Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,869
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 18...
Kila mtu kijijini alimuheshimu msichana huyo ambaye kwa kipindi hicho alikuwa akisubiria majibu ya mtihani wake wa kidato cha nne aliokuwa ameufanya.
Hakumkumbuka Peter, alimchukulia kama rafiki yake wa kawaida ambaye angeweza kuja na kuondoka, kwake, Mungu alikuwa wa kwanza, walifuata wazazi wake na watu wengine, lakini kwa Peter, hakukuwa hata na siku moja ambayo aliweza kumkumbuka.
Baada ya kupita siku kadhaa tangu Peter aondoke kijijini hapo, akasikia kanisani mtu wa matangazo akitangaza kwamba kulikuwa na barua moja ambayo alikuwa ametumiwa Tatiana.
Kwanza kanisa zima halikuamini, si wao tu bali hata Tatiana mwenyewe hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angeweza kumtumia barua na wakati kila mmoja alifahamu kwamba alikuwa kipofu.
Ukiachana na maswali yote aliyokuwa akijiuliza, pia alijiuliza kuhusu mtumaji wa barua hiyo nani. Hakuwahi kutoa anuani za kanisa kwa mtu yeyote yule, sasa ilikuwaje leo hii apokee barua kutoka kwa mtu ambaye hakuamini kwamba alikuwa akimfahamu?
Hakutaka kujiuliza sana, alichokifanya ni kuchukua barua hiyo na muda wa kwenda nyumbani ulipofika, akaondoka huku akitangulizana na mama yake.
Moyo wake ulikuwa na kimuemue cha kutaka kuona humo ndani ya barua hiyo kuliandikwa nini. Alitamani afike nyumbani haraka iwezekanavyo na amwambie mama yake amsomee barua ile ambapo mpaka katika kipindi hicho, hakumfahamu mtumaji.
Baada ya kufika nyumbani, akaelekea chukmbani kwake na kutulia. Mkononi alikuwa na barua ile, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuipapasa tu na kisha kuifungua, hakuweza kuona chochote kile, alichoklifanya ni kumuita mama yake.
“Unasemaje binti yangu?”
“Sijui hii barua nimeandikiwa na nani.”
“Nikusaidie nini Tatiana? Kuisoma”
“Ndiyo! Nataka unisaidie kusoma mama,” alijibu Tatiana huku akinyoosha mkono wake na kumpa mama yake barua ile.
Bi Frida akaipokea na kisha kukaa kitandani pale. Kabla ya kuisoma kwa sauti, akaanza kuisoma kimoyomoyo, akatoa mguno uliomchanganya Tatiana ambaye akashikwa na hamu zaidi ya kutaka kujua kilichoandikwa ndani.
“Inasemaje mama?” Itaendelea.
Kila mtu kijijini alimuheshimu msichana huyo ambaye kwa kipindi hicho alikuwa akisubiria majibu ya mtihani wake wa kidato cha nne aliokuwa ameufanya.
Hakumkumbuka Peter, alimchukulia kama rafiki yake wa kawaida ambaye angeweza kuja na kuondoka, kwake, Mungu alikuwa wa kwanza, walifuata wazazi wake na watu wengine, lakini kwa Peter, hakukuwa hata na siku moja ambayo aliweza kumkumbuka.
Baada ya kupita siku kadhaa tangu Peter aondoke kijijini hapo, akasikia kanisani mtu wa matangazo akitangaza kwamba kulikuwa na barua moja ambayo alikuwa ametumiwa Tatiana.
Kwanza kanisa zima halikuamini, si wao tu bali hata Tatiana mwenyewe hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angeweza kumtumia barua na wakati kila mmoja alifahamu kwamba alikuwa kipofu.
Ukiachana na maswali yote aliyokuwa akijiuliza, pia alijiuliza kuhusu mtumaji wa barua hiyo nani. Hakuwahi kutoa anuani za kanisa kwa mtu yeyote yule, sasa ilikuwaje leo hii apokee barua kutoka kwa mtu ambaye hakuamini kwamba alikuwa akimfahamu?
Hakutaka kujiuliza sana, alichokifanya ni kuchukua barua hiyo na muda wa kwenda nyumbani ulipofika, akaondoka huku akitangulizana na mama yake.
Moyo wake ulikuwa na kimuemue cha kutaka kuona humo ndani ya barua hiyo kuliandikwa nini. Alitamani afike nyumbani haraka iwezekanavyo na amwambie mama yake amsomee barua ile ambapo mpaka katika kipindi hicho, hakumfahamu mtumaji.
Baada ya kufika nyumbani, akaelekea chukmbani kwake na kutulia. Mkononi alikuwa na barua ile, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuipapasa tu na kisha kuifungua, hakuweza kuona chochote kile, alichoklifanya ni kumuita mama yake.
“Unasemaje binti yangu?”
“Sijui hii barua nimeandikiwa na nani.”
“Nikusaidie nini Tatiana? Kuisoma”
“Ndiyo! Nataka unisaidie kusoma mama,” alijibu Tatiana huku akinyoosha mkono wake na kumpa mama yake barua ile.
Bi Frida akaipokea na kisha kukaa kitandani pale. Kabla ya kuisoma kwa sauti, akaanza kuisoma kimoyomoyo, akatoa mguno uliomchanganya Tatiana ambaye akashikwa na hamu zaidi ya kutaka kujua kilichoandikwa ndani.
“Inasemaje mama?” Itaendelea.
