Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

SEHEMU YA 138

“Nyie ni wakina nani?”
“Wazazi wake.”
“Hamruhusiwi kumuona.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Kisa?”
“Nyie jueni kwamba hamruhusiwi kumuona,” alisema polisi aliyekuwa kaunta maneno ambayo yaliungwa mkono na kila polisi.
Baba yake Nathan hakutaka kuhangaika, alichokifanya ni kunyanyua simu yake na kuanza kupekua majina kadhaa yaliyokuwa humo, alipolipata jina alilokuwa akilitaka, akabonyeza kitufe cha kupiga simu na baada ya sekunde kumi, mtu wa upande wa pili akapokea simu, alikuwa swahiba wake mkubwa, waziri mkuu wa nchi hiyo na kuanza kuzungumza naye.

Alimwambia mengi tu lakini kubwa zaidi ni yeye kuzuiliwa kumuona mtoto wake. Hilo wala halikuwa tatizo kubwa, akaambiwa ampe simu mkuu wa kituo hicho ambaye baada ya kukabidhiwa akaanza kufokewa kama mtoto kwa kile kilichokuwa kimetokea kituoni kwake.
“Samahani mzee,” alisema mkuu wa kituo baada ya simu kukatwa.

“Hakuna cha samahani, nionyesheni kijana wangu haraka,” alisema baba yake Nathan na hapohapo wakachukuliwa na kupelekwa ndani ya chumba kimoja kwa heshima kubwa na kuambiwa kusubiri hapo.

Wala haukuchukua muda mrefu, Nathan akaletwa chumbani hapo. Hakuwa amejeruhiwa, hakupigwa hata kidogo. Akawekwa kwenye kiti huku akiwa amefungwa pingu. Hapohapo baba yake akaagiza afunguliwe zile pingu kitendo kilichofanyika haraka sana.
“Nathan, nini kimetokea?” aliuliza baba yake.

“Baba! Unamkumbuka yule mwanamke aliyenifanya nimuache Dassy?”
“Ndiyo!”
“Ndiye huyu niliyetaka kumuua!”
“Unasemaje?”
“Ndiye huyuhuyu niliyetaka kumuua. Ameniumiza sana, hatakiwi kuishi hata mara moja,” alisema Nathan huku machozi yakianza kumbubujika mashavuni mwake.

“Nathan....”
“Baba! Ameniumiza sana, nimemuacha mwanamke aliyekuwa akinipenda kwa moyo wa dhati, halafu leo anafanya hivi! Anafanya hivi ili iweje? Baba, nina hasira naye mno,” alisema Nathan huku akionekana kumaanisha kile alichokuwa akikisema.

Mama yake akashindwa kuvumilia, naye akajikuta akibubujikwa na machozi kwani kitendo cha kuyaona machozi ya mtoto wake kilimuumiza mno moyoni mwake. Alimpenda sana, hakutaka kumuona akilia, hakukuwa na mtu aliyekuwa akimpenda kama Nathan.
 
SEHEMU YA 139

Muda huo, Nathan akaanza kusimulia kila kitu kilichotokea tangu siku ya kwanza alipokutana na Tatiana na kile kilichoendelea katika maisha yao ambapo kwake ilionekana kama maisha yaliyojaa maumivu makali mno.

“Unataka tukufanyie nini?” aliuliza baba yake.
“Chochote kile ili nitoke na kumuua Tatiana.”
“Hapana! Hatutaki utoke na kumuua huyo malaya. Naomba uachane naye na urudi kwa Dassy,” alisema baba yake.
“Ataweza kukubali?”

“Hana tatizo. Amekuwa na maisha yenye majonzi siku zote, amekuwa akilia sana, amekataa kuolewa na mwanaume mwingine, aliwaambia wazazi wake kwamba kama hatoolewa na wewe, kamwe hatoweza kuolewa na mwanaume mwingine yeyote yule na ni bora aishi hivyohivyo maishani mwake bila mume. Nathan, Dassy anakupenda mno, achana na huyu malaya, rudi kwa Dassy,” alisema mama yake huku akiyafuta machzoi yake.
“Ila Tatiana amaniumiza mama!”

“Mungu atamlipia. Hautakiwi kulipiza mabaya kwa mabaya, haujawahi kusoma hivyo kwenye Biblia?” aliuliza mama yake.
“Nishasoma mama.”
“Achana naye na urudi kwa Dassy,” alisema baba yake.

Moyo wake ulimchukia mno Tatiana lakini hakuwa na jinsi, maneno waliyoyaongea wazazi wake yakaanza kuubadilisha moyo wake na hatimaye kukubaliana nao kwamba mara atakapoachiwa huru basi atarudi nchini Liberia na kuungana na msichana wake wa kipindi cha nyuma, Dassy na hatimaye aweze kumuoa.
 
SEHEMU YA 140

Siku hiyo alirudishwa tena sero ambapo baada ya siku mbili akapelekwa mahakamani. Huko, ni rushwa na uswahiba wa ba ba yake ndiyo uliokuwa umekolea kiasi kwamba mwisho wa siku Nathan hakuonekana kuwa na hatia yoyote lile kwani ushahidi haukuwa umejitosheleza na hivyo kushinda kesi katika mazingira yaliyojaa utata mwingi.
Alichokifanya baada ya kushinda kesi hiyo ni kurudi nchini Liberia. Japokuwa magazeti mengi yaliandika juu ya utata huo lakini hakukuwa na watu waliopeleka kesi hiyo tena mahakamani hivyo Nathan kuwa huru kwa asilimia mia moja.

“Dassy!” alimuita msichana wake, Dassy akayainua macho na kumwangalia Nathan machoni.
“Naomba unisamehe kwa yote niliyotenda, ninaahidi kukupenda kwa moyo wangu wote,” alisema Nathan huku akibubujikwa na machozi.

Dassy hakupindua kwa Nathan, alimpenda kwa moyo wote. Kitendo alichokuwa amefanyiwa kilikuwa kibaya lakini hakutaka kukumbuka chochote kile, akaamua kumsamehe Nathan na baada ya mwezi mmoja wawili hao wakafunga ndoa kanisani na kuwa mke na mume.
“Nitakupenda milele,” alisema Nathan huku uso wake tu ukionyesha kumaanisha alichokuwa akikisema.
“Nitakupenda pia,” alisema Dassy na kisha kukumbatiana.
 
SEHEMU YA 141

Japokuwa moyo wake haukuridhika kama alivyotaka lakini hakuwa na jinsi, akaamua kuachana na Tatiana kwani kwa kile alichokifanya moyo wake ulimwambia kwamba lingekuwa fundisho kwa msichana huyo katika maisha yake yote.
Akawa bize na masomo na baada ya kumaliza mwaka mmoja uliobakia tu, akaanza kufanya mipango ya kusomea uchungaji kwani hakutaka tena kujichanganyachanganya kama alivyokuwa akifanya.

Chuki aliyokuwa nayo dhidi ya Tatiana, akaamua kuitoa na kutengeneza maisha yake na Mungu. Alidhamiria kwa moyo mmoja kumtumikia Mungu, baada ya kukubaliana na mchumba wake, Lydia, moja kwa moja Peter akaanza masomo katika Chuo cha Biblia kilichokuwa Dodoma.

Penzi lake kwa msichana Lydia lilizidi kuongezeka, katika maisha yake yote, msichana huyo alikuwa kila kitu. Mara kwa mara walipokuwa likizo, ilikuwa ni lazima kuwasiliana na Lydia na kisha kumfuata mkoani Morogoro ambapo walikuwa wote katika kipindi chote pasipo kufanya mapenzi, walitaka kufanya hivyo mpaka watakapoingia ndani ya ndoa.
Baada ya mwaka wa kwanza chuoni kumalizika, hapo ndipo alipopata mdhamini ambaye alitaka kumsomesha katika Chuo cha Biblia cha Holly Jehovah kilichokuwa ndani ya Jiji la Toronto nchini Canada.

Hiyo ilikuwa ni nafasi yake ya kipekee ambayo hakutaka kuiona ikipita. Kwa kuwa alikuwa ameandaliwa kila kitu, kilichokuwa kimebaki kilikuwa ni safari tu. Akawaambia wazazi wake, wote hawakuamini, walijua fika kwamba kijana wao alikuwa na ndoto za kufika mbali, alikuwa na kiu ya kuwa mchungaji mkubwa hapo baadae.

“Tunamshukuru Mungu kwa hilo, hakika baraka zake ni za milele,” alisema baba yake, mchungaji Lazaro.
Hakukuwa na cha kusubiri, baada ya wiki moja, wazazi wake na mchumba wake, Lydia wakamsindikiza mpaka uwanja wa ndege ambapo akaingia ndani ya ndege ya Shirika la Alliance Air na safari ya kuelekea nchini Canada kuanza.

Njiani, Peter alikuwa na furaha tele, hakukuwa na kitu alichokuwa akikipenda kama kwenda kuchukua digrii yake ya kwanza nchini humo. Alijiona kupewa heshima kubwa ambayo isingeweza kusahaulika maishani mwake.
 
SEHEMU YA 142

Alipofika nchini Canada, akapokelewa uwanjani hapo kwa gari la chuo na kisha kuanza kupelekwa kilipokuwa chuo cha Holly Jehovah. Njiani, macho yake yalikuwa yakiangalia huku na kule, kila kitu alichokuwa akikiona mbele yake kilimshangaza kwani hakuwahi kuwa kwenye nchi nzuri kama ilivyokuwa Canada.

Moyo wake ulifurahi sana, akajikuta akianza kumshuru Mungu mulemule ndani ya gari kwani kile kilichokuwa kikitokea kwake kilionekana kuwa kama muujiza ambao hakuutegemea kabisa maishani mwake.
Baada ya kuchukua dakika ishirini njiani, gari likaanza kuingia ndani ya eneo la chuo hicho. Kilikuwa miongoni mwa vyuo vikubwa vya dini, kilijengwa vizuri na kilikuwa na eneo kubwa la kupumzikia na hata kujisomea.

Alipoteremka kutoka garini tu, Peter akainyanyua mikono yake juu na kuanza kumshukuru Mungu. Hapo ndipo alipoanza safari ndefu ya kumtumikia Mungu maishani mwake, hakutaka kukumbuka kitu chochote kilichotokea, alichokuwa akikitaka ni kuwa karibu na Mungu tu. ****

Ilichukua mwezi mmoja na nusu na ndipo Tatiana akayafumbua macho yake kitandani pale. Mwili wake ulipungua mno, alionekana kuchoka kupita kawaida. Mtu wa kwanza kabisa kumuona msichana huyo wakati amefumbua macho alikuwa nesi ambaye kwa furaha kubwa akatoka chumbani mule na kwenda nje.

“Vipi?” aliuliza Buffet ambaye alikuwa amekaa kitini, kasi aliyotoka nayo nesi yule ilimbidi ashangae na kumuuliza.
‘Tatiana...”
“Amefanya nini?” aliuliza lakini nesi hakujibu swali hilo, akakimbia kuelekea katika ofisi ya Dk. Mundesh.

Buffet akashikwa na hofu, akahisi kwamba inawezekana Tatiana akawa amefariki dunia, akajikuta moyo wake ukianza kudunda kwa hofu kubwa, ila mbali na hofu hiyo, akaanza kujiuliza juu ya tabasamu alilokuwa amelitoa nesi huyo wakati akimpa taarifa, akahisi kwamba inawezekana Tatiana alikuwa amefumbua macho.

Hakutaka kubaki kitini pale, alichokifanya ni kukimbilia chumbani, akapiga hatua kuelekea katika kitanda alichokuwa Tatiana, kile alichohisi ndicho kilichotokea, Tatiana alikuwa macho, alikuwa akiangalia huku na kule japokuwa hakuonekana kuwa na nguvu.
“Tatiana mpenzi...” alijikuta akiita Buffet huku machozi yakianza kumbubujika mashavuni mwake.
 
SEHEMU YA 143

Hakuamini kile alichokuwa akikiona, baada ya mwezi miezi karibia miwili kuwa kimya kitandani, hatimaye mwisho wa siku Tatiana akayafumbua macho yake na kuona tena. Kwa Buffet, wakati mwingine alihisi kama yupo katika usingizi wa kifo ambapo baada ya muda angeshtuka kutoka kitandani, kilichokuwa kikitokea, hakikuwa ndoto, lilikuwa tukio halisi lililotokea katika maisha yake.
Tatiana hakuzungumza chochote kile, Buffet alibaki akimwangalia mpaka pale Dk. Mandesh alipofika chumbani mule akiwa na manesi wengine. Kila mmoja akaonekana kufurahia maendeleao ya Tatiana, hapohapo wakamuona Buffet atoke chumbani mule ili wafanye kazi yao.

“Usihofu, kazi imekamilika, amini kwamba atarudi kama alivyokuwa mwanzo,” alisema Dk. Mandesh huku akionekana kuwa na furaha tele.
*****
Mzee Sangiwa na mkewe wakafika nchini India, walifurahia kile walichokuwa wamekutana nacho kwamba binti yao mpendwa alikuwa amerudiwa na fahamu. Hizo ndizo stori zilizosambaa duniani kwamba mwanamuziki yule aliyekuwa amepoteza fahamu, alikuwa amerudiwa na fahamu.

Ilikuwa fuiraha kwa kila mtu aliyeipata habari hiyo, watu wengi wakiwemo masupastaa wakajitolea kumtembelea nchini India na kumjulia hali kwani maendeleo yake yalimshangaza kila mtu kwani wengi walidhani kwamba angekufa kitandani.
Siku zikakatika, wiki zikakatika na hatimaye Tatiana akarudi katika hali yake ya kawaida, akawa na nguvu na hivyo kuruhusiwa kurudi nchini Tanzania kuendelea na majukumu yake.

Kama kawaida Watanzania wakajikusanya uwanja wa ndege kwa ajili ya kumpokea na kumpongeza kwa namna alivyoweza kupambana kitandani mpaka kuwa kamaalivyokuwa kipindi hicho.
Alipoanza kuteremka ndani ya ndege, kelele za watu zikaanza kusikika uwanjani hapo, japokuwa Tatiana alionekana kukonda sana lakini wala hakukuwa na mtu aliyejali, kitendo cha kuonekana akiwa mzima wa afya kilimfurahisha kila mtu aliyekuwa akimwangalia.

Baada ya kupokelewa, akapelekwa hotelini na wazazi wake ambapo baada ya siku mbili safari ya kuelekea Shinyanga ikaanza. Katika kila kona aliyotokeza, watu walikuwa wakishangilia, hakukuwa na aliyeruhusiwa kupiga picha na msichana huyo tena kwani waliogopa kutokea kitu kama kile kilichotokea chuo kikuu.
 
SEHEMU YA 144

“Ninahitaji kuolewa,” alisema Tatiana, alikuwa amewaweka wazazi wake kwenye kikao cha usiku, alitaka kuzungumza nao kuhusu mipango yake ya ndoa na Buffet.
“Umeamua kutoka moyoni?”
“Ndiyo baba! Ninataka kuolewa sasa,” alisema Tatiana.
“Hakuna tatizo, sisi kama wazazi, tunaruhusu hilo kwa moyo mmoja,’ alisema mzee Sangiwa.

