Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
- Thread starter
- #261
SEHEMU YA 138
“Nyie ni wakina nani?”
“Wazazi wake.”
“Hamruhusiwi kumuona.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Kisa?”
“Nyie jueni kwamba hamruhusiwi kumuona,” alisema polisi aliyekuwa kaunta maneno ambayo yaliungwa mkono na kila polisi.
Baba yake Nathan hakutaka kuhangaika, alichokifanya ni kunyanyua simu yake na kuanza kupekua majina kadhaa yaliyokuwa humo, alipolipata jina alilokuwa akilitaka, akabonyeza kitufe cha kupiga simu na baada ya sekunde kumi, mtu wa upande wa pili akapokea simu, alikuwa swahiba wake mkubwa, waziri mkuu wa nchi hiyo na kuanza kuzungumza naye.
Alimwambia mengi tu lakini kubwa zaidi ni yeye kuzuiliwa kumuona mtoto wake. Hilo wala halikuwa tatizo kubwa, akaambiwa ampe simu mkuu wa kituo hicho ambaye baada ya kukabidhiwa akaanza kufokewa kama mtoto kwa kile kilichokuwa kimetokea kituoni kwake.
“Samahani mzee,” alisema mkuu wa kituo baada ya simu kukatwa.
“Hakuna cha samahani, nionyesheni kijana wangu haraka,” alisema baba yake Nathan na hapohapo wakachukuliwa na kupelekwa ndani ya chumba kimoja kwa heshima kubwa na kuambiwa kusubiri hapo.
Wala haukuchukua muda mrefu, Nathan akaletwa chumbani hapo. Hakuwa amejeruhiwa, hakupigwa hata kidogo. Akawekwa kwenye kiti huku akiwa amefungwa pingu. Hapohapo baba yake akaagiza afunguliwe zile pingu kitendo kilichofanyika haraka sana.
“Nathan, nini kimetokea?” aliuliza baba yake.
“Baba! Unamkumbuka yule mwanamke aliyenifanya nimuache Dassy?”
“Ndiyo!”
“Ndiye huyu niliyetaka kumuua!”
“Unasemaje?”
“Ndiye huyuhuyu niliyetaka kumuua. Ameniumiza sana, hatakiwi kuishi hata mara moja,” alisema Nathan huku machozi yakianza kumbubujika mashavuni mwake.
“Nathan....”
“Baba! Ameniumiza sana, nimemuacha mwanamke aliyekuwa akinipenda kwa moyo wa dhati, halafu leo anafanya hivi! Anafanya hivi ili iweje? Baba, nina hasira naye mno,” alisema Nathan huku akionekana kumaanisha kile alichokuwa akikisema.
Mama yake akashindwa kuvumilia, naye akajikuta akibubujikwa na machozi kwani kitendo cha kuyaona machozi ya mtoto wake kilimuumiza mno moyoni mwake. Alimpenda sana, hakutaka kumuona akilia, hakukuwa na mtu aliyekuwa akimpenda kama Nathan.
“Nyie ni wakina nani?”
“Wazazi wake.”
“Hamruhusiwi kumuona.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Kisa?”
“Nyie jueni kwamba hamruhusiwi kumuona,” alisema polisi aliyekuwa kaunta maneno ambayo yaliungwa mkono na kila polisi.
Baba yake Nathan hakutaka kuhangaika, alichokifanya ni kunyanyua simu yake na kuanza kupekua majina kadhaa yaliyokuwa humo, alipolipata jina alilokuwa akilitaka, akabonyeza kitufe cha kupiga simu na baada ya sekunde kumi, mtu wa upande wa pili akapokea simu, alikuwa swahiba wake mkubwa, waziri mkuu wa nchi hiyo na kuanza kuzungumza naye.
Alimwambia mengi tu lakini kubwa zaidi ni yeye kuzuiliwa kumuona mtoto wake. Hilo wala halikuwa tatizo kubwa, akaambiwa ampe simu mkuu wa kituo hicho ambaye baada ya kukabidhiwa akaanza kufokewa kama mtoto kwa kile kilichokuwa kimetokea kituoni kwake.
“Samahani mzee,” alisema mkuu wa kituo baada ya simu kukatwa.
“Hakuna cha samahani, nionyesheni kijana wangu haraka,” alisema baba yake Nathan na hapohapo wakachukuliwa na kupelekwa ndani ya chumba kimoja kwa heshima kubwa na kuambiwa kusubiri hapo.
Wala haukuchukua muda mrefu, Nathan akaletwa chumbani hapo. Hakuwa amejeruhiwa, hakupigwa hata kidogo. Akawekwa kwenye kiti huku akiwa amefungwa pingu. Hapohapo baba yake akaagiza afunguliwe zile pingu kitendo kilichofanyika haraka sana.
“Nathan, nini kimetokea?” aliuliza baba yake.
“Baba! Unamkumbuka yule mwanamke aliyenifanya nimuache Dassy?”
“Ndiyo!”
“Ndiye huyu niliyetaka kumuua!”
“Unasemaje?”
“Ndiye huyuhuyu niliyetaka kumuua. Ameniumiza sana, hatakiwi kuishi hata mara moja,” alisema Nathan huku machozi yakianza kumbubujika mashavuni mwake.
“Nathan....”
“Baba! Ameniumiza sana, nimemuacha mwanamke aliyekuwa akinipenda kwa moyo wa dhati, halafu leo anafanya hivi! Anafanya hivi ili iweje? Baba, nina hasira naye mno,” alisema Nathan huku akionekana kumaanisha kile alichokuwa akikisema.
Mama yake akashindwa kuvumilia, naye akajikuta akibubujikwa na machozi kwani kitendo cha kuyaona machozi ya mtoto wake kilimuumiza mno moyoni mwake. Alimpenda sana, hakutaka kumuona akilia, hakukuwa na mtu aliyekuwa akimpenda kama Nathan.