Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

SEHEMU YA 18...
Kila mtu kijijini alimuheshimu msichana huyo ambaye kwa kipindi hicho alikuwa akisubiria majibu ya mtihani wake wa kidato cha nne aliokuwa ameufanya.
Hakumkumbuka Peter, alimchukulia kama rafiki yake wa kawaida ambaye angeweza kuja na kuondoka, kwake, Mungu alikuwa wa kwanza, walifuata wazazi wake na watu wengine, lakini kwa Peter, hakukuwa hata na siku moja ambayo aliweza kumkumbuka.
Baada ya kupita siku kadhaa tangu Peter aondoke kijijini hapo, akasikia kanisani mtu wa matangazo akitangaza kwamba kulikuwa na barua moja ambayo alikuwa ametumiwa Tatiana.

Kwanza kanisa zima halikuamini, si wao tu bali hata Tatiana mwenyewe hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angeweza kumtumia barua na wakati kila mmoja alifahamu kwamba alikuwa kipofu.
Ukiachana na maswali yote aliyokuwa akijiuliza, pia alijiuliza kuhusu mtumaji wa barua hiyo nani. Hakuwahi kutoa anuani za kanisa kwa mtu yeyote yule, sasa ilikuwaje leo hii apokee barua kutoka kwa mtu ambaye hakuamini kwamba alikuwa akimfahamu?

Hakutaka kujiuliza sana, alichokifanya ni kuchukua barua hiyo na muda wa kwenda nyumbani ulipofika, akaondoka huku akitangulizana na mama yake.
Moyo wake ulikuwa na kimuemue cha kutaka kuona humo ndani ya barua hiyo kuliandikwa nini. Alitamani afike nyumbani haraka iwezekanavyo na amwambie mama yake amsomee barua ile ambapo mpaka katika kipindi hicho, hakumfahamu mtumaji.

Baada ya kufika nyumbani, akaelekea chukmbani kwake na kutulia. Mkononi alikuwa na barua ile, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuipapasa tu na kisha kuifungua, hakuweza kuona chochote kile, alichoklifanya ni kumuita mama yake.
“Unasemaje binti yangu?”

“Sijui hii barua nimeandikiwa na nani.”
“Nikusaidie nini Tatiana? Kuisoma”
“Ndiyo! Nataka unisaidie kusoma mama,” alijibu Tatiana huku akinyoosha mkono wake na kumpa mama yake barua ile.
Bi Frida akaipokea na kisha kukaa kitandani pale. Kabla ya kuisoma kwa sauti, akaanza kuisoma kimoyomoyo, akatoa mguno uliomchanganya Tatiana ambaye akashikwa na hamu zaidi ya kutaka kujua kilichoandikwa ndani.
“Inasemaje mama?” Itaendelea.
 
SEHEMU Ya 19...
“Ni barua nzuri na mbaya pia.”
“Kwa nini? Nani ameandika?”
“Peter!”
“Peter?”
“Ndiyo.”
“Peter nani?”
“Lazaro! Yule mtoto wa mchungaji.”
“Ameandikaje?”
“Subiri nikusomee,” alisema bi Frida.
Tatiana akajiweka vizuri kitandani pale, alitaka kusikia maneno aliyoyaandika Peter katika barua ile. Alitaka kujua kila neno kwani aliamini kwamba mguno wa mama yake ulitokana na maneno yaliyoandikwa ndani ya barua ile, hivyo naye alitaka kuyasikia. Barua hiyo iliandikwa hivi.... Kwako Tatiana.

Namshukuru Mungu kwa kutufikisha nyumbani salama, nashukuru kwa maombi yako na kanisa kwa ujumla. Sisi huku kwa upande wetu, tupo salama na tunaendelea vizuri na majukumu.
Dhumuni la barua hii ni kutaka kukushukuru kwa kila kitu, hasa kwa kukubali urafiki pamoja nami. Tattie nashindwa kujizuia, naomba unisamehe kama nitakuwa nimekosea sana kwa kuvuka mipaka juu ya kile tulichokuwa tumekubaliana kwamba tuwe marafiki tu.
Kiukweli umetokea kuuteka moyo wangu sana (Kama ni dhambi, Mungu anisamehe). U msichana mzuri sana, mwerevu, na ninafurahia kuona kwamba unampenda Mungu na umetoka katika familia za wokovu kama nilivyo mimi.
Tattie, siwezi kukaa kimya, siwezi kuvumilia kutokukwambia hili kwamba umeuteka moyo wangu vilivyo. Sijui niseme nini, ninakupenda zaidi ya maelezo, kama ningeambiwa ni kitu gani nichague ili niendelee kuwa nacho maishani mwangu, hakika ningekuchagua wewe.

Sitaki kukuchezea, sitaki tuishie hapa, ninataka kuendelea kuishi na wewe milele, ninataka nikuoe na mwisho wa siku nawe uwe mama mchungaji kama alivyokuwa mama yangu. Natamani nikuone, natamani nije tena huko kwa ajili yako tu.
Naomba ujifikirie juu ya hilo na unijibu haraka sana kwani kila ninapokaa chumbani, nahisi kuna siku naweza kufa kwa kukuwaza wewe, na kama si kufa, basi naweza kupata presha itakayonilaza kitandani miaka yote.

Nakupenda Tattie, natumaini kupokea majibu hivi karibuni kama upo tayari kuwa na mimi au ndiyo unaamua kunichinjia baharini.
Mungu akulinde.

Peter Lazaro

Itaendelea.
 
SEHEMU YA 20...
Ilikuwa ni barua ndefu, baada ya bi Frida kumaliza kuisoma, uso wa Tatiana ulijawa na tabasamu pana, maneno matamu yaliyoandikwa ndani ya barua ile yakaufanya moyo wake kufarijika mno.
Hakujali kama mbele yake alikuwepo mama yake, barua ile iliugusa moyo wake kupita kawaida. Mama yake aliyekuwa mbele yake, akamsogelea na kumkumbatia, bi Frida akashindwa kujizuia, machozi yakaanza kumbubujika mashavuni mwake.

Tatiana alikata tamaa, hakuamini kama kwenye maisha yake angetokea mwanaume ambaye angetamka kwamba alikuwa akimpenda mno. Mbali na uzuri aliokuwa nao, alikuwa msichana kipofu ambaye angeshindwa kufanya kitu chochote katika maisha yake, kitendo cha kusikia kwamba Peter alikuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati, kwake ikaonekana kuwa faraja kubwa.
Hicho ndicho kilichokuwepo hata kwa mama yake, hakutegemea kama ingetokea siku ambayo angekuja mwanaume na kumwambia kwamba anampenda na alitaka kumuoa na hatimaye waishi milele.

Hata kama walimpenda Mungu, hawakutaka kufanya dhambi lakini barua ya Peter ikawafanya wabubujike na machozi muda wote. “Mama! Ninapendwa....” alisema Tatiana huku akilia kama mtoto.
“Unapendwa mwanangu, Mungu amekuletea mwanaume atakayekuwa bora katika maisha yako,” alisema bi Frida huku akijitahidi kuyafuta machozi yake.
Barua ile, ikaifanya mioyo yao kubadilika na kufurahi sana, ila pamoja na hayo, hawakutaka mzee Sangiwa afahamu chochote kile.
“Nimwambieje?”
“Mwambie umekubaliana naye.”
“Kweli?”
“Ndiyo! Huyu mwanaume ameletwa na Mungu! Hii ni baraka,” alisema bi Frida.
Tatiana akaanza kuandika barua ya majibu. Japokuwa alikuwa kipofu, ila alikuwa na uwezo wa kunyoosha mwandiko, hasa kwenye karatasi.
Ila mbali na hayo, alijua kwamba kulikuwa na mapenzi pasipo maumivu, yaani angependa na kupendwa siku zote, asingeumizwa kitu ambacho hakikuwa kweli, kwa kuwa alikubali kuingia kwenye mapenzi, basi ilimpasa kukubaliana na maumivu pia kitu ambacho hakuwa akikielewa kwa wakati huo.

Itaendelea.
 
Wacha weeh
Ila shunie hiyo avatar yako inahamasisha watu kuingia JF mara kwa mara maana hako kanguo dah halafu mtu mwenyewe anaonekana eti anaona aibu. Mungu anakuona lakini
 
Ila shunie hiyo avatar yako inahamasisha watu kuingia JF mara kwa mara maana hako kanguo dah halafu mtu mwenyewe anaonekana eti anaona aibu. Mungu anakuona lakini
Umehamia kwangu tena woiii
 
Sasa hii Shunie mbona arosto yaanza mapema?
 
Kama kawaida yako.. Ndio maana nakupenda katika pendo la Kristo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom