Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

SEHEMU YA 166

Maisha yao yakafana jijini Munich, msichana Tatiana akasahaulika kichwani mwake, hakuwepo moyoni, aliyekuwa akimfikiria kwa wakati huo alikuwa Nikola tu ambaye alikuwa kwenye mapenzi ya dhati huku wakianza kuweka mikakati ya kuanza kuishi pamoja kama mume na mke, kwa kifupi ni kwamba walitaka kufunga ndoa, mpaka mwezi mmoja unakatika, walikuwa kama pete na kidole.

***** Tatiana alikuwa kwenye hali mbaya, pale kitandani hakupata nafuu hata mara moja, siku zilikatika na bado hali yake ilizidi kuwa mbaya kiasi kwamba madaktari wakaogopa mno kwa kuona muda wowote ule mwanamuziki huyo angeweza kufariki dunia.

Dunia nzima ilikuwa kimya, ilikuwa ikisikilizia kile kilichokuwa kikiendelea kule Ujerumani, wengi walishauri kwamba ingekuwa vizuri kama Tatiana angechukuliwa na kupelekwa katika moja ya hospitali nchini Marekani lakini madaktari hawakutaka kutoa ruhusa hiyo kutokana na hali yake mbaya aliyokuwa nayo.

Siku zikakatika, madaktari wakashangaa, hawakuelewa mpenzi wake na Tatiana alikuwa mahali gani kwani tayari wiki nzima ilikuwa imepita lakini mwanaume huyo hakurudi tena hospitalini. Jambo hilo lilizua maswali mengi yasiyokuwa na majibu.

Taarifa juu ya kutokuwepo kwa Buffet hospitalini zikaanza kutolewa, watu walishangaa, hawakujua alipokuwa mwanaume huyo na sababu gani iliyomfanya kumkimbia msichana huyo mrembo katika kipindi alichokuwa hoi hospitalini.

Watu wakahofia kwamba inawezekana Buffet akawa ametekwa na kuuawa na mwili wake kutupwa sehemu lakini mawazo hayo yakafutika kwani polisi nao walikuwa makini kufuatilia lakini hawakuambulia chochote kile.

“Where is this buddy?” (Mshikaji yupo wapi?) aliuliza jamaa mmoja, alikuwa ameshika Gazeti la New York Times la nchini Marekani, lilitoa taarifa kuhusiana na kutoweka kwa Buffet hospitalini.
“I don’t know, maybe he has been kidnapped,” (Sijui, labwa atakuwa ametekwa)

“Impossible.” (Haiwezekani)
“Why not?” (Kwa nini isiwezekane?)
“I don’t know, but it is impossible,” (Sijui lakini haiwezekani)
 
SEHEMU YA 167

Maswali yaliendelea kumiminika juu ya mahali alipokuwa Buffet, hakukuwa na mtu aliyejua ukweli wowote kwamba mwanaume huyo aliamua kumtoroka Tatiana kwa sababu alikutana na msichana wake wa zamani.

Kilichofanyika ni kupigiwa simu na watu wake wa karibu, simu haikupatikana na hata kazini kwake hakuwepo. Watu walisikitika mno kwani kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele bado hali ya Tatiana ilikuwa tete nchini Ujerumani.
Wiki ya pili ilipoingia tangu Tatiana

afikishwe hapo hospitalini, wazazi wake wakafika kwa ajili ya kumjulia hali. Watu wengine walizuiliwa kuingia katika chumba alicholazwa msichana huyo ila wao wakaruhusiwa kwa kibali maalumu na kuingia.

Walichokiona mbele yao, kiliwasikitisha mno, Tatiana alikuwa kimya kitandani, alikuwa akipumulia mashine ya oksijeni, alikuwa hoi na hakukuwa na dalili zozote kama kuna siku angeweza kuinuka kitandani pale.

Wazazi wake wakajikuta wakibubujikwa na machozi, walimsogela na kisha kuanza kumwangalia, mioyo yao iliwauma mno, hakukuwa na picha mbaya ambayo waliiona katika maisha yao kama ile iliyomuonyesha Tatiana kitandani huku akiwa hajitambui kabisa.

“Hii ni laana,” alisema mzee Sangiwa huku akionekana kuwa na majonzi mno.
“Laana?”
“Ndiyo! Haya yote ni kwa sababu ya Peter,” alisema mzee Sangiwa.
“Usiseme hivyo mume wangu!”

“Huu ndiyo ukweli. Tangu amuache Peter, amekuwa kwenye misukosuko mikubwa, huyu ni Peter, mke wangu, kuna kila sababu ya kumuomba msamaha Peter,” alisema mzee Sangiwa huku akiyafuta machozi yaliyokuwa yakimbubujika mashavuni.

Hicho ndicho alichohisi mzee Sangiwa, kila alipokuwa akimwangalia Tatiana kitandani pale alisikia sauti moyoni mwake ikimwambia kwamba kile kilichokuwa kikiendelea kutokea katika maisha ya binti yake kilikuwa ni laana.
Walilia na kulia lakini machozi yao hayakubadilisha kitu chochote kile, bado msichana yule aliendelea kulala kitandani pale huku akiwa hajitambui kabisa.
 
SEHEMU YA 168

Siku zikakatika na wiki ya tatu kuingia, mzee Sangiwa hakutaka kukaa nchini Ujerumani, alichokifanya ni kufanya kila liwezekanalo arudi Tanzania ili atakapokwenda huko arudi na Peter ambaye aliamini kwamba ni laana yake ndiyo iliyomuweka msichana huyo kitandani kwa muda mrefu.

“Hapana! Hautakiwi kwenda, huwezi kuniacha peke yangu, ni bora aje yeye,” alisema mkewe.
“Sasa atakuja vipi?”
“Tuwasiliane na balozi wetu nchini hapa, anaweza kutusaidia,” alishauri mama Tatiana.

Hicho ndicho walichokifanya, wakawasiliana na balozi na kumwambia kilichokuwa kikiendelea hospitalini, walipewa pole na balozi huyo kuahidi kufika hospitalini hapo siku inayofuatia, hivyo hawakumwambia kile walichotaka kumwambia.

Siku iliyofuata, majira ya saa nne asubuhi balozi huyo alikuwa hospitalini hapo, akawapa pole kwa kile kilichokuwa kikitokea na kuwaahidi kwamba kila kitu kingekuwa salama, hivyo alihitaji muda wa kulishughulikia suala la msichana huyo hospitalini hapo.

“Ila kuna jingine,” alisema mzee Sangiwa.
“Lipi hilo?”
“Kuna mtu tunataka aje huku kumuona Tatiana.”
“Nani?”
“Peter!”
“Ndiye nani?”

Hawakuwa na jinsi, kutokana na kile kilichokuwa kikiendelea, wakaamua kumhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea kipindi cha nyuma. Ilikuwa stori yenye kuhuzunisha mno, balozi yule na familia yake walipoisikia, walibaki wakihuzunika tu kwani mambo yaliyokuwa yametokea, hata naye ikaanza kumuingia akilini kwamba inawezekana ile kuwa laana kutokana na kile kilichokuwa kimetokea.

“Nitahakikisha kijana huyo anafika nchini Ujerumani, msijali, nitashughulikia,” alisema balozi yule.
 
Yani hawa jamaa mapimbi kweli kubali kukataliwa ni ujasiri sana kwanza mm namuona tatie yuko sahihi kabisa utapendaje watu huwaoni bhana Sawa wao walimpenda kwa sababu waliuona na walivutiwa na uzuri wake je hawakujifikiria kuwa naye alikuwa na uhuru wa kuchagua aliyevutiwa nae baada ya kuona ?
Tena ukute hata uzuri hawakuwa nao wanazingua tu inawauma sababu hawajala mzigo mbafuuuu kabisa.
 
SEHEMU YA 169

Watu walizidi kuponywa magonjwa yao, huduma aliyokuwa akiifanya Peter ilionyesha ni kiasi gani muinjilisti huyo alivyokuwa na upako mkubwa. Wachawi walibadilisha maisha yao na kumuabudu Mungu, waliokuwa wazinzi, wakaacha njia zao na kumfuata Mungu.

Kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika mikutano mbalimbali ya Injili ilionyesha ni kwa jinsi gani Mungu alikuwa akitenda miujiza kutokana na huduma aliyokuwa nayo muinjilizisti Peter.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake ya kila siku, aliendelea kumtumikia Mungu, aliyabadilisha maisha yake na katika kipindi hicho, mke wake, Lydia alikuwa mjauzito.

Huo ulikuwa mkutano wake wa pili ndani ya mwaka mmoja, Uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza ulijaza watu wengi waliohitaji ukombozi katika maisha yao. Kila siku Peter alikuwa mtu wa kukaa chumbani mwake na kuanza kuomba, hiyo ndiyo ilikuwa siri kubwa ya yale yaliyokuwa yakifanyika, hakujinyakulia utukufu, kila kitu alimuachia Mungu kwa kuamini kwamba yeye ndiye aliyekuwa akifanya yote hayo.

Baada ya siku kadhaa, akapokea wageni kutoka serikalini, walifika nyumbani hapo na kuzungumza naye kwamba alikuwa akihitajika haraka iwezekanavyo nchini Ujerumani. Aliposikia hivyo tu, alijua kwamba hiyo itakuwa ishu ya Tatiana, hakujua ni kitu gani kilichoendelea, ila alichokifanya ni kwenda huko.
Hakutaka kwenda peke yake, aliongozana na mkewe mpaka nchini Ujerumani ndani ya Jiji la Berlin, hapo, wakaunganisha mpaka hotelini ambapo gharama zote zilikuwa kwa balozi huyo. Hotelini hapo, Peter alikuwa na mawazo mno, alimkumbuka Tatiana, aliyakumbuka yote aliyofanyiwa lakini katika yote hayo, hakuonyesha chuki, yalikuwa yamepita na aliyaacha yawe hivyo.

“Usifikirie sana mume wangu kuhusu Tatiana!” alisema mkewe.
“Najua, ni muda mrefu sana, msichana huyu amekuwa kwenye matatizo mengi sana, nahisi Mungu anataka kufanya kitu kwa ajili ya maisha yake,” alisema Peter huku akiifungua Biblia na kuanza kupitia vitabu kadhaa.

“Hata mimi nakubaliana nawe, cha msingi tukamuone tu, nahisi kuna mengi Mungu atataka kufanya kwa ajili ya maisha yake,” alisema mke wake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom