, bado walitaka kufahamu mengi kuhusu muinjilisti Peter hivyo walichokifanya ni kuanza kuangalia fedha zilizokuwa kwenye akaunti yake. Zilikuwa fedha ndogo sana ambazo waliamini asingeweza kufanya harakati za kummaliza Tatiana kwa kumlipua na bomu au hata kusababisha ajali.

“Turudini Marekani,” hilo ndilo walilolifanya, wakarudi zao nchini humo pasipo kugundua kwamba mtu huyo ndiye aliyehusika katika kumchoma kisu Tatiana, ila kwa kuwa walikwenda kwa ajili ya kupeleleza juu ya ajali hiyo, hawakutaka kujali sana.

Wapelelezi wengine waliendelea na zoezi lao nchini Marekani kuona ni nani hasa alikuwa nyuma ya kila kitu. Walichokuwa wakikifanya ni kuchukua simu ya Tatiana na kuangalia mawasiliano yake aliyokuwa akifanya na watu wengine tangu mwaka huo uingie, hawakuwafanikiwa kuona kitu chochote kile, walijaribu hata kuangalia mtiririko wa meseji, kote huko hawakugundua kitu.

Hawakuishia hapo, walichohisi ni kwamba inawezekana akawa anawasiliana na mtu kupitia barua pepe lakini napo huko hawakuambulia kitu chochote ambacho kingeweza kuwasaidia, wakaendelea kuvisumbua vichwa vyao.

“Tufanye nini?” aliuliza mmoja wa wapelelezi.
“Na vipi kuhusu mpenzi wake?”
“Nani? Buffet?”
“Ndiyo!”
“Mmh! Sidhani!”
“Tujaribu.”

Hawakuwa na jinsi, walikuwa kwenye wakati mgumu kuliko nyakati zote, walitaka kuhakikisha kwamba kila kitu walichotakiwa kukifanya walikifanya. Wakaanza kurudi tena katika chumba cha mitambo, kulikuwa na wafanyakazi wengi lakini kila mmoja alikuwa bize na mambo yake.

Wakaanza kupiga hatua kumfuata kijana mmoja ambaye alionekana kuwa na miaka ishirini lakini alikuwa balaa katika suala zima la kompyuta na network. Huyo ndiye aliyekuwa akihakikisha kila kitu kinafanyika kama kinavyotakiwa.
 
SEHEMU YA 162

Walipomwambia jukumu alilotaka kulifanya kwa kipindi hicho, hakuwa na jinsi, akaiwasha kompyuta yake na kisha kuanza kufanya utaalamu wake, mara akaingia katika barua pepe ya Buffet na kuanza kuangalia kila kitu.

Walipekua na kupekua, walitazama barua pepe zilizoingia, zilizotoka na zile zilizohifadhiwa, hawakuishia hapo, waliangalia mpaka katika mafolda yake lakini kote huko hawakuambulia kitu cha kuweza kuwasaidia.

“Twende simuni, namba yake hii hapa,” alisema mpelelezi mmoja na kisha kuanza kuangalia humo simuni.
Mtu wa kwanza kabisa kuona akiwasiliana naye, yaani simu yake kumpigia na hata kupigiwa alijulikana kwa jina la Nikola, walijaribu kuangalia mahali msichana huyo alipokuwa akiishi, wakajua ni Ujerumani ndani ya Jiji Munich, ila katika kipindi hicho alikuwa ndani ya Jiji la Berlin, hivyo ndivyo kompyuta yao ilivyoonyesha.

“Hebu fuatilia na meseji zote zilizokuwa zikienda kwa huyu binti, kisha ingia na kusikiliza mawasiliano yao kwa njia ya sauti,” alisema mpelelezi mmoja na kisha kuanza kufanya kama alivyoambiwa.
Walichokiona, kikawapa uhakika kwamba binti huyo alikuwa nyumba ya kila kitu. Kwanza wakaanza kuziona meseji zilizoonyesha kwamba alikuwa akilitaka penzi kutoka kwa mwanaume huyo, hawakuishia hapo, walizikuta mpaka meseji zilizokuwa zikisisitiza Buffet afanye jambo fulani la kumuacha Tatiana lakini hakutaka kukubali kulifanya kwa haraka mno.

Waliendelea mpaka meseji zilipokwisha, hivyo wakaona kulikuwa na umuhimu wa kusikiliza mazungumzo yao. Wakafanya hivyo, watu hao hawakuwa wamezungumza sana zaidi ya kutumiana meseji, simu ya mwisho kabisa kuzungumza ilikuwa ni siku ya tukio la ajali lilipotokea ambapo Buffet alikuwa akilalamika juu ya kile kilichokuwa kimetokea. “Unasemaje?” “Nini kinafuata?” “Kuhusu nini?”

“Kwani tulipanga nini? Au bado unampenda?” “Hapana! Ulichokifanya sijakipenda, ni bora ungeacha niachane naye kwa usalama.” “Nimekupa masaa mangapi ufanye hivyo? Mbona hukufanya?”

“Hata kama Nikola, vitu vingine si vya kufanya harakaharaka.”
“Sasa ninataka uniambie, nini kinafuata!”
“Nikola, naomba muda.”
“Muda zaidi! Wa nini?”
“Kwanza apone.”
 
SEHEMU YA 163

“Haiwezekani Buffet! Yaani hapo haiwezekani kabisa. Hebu niambie kwanza nijue, unanipenda?”
“Nakupenda lakini.....”
“Lakini nini?”
“Ngoja ap...” Waliyasikiliza mazungumzo hayo, hawakutaka kujifikiria, hawakutaka kujiuliza, wakajua moja kwa moja kwamba msichana huyo na Buffet ndiye waliyekuwa wamesababisha ajali hiyo! Mjadala ukafungwa.

“Ni lazima tuwasiliane na polisi wa Ujerumani kuwakamata watu hawa wakati upelelezi zaidi ukiendelea,” alisema mpelelezi mmoja na hapohapo kuwaambia wapelelezi wengi akiwemo kiongozi wao juu ya mchakato mzima walivyokuwa wameuendesha na mwisho wa siku kuwakamata watu waliokuwa wakiwahitaji.
*****

Buffet hakutaka kutoa simu sikioni, alikuwa akisikilizia ili mpenzi wake aipokee na hatimaye kuzungumza naye. Nikola hakupokea simu ile kitu kilichomfanya kujisikia vibaya mno kwani kitu pekee alichokuwa akikitaka ni kuzungumza naye tu.

Alichokifanya ni kutoka chumbani kwake kwa lengo la kwenda chumbani kwa msichana huyo ili aongee naye, alipofika mlangoni, akajaribu kuufungua mlango, ukawa umefungwa kwa ndani, akaanza kugonga hodi.
“Nani?” ilisikika sauti ya Nikola kutoka ndani.
“Buffet.”
“Nikusaidie nini?”

“Naomba nizungumze nawe mara moja.”
“Uzungumze nami kuhusu nini?”
“Naomba ufungue mpenzi.”
Hakukaa sana mlangoni, mlango ukafunguliwa na Nikola kusimama mlangoni. Alionekana kukasirika, uso alikunja ndita, kwa jinsi alivyoonekana, hakuonekana kuwa na furaha hata mara moja jambo lililomfanya Buffet kukosa raha.

“Naomba unisamehe!”
“Nikusamehe umefanya nini?” aliuliza Nikola.
“Naomba unisamehe! Nipo tayari kumuacha akiwa kitandani ili niwe nawe,” alisema Buffet huku akimaanisha alichokisema.

Mpaka kufikia kutoa kauli hiyo, Buffet akakaribishwa ndani na kukalishwa kitandani. Kila alipokuwa akimwangalia Nikola, alikuwa msichana mrembo, mwenye sifa za kuwa mwanamke mzuri duniani.

Japokuwa Tatiana alikuwa mrembo kuliko Nikola lakini kwake msichana huyo alionekana kuwa kila kitu. Buffet alibaki akimeza mate ya tamaa mara baada ya kuuona upaja wa Nikola ambao ulifichwafichwa na nguo ya kulalia ambayo kwa chini ilikuwa na mauamaua fulani..
 
SEHEMU YA 164

“Unamaanisha unachokisema?” aliuliza Nikola, Buffet akayatoa macho yake upajani mwa Nikola na kumwangalia usoni.
“Ndiyo! Ila naomba unipe nafasi moja tu, kisha baada ya hapo, tutaelekea Munich kuanza maisha yetu,” alisema Buffet.
“Nafasi gani?”

“Nataka nirudi hospitalini nikamuage Tatiana, japo kwa kumbusu tu,” alisema Buffet.
“Nikupe dakika ngapi mpaka kurudi?” aliuliza Nikola.
“Saa moja.”

“Sawa. Unaweza kwenda, ukipitiliza, tusijuane,” alisema Nikola.
“Hakuna tatizo.”
Hilo ndilo aliloliomba na kuruhusiwa, alichokifanya ni kuondoka hotelini hapo na kurudi hospitalini. Japokuwa alikuwa ameumia sana lakini hakuwa na la kufanya, ili kuwa na msichana Nikola ilitakiwa amuache Tatiana.

Alijua fika kwamba Tatiana alikuwa msichana mrembo hasa zaidi ya Nikola lakini hakujua kwa nini alimpenda sana Nikola, hakuwa na jinsi, kila kitu alichokuwa akikfanya mahali hapo ni kumfurahisha Nikola na mwisho wa siku kuwa naye tu.

Hakuangalia dunia ingesema nini, hakuangalia watu wangemuonaje, kitu pekee alichokuwa akikihitaji mahali hapo ni kuwa na Nikola tu, hivyo alitakiwa kufanya kile alichokuwa akikihitaji msichana huyo wa Kijerumani.

Hospitalini kulikuwa na idadi kubwa ya watu, wote hao walifika hospitalini hapo kwa ajili ya kumuona mwanamuziki huyo. Kulikuwa na usumbufu mkubwa kwani kila mtu aliyeambiwa aondoke, hakuondoka, alitaka kumuona Tatiana tu.

Kama ni fujo, zilikwishatokea mahali hapo, watu waligoma kabisa, ila kwa kuwa ilikuwa ni hospitalini, polisi hawakufanya kitu zaidi ya kukubaliana na watu hao tu, kusimama nje ya hospitali hiyo, ila kuingia ndani, hakuna aliyeruhisiwa.

Mara baada ya kufika hapo, Buffet akaanza kuufuata mlango, polisi wote walimfahamu, hawakumzuia, wakampa ruhusa ya kuingia ndani ya jengo hilo. Wakati akipiga hatua kuelekea katika chumba alicholazwa Tatiana, machozi yalikuwa yakimbubujika tu, hakuamini kama hiyo ndiyo ingekuwa siku ya mwisho kumuona msichana huyo.
 
Mwendo mzuri sasa ngoja niianze kuisoma sasa, najua mpaka nifike hapa itakua imesha
 
SEHEMU YA 165

Alipofika, akaambiwa asubiri nje kwani ndiyo kwanza mgonjwa alikuwa akiandaliwa mara baada ya kutolewa kutoka katika chumba cha upasuaji, hilo halikuwa tatizo, alichokifanya ni kusubiri huku muda wote macho yake yakiwa kwenye saa yake tu, alikumbuka vilivyo kwamba alipewa saa moja tu.

Baada ya dakika ishirini, daktari akamruhusu kuingia ndani, akaanza kupiga hatua kuelekea katika kitanda alicholala Tatiana, alipomuona tu, jinsi uzuri aliokuwa nao, alijikuta akimpenda zaidi msichana huyo.

Mawazo juu ya Nikola yakapotea kwa muda, mapenzi yake akahisi yakianza kurudi tena, alimwangalia namna alivyokuwa kimya kitandani pale, moyo wake ulimuuma mno, binti mrembo, alikuwa akipumulia mashine ya oksijeni huku akiwa na bandeji kubwa kichwani mwake.

“Tatiana! Amka mpenzi!” alisema Buffet kwa sauti ya chini huku akimwangalia Tatiana kitandani pale na kisha kumbusu shavuni.
Moyo wake uliumia mno ila hakuwa na cha kufanya, kwa muonekano wa harakaharaka kitandani pale, Tatiana alionekana kutokuwa na dalili za kuamka leo wala kesho. Huku akibubujikwa na machoz mashavuni mwake, ghafla akahisi simu yake ikianza kutetemeka mfukoni mwake, alichokifanya, ni kuitoa simu ile na kuangalia mpigaji, alikuwa Nikola.
“Muda unayoyoma,” ilisikika sauti ya msichana huyo simuni.

“Nakuja, nakuja mpenzi,” alisema Buffet.
Mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwa Nikola, akajikuta akiondoka chumbani hapo ili aweze kumuwahi hotelini. Ni kweli alimpenda Tatiana lakini mapenzi ya Nikola yaliusisimua moyo wake mno.
Alipofika hotelini, akaungana na Nikola na hatimaye kuanza safari siku hiyohiyo kuelekea jijini Munich. Kuwa na msichana huyo kulimpa faraja moyoni mwake, hakutaka tena kukumbuka kuhusu Tatiana aliyekuwa hospitalini huku amepoteza fahamu kutokana na ajali mbaya ya gari iliyotokea.

Walitumia masaa mawili kwa usafiri wa treni mpaka kuingia jijini Munich ambapo hapo walitegemea kuanza maisha yao mapya. Maisha yalikuwa ni ya furaha tele, Buffet hakutaka kukumbuka chochote kile kuhusu Tatiana, kwake, alimchukulia kama msichana wa kupita ambaye kwa kipindi hicho aliamua kuishi na Nikola tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom