Penzi bila maumivu

Penzi bila maumivu

SEHEMU YA 96...

Peter hakutaka kuondoka, naye alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa uwanjani hapo ambao walitaka kumuona msichana huyo akiwa jukwaani. Japokuwa moyo wake ulimuuma mno lakini hakuthubutu kabisa kuondoka uwanjani hapo.
Dakika ziliendelea kukatika, watu walizidi kuongezeka zaidi mpaka kufikia watu zaidi ya elfu ishirini uwanjani hapo na hakukuwa na dalili za watu kukata. Ilipofika saa saba kamili mchana, ving’ora vikaanza kusikika, hakukuwa na maswali kwamba yule aliyekuwa akitarajiwa kuingia mahali hapo alikuwa nani.
Watu wakaanza kukimbilia kule kulipokuwa pa kuingilia, kila mtu alitaka kumuona Tatiana tu. Pikipiki mbili zilitangulia mbele na magari mengine kufuata, alionekana kuwa na msafara uliomkaribia rais wa nchi.

Watu wakaanza kupiga kelele huku wakiliimba jina lake ambalo lilionekana kuwa kero kwa Peter aliyekuwa akifuatilia kila kilichokuwa kikiendelea uwanjani hapo. Baada ya magari kusimama, Tatiana akashuka huku akiwa na Buffet kitu kilichoibua shangwe nyingi uwanjani hapo.
“Huyu demu mkali sana, sijui kwa nini sikuonana naye kabla ya kuwa supastaa!” alisikika akisema jamaa mmoja.
“Daah! Halafu Mzungu mwenyewe boya tu ndiye anamchukua dada yetu,” alisema jamaa mwingine.

Tatiana akaanza kupiga hatua kwenda jukwaani, alikuwa akipunga mikono yake hewani, watu walizidi kushangilia, moyoni mwa Peter, alitamani achimbe kaburi na kujizika kwani kila alipokuwa akimwangalia msichana huyo jukwaani, alizidi kuumia. “Ninakuchukia Tatiana,” alisema huku akiuma meno yake kwa hasira.
****

Nathan alimaanisha alipotamka kwamba mara ya kwanza kwamba alitaka kumuua msichana Tatiana, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, japokuwa kipindi kirefu kilipita lakini bado alikuwa na hasira mno na msichana huyo.

Hakutaka kuona akiendelea kuishi, kwa kile alichokuwa amemfanyia, alijiapiza kwamba ilikuwa ni lazima amuue hata kama angetumia kiasi gani cha fedha. Alichokifanya ni kuanza kumfuatilia kwani alikwishajua kwamba Petrov alishindwa hivyo alitaka kuingia kazini yeye mwenyewe.
 
SEHEMU YA 97...
Siku zikaendelea kukatika, hakuacha kumfuatilia msichana huyo, kila siku alihakikisha anaingia katika mitandao na kuona msichana huyo alikuwa akifanya nini kwa kipindi hicho kwani kila siku aliuhisi moyo wake ukiwaka moto kwa hasira.
Alimuacha Dassy kwa ajili ya msichana huyo, aliumia sana kwani alipanga mambo mengi na msichana Dassy lakini mwisho wa siku, kila kitu kikabadilika, ndoto alizokuwa nazo kwa msichana huyo zikapotea kwa sababu ya Tatiana, hakutaka kuona akishindwa kumuua msichana huyo.

“I will kill her myself,” (nitamuua mimi mwenyewe) alisema mara baada ya kuona kwamba kwa mara ya kwanza msichana huyo alitarajiwa kwenda nchini Tanzania.
Hakutaka kukubali, hiyo kwake ikawa nafasi pekee ya kutaka kufanya kile alichotaka kukifanya, hivyo akajiandaa kwa ajili ya kwenda nchini Tanzania ili kukamilisha kile alichokuwa amekipanga.
Ndani ya ndege alikuwa na presha kubwa, alijiona akichelewa kufika nchini Tanzania, alitamani kasi iongezeke na hatimaye ajikute nchini Tanzania akiwa amewahi kabisa kwa ajili ya kumuua msichana huyo.
Ndege ilichukua masaa kumi na moja na ndipo ikaanza kuingia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere. Iliposimama, hakutaka kusubiri, akaanza kuteremka na abiria wengine na kufauta taratibu zote alizotakiwa kufuata kama abiria.