Huo ndiyo uamuzi aliokuwa ameamua, hakutaka kuishi na Buffet kama wapenzi tu badala yake alitaka kuolewa kabisa. Taarifa zilipoanza kutangazwa kuhusu ndoa hiyo, kila mmoja alifurahia huku wengine wakitamani kuona hasuri hiyo itakavyofanyika.
Ili kama maandalizi, baada ya kurudi nchini Marekani, Tatiana akaitwa katika majarida mbalimbali kwa ajili ya kupiga picha, alifanyiwa mambo mengi hata zaidi ya alivyofanyiwa Kim Kardashian wakati alipotaka kuolewa na Kanye West.
Jina lake lilikuwa kubwa mno, hivyo watu walipoona majarida mengi yakiwa na picha zake kwa mbele huku amevaa shela, kila mmoja akayapapatikia na kuyanunua kwa wingi. Hakukuwa na mwanamuziki aliyekuwa akipendwa sana duniani kama Tatiana.

“Ninakupenda Buffet! Ninakupenda mume wangu mtarajiwa,” alisema Tatiana huku akiwa na furaha mno, hakuamini kama alikuwa akienda kuolewa mwaka wa pili mara baada ya kupata jina kubwa duniani.
“Ninakupenda pia, ninakuahidi kukuoa kipenzi,” alisema Buffet huku akionekana kuwa na furaha.

Wakati tetesi juu ya harusi hizo zikiendelea kusikika kote duniani, ndicho kilikuwa kipindi ambacho albamu yake ya kwanza iitwayo Love Revenge ilipokuwa ikitoka hivyo kuanzisha ziara maalumu iliyopewa jina la Last Trip ambapo alipanga kutembea nchi mbalimbali kwa ajili ya kuitangaza.

Tatiana alifanya kila alichoweza, hakutaka kubaki alipokuwa, bado aliendelea kukusanya fedha, katika kila tamasha alilokuwa akilifanya, watu walikuwa wakijazana, tiketi zilikwishaisha katika sehemu zote ambazo alitarajiwa kwenda kufanya tamasha huko.

“Ni nchi tatu ndizo zilizobaki, Ujerumani, Romania na Finland,” alisema Tatiana, wakati huo walikuwa nchini Uingereza.
“Kote tutakuwa pamoja. Hivi nilishawahi kukwambia kwamba baba yangu ni Mjerumani?” aliuliza Buffet.
“Hapana!”
 
SEHEMU YA 145 “Baba yangu ni Mjerumani, mama yangu ni Mmarekani, kwa hiyo tunakwenda nyumbani,” alisema Buffet huku akionekana kuwa na futraha.
“Nitafurahi kuwaona mashemeji zangu,” alisema Tatiana pasipo kujua kwamba kile kitakachotokea nchini humo ndicho kilichobadilisha maisha yake yote, kitu kilichomfanya kulia kila siku na hata wakati mwingine kutamani kujiua.
*****

Miongoni mwa wanachuo walioonyesha msimamo wao mkubwa kwa Mungu alikuwa Peter, kila siku chuoni hapo alikuwa akiamka asubuhi sana, anasali mpaka muda wa kwenda kunywa chai kisha kuingia darasani.
Mbali na kusoma, maisha yake yalitawaliwa na maombi tu, kila wakati alipokuwa, alikuwa akichezesha lipsi zake kumaanisha kwamba alikuwa akiomba kitu kilichomfanya kuamini kwamba alisogea karibu na Mungu.

Hakufikiria kitu chochote kile, kila kitu kilichopita alikichukulia kuwa kama historia ambayo kamwe isingeweza kujirudia maishani mwake, aliamua kwa asilimia mia moja kuyakabidhi maisha yake mikononi mwa Mungu.

Mchungaji ambaye alitamani sana siku aje kuwa kama yeye ni Reginald Bonke ambaye alipokuwa akiombea wagonjwa, waliponywa na hata wale waliokuwa na ulemavu wowote ule mwilini mwao walipokea uponyaji.
“Nitafanya nini ili niwe kama Bonke?” aliuliza Peter.

“Unatakiwa kuomba sana,” alijibu profesa wa chuo hicho, mchungaji Kennan Willton.
“Hilo tu?”
“Hapana! Maombi yako yasiwe hivihivi, ni lazima ufunge pia, jitahidi kuwa karibu na Mungu na ninakuahidi kwamba utakwenda kuona miujiza yake mingi,” alisema mchungaji Willton.
“Sawa, nitafanya hivyo!”

Hakutaka kuishia kimaneno tu bali alichokifanya ni kuanza kufanya kile alichokuwa ameambiwa, alianza kuomba sana, kila wakati akawa mtu wa kuomba, hakutaka kupata muda mwingi wa kula, hata muda wa mapumziko haukuwa ukitosha, alichokuwa akikifanya ni kuomba tu.

Wakati mwingine akawa akifunga kwani maombi ya mfungo yalikuwa na nguvu mno, siku ambayo alifunga, alijifungia chumbani kwake siku nzima akiomba tu. Maisha yake yakaanza kubadilika kwa kiasi kikubwa mno, kila siku akawa mtu wa kumuabudu Mungu tu.
 
SEHEMU YA 146

Alikaa chuooni hapo mwaka mzima, hatimaye akarudi nchini Tanzania. Alikuwa na nguvu mno, alipokuwa akiingia kanisani, kwa kumwangalia tu, watu walikuwa wakiogopa, uwepo wa Mungu ulionekana mwilini mwake kiasi kwamba kila mtu aliyekuwa akizungumza naye alizungumza naye kwa kutokujiamini kabisa.

Kanisa hilo lilipoandaa mkutano, Peter akaanza kuwaombea watu waliokuwa wakifika uwanjani hapo. Miujiza mikubwa ikatokea kiasi kwamba watu hawakuamini kile walichokuwa wakikiona, mtoto yule wa mchungaji ambaye aliondoka nchini Tanzania kwenda kusoma nchini Canada, leo hii alikuwa na upako mkubwa mno mpaka wa kuponya wagonjwa, watu hawakuamini.

Jina lake likaanza kukua, kila alipoambiwa kwa kupewa sifa aliweka wazi kwamba si yeye aliyekuwa akifanya hivyo bali ni Mungu aliye juu. Hakuwa mbali na Lydia, alichokifanya ni kutangaza ndoa na baada ya mwezi mmoja, Peter akamuoa msichana huyo kanisani na hata aliporudi Canada kuendelea na masomo, alikuwa na pete yake kidoleni.

“Mchungaji.....”
“Hapana! Mimi si mchungaji, mimi ni Mwinjilisti.”
“Sawa Muinjilisti, Mungu amekupa nguvu kubwa sana ambazo kila mtu anatamani kuwa nazo, siri ya kuwa hivyo ni nini?”
“Kumuomba Mungu kila wakati, hiyo ndiyo siri yenyewe,” alisema Peter.
Chuo kizima akawa gumzo bado aliendelea kumuomba Mungu kila siku. Baada ya kumaliza mwaka huo, akarudi nyumbani na watu wengi akiwemo baba yake kumshauri kufungua kanisa lakini Peter hakutaka kukubaliana nao.

“Haiwezekani, hakuna Mwinjilisti mwenye kanisa, wenye kanisa ni wachungaji,” alisema Peter.
Hayo ndiyo yakawa maisha yake, kila siku alikuwa na kazi ya kuwaombea watu kitu kilichowafanya wengi kumshangaa kutokana na nguvu alizokuwa nazo.

Alijijengea heshima, watu wengi waliokuwa na wagonjwa wao wakampeleka kwa Peter ambaye alifanya miujiza mingi na watu kubaki midomo wazi kwa kutokuamini kile walichokuwa wakikiona.
“Au jamaa anapanga nao?”
“Hakuna bwana! Unamjua Chungua?”
“Ndiyo! Si yule mlemavu wa mtaa wa pili?”
“Ushamuona sasa hivi?”
 
SEHEMU YA 147

“Hapana! Mara ya mwisho kumuona ni wiki iliyopita.”
“Sasa nnikwambie kitu! Jamaa alimuombea Chungua, ule ulemavu umeondoka,” alisema jamaa huyo.
“Acha masihara!”
“Ndiyo hivyo!”
Kila kitu alichokuwa kikifanya alisema kwamba utukufu ulitakiwa kubaki kwa Mungu, hakujipa utukufu kwa kuaminikwamba si yeye aliyekuwa akifanya hivyo, kuponya watu na kutenda miujiza.

Kutokana na kile kilichokuwa kikiendelea, Peter akajikuta akiwa mtu maarufu nchini Tanzania, kanisa lao lilizidi kupata watu, watu wakamjua zaidi Peter kuliko hata mchungaji wa kanisa hilo.
*****

Watu zaidi ya Elfu sitini walikata tiketi kwa ajili ya kuangalia tamasha kubwa lililotarajiwa kufanyika ndani ya Jiji la Berlin katika Uwanja wa mpira wa Timu ya Hertha Berlin, Olympio, tamasha la mwanamuziki aliyekuwa akivuma kwa kasi kipindi hicho, Tatiana ambaye alikuwa akifanya ziara yake kuzunguka sehemu mbalimbali duniani.

Ziara hiyo kwenda nchini Ujerumani ikatangazwa sana, kila mtu akapania kumuona msichana huyo jukwaani, watu hawakulala vizuri, wengi walikuwa na hamu ya kumuona msichana huyo aliyekuwa na uzuri wa ajabu mno.
 
SEHEMU YA 148

Wakati watu wakimsubiri kwa hamu kubwa, hapo ndipo kulipoanza kuvuma uvumi kuhusiana na suala zima la ubaguzi wa rangi. Kukaokotwa makaratasi kadhaa yaliyoyokuwa yakimdhihaki Tatiana kutokana na ngozi yake, tena makaratasi yote hayo yalikuwa yakitupwa mitaani, watu walipoyaokota na kuyasoma, waliompenda, walichukia mno.

Hilo lilikuwa moja ya jambo lililoumiza vichwa vya wengi, wakataka kufahamu ni nani aliyetuma makaratasi hayo jijini Berlin lakini hakukuwa na mtu aliyefahamu lolote lile, yaani hata wao walipigwa na upofu mkubwa wa kutokujua chanzo cha karatasi zile mitaani.

Tatiana akashikwa na hofu, historia ya nyuma juu ya nchi hiyo kuwa ya kibaguzi mno ikajirudia kichwani mwake na kuanza kuogopa mno. Washauri wake walimwambia asiende nchini Ujerumani lakini Tatiana hakutaka kujali kelele za kibaguzi, alichokuwa akikitaka ni kwenda nchini humo tu.

Alikaa na mpenzi wake, Buffet na kujadiliana naye kwa muda mrefu juu ya wao kwenda nchini Ujerumani, walikubaliana kwa moyo mmoja kwamba walitakiwa kwenda kwani tayari watu walitoa kiasi kikubwa cha fedha ili kumuona, hivyo kuahirisha ziara kilikuwa kitu ambacho kingepunguza mvuto wake kwa mashabiki wake.

“We have nothing to do, we have to get there,” (Hatuna cha kufanya, twende huko) alisema Buffet.
Hawakuwa na jinsi, ili Tatiana asiweze kupoteza mashabiki wake walitakiwa kwenda huko, hawakutakiwa kuhofia kitu chochote kile, ilikuwa ni lazima wafanye kila liwezekanalo ili ile heshima aliyokuwa nayo iwe kama kawaida.

Makaratasi yaliendelea kusambazwa, kukaonekana kuwa na kamchezo fulani kalichokuwa kakichezwa na kikundi fulani cha watu, japokuwa serikali ya nchini Ujerumani ilijitahidi sana kufanya kila linalowezekana ili kuwagundua watu hao lakini hawakufanikiwa kabisa.

Maandalizi makubwa kuliko sehemu zingine yakaanza kufanyika, baada ya kukaa siku mbili, wakaanza safari ya kuelekea nchini Ujerumani tayari kwa kufanya shoo moja babu kubwa ambayo aliamini kwamba ingewaacha watu midomo wazi.
 
Pesa mwanaharam, jamaa yangu Peter japo umefanya kosa kubwa kutaka kumuua huyo Tatiana nashukuru hujakamatwa bora utulie na shemeji yetu mpya achana na Tatiana.
 
SEHEMU YA 149

“Ich liebe immer noch Partner , deine Liebe zu mir tut.“(Bado ninakupenda mpenzi, penzi lako kwangu halitokufa)
“Sind Sie sicher?“ (Una uhakika?)
“Warum liebst du sie?” (Ndiyo! Kwani huyo malaya umempendea nini?)
“Nur seine Popularität,“ (Umaarufu wake tu.)

“Verließ ihn , Popularität nicht etwas haben, gerade jetzt, dass ich ufuike schnell , nicht möglich ist, treffen Sie angekommen?“
(Achana naye, umaarufu hauna kitu sasa hivi, naomba ufuike haraka, si inawezekana kuonana ukifika?)
“Vollständig , dies sehr seltsam.“(Sijajua kabisa, huyu malaya kaniganda sana.)

“Struggling Partner! Aber ich werde es nicht mehr reagiert Tonhöhe sein, werden Sie im Hotel ein beliebter präsentieren.“ (Jitahidi mpenzi! Hata mimi nitakuwa uwanjani hapo kukupokea, nitakuwepo katika hoteli mtakayokuwepo kipenzi.)

Buffet alikuwa bize akichati simuni, muda wote aliokuwa akichati, uso wake ulijawa na tabasamu pana, alifurahia kile alichokuwa akiandikiwa, moyo wake ukajisikia amani kubwa.
Pembeni yake alikuwepo mpenzi wake, Tatiana aliyeonekana kuchoka mno, alipokuwa amelala, akachukua nafasi hiyo kuchati na msichana wake aliyekuwa nchini Ujerumani, msichana ambaye alimpenda kwa moyo wa dhati kuliko alivyompenda Tatiana.

Msichana huyu aliitywa Nikola, alikuwa Mjerumani halisi ambaye alikuwa mtoto pekee wa tajiri mkubwa nchini Ujerumani, bwana Kurt. Wawili hawa walionana zamani mno, walipendana kwa kuwa walisoma shule moja na mpaka Buffet alipokuwa akifika nchini Ujerumani, mtu wake wa kwanza kuonana naye alikuwa msichana Nikola.

Mapenzi yao hayakufa, waligombana mara kwa mara na kurudiana, waliishi pamoja na baadae kugombana tena, ndivyo walivyoishi na hata katika kipindi ambachjo msichana Nikola aliposikia kwamba Buffet kapata msichana aitwaye Tatiana, moyo wake ulimuuma mno.

Hakuwa na cha kufanya, kila alipokuwa akiona picha walizopiga Tatiana na Buffet, moyo wake ulimuuma mno ila hakuwa na cha kufanya, akabaki na maumivu makali ya moyo.
Siku ziliendelea kukatika, alipoanza kusikia kwamba mwanamuziki huyo alikuwa njiani kufanya shoo nchini Ujerumani, kitu cha kwanza kabisa akaanza kuwasiliana na Buffet kwa lengo la kurudiana tena kama uilivyokuwa kawaida yao.
 
SEHEMU YA 150

Buffet hakuwa na kipingamizi, japokuwa alikuwa na Tatiana aliyemfanya kuwa maarufu pia lakini kwa Nikola hakupindua, akajikuta moyo wake ukianza kumpenda tena msichana huyo na kumuona Tatiana kama takataka.

Alichokifanya Nikola ni kuandaa watu wake kwa ajili ya kumchafua Tatiana, tena huku akiwalipa kiasi kikubwa cha fedha, hakutaka Wajerumani wampende kwa kuwa alikuwa mtu mweusi, hivyo akachapisha karatasi nyingi kwa ajili ya kuzisambaza tu ili jina la Tatiana liharibike.

Akafanikiwa na hakugundulika kabisa. Baada ya siku kadhaa, Buffet akaanza kuelekea nchini Ujerumani huku akiwa na mpenzi wake, Tatiana pembeni. Ndani ya ndege, muda mwingi alikuwa akiwasiliana na Nikola na kupanga kile kilichotakiwa kufanyika lakini mwisho wa siku wawili hao waweze kuwa tena kama ilivyokuwa zamani.

Wakakubaliana, mioyo yao ikarudi mapenzini kwa mara nyingine tena, Buffet, hakutaka kuwa na Tatiana tena, moyo wake ukaanza kumrudia Nikola ambaye aliona wivu sana kumuona Buffet akiwa na msichana huyo, alitaka kufanya kila liwezekanalo, hata kuua aue lakini mwisho wa siku aweze kuwa na Buffet.
Tatiana hakulifahamu hilo.
****

“I wantto sleep my love...” (Ninataka kulala mpenzi wangu) alisema Tatiana kwa sauti ya chini iliyoonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa amechoka.
“Don’t you wan’t to eat?” (Hautaki kula?)

“I’m tired, I cant’t do anything else, let me sleep.” (Nimechoka, siwezi kufanya kitu kingine chochote, acha nilale)
Safari ndefu kutoka nchini Marekani mpaka Ujerumani ilimchosha mno Tatiana, hakuwa na hamu ya kula, kitu alichokuwa akikifikiria ni kulala tu. Kwa Buffet, alikuwa amechoka lakini kwake ilionekana hiyo kuwa nafasi kubwa na ya kipekee aliyokuwa akiililia sana.

Hakutaka kulala, tayari alikwishawasiliana na Nikola na kuambiwa kwamba alikuwa hotelini humohumo chumba namba 72 hivyo walitakiwa kuonana. Hakutaka kupoteza muda, kwa kuwa tayari alizungumza naye kwa kirefu, akatoka chumbani humo, kwa mwendo wa kunyata na kisha kuanza kuelekea nje huku akiwa na kisingizio kichwani mwake kwamba alifuata chakula.
 
SEHEMU YA 151

Kwa mwendo wa harakaharaka akaanza kutembea kuelekea kulipokuwa na chumba cha Nikola, alipofika, hakugonga hodi, kwa kuwa mlango uliachwa wazi, akaufungua na kuingia ndani.
Nikola alikuwa kitandani, hakuwa na nguo yoyote mwilini mwake, alipomuona mpenzi wake wa kitambo akiingia chumbani, akanyanyuka na kuanza kumsogelea, wote wawili wakakumbatiana kimahaba na kuangushana mpaka kitandani.

“Nimekukumbuka mpenzi,” alisema Nikola huku machozi yakianza kukusanyika machoni mwake.
“Nimekukumbuka pia, umekuwa mzuri sana mpenzi wangu,” alisema Buffet huku akionekana kuchanganyikiwa kwa furaha.
Hakutaka kumkumbuka Tatiana mahali hapo, mtu ambaye alimfikiria sana, aliyempagawisha kuliko wote alikuwa Nikola tu. Umbo lake lilikuwa zuri, sura yake ya kitoto ikampagawisha zaidi mpaka kuhisi kwamba chumbani humo alikuwa na msichana mpya ambaye hakuwahi kuonana naye kabla.

“Nikupe nini?” aliuliza Nikola.
“Mapenzi yako motomoto,” alijibu Buffet na kisha kuanza kubusiana.
Usiku huo wakakumbushia enzi, kipindi chote hicho Tatiana alikuwa amelala chumbani na hakushtuka kuona uchafu aliokuwa akiufanya mpenzi wake katika chumba kingine na msichana mwingine.
Buffet alitumia masaa mawili kuwa chumbani humo na kisha kutoka na kuelekea mgahawani kuchukua juisi na kisha kurudi chumbani ambapo bado alimkuta Tatiana akiwa usingizini.

Hakutaka kukaa kimya, akaanza kuchati na Nikola huku akimwambia namna alivyompagawisha kitandani na kumfanya kukumbuka mbali. Hakutaka tena kuwa na msichana kama Tatiana, kwa kuwa alikuwa amekwisharudiana na Nikola, akatafuta njia ya kuachana na msichana huyo.

Mpaka inafika asubuhi, Buffet alikuwa akichati na Nikola tu simuni, penzi lao likafufuka upya na kila mtu akawa na hamu ya kutaka kuchati na mwenzake zaidi. Hakukuwa na mtu aliyeweza kuwatenganisha tena,

Siku hiyo ilikuwa ni ya kuzunguka huku na kule, kulitembelea Jiji la Berlin ambalo lilikuwa na vivutio vingi. Kila alipopita, watu walitaka kupiga naye picha, kumuona mwanamuziki huyo ilikuwa ni bahati kubwa, hivyo kumuacha akipita lilikuwa suala gumu.

“Mbona una mawazo mpenzi?” aliuliza Tatiana, kila alipokuwa akimwangalia Buffet, alishindwa kuelewa kuna tatizo gani.
“Sina mawazo.”
 
SEHEMU YA 152

“Sasa tatizo nini?”
“Nahisi kuumwa.”
“Jamani! Basi changamka mpenzi, huoni picha zinavyopigwa mfululizo, changamka basi,” alisema Tatiana.
Mawazo ya Buffet hayakuwa hapo kabisa, alikuwa akimfikiria msichana Nikola tu. Kichwa chake kilivurugika kwa msichana huyo, hakutaka kusikia kitu chochote kile, alichokuwa akikifikiria ni kuwa na msichana huyo tu.

Hakujua ni kwa namna gani angeweza kuachana na Tatiana na mwisho wa siku kurudi kwa mwanamke ambaye aliutesa mno moyo wake. Alijaribu kufikiria mengi, yale aliyotakiwa kufanya lakini mwisho wa siku hakujua afanye nini.
“Ushamwambia?” aliuliza Nikola simuni.
“Kumwambia nini?”
“Kwamba haumtaki!”
“Naogopa sana Nikola.”
“Unaogopa nini?”

“Sijui naogopa nini, ila naogopa kufanya hivyo,” alisema Buffet.
“Kwa hiyo nikusaidie?”
“Utanisaidieaje?”
“Kesho, muda atakaotoka uwanjani, naomba usipande naye gari moja,” aliandika Nikola.
“Huwa hatupandi pamoja hasa anapokuwa kikazi.”
“Sawa. Kesho shoo yake ikiisha, usipande naye gari moja.”
“Kwa nini?”

Nikola hakutaka kujibu swalihilo, hakutuma tena meseji na hata Buffet alipojaribu kumpigia, msichana huyo hakuwa akipatikana kitu kilichomuacha kwenye wakati mgumu wa kufahamu juu ya meseji ile ya mwisho aliyokuwa amemwandikia.
*****

Watu walijazana ndani ya Uwanja wa Olympio, kila mtu aliyekuwa uwanjani hapo alikuwa na shauku ya kuangalia tamasha kubwa lililotangazwa sana katika vyombo vya habari duniani juu ya mwanamuziki aliyekuwa na nyota ya kupendwa sana, Tatiana ambaye alitarajiwa kufanya onyesho katika uwanja huo.

Watu wengi waliokuwa ndani ya uwanja huo walikuwa na fulana zilizokuwa na picha ya Tatiana ambaye alitarajiwa kushusha shoo kubwa ambayo haikuwahi kutokea tangu nchi ya Ujerumani kuanzishwa.

Uwanja ulijaza, watu walijaa kila sehemu na hakukuwa na nafasi kabisa, watu wote walijazana uwanjani hapo kwa ajili ya kumwangalia mwanamuziki aliyekuwa akishika nyoyo za kila mtu kipindi hicho, Tatiana.
 
Maskini Tatiana, kumbe Buffet anamkula papuchi tuu moyo upo kwa Nikola! Mapenzi acha yaitwe mapenzi...
 
SEHEMU YA 153

Ilipofika saa moja usiku baada ya maandalizi kukamilika, Tatiana akapanda jukwaani hapo na kuanza kutumbuiza. Uwanjani ilikuwa mshikemshike, hata wale walinzi waliokuwa uwanjani hapo, walionekana kutokufaa kutokana na wingi wa watu waliokuwa wakitaka kupanda jukwaani japo kumshika msichana huyo.

Wengine wakashindwa kuvumilia, wakaanza kulia huku wakishangilia, msichana mweusi aliyekuwa akibaguliwa nchini Ujerumani, matokeo yake akaanza kuwaliza Wazungu kitu ambacho hakikuwahi kufanywa na mwanamuziki mweusi yeyote yule.

Wakati Tatiana akiendelea kutumbuiza, Buffet alikuwa njeya uwanja huo, hakutaka hata kuwepo ndani kwani moyo wake ulikuwa ukimfikiria Nikola tu. Hapo nje hakuwa peke yake, kwa kuwa kulikuwa na mgahawa mkubwa, akaelekea hapo ambapo akaonana na Nikola na kuanza kuzungumza nayehuku kwa mbali akiisikia sauti ya mpenzi wake ikitumbuiza.
“Unaogopa nini?” aliuliza Nikola.
“Namheshimu tu.”

“Kwa hiyo huwezi kumuacha?”
“Sijajua, ila unataka ufanye nini?”
“Nimuue!”
“Umuue Tatiana?”
“Ndiyo!”
“Haiwezekani! Naomba usifanye hivyo!”
“Haina jinsi Buffet.”

Nikola hakutaka kukaa sana mahali hapo, alichokuwa amekisema ndicho alichotaka kuona kikitokea. Alimchukia Tatiana na ilikuwa ni lazima amuue, alitaka kusababisha ajali kama ile iliyomuua mwanamuziki wa Kimarekani, Aaliyah.
Buffet alibaki akiwa na mawazo tele, japokuwa alihisi kwamba moyo wake ulikuwana mapenzi ya dhati kwa msichana Nikolalakini kuna kipindi alifikiria kwamba alikuwa na chembechembe za mapenzi kwa msichana huyo mrembo, Tatiana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom