Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
- Thread starter
- #201
SEHEMU YA 96...
Peter hakutaka kuondoka, naye alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa uwanjani hapo ambao walitaka kumuona msichana huyo akiwa jukwaani. Japokuwa moyo wake ulimuuma mno lakini hakuthubutu kabisa kuondoka uwanjani hapo.
Dakika ziliendelea kukatika, watu walizidi kuongezeka zaidi mpaka kufikia watu zaidi ya elfu ishirini uwanjani hapo na hakukuwa na dalili za watu kukata. Ilipofika saa saba kamili mchana, ving’ora vikaanza kusikika, hakukuwa na maswali kwamba yule aliyekuwa akitarajiwa kuingia mahali hapo alikuwa nani.
Watu wakaanza kukimbilia kule kulipokuwa pa kuingilia, kila mtu alitaka kumuona Tatiana tu. Pikipiki mbili zilitangulia mbele na magari mengine kufuata, alionekana kuwa na msafara uliomkaribia rais wa nchi.
Watu wakaanza kupiga kelele huku wakiliimba jina lake ambalo lilionekana kuwa kero kwa Peter aliyekuwa akifuatilia kila kilichokuwa kikiendelea uwanjani hapo. Baada ya magari kusimama, Tatiana akashuka huku akiwa na Buffet kitu kilichoibua shangwe nyingi uwanjani hapo.
“Huyu demu mkali sana, sijui kwa nini sikuonana naye kabla ya kuwa supastaa!” alisikika akisema jamaa mmoja.
“Daah! Halafu Mzungu mwenyewe boya tu ndiye anamchukua dada yetu,” alisema jamaa mwingine.
Tatiana akaanza kupiga hatua kwenda jukwaani, alikuwa akipunga mikono yake hewani, watu walizidi kushangilia, moyoni mwa Peter, alitamani achimbe kaburi na kujizika kwani kila alipokuwa akimwangalia msichana huyo jukwaani, alizidi kuumia. “Ninakuchukia Tatiana,” alisema huku akiuma meno yake kwa hasira.
****
Nathan alimaanisha alipotamka kwamba mara ya kwanza kwamba alitaka kumuua msichana Tatiana, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, japokuwa kipindi kirefu kilipita lakini bado alikuwa na hasira mno na msichana huyo.
Hakutaka kuona akiendelea kuishi, kwa kile alichokuwa amemfanyia, alijiapiza kwamba ilikuwa ni lazima amuue hata kama angetumia kiasi gani cha fedha. Alichokifanya ni kuanza kumfuatilia kwani alikwishajua kwamba Petrov alishindwa hivyo alitaka kuingia kazini yeye mwenyewe.
Peter hakutaka kuondoka, naye alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa uwanjani hapo ambao walitaka kumuona msichana huyo akiwa jukwaani. Japokuwa moyo wake ulimuuma mno lakini hakuthubutu kabisa kuondoka uwanjani hapo.
Dakika ziliendelea kukatika, watu walizidi kuongezeka zaidi mpaka kufikia watu zaidi ya elfu ishirini uwanjani hapo na hakukuwa na dalili za watu kukata. Ilipofika saa saba kamili mchana, ving’ora vikaanza kusikika, hakukuwa na maswali kwamba yule aliyekuwa akitarajiwa kuingia mahali hapo alikuwa nani.
Watu wakaanza kukimbilia kule kulipokuwa pa kuingilia, kila mtu alitaka kumuona Tatiana tu. Pikipiki mbili zilitangulia mbele na magari mengine kufuata, alionekana kuwa na msafara uliomkaribia rais wa nchi.
Watu wakaanza kupiga kelele huku wakiliimba jina lake ambalo lilionekana kuwa kero kwa Peter aliyekuwa akifuatilia kila kilichokuwa kikiendelea uwanjani hapo. Baada ya magari kusimama, Tatiana akashuka huku akiwa na Buffet kitu kilichoibua shangwe nyingi uwanjani hapo.
“Huyu demu mkali sana, sijui kwa nini sikuonana naye kabla ya kuwa supastaa!” alisikika akisema jamaa mmoja.
“Daah! Halafu Mzungu mwenyewe boya tu ndiye anamchukua dada yetu,” alisema jamaa mwingine.
Tatiana akaanza kupiga hatua kwenda jukwaani, alikuwa akipunga mikono yake hewani, watu walizidi kushangilia, moyoni mwa Peter, alitamani achimbe kaburi na kujizika kwani kila alipokuwa akimwangalia msichana huyo jukwaani, alizidi kuumia. “Ninakuchukia Tatiana,” alisema huku akiuma meno yake kwa hasira.
****
Nathan alimaanisha alipotamka kwamba mara ya kwanza kwamba alitaka kumuua msichana Tatiana, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, japokuwa kipindi kirefu kilipita lakini bado alikuwa na hasira mno na msichana huyo.
Hakutaka kuona akiendelea kuishi, kwa kile alichokuwa amemfanyia, alijiapiza kwamba ilikuwa ni lazima amuue hata kama angetumia kiasi gani cha fedha. Alichokifanya ni kuanza kumfuatilia kwani alikwishajua kwamba Petrov alishindwa hivyo alitaka kuingia kazini yeye mwenyewe.