Pengo kamsamehe mlopokaji Gwajima!? Sasa presha itabakia ktk mali amezipata wapi wakati yy ni mtumish wa kanisa kama anavyojinasibu wakati wajanja wanajua yeye mfuasi wa dini ya shetani.
askofu mkuu wa jimbo la dar es salaam mwadhama pengo amesema amemsamehe mchungaji gwajima na wote walioguswa .
ameyesema hayo wakati wa ibada ya Leo jumapili katika kanisa la st joseph
amesema "naomba niseme kutokana na hali iliyopo kuwa kutoka moyoni kabisa nimesamehe yote yaliyosemwa na naomba tumuombee na kuwaombea wote walioguswa sina kinyongo chochote"
waamini walilipuka kwa makofi baada ya kusikia kauli ya mwadhama
Mytake:niishauri serikali kuachana na gwajima madam mwadhama ametamka tena huku akiwa amekalia kiti cha kiaskofu kwa sisi wakatoliki nadhani tunajua maana ya tamko linapotolewa huku askofu akiwa amekalia kiti chake maana yake Mungu ameupokea msahama
source Mimi mwenyewe nilikuwepo kwenye misa
Gwajima ni wa kumsamehe tu, hana akili nzuri. Kuna clip nimemskia akidai alikuwa anamkemea askofu mwenzake. Yaani Gwajima askofu wa mtaani anataka kujilinganisha na Pengo!!?
Alafu anadai mwenyekiti wa maaskofu wa katoliki ndiye mkuu wa kanisa katoliki Tanzania. Ana uelewa mdogo sana. Sijui anawezaje hata kuwatapeli wafuasi wake kiasi hicho.
Huko polisi alienda kufanya nini?Nani kamsababishia mwenzake matatizo? Salary slip, sikujui, lakini huwa naona post Zako za mtu msomi! Sasa hii statement yako inanipa mashaka makubwa sana. Nani kamsababishia mwenzake matatizo, nifafanulie
Huko polisi alienda kufanya nini?
Hata kama hakwenda polisi kushitaki,lakini si bado angeweza kuwataka polisi wamfutie mashitaka hayo?Sasa amekaa kimya anasubiri atangaze msamaha siku ya ibada mbele ya waumini ili iweje?
Kwa kiongozi wa kiroho mwenye kujua maama ya kusamehe tofauti na mtu wa kawaida asingefikisha jambo hili polisi au baada ya kuona Gwajima anapelekwa polisi basi angewataka polisi kumfutia mashitaka na si kusubiri kutangaza msamaha siku ya ibada.
Isitoshe,alipaswa kuwa amenda kumuona hospitali aliko lazwa.
Ndugu yangu,siku hizi hatuna viongozi wa kiroho bali tuna viongozi wasanii tu kama hawa wa kisiasa.
kwani wewe unafikiri mkuu wa kanisa katoliki ni pengo! basi wewe ndo unauelewa mdogo
Sio kusamehe tu na YEYE ameomba msamaha wakristu kwa kutusaliti??..Yeye ni msaliti,Awaombe msamaha maaskofu wenzie kwa usaliti huu mkubwa na kufanya kazi isiyo yake
Pengo ni mnafiki anaungana na polisi wanataka wamwue Gwajima kisa elekopta,wakati elekopta ni usafiri Wa kawaida, mbona polisi wanashindwa kuoji hela anazogawa Lowasa kwa wenye mtindio Wa ubongo kumshawishi agombee urais
Anyway,inawezekana ingawa nina mashaka.Makosa ya gwajima ni criminal! jamhuri ndiye inayemshitaki, Pengo ni shahidi, hana mamlaka ya kuiambia polisi waache utaratibu wao wa kushughulikia makosa ya jinai! Kama una rafiki mwanasheria muulize. Sheria ya jinai iko hivyo.
Pengo lililo katika uwezo wake ni civil tort against Gwajima! hilo anaweza akaiambia mahakama kuwa amesamehe, not criminal! Jamhuri ikiamua hata ukasema nimemsamehe wao wana mamlaka ya kisheria kuendelea na kesi!
Pengo ndio kiongozi wa kanisa Katoliki Tanzania
Mimi Mkatoliki na mseminary lakini namwelewa zaidi Gwajima kuliko Pengo . Pengo alitakiwa kuomba Wakatoliki wa Tanzania msamaha kwa ushirika wake na CCM kabla ya kusema amesamehe Gwajima .
askofu mkuu wa jimbo la dar es salaam mwadhama pengo amesema amemsamehe mchungaji gwajima na wote walioguswa .
ameyesema hayo wakati wa ibada ya Leo jumapili katika kanisa la st joseph
amesema "naomba niseme kutokana na hali iliyopo kuwa kutoka moyoni kabisa nimesamehe yote yaliyosemwa na naomba tumuombee na kuwaombea wote walioguswa sina kinyongo chochote"
waamini walilipuka kwa makofi baada ya kusikia kauli ya mwadhama
Mytake:niishauri serikali kuachana na gwajima madam mwadhama ametamka tena huku akiwa amekalia kiti cha kiaskofu kwa sisi wakatoliki nadhani tunajua maana ya tamko linapotolewa huku askofu akiwa amekalia kiti chake maana yake Mungu ameupokea msahama
source Mimi mwenyewe nilikuwepo kwenye misa