Alipotoka nje ya jengo la uwanja huo, akachukua teksi ambayo ilimpeleka mpaka katika Hoteli ya Serena ambapo akateremka na kuchukua chumba. Chumbani, akili yake haikutulia, muda wote alikuwa akifikiria kufanya mauaji tu.

Zilibakia siku mbili hata kabla Tatiana hajaingia nchini Tanzania hivyo alichokifanya ni kuanza kutafuta bastola ndogo kwa ajili ya kufanya kazi aliyotaka kuifanya. Kazi haikuwa nyepesi hata mara moja kwani hakuwa akifahamu sehemu zozote nchini Tanzania ambapo kungemfanya kupata bastola kwa urahisi sana, hivyo baada ya kutafuta kwa kipindi kirefu, akaona njia nyepesi ya kumuua msichana huyo ilikuwa ni humohumo hotelini alipokuwa amefikia.
 
SEHEMU YA 98...

Alichokifanya ni kusikilizia juu ya hoteli ambayo angefikia msihana huyo ambapo aliamini kwamba angefanikiwa kufanya mauaji hayo, hivyo moyo wake ukabaki na kimuemue.
“Anatajia kuingia lini?” ilisikika sauti simuni, alikuwa akizungumza na Petrov.
“Kesho!”
“Nataka nije Tanzania.”
“Unasemaje?”
“Nataka kuja kumalizia pale nilipoachia,” alisikika Petrov.

Japokuwa Nathan alikuwa amefika nchini Tanzania kwa ajili ya kukamilisha kazi aliyokuwa ameipanga kwa kuwa Petrov alishindwa, mwanaume huyo naye hakutaka kubaki Liberia, kiasi cha fedha alichokuwa amelipwa pasipo kazi kufanyika ikamuuma sana hivyo akataka kusafiri kwenda nchini Tanzania.
Usafiri wake ulikuwa ni wa meli kubwa ya mizigo, kuna kipindi aliteremka na kupanda boti iendayo kasi huku lengo likiwa ni kufika nchini Tanzania pasipo kukamatwa.

Kwa Nathan, mambo yalikwenda kama alivyotaka, mpaka siku ambayo Tatiana alikuwa akishuka kutoka kwenye ndege na kuanza kuelekea hotelini alikuwa akifuatilia kila hatua, alionekana kuwa na hasira mno, kila alipomwangalia msichana huyo, alitamani kumuua.
Msafara huo mkubwa ukaishia katika Hoteli ya Blue Pearl, hapo ndipo Nathan alipotaka kufanya mauaji yake, hivyo alipoona kwamba msichana huyo amechukua chumba hotelini hapo, na yeye akaenda kuchukua chumba.
“Utakaa muda gani?” aliuliza msichana wa mapokezini.
“Wiki moja.”

“Naomba passport yako,” alimwambia Nathan, akampatia.
“Sawa. Karibu sana, jisikie huru,” alisema msichana wa mapokezi, akamuita kijana ambaye akabeba mizigo yake na kuanza kuelekea kwenye lifti kwa ajili ya kupanda juu mpaka kilipokuwa chumba chake.
Walipofika katika ghorofa iliyokuwa na chumba chake, akateremka na kijana yule kisha kuanza kukifuata. Akachukua kadi maalumu ya kufungua milango na kuipitisha kwenye kimashine kidogo na mlango kufunguka.

“Nashukuru sana,” alimwambia kijana aliyembebea mizigo, akaingiza mkono mfukoni na kutoa dola kumi na kumpatia.
“Nashukuru pia.”
“Ila samahani.”
“Bila samahani.”
“Hivi naye Tatiana yupo hoteli hii?”
“Yeah! Yupo, amefika leo mchana.”
“Daah! Nitatamani kumuona, nimesafiri kutoka Marekani mpaka hapa kwa ajili yake, ninatamani sana nimuone,” alisema Nathan.
 
SEHEMU YA 99...

“Nafikiri utamuona tu.”
“Utaweza kunisaidia?”
“Kumuona Tatiana?”
“Hapana! Yaani kama nitakuwa na uhitaji wa baadhi ya vitu.”
“Hakuna tatizo. Namba yangu hii,” alisema mhudumu yule huku akimpa kikaratasi kilichokuwa na namba yake.
Alihitaji msaada, alijua kwamba asingeweza kufanya kila kitu peke yake hivyo kulikuwa na baadhi ya vitu ambavyo angehitaji kununuliwa na kijana huyo kwani hakujua mahali kulipokuwa na maduka.

Usiku wa siku hiyo, hakulala, alikuwa akifikiria ni kwa namna gani angefanikiwa kufanya kile alichotaka kukifanya, kile kilichomfanya kusafiri kutoka nchini Liberia mpaka nchini Tanzania. Alijipa moyo kwamba angefanikiwa kufanya kile alichopanga kukifanya hivyo alitaka kusubiri muda ufike ili akamilishe.
Alikosa bunduki, hivyo aliona kitu kizuri kufanya mauaji ni kumuua Tatiana kwa sumu tu kitu kilichoonekana kuwa chepesi sana kufanyika, tena kingefanyika pasipo kugundulika. ***** “Ninawapenda Watanzania wenzangu,” alisema Tatiana, watu wote waliokuwa uwanjani wakapiga kelele za shangwe.

Siku hiyo alikuwa akizungumza mbele ya maelfu ya Watanzania kwa mara ya kwanza. Msichana huyo alionekana kuwa mrembo mno, watu hawakuamini kila walipokumbuka kwamba alikuwa msichana masikini aliyetoka mkoani Shinyanga, tena vijijini huku akiwa kipofu.
Hapo ndipo walipoamini kwamba fedha zilikuwa na uwezo wa kumbadilisha mtu yeyote yule, kila alipokuwa, Tatiana alionekana kuwa mtu mwenye fedha nyingi, aliishi ndani ya maisha ya kifahari, alitembelea fedha, kila alipopumua, wakati mwingine alihisia akipumulia fedha tu.

Peter ambaye alikuwa miongoni mwa maelfu ya watu waliokuwa uwanjani hapo aliendelea kufuatilia kila kitu, moyo wake uliumia mno, hakuamini kama msichana yule aliyesimama jukwaani aliwahi kuwa mpenzi wake aliyempenda kwa penzi la dhati.

Akabaki akimwangalia huku akionekana kuumia mno moyoni mwake. Kuna wakati alijikuta akibubujikwa na machozi, aliyafuta na kuendelea kumtazama msichana yule.
“Nawashukuru sana....basi acha iwe muda wa picha,” alisema Tatiana na kuelekea kulipokuwa na viti na kutulia.
 
SEHEMU YA 100...

Watu hawakutaka kutulia, waliposikia kwamba Tatiana alitaka kupiga picha na watu waliokusanyika mahali hapo, kila mtu akajiandaa vilivyo, kila mmoja alitaka kuwa mbele ili aweze kupiga picha na msichana huyo.
Japokuwa mkuu wa chuo alikuwa akizungumza, hakukuwa na mwanachuo aliyemsikiliza, walichokuwa wakikitaka mahali hapo ni kupiga picha na msichana huyo tu. Tatiana alichukulia kila kitu kuwa kawaida, hakufikiria kuhusu fujo ambazo zingetokea mahali hapo, alichikfanya mara baada ya mkuu wa chuo kumaliza ni kuteremka jukwaani, walinzi walitaka kumzuia, akawakataza kwa kuamini kwamba Watanzania walikuwa watu wa amani.

Alipofika chini, watu wakaanza kumsogelea na kila mmoja kung’ang’ania kupiga naye picha. Zilionekana kama fujo fulani lakini kwa Tatiana alikuwa akijsikia furaha tu, waliokuwa na kamera au simu zenye kamera ni miale ya kamera tu ndiyo iliyokuwa ikimulika.
Watu wengi wakamvamia huku wakimshika huku na kule, wengine wakijipiga naye picha, wala hazikupita dakika nyingi, Tatiana akaanza kuhisi kitu, ghafla, hata kabla hajajua ni kitu gani kilikuwa kimetokea, akaanza kuona giza mbele yake hali iliyomfanya kila mtu kumshangaa, hata Buffet ambaye alikuwa kule jukwaani, akaonekana kugundua kitu kwani msichana huyo aliyekuwa katikati ya watu waliokuwa wamemzunguka alionekana kuwa tofauti.
“Damu...damu...damu....” zilisikika kelele, kila mtu aliyesikia hivyo akasogea pembeni.

Buffet akashtuka, maprofesa wakashtuka mara baada ya kusikia wanachuo wakipiga kelele kusema kwamba waliona damu, kwa harakaharaka wakaanza kushuka jukwaani kumfuata Tatiana kwani tayari alianza kulegea na hapohapo akaanguka chini, damu zilikuwa zikimtoka, nguo nzima ililowanishwa na damu.

“Sogea pembeni, sogea pembeni,” alisema Buffet mara baada ya kufika pale chini.
Tatiana alikuwa hoi chini, damu zilikuwa zikimtoka, kitu cha kwanza kabisa alichokifanya Buffet ni kuchukua shati lake kwa ajili ya kuzuia damu iliyokuwa ikimtoka Tatiana.
 
SEHEMU YA 66...
Mtu wa kwanza kabisakumuona mbele yake alikuwa Dk. Buffet. Alivalia koti refu jeupe huku shingoni mwake akiwa ameipitisha mashine ya kusikilizia mapigo ya moyo. Kwa kumwangalia tu, alikuwa mwanaume mzuri wa sura ambaye kila alipokuwa akitabasamu, uzuri wake uliongezeka zaidi.

Tatiana alipomuona Dk. Buffet, akausikia moyo wake ukimripuka kwa furaha, hakuamini kama duniani kulikuwa na watu wenye sura nzuri kama alivyokuwa daktari huyo. Hapohapo, akauhisi moyo wake ukimuingiza daktari huyo na kumpenda kwa mapenzi ya dhati.
Hakujua Smith alionekanaje, hakujua sura yake ilikuwa vipi lakini kitu alichokuwa akikiamini ni kwamba mwanaume huyo hakuwa na sura nzuri kama aliyokuwa nayo Smith. Dk. Buffet alipokuwa akitabasamu, Tatiana alijiona kama anamwangalia malaika.

Kuna wakati alitamani kumvutia kwake, ambusu kwani hakukuwa na kitu alichokuwa na hamu kukifanya kwa daktari huyo kama hicho. Kila wakati alipokuwa akimwangalia, mapigo yake ya moyo yalikuwa yakimdunda tu huku akihisi damu yake ikizunguka kwa kasi kubwa mishipani mwake.
“Vipi?” aliuliza Dk. Buffet kwani hata macho aliyokuwa akimwangalia yalionekana tofauti.

“Poa, nafurahi kuona,” alisema Tatina kwa sauti iliyojaza mahaba tele, sauti ndogo ambayo hakutaka manesi waliokuwa chumbani humo kuisikia.
Huo ndiyo ulikuwa wakati wake wa kuangukia katika penzi la mtu mwingine kabisa ambaye hakuwa amemtegemea kabisa maishani mwake. Hata Smith alipokuja hospitalini hapo na kumwangalia, hakuvutiwa naye kama alivyokuwa Dk. Buffet ambaye kila alipokuwa akitabasamu tu, moyo wake ulikuwa hoi.

Siku hiyo ambayo alitakiwa kubaki hospitalini hapo alitaka kuitumia vilivyo, hakutaka kuona akiendelea kuteseka mapenzini na wakati mtu ambaye alimuweka katika hali hiyo alikuwa na uwezekano mkubwa wa kumpata.
Alichokifanya usiku alipokuwa kitandani akichati na Smith ni kumuomba nesi amuitie Dk. Buffet ambaye pasipo kuhisi chochote kile alifika haraka chumbani hapo.

“Naomba manesi watoke, kuna kitu nataka kukwambia,” alisema Tatiana kwa sauti ndogo, hilo halikuwa tatizo, Dk. Buffet akafanya hivyo na kubaki wawili chumbani.
Tatiiiiiiiii......hiyo tabia umeitoa wapi, bora ungeomba kukutanishwa na Peter na Nathan ili umchague mmojawapo....lol mtoto wewe mbona unataka kuleta majanga, umeisahau bastola ya Smith uliyoiota eeh
 
Nipo page namba moja japo hii nilishawahi kuisoma lakini sio vibaya kujikumbusha
 
SEHEMU YA 101...
Ubavuni mwake, upande wa kushoto alikuwa amechomwa kisu huku mkono wake maeneo ya kiwiko kwa mbele alichanwa na kisu hicho hali iliyoufanya mshipa wake wa damu ambao ulidhibiti mkono na vidole kuchanwa vibaya na hiuvyo kusababisha damu nyingi kuanza kumtoka.

Hakukuwa na mtu aliyefahamu ni nani alikuwa amemchoma kisu msiahcna huyo. Hapohapo polisi wakaanza kuzunguka huku na kule kuona kama wangeweza kumpata mtu aliyekuwa na kisu mkononi lakini hawakuweza kumpata mtu yeyote yule.

Tatiana aliugulia maumivu pale chini, kadiri muda ulivyozidi kwenda ndivyo damu zile zilipozidi kumtoka. Buffet akachanganyikiwa, alijitahidi sana kuzizuia damu za Tatiana kutoka lakini hazikuweza kukata, bado ziliendelea kumtoka mfululizo hali iliyomaanisha kwamba kama wasingefanya haraka iwezekanavyo basi msichana huyo angeweza kufariki dunia.

Kwa haraka sana gari likasogezwa, akapakizwa na kisha kuanza kupelekwa katika Hospitali ya Marie Stoppes ambayo haikuwa mbali na chuo hicho. Ndani ya gari, bado damu ziliendelea kumtoka Tatiana, kila mmoja akaona kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wa msichana huyo kuvuta pumzi ya dunia hii.
 
SEHEMU YA 102...
Hasira ilimkaba Peter kwa kiwango cha mwisho kabisa kiasi kwamba akashindwa kuvumilia, kila aliposimama mahali pale alihisi akishindwa kabisa kuzizuia hasira zake, hakutaka kuendelea kubaki hapo kwani kila alipokuwa akimwangalia Tatiana aliyekuwa amekaa kule jukwaani, alishikwa na hasira zaidi.

Akaondoka uwanjani hapo, kitu alichokuwa amedhamiria siku hiyo kilikuwa ni kumuua msichana huyo tu, alipoondoka, safari yake iliishia nje ya eneo la chuo, karibu na geti la kuingilia Mlimani City upande wa Chuo cha Ardhi ambapo kulikuwa na vibanda vingi, akakifuata kibanda kimoja na kununua kisu ambacho akataka kinolewe kabisa.
“Ni lazima nimuue, aliniumiza sana, siwezi kumuacha,” alijisemea Peter na kuondoka mahali hapo kurudi chuoni.

