Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,869
- Thread starter
- #241
SEHEMU YA 122...
Hakukuwa na mtu aliyemuona, na hata wale waliomuona, hawakuwa wakihusika chochote kile na hospitali hiyo hivyo hawakujishughulisha naye kabisa. Huku akiwa ameufikia mlango wa kuingia ndani, mara akashtuka kusikia akiitwa.
“You!! Where you go?” (Unakwenda wapi?) aliuliza mlinzi kwa Kingereza kibovu.
“I’ve gota patient in here,” (Nina mgonjwa humu) alijibu Nathan.
“You no go there, this is not entering,” (Usiende huko, hii si sehemu ya kuingilia) alisema mlinzi huyo huku akiendelea kuiharibu lugha hiyo pasipo kujali chochote kile.
Hicho ndicho alichotaka kukifahamu mahali hapo, alitaka kufahamu ni ulinzi wa aina gani ulikuwepo. Alichokifanya mara baada ya kuambiwa kutoka kule ni kurudi na kuelekea kule kulipokuwa na watu wengi ambao walikuwa wakisubiri ruhusa ya daktari kuingia hospitalini.
“Hamuwezi kuingia wote, wengine bakini, zamu kwa zamu,” alisema daktari mmoja, alikuwa akiwaambia watu zaidi ya mia nne waliokuwa wamekusanyika mbele yake.
Watu wakagawanywa, wengine walitakiwa kuingia ndani lakini wengine walitakiwa kubaki kwani walikuwa wengi mno, hivyo wangeingia zamu kwa zamu. Hilo halikuwa tatizo, walichokuwa wakikitaka ni kuingia ndani tu na kumuona msichana huyo aliyekuwa akiteseka kitandani.
Ndani ya hospitali hiyo, madaktari walikuwa wamejitahidi sana kumtibu Tatiana kiasi kwamba kikafika kipindi wakaona kwamba walifikia mwisho. Walitumia ujuzi wao wote, kidogo Tatiana akaanza kuonyesha nafuu, yaani kile kidonda alichokuwa nacho kikaanza kukauka hali iliyoonyesha kwamba muda wowote ule msichana yule angeweza kurudiwa na fahamu.
“Kidogo kuna nafuu,” alisema Dk. Mandesh na kisha kuwashukuru madaktari wenzake kwa kazi kubwa waliyokuwa wameifanya mpaka hatua ile ya kidonda kile kuanza kukauka.
Buffet hakuwa na cha kushukuru zaidi, kama ni maneno ya shukrani, alihakikishia anawapa kila siku kwani kwa jinsi alivyowaona madaktari wale, walikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba mgonjwa yule akipona. Kuna wakati walikataa kula, walikataa kupumzika kwa ajili ya Tatiana kitu ambacho kwa Buffet kilionekana kuwa zaidi ya kujitolea, hivyo shukrani hazikumuisha mdomoni mwake.
Hakukuwa na mtu aliyemuona, na hata wale waliomuona, hawakuwa wakihusika chochote kile na hospitali hiyo hivyo hawakujishughulisha naye kabisa. Huku akiwa ameufikia mlango wa kuingia ndani, mara akashtuka kusikia akiitwa.
“You!! Where you go?” (Unakwenda wapi?) aliuliza mlinzi kwa Kingereza kibovu.
“I’ve gota patient in here,” (Nina mgonjwa humu) alijibu Nathan.
“You no go there, this is not entering,” (Usiende huko, hii si sehemu ya kuingilia) alisema mlinzi huyo huku akiendelea kuiharibu lugha hiyo pasipo kujali chochote kile.
Hicho ndicho alichotaka kukifahamu mahali hapo, alitaka kufahamu ni ulinzi wa aina gani ulikuwepo. Alichokifanya mara baada ya kuambiwa kutoka kule ni kurudi na kuelekea kule kulipokuwa na watu wengi ambao walikuwa wakisubiri ruhusa ya daktari kuingia hospitalini.
“Hamuwezi kuingia wote, wengine bakini, zamu kwa zamu,” alisema daktari mmoja, alikuwa akiwaambia watu zaidi ya mia nne waliokuwa wamekusanyika mbele yake.
Watu wakagawanywa, wengine walitakiwa kuingia ndani lakini wengine walitakiwa kubaki kwani walikuwa wengi mno, hivyo wangeingia zamu kwa zamu. Hilo halikuwa tatizo, walichokuwa wakikitaka ni kuingia ndani tu na kumuona msichana huyo aliyekuwa akiteseka kitandani.
Ndani ya hospitali hiyo, madaktari walikuwa wamejitahidi sana kumtibu Tatiana kiasi kwamba kikafika kipindi wakaona kwamba walifikia mwisho. Walitumia ujuzi wao wote, kidogo Tatiana akaanza kuonyesha nafuu, yaani kile kidonda alichokuwa nacho kikaanza kukauka hali iliyoonyesha kwamba muda wowote ule msichana yule angeweza kurudiwa na fahamu.
“Kidogo kuna nafuu,” alisema Dk. Mandesh na kisha kuwashukuru madaktari wenzake kwa kazi kubwa waliyokuwa wameifanya mpaka hatua ile ya kidonda kile kuanza kukauka.
Buffet hakuwa na cha kushukuru zaidi, kama ni maneno ya shukrani, alihakikishia anawapa kila siku kwani kwa jinsi alivyowaona madaktari wale, walikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba mgonjwa yule akipona. Kuna wakati walikataa kula, walikataa kupumzika kwa ajili ya Tatiana kitu ambacho kwa Buffet kilionekana kuwa zaidi ya kujitolea, hivyo shukrani hazikumuisha mdomoni mwake.