Alipofika, akakificha vizuri kisu chake kiunoni kwa kulishusha zaidi shati lake na kisha kukaa katikati ya wanachuo waliokuwa pale uwanjani. Mpaka Tatiana anasimama na kuanza kuzungumza, tayari hasira alizokuwa nazo zilimkaba kooni kabisa na akashindwa kuvumilia.
Tatiana alianza kwa kuongea mambo mengi, wanachuo walikuwa wakipiga makofi, kuna wengine aliwasikia wakiusifia uzuri wa msichana yule, kuna wengine walikuwa wakizungumza mengi kuhusu Tatiana lakini Peter hakutaka kujali, lengo alilokuwa ameliweka kichwani mwake ni kumuua msichana huyo tu.
Muda wa kupiga picha ulipofika, naye akajichanganya katikati ya watu, akamfuata Tatiana kwa nyuma. Kutokana na idadi kubwa ya watu kumzongazonga Tatiana, hakukuwa na mtu aliyemuona pale alipotoa kisu kisiri, akamsogelea Tatiana, watu walipoendelea kusukumana, akamchoma msichana huyo kisu cha ubavuni kisha kumkata mkononi, sehemu alipoamini kulikuwa na mshipa mkubwa wa damu ukipita.

Alipofanya hivyo, hakutaka kukaa, kwa haraka sana akakiweka kisu kiunoni na kuondoka mahali hapo kabla hajashtukiwa na mtu yeyote yule. Kilichotokea nyuma, hakutaka kukifuatilia kwani alijua iwe isiwe ilikuwa ni lazima Tatiana afe.
“Mchungaji,” aliita msichana mmoja, alikuwa amemuona Peter akielekea darasani.
“Naam!”
“Una damu tumboni,” alisema msichana yule,
 
SEHEMU YA 103...
Peter akaangalia, akaona kweli alikuwa na damu zilizotoka kwenye kisu kile alichokificha, hazikuwa nyingi ila kutokana na shati jeupe alilolivaa, zilionekana vizuri.
“Mungu wangu! Kumbe nimechunika!”
“Vipi tena.”
“Nilijaribu kuruka zile seng’enge!”
“Hahha! Wewe si wa kwanza, wengi washawahi kujichana nazo, nenda kanawe,” alisema msichana yule.

Peter akashusha pumzi, alichokifanya ni kwenda bafuni na kisha kunawa, akalivua shati lake na kuondoka kuelekea katika chumba alichokuwa akiishi mmoja wa rafiki yake na kuchukua shati kisha kuondoka katika mazingira ya chuo.
Moyo wake ukawa na furaha mno, hakuamini kama angeweza kufanikisha kile alichokuwa amekipanga, kila alipokuwa, alikenua, aliona kufanya jambo moja kubwa tena kwa ujasiri mkubwa mno. Kila alipokuwa, tabasamu pana lilikuwa usoni mwake.

Kile alichokuwa amekifanya, kwake kikaonekana kuwa sahihi, hakutaka kumuomba Mungu msamaha kwa dhambi aliyokuwa ameifanya, wakati mwingine, alijipa haki ya kufanya jambo lile kwa kisingizio cha Tatiana alistahili kufanyiwa unyama kama ule.
***** “Jamani kuna nini tena?” aliuliza nesi.

“Mchukueni kwanza.”
“Kwanza tuambieni nini kimetokea,” alisema nesi yule, hakuwa akijua kama wale waliomleta Tatiana alikuwepo na mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Slaam.
“Nesi! Mazungumzo baadae, okoa maisha kwanza.”
“Amefanya nini? PF3 iko wapi?” aliuliza nesi yule.

Hali ya Tatiana iliendelea kuwa mbaya, wasingeweza kubaki pale nje huku wakizungumza na nesi yule, walichokifanya ni kuingia ndani huku kila mmoja akionekana kuchanganyikiwa.
Kila mtu aliyemuona Tatiana, alibaki akisikitika, damu ziliendelea kumtoka mfululizo hali iliyoonyesha kwamba muda wowote ule angeweza kufariki dunia jambo ambalo hakukuwa na mtu aliyetaka kuliona,

Walipofika mapokezini, wakamtambulisha Tatiana, kila mtu aliyesikia akashtuka, kwa haraka wakamchukua na kumpeleka katika chumba cha upasuaji ambapo huko kazi ikaanza rasmi.

Buffet na mkuu wa chuo pamoja na baadhi ya wanachuo waliotangulizana nao walibaki nje, kila mmoja alionekana kuwa na mawazo, tukio lililokuwa limetokea lilimstaajabisha kila mtu kwani hakukuwa na tukio kama hilo ambalo liliwahi kutokea tangu chuo hicho kianzishwe.
 
104...
Buffet ndiye aliyeonakana kuchanganyikiwa zaidi, kila alipokaa, alikuwa akiongea peke yake tu. Hakukuwa na mtu aliyemuongelesha mwenzake kwa kipindi hicho, kila mmoja akabaki na lake moyoni mwake.
Madaktari walijifunugia ndani ya chumba kile cha upasuaji wakimshughulikia Tatiana, baada ya dakika ishirini, tayari waandishi wa habari wakafika hospitalini hapo kwa ajili ya kutaka kuchukua matukio yaliyokuwa yakiendelea.
“Imekuwajekuwaje tena?” aliuliza Consolatha, mwandishi mahiri kutoka katika Gazeti la Undani.

“Naomba mtuache kwanza, hali haipoa sawa.”
“Amekufa?”
“Consolatha, maneno gani hayo unayozungumza!” alisema mwanachuo mmoja, kutokana na umaarufu wa mwandishi huyo kwenye habari za udaku, alikuwa akijulikana sana.
Kila daktari aliyekuwa akitoka ndani ya chumba kile, alifuatwa na wanachuo hao akiwemo Buffet wakitaka kujua kile kilichokuwa kikiendelea ndani juu ya hali ya Tatiana. Hakukuwa na mtu yeyote aliyezungumza lolote lile ila nyuso zao zilionyesha dhahiri kwamba hali ndani haikuwa nzuri hata mara moja.

Hapo ndipo walipoanza kujiuliza juu ya mtu aliyefanya tukio lile, hawakumjua zaidi ya kushtukia msichana huyo akitokwa na damu tu, Umati mkubwa wa wanafunzi waliokuwa wamemzunguka ndiyo uliowafanya kutokugundua ni nani aliyekuwa amefanya jambo lile.
“Ni lazima uchunguzi ufanyike, hii ni aibu kubwa professa,” alisema mwanachuo mmoja, alikuwa akimwambia professa.
“Ndiyo hivyo! Hivi ilikuwajekuwaje?”
“Hata mimi sikuona vizuri, nilishtukia akitokwa damu.”

“Hii ni hatari sana. Ni lazima aliyefanya unyama huu apatikane, tunataka kujua na sababu pia,” alisema professa.
Taarifa za kuchomwa kisu kwa Tatiana zikaanza kusambaa kama upepo, mitandaoni, watu wakawa wa kwanza kuziandika kitu kilichopeleka kusambazwa duniani kwa haraka sana. Kila mtu aliyezisoma taarifa hizo alipigwa na mshangao, hawakuamini kile kilichokuwa kimetokea, nchi ambayo watu waliita kuwa ya amani, kutokea kitendo kama kile cha kikatili kilishusha heshima ya nchi.

Duniani kukawa gumzo, nchi ya Tanzania ikaanza kusikika tena kutokana na kile kilichokuwa kimetokea. Hapo ndipo watu walipogundua kwamba msichana huyo alikuwa na maadui wengi duniani hivyo alitakiwa kupewa ulinzi wa nguvu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom